Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)

Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)

Hanithi ni nini?


Hanithi kibiblia ni mwanaume anayeingiliwa kinyume na maumbile, (Kwa lugha ya sasa wanajulikana kama mashoga), watu wote waliokuwa wanafanya hivi vitendo, waliitwa mahanithi,  na adhabu yake ilikuwa ni mpaka kifo.

Kumbukumbu 23:17 “Pasiwe na kahaba katika binti za Israeli, wala pasiwe na hanithi katika wana wa Israeli wanaume”.

Zamani katika Israeli watu wote waliokuwa wanahudumu kwenye madhabahu za miungu kama vile maashera n.k., walikuwa na desturi ya kufanya hivi vitendo kwa heshima ya miungu yao.

1Wafalme 14:23 “Maana hao pia wakajijengea mahali pa juu, na nguzo, na maashera, juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti wenye majani mabichi.

24 Na mahanithi walikuwako katika nchi, wakafanya sawasawa na machukizo yote ya mataifa Bwana aliowafukuza mbele ya wana wa Israeli”.

 

1Wafalme 15:11 “Basi, Asa akafanya yaliyo mema machoni pa Mungu, kama alivyofanya babaye Daudi.

12 Akawafukuza mahanithi katika nchi, akaziondoa sanamu zote walizozifanya baba zake”.

 

2Wafalme 23:7 “Akaziangusha nyumba za mahanithi, waliokuwamo nyumbani mwa Bwana, wanawake walipofuma mapazia ya Ashera”.

Hii ni roho ambayo mpaka sasa inatenda kazi, na katika hizi siku za mwisho, ilitabiriwa itajirudia kwa nguvu kama ilivyokuwa katika siku za Sodoma na Gomora, Unaweza kuona leo hii wimbi hili la watu linavyozidi kuongezeka kwa kasi duniani kiasi kwamba hata sheria za nchi zinaruhusu, na baadhi ya dini za uongo, na mpaka wanayo bendera yao duniani, kama unavyoweza kuiona katika picha juu, bendera hiyo yenye rangi ya upinde wa mvua, ndio kauli mbiu yao kuwa Mungu hataiangamiza dunia tena kama alivyoahidi, hivyo ndivyo wanavyojidanganya.. Lakini hawajui kuwa Mungu alisema  kweli hataigharikisha dunia kwa maji, lakini alisema ataiangamiza kwa moto.

2Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.

7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu”.

Unaona? Hiyo ni dalili ya wazi kuwa hii dunia inakwenda kuangamizwa wakati sio mwingi.

Lakini sisi tuyoanapo hayo, ni wajibu wetu kujiimarisha na kusimama imara katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho, kwasababu Unyakuo upo karibu.

Swali ni Je! Tumejiwekaje tayari kwa Kurudi kwa Bwana mara ya pili?

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

MAONO YA NABII AMOSI.

HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Emmanuel Aaron
Emmanuel Aaron
1 year ago

Ningependa kupata mafundisho zaidi kupitia email yangu