Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

Jibu: Tusome..

Warumi 5:20 “Lakini sheria iliingia ili kosa lile liwe kubwa sana; NA DHAMBI ILIPOZIDI, NEEMA ILIKUWA NYINGI ZAIDI”.

Ili tuweze kuelewa vizuri labda tujifunze katika mfano mmoja au miwili ya kimaisha.

Umewahi kujiuliza ni kwanini gharama za usafiri wa Umma zipo chini, kuliko zile za usafiri binafsi?. Leo hii ukisafiri kutoka mkoa mmoja hadi mwingine, kwa kutumia basi la umma, utaona gharama zipo chini, kuliko ukitumia usafiri wako binafsi.

Sasa ni kwasababu gani iko hivyo?..Ni kwasababu mnapokuwa wengi mnachangia zile gharama, na hivyo kusababisha nauli kuwa ndogo kwa kila mmoja, lakini ukiwa peke yako itakubidi ubebe wewe gharama zote za usafiri, Maana yake badala ya kutoka Dar es salaam mpaka Dodoma kwa Tsh. Elfu 20, utajikuta unatumia laki 2 kwa safara hiyo hiyo, endapo utatumia usafiri binafsi.

Kwahiyo kwa ufupi tunaweza kusema “wenye uhitaji wa kusafiri wanapokuwa wengi, basi kunakuwa na neema ya punguzo la bei)”.

Au umewahi kujiuliza ni kwanini baadhi ya dawa au chanjo za magonjwa sugu ambayo yanaathiri watu wengi kwa wakati mmoja, kama Kifua kikuu, Ukimwi, au CORONA yanatolewa bure bila malipo?..si kwasababu madawa hayo ni ya gharama za chini, la! Ni ya gharama kubwa sana, lakini kwasababu yana waathiri watu wengi kwa wakati mmoja, nchi inafanya juhudi dawa hizo zipatikane bila malipo, ili hasara isiwe kubwa kwa taifa!..

Hivyo itaingia gharama ya kuyanunua madawa hayo kwa bei ya juu, na kuyagawa bure kwa wananchi!.

lakini laiti kama magonjwa hayo yangekuwa yanawaathiri watu wachache tu!, basi yangepatikana kwa gharama zile zile za juu tu!

Vivyo hivyo katika Imani, dhambi ya mtu mmoja pekee isingetosha kumleta Kristo ulimwenguni.. Kwasababu gharama ya kumwokoa mwanadamu ni kubwa sana si ndogo!. (Mungu kumtoa mwana wake wa pekee si gharama ndogo!). 1Wakorintho 7:23 “Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu”. Soma pia 1Petro 1:18.

Hivyo ilibidi wakosaji tuwe wengi, ili Neema nayo iwe nyingi!!…iweze kupatikana bure!! Hiyo ndiyo sababu kwanini Kristo hakuja ulimwenguni siku ile ile Adamu alipoasi.. Bali alikuja miaka mingi baadaye..

Warumi 5:16 “…….kwa maana hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja ikaleta adhabu; BALI KARAMA YA NEEMA ILIKUJA KWA AJILI YA MAKOSA MENGI, IKALETA KUHESABIWA HAKI”.

Hiyo ndio sababu pia kwanini kanuni ya kuupokea wokovu imerahisishwa namna hii!.. Ni kitendo tu cha KUMWAMINI Bwana YESU, na KUTUBU!, kwa kudhamiria kuacha dhambi, na KUBATIZWA katika ubatizo sahihi, na KUPOKEA ROHO MTAKATIFU. Basi!.. Ukiifuata hiyo kanuni, utakuwa umeupokea Wokovu kamili, na umeipokea Neema ya Mungu katika Maisha yako.

Itii injili leo, inapokuonya juu ya uvaaji wako mbaya, juu ya vimini unavyovaa na wigi unazovaa, juu ya wanja unaoupaka, juu ya lipstick unazotumia, juu ya suruali unazozivaa, juu ya mitindo yote ya kidunia uliyo nayo.. juu ya ulevi wako, na anasa na utukanaji ulionao!. Tubu leo na kuitii injili, kabla ya ule mwisho kufika..

Ukiyadharau maneno ya Mungu ya Uzima yanayokuonya leo, utafika wakati utatamani wokovu utaukosa.. na wakati huo, upo karibu kufika, wakati mlango wa neema utakuwa umefungwa!.. kitakachokuwa kimesalia ni hukumu ya ziwa la Moto!.

Waebrania 10:28 “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29 MWAONAJE? HAIKUMPASA ADHABU ILIYO KUBWA ZAIDI MTU YULE ALIYEMKANYAGA MWANA WA MUNGU, NA KUIHESABU DAMU YA AGANO ALIYOTAKASWA KWAYO KUWA NI KITU OVYO, NA KUMFANYIA JEURI ROHO WA NEEMA?.

Kama hujampokea Yesu na kubatizwa na ungehitaji kumpokea leo na kubatizwa, basi tumia namba hizo hapo chini, kuwasiliana nasi ili tukusaidie juu ya hilo, pale mahali ulipo. Au tafuta kwa bidi mahali popote ambapo utaweza kupata msaada huo mapema sana kabla mambo hayajaharibika Zaidi.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group


Mada Nyinginezo:

GHARAMA YA UFALME WA MBINGUNI.

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

KAMA SI YESU, HABARI YETU INGEKUWA IMEISHA ZAMANI SANA.

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

TUNALINDWA NA NGUVU ZA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
6 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Isaya Nyondo
Isaya Nyondo
1 year ago

Bwana awabariki na kuwaongeza.

William lasway
William lasway
2 years ago

Ameni

William lasway
William lasway
2 years ago

Barikiwa mtumishi

Cleven Nassary
Cleven Nassary
2 years ago

Amen ubarikiwe kwa somo zuri