Kwa faida yako na yangu alijitoa kwa ajili yetu, ili sisi tupate msamaha wa dhambi na tupate mema yote ya nchi, hivyo anakuita leo kwa mara nyingine.Una masononeko, suluhisho sio daktari wala sio mimi, una uchungu, una dhambi, una hofu, una shida, una huzuni,una mashaka, umekata tamaa ya kuishi, unahofu ya kukataliwa, Nataka nikuambie Wanadamu wala shetani bado hatujaifikia hiyo sayansi yakutibu hayo mambo magumu ya rohoni, hakuna daktari wala mganga awezaye kutibu hayo mambo na hivyo hata ukienda kwao hawatakusaidia..