Tofauti kati ya makuhani na walawi ni ipi?

Tofauti kati ya makuhani na walawi ni ipi?

SWALI: Na je! Walawi na makuhani katika kanisa la sasa ni watu wa namna gani?

JIBU: Mungu alilichagua kabila moja kati ya kumi na mbili liwe kabila lake takatifu litakalosimama katika kazi na shughuli zote za kidini na ibada Israeli.

Sasa katikati ya hawa walawi ndipo walipotolewa makuhani ndani yake. Hivyo makuhani wote walikuwa ni walawi lakini walawi wote si makuhani.

Hizi ndizo kazi za walawi.

  1. Walawi wanasimama kama wasaidizi wa makuhani katika shughuli zote za kiibada mbele za Mungu. Hesabu 1:50
  2. Walisimama pia kama waandishi wa torati,  kufundisha na kutafsiri maandiko kum 33:10,
  3. Walisimama kama walinzi wa mazingira yote ya hema/ hekalu hesabu 3:21-26
  4. Walisimama kama wajenzi wa hema, na kulihamisha na kulijenga tena pale walipobadili makazi, Hesabu 1:48-54
  5. Walisimama pia kama waaamuzi, walitoa hukumu ya mambo ya sheria. kumb 17:8-13
  6. Vilevile walisimama kama waimbaji mbele ya hekalu la Mungu daima, 1Nyakati 9:33

Na hizi ndizo kazi za makuhani.

  1. Walifanya kazi za upatanisho wa dhambi na makosa ya watu, kwa sadaka za kuteketezwa na damu ipelekwayo ndani ya hema mbele ya madhabahu.(Waebrania 10:11-18)
  2. Waliwajibika kuwabariki watu. Kumb 10:8
  3. Pia walifanya kazi ya kulibeba sanduku la agano, popote pale walipokwenda. kumb 31:9

Kwasasa, kila mkristo, ni Mlawi. Kwasababu tayari ameshapewa uwezo ndani yake na karama, ya kuifanya kazi ya Mungu pale tu anapookoka. Kila mmoja ni kiungo kwa mwenzake ndani ya kanisa. Lakini mkristo anabadilika kutoka kuwa mlawi mpaka kuwa kuhani pale anaposimama hasaa kwa ajili ya huduma/kazi  ya Mungu kwa watu wake.

Anapobeba maono Fulani, labda  tuseme kulichunga kanisa, huyo ni kuhani wa Mungu, na hivyo anaposimama na kuwabariki watu basi Baraka hizo huwafikia watu moja kwa moja kutoka kwa Mungu, mfano tu wa makuhani wa agano la kale. Au anapotumika katika kuwafundisha, kuwaombea wengine, kuwasimamia wengine, haijalishi ngazi aliyopo, au mahali au jinsia, huyo rohoni ni kuhani wa Mungu.

Hivyo kila mkristo anaouwezo wa kuwa kuhani wa Mungu, kwasababu lengo la Mungu ni sote tuwe makuhani wake, sio tu walawi, Na Yesu Kristo Bwana wetu akiwa ni kuhani Mkuu.

1Petro 2:9  Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;

Bwana akubariki.

Je! Kristo yupo moyoni mwako?

Kama ni hapana, basi wakati ndio huu, mgeukie, akusamehe dhambi zako, kwa kutubu na kumaanisha kabisa kuziacha, naye atakukomboa. Ikiwa upo tayari kwa ajili ya mwongozo huo, basi waweza fungua hapa kwa mwongozo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Kwa namna gani tumefanyika Makuhani na Ufalme?.(Ufunuo 1:6)

WALAWI WALIKUWA WENYE MIOYO YA ADILI KWA KUJITAKASA KULIKO MAKUHANI.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Kwanini Yesu aliwaambia wale wakoma wakajionyeshe kwa makuhani?

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments