Je tutakaa mbinguni milele?

Je tutakaa mbinguni milele?

 Maandiko yanasema katika 1Wathesalonike 4:17 tutakaa na Bwana milele mbinguni, sasa iweje tushuke tena kutawala na Yesu duniani kwa miaka 1000?.. Au tutarudi tena mbinguni, baada ya utawala huo kuisha?

Jibu: Tusome..

1Wathesalonike 4:16 “Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; NA HIVYO TUTAKUWA PAMOJA NA BWANA MILELE.

18 Basi, farijianeni kwa maneno hayo.

Kama ukitafakari maandiko hayo kwa makini yanasema “Tutakuwa pamoja na Bwana milele”. Na sio “tutaishi na Bwana mbinguni milele”.. 

Kuna tofauti ya kuwa na mtu milele na kuishi na mtu mahali fulani milele.
Kuwa na Yesu milele maana yake ni kwamba popote atakapokuwepo tutakuwepo naye, popote atakapokwenda tutakwenda naye..hatutamwacha wala yeye hatatuacha, kama alivyotuacha sasa na kwenda mbinguni.

Lakini baada ya sisi kwenda mbinguni huko alipo ,tutakuwa naye milele, hata wakati atakaporudi kwaajili ya hukumu ya vita vya harmagedon tutakuwa naye hatatuacha mbinguni..maandiko yanasema hivyo..

Yuda 1:14 “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu”.

Umeona hapo?..

Kwahiyo mbinguni tutakwenda na vile vile tutarudi kutawala na Kristo kwa miaka elfu hapa duniani..

Kulingana na maandiko mbinguni tutakaa kwa kipindi cha miaka saba tu!..baada ya hapo tutarudi kutawala na Kristo hapa duniani kwa miaka elfu, na hatitarudi tena mbinguni..Kwani Mji wa kimbinguni Yesrusalemu mpya utashuka hapa, na hapa patageuzwa kuwa mbingu mpya na nchi mpya.

Kwa maelezo marefu kuhusu mbingu mpya na nchi mpya unaweza kufungua hapa >> Mbingu mpya na nchi mpya

Hivyo hatuna budi kupiga mbio ili tuweze kuwa miongoni mwa watakaokuwa na Bwana milele.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.

Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je mbinguni itakuwa ni kuimba tu wakati wote?.

Tofauti kati ya ufalme wa mbinguni na ufalme wa Mungu ni ipi?

KUJIFUNUA KWA YESU KWA PILI.

Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

Jeshi la Mbinguni wana wa Israeli waliloliabudu ni lipi?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Yohana sai
Yohana sai
2 years ago

Ubarikiwe