Nini maana ya ‘Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu’ ?

Nini maana ya ‘Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu’ ?

SWALI: Naomba kufahamu maana ya mstari huu ; Mithali 16:1 “Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana”.


JIBU: Mstari huu unatukumbusha kuwa si kila jambo tunalolipanga katika maisha tunaweza kulitolea maamuzi  yake asilimia mia. Ni kweli Mungu anaturuhusu tupange mipango yetu mingi kwa jinsi  tupendavyo, lakini tunapaswa tukumbuke  pia sio kila mpango tulioupanga ni lazima uje kama tulivyotarajia.

Kwamfano utaona Balaamu alipomwendea Mungu ili kuwalaani Israeli, jibu la Mungu lilikuwa ni kuwabariki badala ya kuwalaani. (Hesabu 22-24).  Utaona alikwenda kweli na mipango yake kwa Mungu ili kumridhisha Balaki, akidhani utakuwa ni vema pia kwa Mungu, lakini badala yake aliambiwa aibariki Israeli badala ya kuilaani.

“Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana”

 Hivyo tunapopanga mipango yetu, tunapaswa tujinyenyekeze kwa kusema Bwana akipenda kama biblia inavyotuasa hapa,

Yakobo 4:13 “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida;

14 walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka.

15 Badala ya kusema, Bwana akipenda, tutakuwa hai na kufanya hivi au hivi.

16 Lakini sasa mwajisifu katika majivuno yenu; kujisifu kote kwa namna hii ni kubaya”.

Unaweza kweli ukawa umepanga uje kuwa daktari ukubwani, lakini mipango yako au ndoto zako  ghafla zimevuruguka kuona kwamba unalazimika kwenda kusomea kitu ambacho hujakipenda, sasa unapokuwa katika hali kama hiyo na wewe ni mkristo kumbuka huu mstari.. “Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana”

Unaweza ukawa umepanga, ufanikishe jambo fulani, mwaka uliopita lakini haujafanikisha kutoka na vikwazo fulani, pengine ukaanza kulaumu kwanini haikuwezekana, sasa ukijikuta katika hali kama hiyo na wewe ni mkristo ambaye unaouhakika umeokolewa na Kristo, hupaswi kuwa na huzuni, ujue ipo mipango mingine mzuri zaidi ambayo Mungu kaiweka mbele yako, pengine unaweza usiione sasa hivi, lakini baadaye ukaiona na kumshukuru Mungu, na kusema asante Mungu kwa kunipitisha njia hii leo.

Hivyo kila jambo ulifanyalo, usilipe asilimia mia kwamba ni lazima liwe kama ulivyolipanga, kumbuka wewe sio Mungu, anayejua kesho kwa asilimia yote ni Mungu peke yake..Kwahiyo wewe amka asubuhi, panga mipango yako, kisha mshirikishe Mungu na  umalizie na Neno IKIWA ITAKUPENDEZA MUNGU..

Ikiwa imempendeza basi litafanikiwa kama ulivyopanga lakini ikiwa halikumpendeza basi atakuandalia njia nyingine iliyo bora zaidi.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)

Tofauti kati ya lijamu na hatamu ni ipi kibiblia?

JE SALA YA ROZARI TAKATIFU NI YA KIMAANDIKO?

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

CHAPA YA MNYAMA

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments