Shubaka ni nini kibiblia? (Mithali 7:6)

Shubaka ni nini kibiblia? (Mithali 7:6)

Shubaka ni dirisha, lililojengwa kwa kupishanisha vipande vya mbao au chuma au kitu kingine chochote, kama pazia, katikati ya dirisha hilo. Tazama picha.

Nikaona katikati ya wajinga, Nikamtambua miongoni mwa vijana, Kijana mmoja asiyekuwa na akili,

Ujenzi wa madirisha mengi ya kisasa, Haupo kwa muundo huo. Madirisha ya kisasa, yapo wazi sana, nikiwa na maana huwezi kuona kitu chochote kimekatiza katikati,pengine utakuta ni kioo tupu eneo lote, lakini kwa zamani madirisha ya shubaka yalikuwa ni kawaida kuyakuta karibu katika nyumba zote.

Neno hilo kwenye biblia utalipata katika habari hii;

Mithali 7:4 “Mwambie hekima, Wewe ndiwe umbu langu; Mwite ufahamu jamaa yako mwanamke.

5 Wapate kukulinda na malaya, Na mgeni akubembelezaye kwa maneno yake.

6 Maana katika dirisha la nyumba yangu Nalichungulia katika SHUBAKA YAKE;

7 Nikaona katikati ya wajinga, Nikamtambua miongoni mwa vijana, Kijana mmoja asiyekuwa na akili,

8 Akipita njiani karibu na pembe yake, Akiishika njia iendayo nyumbani kwake, 9 Wakati wa magharibi, wakati wa jioni, Usiku wa manane, gizani.

10 Na tazama, mwanamke akamkuta, Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;

11 Ana kelele, na ukaidi; Miguu yake haikai nyumbani mwake.

12 Mara yu katika njia kuu, mara viwanjani, Naye huotea kwenye pembe za kila njia.

13 Basi akamshika, akambusu, Akamwambia kwa uso usio na haya,

14 Kwangu ziko sadaka za amani; Leo hivi nimeziondoa nadhiri zangu;

15 Ndiyo maana nikatoka nikulaki, Nikutafute uso wako kwa bidii, nami nimekuona.

16 Nimetandika kitanda changu, magodoro mazuri, Kwa matandiko ya Kimisri yenye mistari.

17 Nimetia kitanda changu manukato, Manemane na udi na mdalasini.

18 Haya, na tushibe upendo hata asubuhi, Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba. 19 Maana mume wangu hayumo nyumbani, Amekwenda safari ya mbali;

20 Amechukua mfuko wa fedha mkononi; Atarudi wakati wa mwezi mpevu.

21 Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi, Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.

22 Huyo akafuatana naye mara hiyo, Kama vile ng’ombe aendavyo machinjoni; Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu;

23 Hata mshale umchome maini; Kama ndege aendaye haraka mtegoni; Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.

24 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Mkayaangalie maneno ya kinywa changu.

25 Moyo wako usizielekee njia zake, Wala usipotee katika mapito yake.

26 Maana amewaangusha wengi waliojeruhi, Naam, jumla ya waliouawa naye ni jeshi kubwa.

 27 Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti”.

22 Huyo akafuatana naye mara hiyo, Kama vile ng'ombe aendavyo machinjoni; Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu;

Hiyo ni kutukumbusha kuwa, Mungu pia, anatutazama kutoka juu mbinguni akiyaangalia matendo yetu, na mienendo yetu katika madirisha na shubaka zake mbinguni, yeye ndiye anayechunguza na kujua siri zote za mioyo ya watu, na mwisho wake utakuwaje. Hivyo ni wajibu wetu tusiwe wajinga kama yule kijana, bali tuikwepe mitego ya ibilisi kwa kuzishika amri za Mungu na kuziishi.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments