Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

JIBU: Ndoto ni mfululizo wa picha na mawazo na hisia zinazokuja wakati mtu amelala, Na hizo zinakuja pasipo hiyari ya mtu, kwamba mtu hapangi au haamui ni nini cha kuota! zinakuwa zinajitengeneza zenyewe tu!..Na ndoto zinaweza kuathiriwa na shughuli zetu tunazozifanya kila siku au mazingira yanayotuzunguka au yaliyokuwa yanatuzunguka kipindi kifupi nyuma (Mhubiri 5:3, Isaya 29:8),

Na kuna ndoto zinatokana na shetani na nyingine zinazotokana na Mungu (Mwanzo 28:12, 37:5-10).


Na Maono hayana tofauti sana na ndoto, Maono ni mawazo ya picha na hisia yanayokuja wakati mtu akiwa hajalala…Na haya vile vile hayaji kama atakavyo mtu, wala mtu haamui ni aina gani ya maono ayaone wala huwezi kuyavuta kama mtu anavyovuta usingizi…. anajikuta tu ghafla anaona kitu ambacho sio cha kawaida au cha kawaida, au unakuta anaona tukio Fulani kama vile anaota, na anaporudi anajikuta alikuwa hajalala, pengine alikuwa anatembea au amesimama au alikuwa anaongea na mtu na analikumbuka lile tukio aliloliona kwenye hilo ono.

Na maono yapo yanayotokana na shughuli nyingi, hususani watu ambao wana msongo mkubwa wa mawazo na walioathirika na matumizi ya madawa makali, kadhalika yapo yanayoletwa na shetani haya yanawatokea wengi ambao ni wachawi au wenye roho za mapepo..na yapo yanayoletwa na Mungu.

Tofauti na inavyoaminiwa na wengi kuwa ni lazima kila mtu aliyezaliwa mara ya pili aone maono ya kiMungu, ukweli ni kwamba sio lazima kila mtu aone maono, mtu anaweza akazaliwa mara ya pili na hadi anakufa akawa hajawahi kuona ono hata moja na akaenda mbinguni..Kwasababu suala la kuona maono au kutabiri hivyo ni vipawa vya Roho Mtakatifu, na anapanga nani ampe na nani asimpe, ambaye hajapewa basi atakuwa amepewa kipawa kingine cha kipekee tofauti na hicho, na aliyepewa atakuwa amenyimwa vipawa vingine vya Roho. Haiwezekani watu wote wafanane au wawe na karama zinazofanana na haiwezekani mtu mmoja akawa na karama zote yeye peke yake (1 Wakorintho 12:29-31).


Jambo la muhimu ni kuzaliwa mara ya pili na kuwa kiumbe kipya,(Wagalatia 6:15) na kuishi kulingana na Neno, kuona maono au kutabiri au kufundisha hivyo sio vipimo vya utakatifu au tiketi za kwenda mbinguni (Mathayo 7:22).


Bwana akubariki.

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye
namba hizi: +255789001312/ +255693036618

 
 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mana zinazoendana:

NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA.

TUSIPOUTHAMINI WOKOVU TUTAPATAJE KUPONA?

NI TAMAA IPI HIYO HAWA ALIAMBIWA ITAKUWA KWA MUMEWE?

JE! ASKARI MAGEREZA AKIAMURIWA KUMNYONGA MTU ANATENDA DHAMBI?

 


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Adam
Adam
1 year ago

Amen

Getrude Charles
Getrude Charles
2 years ago

Amen

Emmanuel Thomas
Emmanuel Thomas
2 years ago

God bless you for, i am great to understand the difference between vision and dream.