Mata ni nini (Mwanzo 27:3).

Mata ni nini (Mwanzo 27:3).

Mata ni kitu gani na imebeba  ujumbe gani kiroho?


Jibu: Turejee,

Mwanzo 27:2 “Akasema, Tazama, sasa mimi nimekuwa mzee, wala sijui siku ya kufa kwangu.

3 Basi, nakuomba, chukua MATA yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo;  4 ukanifanyie chakula kitamu namna ile niipendayo, ukaniletee, ili nile; na roho yangu ikubariki, kabla sijafa”.

“Mata” Ni jina jingine la “Silaha”. Kwahiyo badala ya kutumia neno “silaha” ni sahihi pia kutumia neno “Mata”.

Kwahiyo mstari huo wa tatu (3) ni sahihi kuuweka hivi,… “chukua SILAHA yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo ”

Na silaha hiyo inaweza kuwa mkuki, mshale au upanga, lakini katika andiko hilo silaha (Mata), iliyomaanishwa pale ni “Mshale”. Na kwanini ni mshale na si upanga wala mkuki?.. ni kwasababu kuna Podo imetajwa pale na upinde..

Maana yake huwezi kubeba upanga na upinde bila mshale, hivyo ni wazi kuwa Mata iliyomaanishwa pale ni mshale, kwasababu kuna upinde na Podo.

Sasa kwa maarifa kuhusu “Podo” na ufunuo wake kiroho waweza fungua hapa >>> Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?

Sasa hizi zote ni silaha za mwili, lakini biblia inatufundisha kuwa zipo silaha za roho ambazo kila mkristo ni lazima azivae, na silaha hizo tunazisoma katika kitabu cha Waefeso 6:10-18, ambazo ni Chapeo ya Wokovu, Dirii ya Haki, Ngao ya Imani, Kweli, Upanga wa Roho, na Utayari miguuni pamoja na sala na maombi.

Na kwa silaha hizo pekee ndio tutaweza kumshinda adui yetu shetani, kwa mapana kuhusiana na silaha hizi jinsi ya kuvizaa na namna zinavyotenda kazi fungua hapa >>>MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UTHABITI WA AGANO LA MUNGU KWA MKRISTO.

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

KWANINI UPIGE MISHALE CHINI?

NDUGU,TUOMBEENI.

Nini maana ya  Mithali 21:1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana;

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments