Tamaa yako itakuwa kwa mumeo.Ni tamaa ipi ya Hawa?

Tamaa yako itakuwa kwa mumeo.Ni tamaa ipi ya Hawa?

SWALI: Ndugu zangu baada ya yule mwanamke Hawa kuvuka mpaka wa maagazo ya Bwana na kula lile tunda alilokatazwa asile:Baada ya Pale tunaona Bwana akimuadhibu kwa adhabu tofauti-tofauti mojawapo ni kuzidishiwa uchungu wa kuzaa. Nataka kufahamu hii adhabu nyingine hapa anaambiwa [TAMAA YAKO ITAKUWA KWA MUMEO.Mwanzo3:16]-Ni tamaa Ipi hiyo Bwana Mungu aliyozungumzia hapo ndugu zangu?


JIBU: Kumbuka jambo la kwanza shetani alilolidadisi kwa mwanamke kwa muda mrefu na kuliona ndani yake ni TAMAA. Tamaa ya kuwa fulani, tamaa ya kuwa juu, tamaa ya kuwa juu ya vitu vyote, tamaa ya kutawala, tamaa ya kudiriki hata kutaka kuwa kama Mungu mwenyewe aliyemuumba..Na ndio maana nyoka alipokuja kumdanganya mwanamke hakumwambia maneno mengine yeyote labda utakuwa mzuri, au utapendwa zaidi au vinginevyo lakini badala yake alimwambia pindi utakapokula tunda utafumbuliwa macho na KUWA KAMA MUNGU!..

 Unaona? “Kuwa kama Mungu”.

Jambo hilo lilimfurahisha sana, pengine labda kwa kujiona yeye aliumbwa wa mwisho zaidi ya viumbe vingine vyote, halafu leo hii anasikia habari za kuwa kama Mungu lilimpa faraja sana..Lakini jambo hilo halikuwa ndani ya Adamu wakati wowote, japo yeye ndiye aliyeumbwa wa kwanza hakuwahi kutamani kuwa kitu fulani zaidi ya pale alipo, hakuwahi kuwa na tamaa ya kuwa juu ya kila kitu japo Mungu alimtawaza juu ya vyote, wala hakuwahi kumtawala mwanamke japo alitoka katika ubavu wake,. Sasa mwanamke alipoasi tu, mambo yakageuka, Ndipo Mungu akamlaani na kumwambia “tamaa yako itakuwa kwa mumeo”..

Hiyo tamaa ya kutaka kuwa juu, hiyo tamaa ya kutaka kuwa kichwa, ya kutaka kutawala sasa imehamishwa na kupelekwa kwa mumeo na matokeo yake, yeye ndiye atakayekutawala. Na ndio maana hayo mambo tunayaona sasa..wanaume wanatawala nyumba zao kwa nguvu, wanataka kujionyesha kuwa wao ni vichwa kati ya wake zao,wanawatiisha wanawake chini, wanataka waonekane kuwa wao ni watawala tu, wao wapo juu tu na wanawake wapo chini. jambo ambalo kiuhalisia halikupaswa kuonyeshwa kwa mwanaume yeyote yule, japo yeye ndiye aliyeumbwa wa kwanza. Umeona hiyo ndiyo laana iliyomkumba mwanamke.. na ndio maana mpaka leo jambo hilo ni Mwiba kwao, hususani kwa wanaume ambao hawajampa Bwana maisha yao, Lakini pia kumbuka Laana sio maagizo..Hatujaagizwa kuwatawala wanawake kwa mabavu katika maandiko.

 Tunanapokuwa wakristo na kumpa Bwana maisha yetu, tunabadilika kutoka katika laana hiyo, na badala yake tunakuwa sio wa kuwaonyesha mabavu yetu kwa wanawake badala yake tunatumia mamlaka yetu KUWAPENDA na kuwajali na kuwatunza kama vile Kristo alivyoonyesha kielelezo kwa kanisa.. mwanaume anapaswa ampende mke wake, kwa Upendo wote…Lakini hilo haliwapi wanaume mamlaka ya kuwatawala wanawake kwa namna isiyopasa bali tuwapende na tusionyeshe tabia kama hizo katika ndoa zetu. 

Waefeso 5:25 “Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;

26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;

27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.

28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.

29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa.

30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake”. 

Unaona?. Kristo hatupigi sisi, Kristo hatutesi sisi, Kristo haonyeshi tabia ya kutokutujali sisi, au kutokutupenda sisi..Vivyo hivyo na wanaume wanaomcha Mungu wanapaswa waonyeshe tabia hizo hizo kwa wake zao.. Na wanawake pia wafahamu wasipojinyenyekeza na kujishusha na badala yake kutaka wao wawe vichwa katika nyumba, hawatawaki kuwatii waume zao, wafahamu kuwa laana hiyo haikwepeki juu yao..Watatawaliwa tu kwa mabavu, wapende au wasipende!!.

Ndio maana ya hilo neno Tamaa yako itakuwa kwa mumeo

Ubarikiwe.


Mada nyinginezo:

UZAO WA NYOKA.

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

MUNGU WANGU,MBONA UMENIACHA?.

SI SHETANI BALI NI WEWE. (CHAGUA MEMA)

DHAMBI ZINAZOTANGULIA NA ZINAZOFUATA.

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

UKWELI UNAOPOTOSHA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Getrude Charles
Getrude Charles
1 year ago

Amina Mpendwa katika Kristo Yesu, umefafanua sana.

Barikiwa sana.