JE NI LAZIMA MKRISTO AOE/AOLEWE?

JE NI LAZIMA MKRISTO AOE/AOLEWE?

Shalom karibu tujifunze biblia.

Mojawapo wa uhuru Mungu aliompa mwanadamu ni kuoa/kuolewa…Mtu yeyote anayeoa/kuolewa sawasawa na maagizo ya Mungu (yaani ndoa ya mume mmoja na mke mmoja) basi anabarikiwa.

Mathayo 19:4 “Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?”.

Lakini Pamoja na hayo sio lazima pia kuoa au kuolewa kwa sababu maalumu.

Kwamfano biblia inasema katika..

1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. YEYE ASIYEOA hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.

34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. YEYE ASIYEOLEWA HUJISHUGHULISHA NA MAMBO YA BWANA, APATE KUWA MTAKATIFU MWILI NA ROHO. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe”.

Hivyo sababu kuu ya mtu kujizuia kuoa au kuolewa ni ili apate nafasi kubwa ya kujishughulisha na kazi ya Mungu.. Ni kweli Mume au Mke ni msaidizi mzuri pia katika kazi ya Mungu lakini…kuwa kumtumikia Mungu binafsi pia ni vizuri Zaidi.. Kwasababu ukiwa na mke/mume kuna mambo ya kidunia ambayo hautayakwepa…kwamfano vitakuwepo vipindi vya kutunza Watoto, vitakuwepo vipindi vya kutafuta sana vya kidunia ili kuitunza familia na mke au mume. Vitakuwepo vipindi vya kukaa pamoja faragha!..

Huwezi kusema unasafiri miezi 5 mbali na mke/mume wako umeenda kufanya huduma…ni lazima kwa sehemu Fulani utamkwaza tu mwenzako! au utakuwa hujamtendea haki. Na biblia inasema ukishaoa/ukishaolewa..mwili wako ni mali ya mwenzako, huna amri juu ya mwili wako(kasome 1Wakorintho 7:3-5)..Sasa hayo ndio baadhi ya mapungufu katika kuoa/kuolewa.

Lakini usipooa au usipoolewa…utakuwa huru Zaidi..unaweza kufunga safari muda wowote unaotaka kuifanya kazi ya Mungu, unaweza kufunga siku nyingi bila usumbufu, unaweza kwenda kusali mlimani kipindi kirefu au kuhubiri bila kukumbuka una jukumu Fulani umeliacha nyumbani …kadhalika, hutapata usumbufu wa Watoto wanahitaji hiki, wanahitaji kile.. kadhalika hutaishi kwa matakwa ya mtu Fulani, bali kwa kile Mungu anachokuongoza kila mara. Jambo ambalo lina faida katika ufalme wa mbinguni mara dufu kuliko hilo lingine.

Wa kwanza kabisa ambaye tunaona hakuoa na huduma yake iliikuwa na matokeo makubwa sana ni Bwana wetu Yesu. Mwingine ni Paulo ambaye ndiye aliyeandika mistari hiyo hapo juu kwa uwezo wa roho..Paulo hakuwa miongoni mwa Mitume 12 wa Bwana Yesu, lakini alifanya kazi kubwa kuliko hata mitume wa Yesu (kasome1Wakorintho 15:10), na wengine ni Yohana Mbatizaji na Eliya Mtishbi.

Lakini hilo sio lazima na wala sio amri, kwamba kila mtu ni lazima asiolewe/asioe. Ni jinsi mtu aonavyo yeye kwamba anaweza kujizuia au la!…Wapo wanaoweza kujizuia na wapo wasioweza!…Biblia inasema kama huwezi kujizuia ni afadhali uoe/uolewe kuliko kuwakwa na tamaa.

1Wakorintho 7:8 “Lakini nawaambia wale WASIOOA BADO, na wajane, Ni heri wakae kama mimi nilivyo. LAKINI IKIWA HAWAWEZI KUJIZUIA, NA WAOE; maana ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa”……

 

1Wakorintho 7:1 “Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke. 2 Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe”.

Bwana akubariki.

Kumbuka kama unaishi na mwanamke/mwanaume ambaye hamjafunga ndoa..basi mnaishi katika uzinzi!..haijalishi mmeishi miaka mingapi Pamoja, au mmezaa Watoto wangapi..Mnapaswa mkatubu na kufunga ndoa takatifu, mbele ya kanisa la Kristo, ndipo mbarikiwe (na ndoa sio sherehe na matarumbeta)..mmeshaishi miaka yote hiyo, sherehe ya nini tena?..hatua mliyopo ni ya kutubu tu, na kwenda mbele ya kanisa kufungishwa ndoa mbele ya mashahidi na kurudi nyumbani kuendelea na maisha basi haihitaji maandalizi kana kwamba ndio mmketana kwa mara ya kwanza!. Lakini msipofanya hivyo mkifa leo mtahukumiwa, hiyo ni kulingana na maandiko.

Na mwisho kama hujaolewa na unatafuta wa kukuoa..Ni vizuri ukamtafuta kwanza Mwokozi. Kwasababu ukifa leo bila mwokozi utapotea milele, na Zaidi ya yote mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa, hayo mambo yataishia humu humu duniani..miili tutakayopewa tukifika kule haina hisia za kimwili. Huko tutaishi na Kristo milele. Hivyo Wokovu ni muhimu na wa kwanza katika Maisha, hayo mengine ndio yafuate.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Bwana alimaanisha nini kusema JIKANE mwenyewe?(Mathayo 6:24)

 MAVUNO NI MENGI

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

KUOTA UNASAFIRI.

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments