Kwanini Bwana Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wakanunue upanga?

Kwanini Bwana Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wakanunue upanga?

Naomba kufahamu Kwanini Bwana Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wakanunue upanga?. Na tunafahamu kazi ya upanga si njema?

Tusome

Luka 22:35 “Akawauliza, Je! Hapo nilipowatuma hamna mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu? Wakasema, La!

36 Akawaambia, Lakini sasa mwenye mfuko na auchukue, na mkoba vivyo hivyo; naye asiye na upanga, na auze joho yake akanunue”.

Maneno haya aliwaambia wanafunzi wake, alipokaribia mwishoni kabisa mwa huduma yake, akimaanisha kuwa majira yamebadilika, sasa sitawatuma, na kama siwatumi basi na faida zile zinazombatana na wito wangu mtazikosa, hivyo kama ulikuwa huna tabia ya kutunza pesa zako, basi sasa anza kuzitunza, maana yake jiwekee akiba kwenye mfuko wako, jihifadhie vitu vyako, kwa matumizi ya baadaye kwasababu kuna kupungukiwa huko mbele, vivyo hivyo na kama huna upanga, ukauze joho lako ukaununue!

Lakini swali linakuja kwanini uwe ni Upanga tena, wakati upanga ni wa kuulia?. Hata mitume nao walifikiri Bwana anamaanisha hivyo hivyo, kwamba wakanunue upanga kwa ajili ya kujilinda, au kuwapiga maadui zao pale wanapotaka kuwadhuru.. Na ndio maana muda huo huo wakamwambia Bwana maneno haya;

Luka 22:38 “Wakasema, Bwana, tazama, hapa pana panga mbili. Akawaambia, Basi”.

Wakidhani, kuwa Kristo alimaanisha wazitumie hizo kujilindia au kuwapiga maadui zao.. Utaona mawazo hayo bado yalikuwa vichwani mwao, hata baadaye kidogo, majeshi ya makuhani yalipokuja kumkamata Yesu, yakiwa na marungu na mapanga, utaona Petro alichukua upanga wake, na kwenda kumpiga na kumata sikio mtumwa wa kuhani Mkuu. Kitendo ambacho kilimuudhi sana Bwana, akawakemea, na kuwaambia auye kwa kwa upanga atauawa kwa upanga(Mathayo 26:52),.

Luka 22:49 “Na wale waliokuwa karibu naye walipoona yatakayotukia, walisema, Bwana, tuwapige kwa upanga?

50 Mmoja wao akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio la kuume.

51 Yesu akajibu akasema, Mwe radhi kwa hili. Akamgusa sikio, akamponya”.

Hapo ndipo wakagundua kuwa Panga walizoambiwa wakanunue si kwa lengo la kujihami au kuwadhuru wengine.

Bali Bwana alichomaanisha, aliposema mkanunue Panga, ni kwa lengo la kujipatia rizki, panga hapo linawakilisha vitu vyote vikali aidha vya kukatia, kuulia, kuchinjia, au kupasua. Kama vile kisu, shoka, mkuki, n.k. Kwamfano katika kupika utahitaji kisu tu mahali Fulani, kama huna kisu huwezi kukata nyama, au kitunguu, nyanya n.k. hivyo hapo mwanzo ulikuwa huna vitu hivi nyumbani kwako nenda kanunue kwasababu vitakufaa sana wakati huu.

Vilevile kama wewe ni mvuvi kama Petro utahitaji tu Kisu cha kuparulia samaki, hakuna namna utakikwepa. Kama wewe ni mwindaji, utahitaji mkuki au upanga, kama wewe ni mkulima utahitaji shoka, au rato n.k.

Hicho ndicho Bwana alichokimaanisha, kwamba wakajitafutie kitu chochote, kinachoweza kuwafaa kwa ajili ya kukidhi mahitaji yao ya mwilini, lakini sio upanga wa kuulia watu.

Ni nini Bwana anatufundisha katika kauli hiyo? Ni kuwa anapotuita katika utumishi wake tusiwe na wasiwasi tutakula nini, au tutakunywa nini, yeye mwenyewe atahakikisha anatuhudumia kwa kila kitu, kama alivyowahudumia mitume wake mpaka dakika ya mwisho, kwasababu anajua muda wote tunaupoteza kwake, hivyo yeye mwenyewe atahakikisha tunaishi kwa namna yoyote ile, Lakini kama hatupo katika utumishi wake, hatuna budi kuitunza mifuko yetu, kujiwekea akiba zetu, na kujitafutia mawindo yetu, na yeye atatubariki kwa njia hiyo.

Lakini baada ya pale, mtume walifurahia kuendelea na utume wa Bwana, hata siku ya pentekoste ilipofika, na kazi ya utume ulipoanza, Kristo alikuwa nao wakati wote akiwahudumia kama alivyowahidia katika Mathayo 28:20

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

Kwanini Yesu aliwaambia wale wakoma wakajionyeshe kwa makuhani?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments