Makanda ni nini?

by Admin | 21 December 2022 08:46 am12

Makanda ni neno lingine la KAPU.

Ambalo hutumika kuhifadhi au kubebea vitu mbalimbali hususani vyakula au nafaka.

Katika biblia Neno hilo utakutana nalo katika vifungu kadha wa kadha, mfano wapo ni hivyo ni hivi; 

Mathayo 15:37

[37]Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa.

Marko 8:8

[8]Wakala, wakashiba, wakakusanya mabaki ya vipande vya mikate makanda saba.

Luka 16:6-7

[6]Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini.

[7]Kisha akamwambia mwingine, Na wewe wawiwani? Akasema, Makanda mia ya ngano. Akamwambia, Twaa hati yako, andika themanini.

Luka 16:5-7

[5]Akawaita wadeni wa bwana wake, kila mmoja; akamwambia wa kwanza, Wawiwani na bwana wangu?

[6]Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini.

[7]Kisha akamwambia mwingine, Na wewe wawiwani? Akasema, Makanda mia ya ngano. Akamwambia, Twaa hati yako, andika themanini.

Ni nini twapaswa kujua nyuma ya makanda ya mikate waliyoyakusanya wanafunzi wa Yesu ambayo baadaye waliyasahau mpaka wakaanza kulalamikiana na kulaumiana..Hadi Yesu akawakemea..(Marko 8:14-21)

Ni kwamba waliweka mioyo yao katika makapu yao, katika hazina zao, hata waliposahau wakapaniki.

Ni hali iliyopo sasa miongoni mwetu sisi, tuliookolewa. Tunafikiri sana makapu yetu yana nini, kwa miezi 10 mbele, kwa miaka 3 ijayo..na pale tunapopungukiwa hata uhusiano wetu na Mungu unakufa..Lakini Bwana Yesu anatuambia tusiwe wasiwasi, wala tusiyasumbukie hayo..bali tuutafuta kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine atatuzidishia..kwasababu maisha ni zaidi ya chakula.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ila atapewa mara mia sasa,Ndugu wake(Marko 10:30)

JE! UNAMPENDA BWANA?

Mtu akizaa watoto mia, lakini nafsi yake haikushiba mema;

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/12/21/makanda-ni-nini/