SI KILA KILICHO HALALI KINAFAA.

SI KILA KILICHO HALALI KINAFAA.

(Jihadhari na Marashi)

Si mambo yote yanayokubalika katika jamii basi yanafaa kwa mkristo.. Si mambo yote yanayokubaliwa na wengi basi yanafaa..ni muhimu kuchuja kila tunaloambiwa au tunayokutana nalo, kabla ya kulikubali, ndivyo biblia inavyotufundisha.

1Wakorintho 10:23  “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”.

Mojawapo ya jambo ambalo ni muhimu kuchukua nalo tahadhari ni “Matumizi makali ya marashi”. Unapojipulizia marashi ambayo mtu aliye mita 10 mbali nawe anayasikia, basi fahamu kuwa upo katika hatari kubwa sana.

Utauliza kivipi au kwa namna gani? Hebu turejee katika maandiko kidogo..

Utakumbuka ile habari ya yule mwanamke aliyemmiminia Bwana marhamu ya thamani nyingi mwilini mwake, na maneno Bwana Yesu aliyoyasema kuhusu kazi ya ile marhamu aliyomiminiwa?. Biblia inasema marhamu ile ilikuwa ni ya thamani kubwa, maana yake yenye kunukia sana na kwa eneo kubwa, kiasi kwamba mtu aliye mbali anaweza kuisikia harufu ya marhamu ile.

Tusome

Marko 14:3 “Naye alipokuwapo Bethania, nyumbani mwa Simoni mkoma, ameketi chakulani, alikuja mwanamke mwenye KIBWETA CHA MARHAMU YA NARDO SAFI YA THAMANI NYINGI; akakivunja kibweta akaimimina kichwani pake.

4  Palikuwa na watu waliochukizwa katika nafsi zao wakisema, Kwani kupoteza marhamu namna hii?

5  Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa dinari mia tatu na kuzidi, wakapewa maskini. Wakamnung’unikia sana yule mwanamke.

6  Yesu akasema, Mwacheni; mbona mnamtaabisha? Amenitendea kazi njema;

7  maana sikuzote mnao maskini pamoja nanyi, na kila mpendapo mwaweza kuwatendea mema; lakini mimi hamnami sikuzote.

8  Ametenda alivyoweza; ametangulia kuupaka mwili wangu MARHAMU KWA AJILI YA MAZIKO”.

Umeona hapo?.. wakati huyu mwanamke anadhani Marhamu ile ingeweza kumfanya Bwana anukie vizuri mbele za watu na aonekane mtanashati.. lakini Bwana aliyaona yale manukato tofauti na mwanamke alivyoyaona, Bwana Yesu aliona hayafai kwa utanashati, bali kwa MAZIKO!.

Lakini kwasababu mwanamke alikuwa na nia njema ya kutubu na kumthaminisha Bwana ndio maana akapata kibali kwa muda ule, lakini Ujumbe tayari tumeachiwa, “kuwa marhamu kama hizo ni kwaajili ya maziko” so kwaajili ya utanashati.

Hiyo ikimaanisha kuwa kumbe kuna vitu tunaweza kuvipaka mwilini, au kuvivaa, na kumbe ni malighafi za MAUTI, Na KIFO!!. Ijapokuwa kwa nje tunaweza kuonekana watanashati na tunaovutia, lakini kumbe tumejipaka au tumekivaa kifo!.

Bwana Yesu angeweza kuwaambia wale watu kuwa marhamu ile amepakwa kwa kuwekwa tayari kukutana na mkutano ili kwamba wasikie harufu nzuri itokayo mwilini mwake, kwani bado alikuwa na siku kadhaa za kuhubiri mbele za watu kabla ya kufa, lakini wala yeye hakuziona hizo siku bali aliona marhamu ile inafaa kwa matumizi ya MAZIKO! Na si utanashati kama wengine wote walivyotazamia.

Mama/dada jiulize hayo marashi unayojipulizia mwilini mwako je unajiweka tayari kwa nini?..je kwaajili ya maziko yako??..

Na asilimia kubwa ya watu wanaotumia marashi makali ni lazima wanakuwa wanasumbuliwa na roho za mauti au uasherati… hivyo ni muhimu kuchukua tahadhari ya kiroho! Na si kila kitu kuiga kwasababu tu, tumeona ni kitu chenye kukubalika kila mahali.

Mama/dada Kama unatamani kujipamba basi jipambe kwa mapambo ya kibiblia, ambayo ndiyo yale yanayotajwa katika 1Timotheo 2:9 na 1Petro 3:3.

1Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; YAANI, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU.

5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.

6  Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada zinazoendana:

Mafundisho mengine:

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

Mawaa ni nini? Kama tunavyosoma katika biblia?

EPUKA KUCHELEWA IBADA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments