JIANGALIENI BASI JINSI MSIKIAVYO;

JIANGALIENI BASI JINSI MSIKIAVYO;

Mwalimu mmoja aliwapa wanafunzi wake fumbo hili, akawaambia watu wawili walikuwa wanatembea barabara wakielekea katika shughuli zao, na mvua ilipoanza kunyesha kwa Nguvu mtu mmoja hakunyeshewa na mvua ile..je! mnaweza kunielezea maana ya sentensi hii? ..

Mwanafunzi mmoja mwerevu akajibu Ndio ninaweza kwani ni wazi kuwa mmojawapo alikuwa na mwamvuli na mwingine hakuwa nao.

Mwingine akasimama kwa furaha na kusema hapana mmoja alipita pembezoni mwa majengo na mwingine barabarani, hivyo Yule wa barabarani ni lazima alilowesha na mvua.

Mwingine akasema, inawezekana mmoja alivaa koti la mvua, na mwingine hakuwa nalo hivyo Yule mwenzake ni wazi kuwa alilowanishwa na mvua.

Kila mwanafunzi alisema la kwake, na ndipo mwalimu akasema ninyi wote mmepeleka mawazo yenu, “ kwa wale watu wawili tu kana kwamba ndio hao peke yao waliokuwa kwenye hiyo sentensi”..Lakini sentensi inasema “mtu mmoja hakunyeshewa”..Hivyo inawezekana wote wawili walinyeshewa na mvua lakini kulikuwa na mwingine aliyekuwa anapita katika njia hiyo, au yupo kwenye gari lake hakunyeshewa.

Wanafunzi wote wakaingiwa na aibu kwa kulijibu juu juu tu bila ya kufikiria kwa undani.

Ndio maana Bwana Yesu alisisitiza akituambia “Luka 8: 18 “JIANGALIENI BASI JINSI MSIKIAVYO; kwa kuwa mwenye kitu atapewa, na yule asiye na kitu atanyang’anywa hata kile ambacho anadhaniwa kuwa nacho.”

Kwani kama tukiwaangalia hao wanafunzi inawezekana kabisa ni kweli majibu yao yalikuwa ni sahihi, lakini kwa mwalimu wao hayakuwa sahihi.

Unaona kauli hiyo ya Bwana anayosema, ‘hata kile ambacho mtu anadhaniwa kuwa anacho, atanyanganywa’, pale mtu anapojihisi anajua kila andiko, hivyo hakuna haja ya kuhubiriwa na huku anaona kabisa maisha yake hayaakisi kwa namna yoyote maisha ya Kristo. Mtu kama huyo atanyang’anywa hata kile anachodhani anakijua.

Tunaona Maneno hayo Bwana Yesu aliyatamka baada ya kutoa ule mfano wa mpanzi, akisema kuwa wale wote ambao mbegu zao ziliangukia katika miiba,na wengine barabarani, na wengine,na kwenye miamba na wengine kwenye udongo mzuri, wote hao WALISIKIA NENO LA MUNGU kwa wakati mmoja, Ni neno lile lile walilisikia la habari ya Yesu mwokozi, wala hakuna aliyehubiriwa zaidi ya mwingine, lakini viwango vya kusikia vilitofautiana kati ya mmoja na mwingine na ndio maana utaona wengine waliishia njiani, wengine, kwenye miamba, na wengine kwenye udongo mzuri..

Lakini tujiulize Yule aliyeishia kwenye udongo mzuri yeye alisikiaje sikiaje tofauti na wengine mpaka kufikia kuzaa hata 60 mpaka 100, sikio lake lilikuwa ni la namna gani?

Embu tusoma kidogo huo kisha tutapata majibu.

Luka 8:10 “Akasema, Ninyi mmepewa kuzijua siri za ufalme wa Mungu; bali wengine kwa mifano, ili

wakiona wasione, na wakisikia wasielewe.

11 Na huo mfano, maana yake ni hii; Mbegu ni neno la Mungu.

12 Wale wa karibu na njia NDIO WASIKIAO, kisha huja

Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao,wasije wakaamini na kuokoka.

13 Na wale penye mwamba ndio wale ambao WASIKIAPO hulipokea lile neno kwa furaha; nao hawana mizizi, huamini kitambo kidogo, na wakati wa kujaribiwa hujitenga.

14 Na zilizoanguka penye miiba ni WALE WALIOSIKIA, na katika kuenenda kwao husongwa nashughuli na mali, na anasa za maisha haya, wasiivishe lolote.

15 Na zile penye udongo mzuri, ndio wale ambao KWA UNYOFU NA WEMA WA MIOYO YAO HULISIKIA neno, na kulishika; kisha huzaa matunda kwa kuvumilia.

16 Hakuna mtu ambaye akiisha washa taa huifunika kwa chombo, au kuiweka mvunguni, bali huiweka juu ya kiango, ili waingiao wapate kuona nuru yake.

17 Kwa maana hakuna neno lililositirika ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa ambalo halitajulikana na kutokea wazi.

18 JIANGALIENI BASI JINSI MSIKIAVYO; kwa kuwa mwenye kitu atapewa, na yule asiye na kituatanyang’anywa hata kile ambacho anadhaniwa kuwa nacho.”

Unaona hapo, wale waliofanikiwa kufika kwenye udongo mzuri, Bwana Yesu anasema KWA UNYOFU, na KWA WEMA hulililisikia na KULISHIKA, kwa KUVUMILIA.

Ni kwanini kama tukitazama leo hii mtu anahubiriwa injili kila siku, lakini inaonekana haina manufaa, miaka inapita haonyeshi badiliko lolote, si kwamba Neno alilohubiriwa linatofauti na la Yule aliyempokea Kristo na kusimama katika Imani, hakuna tofauti yoyote, isipokuwa huyu wa pili Aliangalia jinsi asikiavyo, alizingatia kwa unyofu wa moyo, na kwa wema wote kutokulidondosha hilo aliloambiwa, alilishika na kwenda kulitafakari, na hivyo kwa kufanya vile Mungu akamfunulia akili zake za rohoni kujua maana zaidi ya kile alichokisikia..na ndicho hicho kilichompa nguvu ya kuchukua uamuzi wa kumwishia Bwana mpaka sasa.

Na kwa kuwa hakutaka kulichukulia suala hilo juu juu tu, bali kwa hofu akijua kuwa siku moja atasimama hukumuni na kutoa hesabu ya yote aliyoyasikia, alijishusha na kutii, hivyo Mungu akampa neema zaidi ya kumwelewa yeye kama alivyotaka amwelewe, na kwa jinsi alivyozidi kuendelea kulipalilia lile Neno ndani yake, ndivyo kidogo kidogo Mungu akamjalia kuzaa matunda mengi baadaye. Anaongezewa na vya ziada kwasababu alizingatia kuangalia jinsi anavyosikia.

Inawezekana Injili ya Kristo haijawa na manufaa yoyote kwako kwa miaka mingi, ni kwasababu hauyachukulii maneno ya Mungu katika unyofu wote, unayaona kama ni siasa, na maneno ya kawaida tu, umekuwa ukiyachukulia juu juu tu, na hivyo Mungu amekuacha uendelee kuyasikia lakini usiyaelewa, uyaone tu lakini usiyatambue. Lakini leo hii Mungu amekupa neema ya kuliambua hilo ufanye tena upya maisha yako.

Itakufaidia nini uupate ulimwengu mzima kisha upate hasara ya nafsi yako?, Embu chagua jambo la msingi kwanza kumtii Mungu uokolewe na hayo mengi yaje huko mbeleni kama yatakuwa na muhimu, okoa roho yako kwanza, Sikia Neno la Mungu leo na ulipokee kwa weupe wa moyo kwa mara nyingine tena, ili Bwana akapate kukufunua akili yako uanze kuona uzuri wa wokovu, ili baadaye ukamzalie matunda.

Ikiwa utakuwa tayari kutubu, basi fanya hivyo kwa kudhamiria kabisa kutoka moyoni mwako, kwamba kuanzia leo utazingatia kutii kile Mungu anachosema na wewe, kuacha maisha ya dhambi na baada ya kutubu kwako unapaswa ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na uwe kwa jina la YESU KRISTO ili upate ondoleo la dhambi zako(Matendo 2:38),, kumbuka ubatizo wa vichanga sio wa kimaandiko, kadhalika ubatizo wa kwa jina la Baba na Mwana, na Roho Mtakatifu sio sahihi kwani umetafsiriwa isivyopaswa kwasababu walioubatizia huo hawakuzingatia JINSI WASIKIAVYO…Ubatizo wa kwa jina la YESU KRISTO ndio wa kimaandiko, na ndio uliotumiwa na mitume wote katika kubatizia kwenye biblia. Soma (Matendo 2:38, 8:16, 10:48, 19:5) utayathibitisha hayo mwenyewe.

Hivyo ukiyakamilisha hayo, basi Bwana mwenyewe kuanzia huo wakati atakupa kipawa cha Roho wake mtakatifu atakayekuongoza katika kweli yote. Na hapo utakuwa umeshazaliwa mara ya pili. Ni Wengi wanaosema wameokolewa lakini hawazingatii vigezo vya wokovu vilivyotolewa na Bwana Yesu. Ubatizo sahihi ni muhimu kwa mtu yoyote anayedai amemwamini Kristo. Hivyo fanya hima ukabatizwe tena, kama ulibatizwa ukiwa mtoto au kama hukuwahi kubatizwa kabisa.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine. Na Mungu atakubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

JE! UNA MASIKIO YANAYOSIKIA?

ANGALIA JINSI USIKIAVYO

UMESIKIA SAUTI AU NGURUMO?

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE


Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
yohana
yohana
3 years ago

bwana YESU asifiwe