Nini maana ya kuruzuku katika biblia?

Nini maana ya kuruzuku katika biblia?

Maana ya Neno “kuruzuku” ni “kutoa Riziki”. Unapompa mtu mwingine riziki hapo umemruzuku. Katika biblia tunaona neno hilo limetokea mara kadhaa Mungu akiwaruzuku watu.

Katika kitabu cha Nehemia tunaona Neno hilo likitajwa..

Nehemia 9: 21 “Naam, muda wa miaka arobaini uliwaruzuku jangwani, wasihitaji kitu; nguo zao hazikuchakaa, wala miguu yao haikuvimba”.

Na pia tunaliona neno hilo katika kitabu cha Zaburi.

Zaburi 65:9 “Umeijilia nchi na kuisitawisha, Umeitajirisha sana; Mto wa Mungu umejaa maji; Wawaruzuku watu nafaka Maana ndiwe uitengenezaye ardhi”.

Na mwisho tunaona neno hilo katika kitabu hicho hicho cha Zabur 68,

Zaburi 68:10 “Kabila yako ilifanya kao lake huko; Ee Mungu, kwa wema wako uliwaruzuku walioonewa”.

Kama Bwana alivyowaruzuku wana wa Israeli Jangwani, mahali ambapo hapakuwa na kilimo wala maji, lakini Mungu wa mbingu na nchi akawapa MANA kutoka mbinguni na maji kutoka mwambani, na nyama kimiujiza, akakupe na wewe mtu wa Mungu uliyempokea na kumwamini Yesu Kristo, riziki zote za mwilini na rohoni. Akakuruzuku kwa riziki nyingi katika jina la Yesu.

Amen

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

NAWAAMBIA MAPEMA!

NAWE UTAGEUZWA KUWA MTU MWINGINE.

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments