Vivyo hivyo na kama tunaamini tutakwenda mbinguni siku moja, na kwamba Bwana atakuja kutunyakua kwenda naye mawinguni..Ni lazima kuanzia sasa tukifanyie kazi kile tunachokiamini, pasipo kulazimishwa wala kusukumwa, ni lazima ndani ya moyo wetu tujikute tunatendea kazi ile Imani iliyo ndani yetu. Hivyo tunapaswa tujiweke mbali na dhambi, lazima tujiweke mbali na uasherati, uchawi, rushwa, utukanaji, uvaaji mbaya, ulevi, uvutaji sigara,anasa, usengenyaji, usagaji, utoaji mimba,ulawiti,ushoga, utazamaji pornography na ufanyaji masturbation, uuaji, chuki,wivu, majigambo, ibada za sanamu na matendo yote ya giza.