Hivyo kwa kanuni hiyo hiyo ya kuponywa pasipo matendo, basi itumie hiyo hiyo kwa ugonjwa ulionao hapo ulipo, kama una HIV, au KISUKARI, au KANSA, au UTASA au Vidonda vya tumbo, au tatizo la figo, au ini, au moyo, au ni kiziwi, au kipofu, au ni kiwete, au tatizo lolote lile katika mwili wako. Kinachohitajika kwako ni IMANI tu!!..Usianze kujishaurishauri wala kuwa na mashaka mashaka, yakatae hayo mashaka, hata kama wakati mwingine bado unaona kuna udhaifu mwilini, hapo ulipo simama juu sema nimeshapona kwa jina la YESU. Kifo kimeshaingia kwenye huo ugonjwa..haupo tena huo ugonjwa, hata kama bado unahisi maumivu yasikuogopeshe tayari kifo kimeshaingia kwenye huo ugonjwa..unaukumbuka ule mtini Bwana Yesu alioulaani?…haukunyauka palepale lakini tayari ulikuwa umeshakufa ndani kwa ndani, hauna uzima tena, mizizi ilikuwa imeshaoza, baada ya masaa kadhaa wanafunzi wanafunzi walipouona umenyauka ndipo wakaelewa kuwa kumbe mti ulikuwa umeshakufa tangu jana Bwana alipoulaani, na sio leo, na ndivyo itakavyokuwa leo kwako na huo ugonjwa ulio ndani yako, usiangalie hali uliyo nayo hapo, amini kwamba tayari kiini cha ugonjwa hakipo…