Uzima wa milele ni nini?

Uzima wa milele ni nini?

Uzima wa milele ni nini kama unavyotajwa sehemu mbalimbali?


Jibu fupi, uzima wa milele ni maisha yasiyokuwa na mwisho. Yaani unaishi tu, na utaendelea kuishi, hivyo hivyo kwa siku zisizokuwa na ukomo, miaka milioni moja itapita, bado utaendelea kuishi, miaka trilioni moja itapita bado utaendelea kuishi, na hapo hata bado hujaanza kuishi, utaendelea na kuendelea, kamwe hakuna siku itakayofika na ukasema leo ni ukomo wa mimi kuwa hai, kamwe hutakaa ufe, utakuwa hai hivyo hivyo daima..huo ndio uzima wa milele.

Jambo kama hilo ukilifikiria sana, kuna mahali hata akili yako itafika na kugota, jaribu uone,, kwasababu ni jambo ambalo tangu umezaliwa halijawahi  kuwa sehemu ya maisha yako, tangu ulipokuwa mdogo mpaka unakua umekuwa ukijua kuwa siku moja maisha yako yatakwisha kwa kifo, lakini pale unaposikia kuwa hutakaa ufe tena, akili yako inaweza kushindwa  kulipokea jambo hilo kwa wakati huo.Lakini ukweli ni kwamba hilo litawezekana, lakini sio kwa kila mtu anayeishi leo hii duniani, bali kwa kundi Fulani tu la watu, si watu wote wataishi milele.

Na ndio maana biblia inasema, Karama ya Mungu ni uzima wa milele.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Karama ni zawadi, hivyo zawadi kubwa kuliko zote ambayo Mungu anaweza kumpa mwanadamu, si nyingine zaidi ya uzima wa milele. Yaani maisha yasiyokuwa na ukomo..Huoni kama hiyo ni zawadi iliyopitiliza?

Lakini kama hiyo mistari inavyojieleza, Mungu haitoi karama hiyo hivi hivi tu, bali  inasema anaitoa “katika Yesu Kristo Bwana wetu”. Yaani kwa kupitia Yesu Kristo, maana yake ni kuwa usipookolewa na Yesu huwezi kupokea uzima wa milele kwa namna yoyote ile, haijalishi una matendo mema kiasi gani.

Huwezi kuupata uzima huo kwa mwanadamu mwingine yoyote duniani au mbinguni, anayejiita, mtume, au nabii, au kuhani n.k. hakuna mwanadamu yoyote zaidi ya Yesu Kristo peke yake ndiye anayeweza kuachilia karama hiyo ya uzima wa milele ndani ya Mtu.

Na ndio maana yeye mwenyewe alisema.

Yohana 3:36 “Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia”.

Hivyo kila mtu anayemwamini na kumpokea, anakuwa tayari na uhakika huo kuwa ndani yake uzima wa milele upo. Hata akifa leo, siku ile ya ufufuo atafufuliwa na kuungana na watakatifu wengine, na kwa pamoja wataishi milele na Mungu mbinguni milele.

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.

Sasa, mtu anampokeaje Yesu?. Anampokea Yesu kwanza kwa kutubu dhambi zake kwa kumaanisha kuziacha, na baada ya hapo anakua tayari kubatizwa katika ubatizo sahihi, Na kupokea Roho Mtakatifu. Hivyo kama wewe ni mmojawapo wa ambao hawana uzima wa milele ndani yao, na upo tayari leo kumruhusu Yesu ayabadilishe maisha yako.

Basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba na maagizo mengine >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Na ikiwa umefuatisha maagizo hayo kwa dhati na kwa moyo wako wote, basi uwe na uhakika kuwa umeshapokea karama hiyo ya uzima wa milele ndani yako

Kwahiyo endelea kujifunza Neno la Mungu, na tafuta kanisa la kiroho litakalokusaidia kukua kiroho na Bwana atakuwa na wewe sikuzote. Mpaka siku ile ya paraparanda ya mwisho.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USIUZE URITHI WAKO.

Nini maana ya maneno haya ya Bwana? “Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32).

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

MADHARA YA KUPUUZIA MAAGIZO YA MSINGI MUNGU ANAYOKUPA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments