Title August 2020

HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.

Luka 16:16 “Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”.

Nataka uone hicho kifungu cha mwisho, “ Na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”..

Bwana Yesu alipotoa habari hiyo, kulikuwa na sababu kubwa kwanini alianza kwanza na habari za agano la kale(Torati na manabii) kisha akaja kwenye agano jipya, na kumalizia kwa kusema, tangu huo wakati kila mtu atakawa anajiingiza kwa nguvu.

Alisema hivyo kuonesha kuwa hapo kabla, kulikuwa hakuhitaji bidii yoyote, au jasho lolote, au nguvu yoyote, kuijua torati, lakini kuanzia wakati wa Yohana, injili ya kweli ambayo inaleta ondoleo la dhambi, ilipoanza kuhubiriwa, injili ya kumfanya mtu awe na maarifa kamili kumuhusu Mungu ilipoanza kuhubiri, injili inayomfungua mtu kweli kweli, basi vipingamizi vikubwa sana vitanyanyuka kiasi kwamba, mpaka mtu aipate ni lazima atumie nguvu nyingi sana kuingia, tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo.

Kwamfano utaona wakati ule tu, kulikuwa na mafarisayo na waandishi, ambao wamesimama hapo, katikati kuhakikisha kuwa mtu yeyote atakayemkiri Yesu hadharani, moja kwa moja atatengwa na sinagogi, (Yohana 9:22)

Na kutengwa kwa zamani sio kama sasa, zamani ukitengwa na sinagogi ni jamii nzima ya Israeli imekutenga mpaka familia yako. Hata misaada ya kijamii ulikuwa hupati, Hivyo suala la kutengwa lilikuwa ni jambo zito sana.

Hivyo haikuwa ni rahisi, hata kidogo, ilibidi watu walazimishe, mambo kwa nguvu, wawe radhi kutengwa tu, wawe tayari kupoteza mahusiano yao tu, lakini wasiukose ufalme wa mbinguni.

Mambo hayo hayo hata sasa, yanaendelea, kuupata ufalme wa mbinguni, ni kujiingiza kwa nguvu nyingi, wapo viongozi wako wa dini wanakuzuia usiokoke, kisa tu imani yao haimini kile biblia inachosema, pengine Imani yao inafundisha kusujudia sanamu, haiamini katika karama za Roho, ndugu usiwaangalie hao, wewe jiingize kwa nguvu katika ufalme wa Mungu,.

Hao ni wale wana-sheria wa dini, ambao Bwana Yesu anasema, kazi yao ni kusimama pale mlango kushikilia funguo, kuwazuia watu wasiingie, na wao wenyewe hawauingii, wanataka mkae wote katika giza la milele pamoja..

Luka 11:52 “Ole wenu, enyi wana-sheria, kwa kuwa mmeuondoa ufunguo wa maarifa; wenyewe hamkuingia, na wale waliokuwa wakiingia mmewazuia”.

Hivyo usiwaangalie hao hata kidogo, achana na mapokeo ya dini, tubu dhambi uokoke, tafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, na sio ule wa kunyunyiziwa ambao haupo katika maandiko.

Jiingize kwa nguvu, hata kama ndugu zako hawakuelewi, Jiingize kwa nguvu hata kama marafiki zako watakuona mshamba, jipenyeze kwa nguvu hata kama dunia itakuona umerukwa na akili..Iokoe roho yako, wakati huu jiepushe na mtu ambaye unaona kabisa anaizuia njia yako ya wokovu.

Wenyewe hawawezi kuona hilo, kwasababu bado wapo gizani, lakini wewe umeiona nuru, usijifananishe na wao, zidi jenga uhusiano wako binafsi ya Yesu. Hizi ni nyakati za mwisho na unyakuo upo karibu sana,

Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.

13 Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana”.

Isiishi kwa kuwapendezesha watu na huku umelisahau Neno, kwasababu kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe (Wagalatia 6:5). Dakika hizi za majeruhi, zinafananishwa na Sodoma na Gomora, ambazo tunajua ni watu 3 tu kati ya mamilioni waliokuwa katika miji ile ndio waliopona….Ndivyo itakavyokuwa siku hizi, litavuka kundi dogo tu, lililoweza kujiingiza kwa nguvu katika ufalme wa mbinguni bila kujali vizuizi vya mpito vya ibilisi.

Unadhani shetani, hajui kuwa mtu akiupata ufalme wa Mungu, amepata kitu cha thamani kubwa sana, anajua hilo, na ndio maana lazima akuletee ugumu ili usijaribu kuuingia, ubakie kwenye giza huko huko..Hivyo vitisho kutoka kwa viongozi wako wa dini na ndugu na marafiki, visikufanye usichukue uamuzi wa kumpokea Yesu.

Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.

35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;

36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.

37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.

39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.

Kama bado hujafanya uamuzi huo basi anza sasahivi, wokovu unapatikana bure, lakini si rahisi si rahisi lakini inahitaji nguvu kujiingiza kwa huo, hivyo jiingize kwa nguvu bila kujali, na huko huko Bwana Yesu atajifunua kwako kwa namna ambayo hukuwahi kumjua hapo kabla, ndipo utakapomjua Mungu, na ndipo atakapotembea na wewe.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

USIUZE URITHI WAKO.

Je! Kiongozi wa dini anaouwezo wa kusamehe dhambi?

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

JIHADHARI NA KUOSHWA MIGUU ISIVYOPASWA.

MWANANCHI WA UFALME WA MBINGUNI

USIISHI BILA KUIFANYA KAZI YA MUNGU KABISA..

Rudi Nyumbani:

Print this post

JUKUMU LA MUHIMU LINALOKWEPWA NA WENGI.

Jukumu moja na kuu tulilonalo sisi ni KUMJUA SANA YESU KRISTO. Wengi wanalikwepa jukumu hili. Na Zaidi wanapenda sana kutafuta kuwajua watumishi wa Yesu kuliko ya Yesu mwenyewe.

Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani NA KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”.

Jitathmini ukiona kuna mahali unamjua mtumishi, zaidi ya Bwana wake mwenyewe ambaye ni Yesu, basi kuna tatizo mahali na pia una laana.(1Wakorintho 16:22)

Kama mtumishi wa Kristo akizungumziwa vibaya inakuuma Zaidi ya Yesu akifanyiwa mzaha, basi kuna tatizo katika uhusiano wako na Yesu.

Kama comedy za kumtania Mwokozi Yesu hazikuhuzunishi sana kama za kumtania  mchungaji wako, au mwalimu wako, basi kuna tatizo mahali.

Kama unakuwa mkali dini yako inapozungumziwa vibaya, au dhehebu lako au mwalimu wako anayekufundisha Neno la Mungu kanisani, na wakati huo huo unakutana na comedy inayomkebehi Kristo waziwazi na wala haikuhumizi  sana Zaidi inakuchekesha!, hebu jitafakari tena, inawezekana humjui kabisa Yesu, wala hayupo maishani mwako.

Kama Maisha yako ya binafsi ya siri, hujawahi kukaa ukazungumza  na mwokozi wala kumshukuru, basi kuna shida.

Dada/kaka usitumie nguvu nyingi kutafuta kumpendeza mtumishi, wala usiwe mshabiki wa dini, wala usiwe mshabiki wa mtumishi wa Mungu.

Tafuta kumjua Yesu, na kumjua Yesu sio kuhama na kubadilisha kanisa…Ni hapo hapo ulipo tu!..Unachopaswa kukifanya baada ya kumpokea Kristo ni kukinunua kitabu kinachoitwa Biblia. Usitegemee ile ya ku-download kwenye simu yako.. Ya kudownload ni nzuri baada ya kuwa na ya KITABU chenye kurasa za karatasi.

Hivyo kinunue hichi kitabu kinachoitwa Biblia. Ukishakipata! Anza kukisoma mwenyewe!..Mungu kakupa macho, kakupa na uwezo wa kusoma, hawezi kukunyima uwezo wa kuelewa!..

Kinachosababisha wengi wasiielewe biblia ni kusoma kwa kutimiza wajibu tu!..na sio kwa kutoka ndani ya mioyo yao, wanasoma tu kwasababu wameambiwa wasome, au kwasababu tu wanahisi ndio wanampendeza Mungu, na anasoma kwa mwezi mara moja…Hivyo biblia inakuwa ni kitabu kigumu sana kwao kukielewa. Na pia wanasoma mstari mmoja kisha wanarukia mwingine…Hawapendi kusoma mwanzo wa kitabu hadi mwisho.

Hivyo soma biblia mwenyewe kwa macho yako mawili. Ukikutana na jambo gumu kuna nguvu Fulani ya asili ambayo Mungu kaiweka ndani yetu itakayokupeleka katika kuutafuta ukweli Zaidi, hapo ndipo kitakuja kitu cha kutafuta msaada Zaidi kwa mahubiri ya watumishi wa Mungu, utaona kuna kitu kinakusukuma kwenda sehemu Fulani labda kanisa Fulani, au kwenye semina Fulani, au katika mahubiri Fulani.. ambapo utaona utapata majibu ya maswali yako, au utakwenda kusoma jumbe Fulani ambazo utaona zitakufaidisha roho  yako. Na kwa njia hiyo ndipo mafunuo ya Roho yanapokuja.

Lakini huwezi kusema naondoka kanisa hili nahamia lile kama hujapata sababu yoyote ya kimaandiko ya kufanya hivyo.. Wengi wanahama kanisa kwasababu tu wameambiwa ukweli..hivyo ule ukweli unawauma na kuishia kuhama, wengine kwasababu wamesikia wakisengenywa, wengine kwasababu wameona kanisani kumepungua watu hivyo na wao wanaondoka…mambo ambayo hayana mashiko kabisa!..Mtu wa namna hiyo hajaongozwa na Mungu, bali kafuata akili zake mwenyewe.

Lakini mtu wa kweli ambaye anaongozwa na Roho, huwa anaondoka sehemu moja hadi nyingine, ni kwasababu anatafuta uelewa wa maandiko Zaidi, anatamani kumjua Yesu zaidi na kukua kiroho.. huyo ndiye anayeongozwa na Roho. Anaona kuna umuhimu wa kutafuta kujifunza Neno Zaidi, kutafuta kufunga Zaidi na kusali. Na si kwasababu kasikia kasengenywa, au kasemwa, au kaudhiwa.

Hivyo siku zote usilisahau hili ndugu yangu mpendwa.. MJUE SANA YESU. Huyo ndio ndiye Mkuu wa Uzima, na ndiye mwenye funguo za Uzima,  na ndiye aliyekabidhiwa mamlaka yote ya mbinguni na Duniani..Tunavyozungumza sasa yupo anaishi! Na atarudi tena kulichukua kanisa lake, Ana nguvu nyingi sana, yeye hadhihakiwi sio yule unayemwona kwenye picha, sio unayemwona kwenye Tv, Yesu ni Mungu, akijifunua kwetu kikamilifu, hata hapa duniani tunaweza tusitamani kuendelea kuishi, Hivyo tumjue yeye kila siku, tujinyenyekeze mbele zake, ajifunue kwetu zaidi na zaidi. Anatamani kujifunua kwetu sana, ni sisi tu.

Bwana atubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?

Kuna haja gani ya kumwamini Yesu aliyezaliwa kama sisi?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUZALIWA KWA YESU.

kuzaliwa kwa Yesu kulikuwaje?


Mathayo 1:18 “Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

19 Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri.

20 Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.

22 Hayo yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii akisema,

23 Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.

24 Naye Yusufu alipoamka katika usingizi, alifanya kama malaika wa Bwana alivyomwagiza; akamchukua mkewe;

25 asimjue kamwe hata alipomzaa mwanawe; akamwita jina lake YESU”.

Yesu mwokozi, kama si kuzaliwa kwake ulimwenguni, leo hii tungekuwa wapi? Kama sio kuimwaga neema yake duniani, tungepatia wapi ondoleo la dhambi?

Mamajusi walitoka nchi ya mbali, kwa furaha tu ya kumwona mwokozi wa Ulimwengu, ambaye hata hakuzaliwa katika nchi yao..lakini kwa kuiona tu nyota yake, hawakusubiri, wahadithiwe, walianza safari..

Lakini Swali la kujiuliza Je! Na wewe amezaliwa moyoni mwako?

Bwana Yesu lipoanza kuitenda kazi ambayo Baba yake amemtumia alisimama na kusema maneno haya..

Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Hiyo ni kazi kubwa ambayo ilimleta duniani, na ndio maana mwishoni kabisa mwa kitabu cha Ufunuo alisema hivi..

Ufunuo 21:6 “Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure”.

Hivyo mpe leo Yesu maisha yako, ayaokoe, akufanye kuwa kiumbe kipya. Hizi ni siku za mwisho, Yesu yupo mlangoni kurudi.Dalili zote zinaonyesha, kuwa mimi na wewe tunaweza kushuhudia tukio la Unyakuo.

Bwana atusaidie sana.

Shalom.

Ikiwa utapenda mafundisho ya biblia yawe yanakufikia kwa njia ya whatsapp, basi tutumie ujumbe kwa namba hii: +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

JIFUNZE NENO LA MUNGU KWA BIDII ZOTE.

EPUKA MUHURI WA SHETANI

https://wingulamashahidi.org/2018/07/19/nyakati-saba-za-kanisa-na-wajumbe-wake/

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Kuhutubu ni nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

USHIRIKINA NA MADHARA YAKE.

Ushirikina na madhara yake, rohoni ni yapi?


Ushirikina ni kitendo cha kwenda kutafuta msaada wa kiroho au wa kimwili katika mamlaka ya giza. Nikisema mamlaka ya giza namaanisha kwa shetani na mapepo na majini yake yote yanayofanya kazi kupitia watu wanaoitwa waganga au wachawi.

Sasa unapoumwa, halafu badala ya kwenda kuwa Mungu upate msaada, wewe unakimbilia kwa waganga wa kienyeji ili upate msaada ya kiganga, hapo moja kwa moja tayari umeshashirikiana na mashetani katika ulimwengu wa roho.

Au unapopitia matatizo Fulani aidha ya kifamilia, au ya kikazi, au unahaja ya jambo Fulani pengine masomo, au ndoa, au cheo, halafu wewe moja kwa moja unakimbilia kwa mganga akusaidie kutatua tatizo lako, ujue kuwa tayari umeshaingizwa katika mtandao wa Mashetani.

Jambo ambalo wengi hawajui ni kuwa, walau kwa mtu wa kawaida yeyote, kunakuwa na ka-ulinzi Fulani kutoka kwa Mungu, ambacho anazaliwa nacho hicho kanamfanya shetani asiweze kujiamulia tu jambo lolote atakalo juu ya huyo mtu, vinginevyo ungekuwa shetani kashawamaliza watu wote duniani, kwa kuwaua, Ndio ni kweli ataweza baadhi  lakini sio yote. Sasa pale mtu anapokwenda kwa shetani mwenyewe kumwomba msaada, maana yake ni  kuwa anasaini naye mkataba rasmi kuwa kuanzia sasa, huy mtu ni wangu na naweza kufanya jambo lolote juu yake.

Haya ndio madhara ya moja kwa moja ya ushirikina.

  1. Unaingiliwa na mapepo:

Angalia vizuri utaona asilimia kubwa ya watu wanaoudhuria kwa waganga wanakuwa wanasumbuliwa na nguvu za giza, au wengine wanapata ulemavu Fulani ambao hapo kabla hawakuwa nao, au ugonjwa Fulani, ambao hauponi, hiyo yote ni kutokana na mtu kujishughulisha na ushirikina.

  1. Unakuwa hatarini kufa:

Kutokana na kuwa tayari umeshajihalalisha kwa shetani, basi shetani kazi yake kubwa iliyobakiwa nayo kwako ni kukuua,..Kwasababu ndio dhumuni lake hapa duniani, kuua biblia inasema hivyo…

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake”.

  1. Chochote unachokifanya hutafanikiwa:

Hata kama kitaonekana kukuletea matokeo mazuri kiasi gani mwanzoni, kumbuka hiyo ni gia tu ya shetani kukuvuta kwake, ili usimwache, lakini katika kipindi cha muda mrefu, hakitakufikisha popote, kama ulikuwa umekwenda kutafuta mali, hizo mali zitapotea tu baada ya kipindi Fulani, kama ulikuwa umekwenda kutafuta kazi, hiyo kama unaweza usiipate, na hata ukiipata haitadumu, utakuwa ni mtu ambaye anafanya jambo lakini baada ya muda mrefu haoni faida ya jambo hilo, au haoni maendeleo yoyote. Na mwisho wa siku unajikuta ni heri usingeenda.

Mithali 11:21 “Hakika, mtu mwovu hatakosa adhabu; Bali wazao wa wenye haki wataokoka”.

Ayubu  21:13 “Siku zao hutumia katika kufanikiwa, Kisha hushuka kuzimuni ghafula”.

  1. Unapoteza Utu na uwezo wa kupambanua mambo ya rohoni:

Kumbuka pale unapokwenda kwa waganga, ni unaonyesha kuwa humuhitaji Roho Mtakatifu kukusaidia, na kazi ya Roho Mtakatifu ni kuwavuta watu kwa Mungu, na kuwapa macho ya rohoni, Hivyo unapojihusisha na ushirikina na uchawi, ni kuwa unapoteza huo uwezo, na matokeo yake unakufa kiroho.. Hapo ndipo unaanza kufanya hata yale mambo ambayo mwanadamu wa kawaida hawezi kufanya,..Hayo unaweza usiyaone leo, lakini kwa jinsi siku zitakavyozidi kwenda mabadiliko hayo utayaona, kwasababu nguvu za giza wakati huo zitakuwa zinakutawala.

2Wakorintho 4:4 “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.

 

  1. Ukifa unakwenda motoni.

Washirikina wote, wachawi wote, biblia inasema sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Ukifa leo na upo katika hali hiyo , basi ni moto wa milele unakuongoja.

Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.

 

Sasa kwanini hayo yote yakukute?

Lakini Habari njema ni kuwa, hata kama umeingia huko, bado unayo nafasi ya kutengenezwa upya. Na anayeweza kufanya hivyo, si mwingine zaidi ya YESU KRISTO tu peke yake..Huyo ndiye aliyetiwa mafuta na Mungu, ili kuwatoa watu katika vifungo vya giza, mwingine yeyote hawezi….

Isaya 61:1 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.

Hivyo kama ulishaingia humo, au bado hujaingia, lakini Kristo bado hayupo ndani yako, basi leo hii fanya uamuzi huo, wa kumkaribisha ndani yako ayaokoe maisha yako moja kwa moja, haijalishi wewe ni muislamu, Yesu anawaokoa wote, wanaomkimbilia yeye kwa moyo wa dhati.

Akikuweka huru, amekuweka huru kweli kweli, haachi hata alama ya uovu ndani yako, akikusamehe amekusamehe kweli kweli, kana kwamba hukuwahi kumkosea, kwa lolote. Atakufungua kutoka katika malango hayo ya mauti ya ibilisi yaliyokufunga, na kukuletea katika ufalme wa wana wa Mungu. Roho Mtakatifu akiingia ndani yako, hakuna pepo lolote litakaloweza kukaa ndani yako, Ukimkaribisha leo hii atakufanya huru, na kuna amani itaingia ndani mwako, ambayo utashangaa imetoka wapi..Huyo ndio Yesu mwokozi.

Hivyo kama upo tayari leo hii kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuacha, na kusema kuanzia sasa namfuata Yesu, sitaki ushirikina, sitaki dhambi, Namfanya Yesu kuwa kiongozi wa maisha yangu basi uamuzi huo ni mzuri na wa busara, basi, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala fupi ya Toba..>>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ubarikiwe sana.

Mada Nyinginezo:

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

EPUKA MUHURI WA SHETANI

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

JE NI KWELI MTU ANAWEZA KUTOKA NJE YA MWILI WAKE?.

MAONO YA NABII AMOSI.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

DUNIA HII ITAHARIBIWA KABISA.

Isaya 24:3 “Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana Bwana amenena neno hilo.

4 Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika.

5 Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele.

6 Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu”.

Nabii Isaya alipotabiri juu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo na bikira (Isaya 7:14), miaka 700 kabla ya Masihi kuja duniani, wapo watu pengine walioona kuwa hizo ni hadithi tu za kufikirikika… Alipotabiri tena juu ya mateso yake yatakayoompata (Isaya 53), nazo pia zikaonekana pengine ni habari tu, lakini wakati ulipofika, hayo yote kutimia kwa ufasaha wote, ndipo wakajua kuwa Neno la Mungu huwa halipiti.

Isaya huyo huyo aliyetabiri ujio wa Kristo kwa uvuvio wa Roho, ni huyu huyu alioonyeshwa pia hatma ya huu ulimwengu utakavyokuja kuwa siku za mwisho, na habari zake kaziandika sehemu nyingi sana kwenye kitabu hicho chenye sura 66, alionyeshwa jinsi hii dunia itakavyokwenda kuwa utupu, na kuharibiwa kabisa, jinsi jua litakavyotiwa giza, jinsi watu watakavyoadimika kama dhahabu duniani, na kibaya zaidi alionyeshwa fedha ya mtu wakati huo haitafanya kazi yoyote, umaarufu wa mtu utakuwa hauna maana, biashara za mtu zitakuwa ni kama takatakata, elimu ya mtu haitafanya kazi..tajiri na maskini wote watakuwa wakiomboleza sawa.

Na nyakati zenyewe ndio hizi tunazoishi mimi na wewe, kila mtu analijua hilo, hata ukimuuliza mtoto mdogo atakuambia, hizi ni nyakati za mwisho, watu wengi wanaposikia maneno haya wanapuuzia wakidhani hichi ni kama kile kipindi cha mitume..Ndugu hichi sio kipindi cha mitume.. Fuatilia mambo yanayoendelea duniani hata kupitia mitandao ndipo utakapojua kuwa tunaishi nyakati nyingine.

Bwana Yesu alisema hivi..

“Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;

33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.

34 Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia” (Mathayo 24:32).

Sasa kama wewe ni msomaji wa Biblia utajua kuwa Mtini unafananishwa na Taifa la Israeli (Yeremia 24), na wakati ule Israeli ilikuwa bado haijachipua (yaani haijawa taifa), ilipitia miaka zaidi ya 2,500 tangu wachukuliwe utumwani Babiloni, na ulipofika mwaka 1948, Israeli ikachipuka tena na kuwa taifa kwa mara ya kwanza,..Na tunajua kabisa agenda ya Mungu ya wokovu itamalizia tena na Israeli pale Yerusalemu.

Hivyo tangu huo wakati Bwana alisema kizazi hiko, (yaani kilichoshuhudia Israeli kuchupuka tena), hakitapita mpaka hayo yote, kutimia,..Mambo yote aliyoyazungumzia katika Mathayo 24, hadi kurudi kwa pili kwake,..Na kizazi huwa hakizidigi miaka 120, sasa piga hesabu hapo, tunaishi katika wakati gani.. (Hatujui siku wala saa lakini tunayajua majira).

Sikuzote, kiwango chako cha maarifa kuhusu Mungu, ndio kinachoelezea maisha ya kiroho unayoishi sasa hivi, kama jicho lako bado halioni kuwa tunaishi katika majira ya unyakuo, na kwamba huu ndio ule wakati ambapo watu watadhanishia mbona ni amani, na salama, na kumbe ule uharibifu unakuja kwa ghafla (1Wathesalonike 5:3)..Kama ilivyokuja Corona kwa ghafulani pasipo ulimwengu kujiandaa…Ndicho kitakachoitokea dunia kipindi sio kirefu.

Sijui kama hilo unalijua ndugu yangu, kanisa hili linaitwa Laodikia, (Sio dhehebu linaloitwa Laodikia! Hapana!..Bali ni hali ya kanisa kwa ujumla inayofananishwa na Kanisa la Laodikia la Nyakati za kwanza, kasome Ufunuo 3:14), na ndio kanisa la mwisho la 7, na hakutakuwa na kanisa lingine baada ya hili, niambie ni dalili ipi ambayo haijatimia Yesu aliyoirodhesha kwenye Mathayo 24.

Internet imeweza kurahisisha mambo, siku hizi haihitaji mtu aende tena kwenye mikutano ya Injili asikie mahubiri, pale pale alipo hata kama ni kijijini akiwa chumbani mwake Injili inamfikia, utasema Injili haijahubiriwa dunia nzima leo?..

Shetani anataka watu waendelee kufikiria hivyo hivyo, kwamba bado sana, anataka watu waangalie upepo wa dunia unavyokwenda, lakini wasiangalie biblia inasema nini kuhusu siku hizi. Usipokuwa mvivu kusoma biblia ndipo utakapojua ni kwa jinsi gani tunaishi katika nyakati za hatari kushinda zote ambazo zilishawahi kupita katika historia.

Hivyo huu ni wakati wa kuamka usingizini..

Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza”.

Kama bado hujaokoka, au umeokoka lakini bado mguu mmoja nje mwingine ndani, Embu anza, kuyaangalia upya maisha yako ya rohoni ndugu, Je! Yesu amekuokoa kweli kweli? Kama sio, basi huu ndio wakati, na sio kesho, unachopaswa kufanya ni kuamua kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha na kutozifanya tena, na kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 3:38,8:16 na 10:48 Upate ondoleo la dhambi zako.(Maagizo hayo ni muhimu sana!). Na Roho Mtakatifu atakuongoza katika kuyaelewa maandiko.

Na kuanzia hapo, anza kuishi maisha ya kama mtu unayemngojea Bwana Yesu kwasababu nyakati hizi, sio za kubembeelezewa wokovu tena, ni kubutuka haraka na kuishindania Imani.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAKOJOA KITANDANI.

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

NI WAKATI WA KUJIPIMA, WEWE KAMA MTUMISHI WA MUNGU!

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

MISTARI YA BIBLIA YA UPONYAJI.

MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WATASHINDANA LAKINI HAWATAKUSHINDA

Watapigana nawe lakini hawatakushinda maana yake ni nini?


Yeremia 1:18 “Maana, tazama, nimekufanya leo kuwa mji wenye boma, na nguzo ya chuma, na kuta za shaba, juu ya nchi yote; juu ya wafalme wa Yuda, na juu ya wakuu wake, na juu ya makuhani wake, na juu ya watu wa nchi hii.

19 Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana, ili nikuokoe”.

Haya ni maneno ambayo alipewa Yeremia baada ya kuitwa na Mungu katika huduma. Lakini kwa hofu ya labda atakapokwenda kuwaeleza  watu juu ya hukumu za Mungu, watakasirika na kumletea madhara ya ghafla labda watampiga mawe, hapo ndipo hapo Mungu akamuhakikishia kuwa ni kweli watakuja kupigana na yeye, lakini hawatamshinda, kwasababu yeye yupo pamoja naye.

Hata sasa adui hawezi kuja kupigana na mtu kama huna huduma ya  Mungu mkononi mwake, mstari huu unapendwa kutamkwa na watu wengi kirahisi rahisi hata watu ambao wapo katika dhambi, wanajidanganya wakisema..

watashindana lakini hawatakushinda

Huo ni uongo, shetani hashindani na watu waovu,hata mara moja, kwasababu tayari alishawashinda siku nyingi. Hivyo ukijiona unapitia vita visivyokuwa na maana angali wewe ni mwenye dhambi ujue hayo sio mapambano.

Lakini ili Neno hili liwe na nguvu ndani yako, ni sharti kwanza, uokoke, umkabidhi Yesu maisha yako kweli kweli, kisha uwe na kazi ya kufanya katika injili yake, ndipo hapo hata shetani akinyanyuka na majeshi yake yote kutaka kukuangusha wewe ni sawa na kazi bure, kwasababu Mungu yupo pamoja na wewe daima.

Wakati huo hata ulimwengu mzima uungane vipi kutaka kukupindua usisonge mbele, watakuwa ni kama wanapoteza Muda kwasababu Mungu yupo upande wako.

Hivyo kama upo tayari leo kuokoka, ili maneno haya yawe na nguvu kwako, basi uamuzi huo ni wa busara, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Mada Nyinginezo

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.

Historia ya wimbo wa tenzi – Ndio dhamana Yesu wangu

KWANINI TUNAOMBA KWA JINA LA YESU?

NAO WATAKAOUAWA NA BWANA WATAKUWA WENGI.

YEREMIA

Rudi Nyumbani:

Print this post

JIFUNZE NENO LA MUNGU KWA BIDII ZOTE.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, libarikiwe!.

Karibu tujifunze Biblia.

Ndege tunazozipanda zinazoruka angani, hazijaundwa na mtu mmoja, kuna jopo kubwa sana la watu wamechangia maarifa katika kuiunda ile.. Utaona aliyegundua injini ya ndege ni mwingine, aliyegundua mfumo wa hewa ndani ya ndege ni mwingine, aliyebuni umbile na mwonekano wa ndege ni mwingine, aliyegundua sayansi ya kuifanya iruke ni mwingine, aliyegundua mfumo wa umeme ndani ya ndege ni mwingine, aliyegundua Mafuta ya ndege ni mwingine, aliyegundua kona ya ndege ni mwingine, aliyebuni matairi ya ndege ni mwingine n.k.

Sasa hao wote kila mmoja akiandika kitabu chake kidogo cha maelezo kuhusu mchango wake huo na vitabu hivyo vikakusanywa Pamoja bila shaka tunaweza kujikuta tuna kitabu kimoja kikubwa kama Biblia au hata Zaidi ya biblia, kilichojaa elimu kuhusu ndege. Maana yake ni kwamba mtu atakayejifunza hicho na kukielewa anaweza naye pia kutengeneza ndege yake.

Hivyo basi kama ilikuwa ni mpango wa Mungu kwamba wanadamu siku moja waruke angani, waende mbali sana kule juu Zaidi ya Tai..kumbe mpango wake haukuwa wa kumpa mtu mmoja maarifa hayo, bali aligawanya ujuzi huo kwa watu tofauti tofauti wanaojulikana kama wanasayansi..ambao katika hao kila mmoja alipochangia ujuzi wake na uvumbuzi wake ndipo kitkapoumbwa kitu kinachoitwa Ndege.

Kama ulikuwa ni mpango wa Mungu siku moja tusafiri kutoka bara moja hadi lingine kwa muda mfupi kwa kutumia ndege, na tena kama ulikuwa ni mpango wa Mungu siku moja turuke mbali sana Zaidi ya mawingi hata kuufikia mwezi kwa kutumia roketi…Basi pia upo mpango mwingine wa Mungu ulio mkubwa Zaidi ya huo, ambao utatufanya tupae Zaidi ya mawingu na mwezi na Zaidi ya nyota… Na huo si mwingine Zaidi ya ule wa kutupeleka mbinguni yeye alipo.

Na kama vile maarifa ya uvumbuzi wa kifaa kinachoitwa ndege au roketi, yalivyogawanyika katikati ya watu tofauti tofauti, vivyo hivyo maarifa ya kwenda mbinguni wamefunuliwa Mitume na Manabii mbalimbali wa kwenye biblia…Wakina Yeremia, Danieli, Musa, Ezekieli,…Wakina Petro, Paulo, Yohana n.k Hao kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu kila mmoja kaandika siri za ufalme wa Mbinguni kwa jinsi alivyojaliwa…ambazo sisi kama wakristo, tunajifunza leo katika kitabu kinachoitwa biblia, na kama tukifuzu kukielewa vyema basi tunaweza kupaa juu Zaidi ya yale mawingu. Tunaweza kutengeneza roketi na kuingia ndani yake na kuruka Zaidi ya yale mawingu, na ndege yetu hiyo au Roketi ni YESU KRISTO.

Yesu ndiye NJIA, KWELI na UZIMA…Mtu hawezi kufika kwa Baba mbinguni isipokuwa kwa Njia yake yeye (Soma Yohana 14:6).

Teknolojia inahubiri injili, ukiona wakati tunaoishi inawezekana kusafiri hewani, basi jua kuna safari kubwa kuliko zote inakaribia. Lakini hayo yote hayaji pasipo maarifa.

Ndugu dada/kaka usiache kusomana kujifunza kamwe biblia, Hakuna sehemu yoyote utaweza kupata maarifa ya kumjua Yesu nje ya biblia. Usiposoma biblia kwa kujifunza utachukuliwa na kila aina ya upepo wa uongo. 

Usipende kusubiria tu kufundishwa biblia, Jifunze kuisoma mwenyewe!.. Hata mwanafunzi anayefanikiwa masomoni ni yule kwanza anayependa kujisomea mwenyewe…Na anapokutana na maswali magumu ndipo anapokwenda kuuliza kwa mwalimu wake!..Lakini mwanafunzi anayependa kufundishwa tu! Na wala hana muda wa kujisomea yeye mwenyewe..kamwe hawezi kufanya vizuri..Na ndivyo hivyo hata sisi, Mungu anataka tuisome biblia wenyewe!.

Kumbuka pia hajayarekodi maneno yake kwa njia ya Audio, kayaweka kwenye kitabu…Ukiona kitu kimewekwa kwenye kitabu maana yake anayekisoma anahitaji kuketi chini mahali pasipo na usumbufu, akiwa na kalamu yake na daftari..Biblia hatuisomi kama gazeti, tunajifunza na ndivyo Roho Mtakatifu anataka tuwe hivyo ili aweze kutufunulia siri zake..

Je unataka kwenda mbinguni?..Mimi nataka sijui wewe?..kama wewe nawe unataka basi Ni lazima tuifahamu biblia sana.

Bwana akubariki

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

USIRUHUSU MUNGU AWEKE UADUI KATI YAKO NA WATU WAKO.

Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAMWENDEA YESU KWA KUSAFIWA lyrics na historia

WAMWENDEA YESU KWA KUSAFIWA lyrics (Are you washed in the Blood?)


Wimbo huu uliandikwa na ndugu mmoja aliyeitwa Elisha Hoffman mwaka 1878, huko Ohio Marekani. Baada ya kuhitimu katika chuo cha biblia alisimikwa na kuwa mchungaji na kutumika kwa miaka mingi katika huduma hiyo, katika maisha yake yote ya huduma alifanikiwa kuandika nyimbo za kikristo zaidi ya 2000. Na huu “Wamwendea Yesu kwa kusafiwa,

” Ulikuwa ni mmojawapo.

 Wimbo huu umechukia maudhui yake kutoka katika sehemu nyingi za biblia ikiwemo;

Ufunuo 7:14 “Nikamwambia, Bwana wangu, wajua wewe. Akaniambia, Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo”.

Wamwendea Yesu kwa kusafiwa.

****

Wamwendea Yesu kwa kusafiwa,
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo?
Je, neema yake umemwagiwa?
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 
Kuoshwa, kwa damu,
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 
Wamwandama daima Mkombozi,
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo?
Yako kwa Msulubiwa makazi,
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 
Kuoshwa, kwa damu,
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 
Atakapokuja Bwana-arusi,
Uwe safi kwa damu ya kondoo!
Yafae kwenda mbinguni mavazi,
Yafuliwe kwa damu ya kondoo.
 
Kuoshwa, kwa damu,
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 
Yatupwe yalipo na takataka,
Na uoshwe kwa damu ya kondoo,
Huoni kijito chatiririka,
Na uoshwe kwa damu ya kondoo?
 
Kuoshwa, kwa damu,
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 

****

Je na wewe uimbapo wimbo huu, maisha yako kweli yameshwa kwa damu ya mwana-kondoo (Yesu Kristo), Je unajua kuwa hukumu haikwepeki kwako ikiwa bado upon je ya Kristo. Hivyo kama hujatubu ni heri ufanye hivyo sasa, Bwana akusafishe uwe safi.

Shalom.

Tazama historia ya tenzi nyingine chini.

Mada Nyinginezo:

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

YESU KWETU NI RAFIKI

USINIPITE MWOKOZI Lyrics

 

UNYAKUO.

EPUKA MUHURI WA SHETANI

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UPO MAKABURINI.

Kuota upo makaburini kuna maanisha nini kibiblia?

Makaburini sikuzote ni mahali wanapolazwa wafu, ikiwa unaota ndoto hii mara kwa mara upo makaburini ni ishara kuwa hali yako ya rohoni ni mfu. Upo mfano mmoja katika biblia wa mtu ambaye makao yake yalikuwa ni makaburini tu maisha yake yote haondoki pale.. Na biblia inatoa sababu kwamba ni nguvu za giza za mapepo zilikuwa zimemfunga..Na mapepo yale yalikuwa hayana lengo lingine zaidi ya kumuua..

Utasema umejuaje hilo? Tumejua hilo pale tulipoona baada ya kukemewa na Yesu, yalimpotoka na kuwaingia wale nguruwe, na moja kwa moja yale mapepo yakawakimbiza wale nguruwe kwenye maji kuwaangamiza..Hiyo yote ni kuonyesha kuwa lengo lao lilikuwa kuua tu na si kingine..Embu tusome kidogo..

Marko 5 :1-15

“1 Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi.

2 Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu;

3 makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo;

4 kwa sababu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, akaikata ile minyororo, na kuzivunja-vunja zile pingu; wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu za kumshinda.

5 Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikata-kata kwa mawe.

6 Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia;

7 akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese.

8 Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu.

9 Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tu wengi.

10 Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile.

11 Na hapo milimani palikuwa na kundi kubwa la nguruwe, wakilisha.

12 Pepo wote wakamsihi, wakisema, Tupeleke katika nguruwe, tupate kuwaingia wao.

13 Akawapa ruhusa. Wale pepo wachafu wakatoka, wakaingia katika wale nguruwe; nalo kundi lote likatelemka kwa kasi gengeni, wakaingia baharini, wapata elfu mbili; wakafa baharini.

14 Wachungaji wao wakakimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani. Watu wakatoka walione lililotokea.

15 Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mwenye pepo, ameketi, amevaa nguo, ana akili zake, naye ndiye aliyekuwa na lile jeshi; wakaogopa”.

Unaona, Vivyo hivyo ikiwa unaota upo makaburini ni ishara kuwa hali yako ya kiroho ni mbaya sana, Lakini habari njema ni kuwa YESU Yule Yule wa zamani ndio huyo huyo wa leo.

Siwezi jua maisha yako upo katika hali gani sasahivi kiroho, pengine upo katika vifungo vya dhambi, au vyovyote vile, lakini Nataka nikuambie ni Yesu pekee tu, ndiye anayeweza kukupa raha maishani mwako, haijalishi wewe ni muislamu au nani, ni Yesu peke yake ndio anayeweza kukupa tumaini la maisha mema, ya hapa duniani na mbinguni.

Yeye (Bwana Yesu) mwenyewe alisema..

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu”;

Unachopaswa kufanya ikiwa unahitaji kumkaribisha Yesu leo maishani mwako, akutengeneze upya, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako, Kumbuka sio hilo tu, yapo na mengine usiyoyajua wewe, Yesu anataka kuyarekebisha katika maisha yako, ni wewe tu kuufungua moyo wako,. Hivyo kama upo tayari leo kutubu, dhambi zako kwa kumaanisha kabisa, na kusema kuanzia leo nitamfuata Yesu, basi ni uhakika kuwa leo leo, atakuja ndani yako na kukuokoa, na utaanza kuona mabadiliko makubwa sana kwenye maisha yako ya rohoni na mwilini..

Ikiwa upo tayari sasa kufanya hivyo basi, na kuanza safari mpya ya wokovu, basi fungua hapa, kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Group la whatsapp  Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.

UNYAKUO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

YESU MPONYAJI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Bawabu ni nani/nini?

Bawabu (kwa kiingereza -Doorkeeper/Porter) ni nani katika biblia?


Bawabu maana yake ni msimamzi wa mlangoni, anayefunga na kufungua, na anayeruhusu na kutoruhusu mtu au vitu kuingia, Hawa wanakuwa hususani katika mageti ya kuingilia miji mikubwa na kwenye majumba ya kifalme na mahekalu,

2Samweli 18:26 Kisha huyo mlinzi akaona mtu mwingine anapiga mbio; mlinzi akamwita bawabu, akasema, Angalia, mtu mwingine anakuja mbio peke yake. Mfalme akasema, Huyu naye analeta habari.

Soma pia 2Wafalme 7:10,11

1Nyakati 9:23 “Basi watu hao na wana wao walikuwa na usimamizi wa malango ya nyumba ya Bwana, yaani, nyumba ya maskani, kwa zamu….

27 Nao wakalala kandokando nyumbani mwa Mungu, kwa kuwa ulinzi wake ulikuwa juu yao, nayo ilikuwa kazi yao kuyafungua malango asubuhi baada ya asubuhi.”.

Kazi hii ni kazi iliyokuwa inaonekana kama nyonge kuliko kazi zote kwenye utumishi wa Majumbani au kwenye ulinzi, hata sasa ndivyo zinavyoonekana..

Lakini Daudi alisema..

Zaburi 84:10 “Hakika siku moja katika nyua zako Ni bora kuliko siku elfu. Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, Kuliko kukaa katika hema za uovu”.

Daudi alitumia kazi yenye cheo cha chini kabisa, katika jumba kubwa akasema kama na kwa Mungu ipo hivyo, basi angependelea walau apate hata kazi hiyo ndogo tu, maadamu ni ya Mungu, kuliko kupata cheo kikubwa na kibali katika mambo ya kidunia.

Akasema tena siku moja nyuani kwa Bwana ni bora kuliko siku elfu penginepo..

Alijua faida ya kazi ya Mungu, hata kama ni ndogo kiasi gani, alijua akipoteza siku moja kuitenda kazi ya Mungu ni sawa zaidi ya siku elfu kujisumbua na shughuli nyingine za kidunia..Firikia siku elfu ni karibia na miaka 3, Hivyo miaka 3 yako wewe kwenye masumbufu yako ni siku moja kwa mtu anayedeki choo cha kanisa.

Hivyo na wewe jiulize kazi yako ni nini kwenye nyumba ya Mungu? Mchango wako wa kusambaza kazi ya Mungu ni ipi? Nguvu zako za kifedha unazimalizia wapi ndugug? Au kwako kazi ya Mungu haina faida yoyote..

Daudi anasema ni heri “Ni heri niwe bawabu nyumbani mwa Mungu..”

Shalom.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara katika email yako au Whatsapp yako basi tutumie ujumbe kwenye namba hii :+255 789001312

Mada Nyinginezo:

Bwana alimaanisha nini kusema JIKANE mwenyewe?(Mathayo 6:24)

JE NI LAZIMA MKRISTO AOE/AOLEWE?

Je Mungu anawapenda watu wote au ana chuki?

Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?

MTU ASIYE PAMOJA NAMI YU KINYUME CHANGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post