SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

(Masomo maalumu kwa Wakristo, Je! Unajijua nafasi yako?.. je unajijua kuwa wewe ni manukato yanayokubalika na pia yasiyokubalika kwa upande mwingine?).

Manukato ni neno lingine la “Marashi”.. Na kazi ya manukato/Marashi ni kukifanya kitu kivutie, hakuna mtu anayejipaka marashi ili mtu amkimbie. Lakini changamoto ni kwamba haijalishi marashi yatakuwa ni mazuri kiasi gani, ni lazima kwa upande mwingine kuna mtu yatamtia kichefuchefu tu. (Si kila marashi yaliyo mazuri kwa mtu, yatakuwa mazuri kwa watu wote).. ni lazima upande mmoja utayakosoa tu.

Na siku zote, marashi yaliyokosolewa huwa yanatia kichefuchefu na hata wakati mwingine kumuumiza Yule anayeyasikia..

Kadhalika biblia inasema kuwa sisi ni Manukato ya Kristo. Na kama ni manukato ni lazima upande mmoja yatakubalika na upande mwingine yatakatalika.. Na siri ya manukato ya Kristo ni kwamba wengi wanayachukia zaidi ya wale wanayoyapenda..

2Wakorintho 2:14 “Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu.

15  KWA MAANA SISI TU MANUKATO YA KRISTO, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea;

16  katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima. Naye ni nani atoshaye kwa mambo hayo?

17  Kwa maana sisi si kama walio wengi, walighoshio neno la Mungu; bali kama kwa weupe wa moyo, kama kutoka kwa Mungu, mbele za Mungu, twanena katika Kristo”.

Wakristo wengi wanadhani kuwa wanapookoka bali wataanza kupendwa, na kukubalika na kupokea kibali kila mahali. Ni kweli hayo yanaweza kutokea kwasababu kwa Mungu yote yanawezekana.. Lakini fahamu kuwa wewe ni marashi mazuri lakini yenye kuleta harufu mbaya kwa wanaopotea..

Maisha ya usafi na ukamilifu unayoishi ni harufu nzuri kwa wanaookolewa, (Maana yake ni mfano mzuri wa kuigwa, kwa waongofu wapya na waaliookoka), kuomba kwako na kufunga kwako na kuhubiri kwako ni harufu nzuri kwa waliookoka kama wewe.

Lakini kwa wale ambao hawamtaki Yesu, fahamu kuwa maisha yako ni kichefuchefu kwao….ni lazima watakupinga tu, ni lazima watakuletea vita tu, ni lazima watakukosa tu, ni lazima watakurushia mishale tu..Kwasababu kwao wewe ni manukato yenye harufu mbaya, tena harufu inayoleta mauti kabisa…yaani maisha yako yanawahukumu..

Hili ni jambo la kufahamu wewe uliyempokea Kristo na kuokoka!.. Kamwe usifikiri kuwa utaendelea furaha yako ndani ya Kristo ni jambo linalovutia machoni pa wengine… Ukristo ni vita, unapoamua kuwa mkristo ni kama mtu aliyevaa kombati na kuingia vitani.. Kwahiyo tegemea kukumbana na maadui wa imani, watakaokukosoa na kukutatisha tamaa..

Yohana 15:18  “Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.

19  Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.

20  Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

Je tunaruhusiwa kujipaka mafuta au kujipulizia marashi?

USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Burton Evaristo
Burton Evaristo
1 year ago

Amen

NEEMA ALICE
NEEMA ALICE
1 year ago

Amen 🙏 Mungu akubariki sana mtumishi wa Mungu Kwa hili neno nimebarikiwa sana,basi acha nami niishi kuwa manukato Kwa Mungu