Kwanini Paulo aungane na wale watu wanne wenye nadhiri?

Kwanini Paulo aungane na wale watu wanne wenye nadhiri?

SWALI: Naomba kuelewa kitendo cha Paulo, kuungana na wale watu wanne wenye nadhiri, alipoenda Yerusalemu kilimaanisha nini?. Au kinaelewekaje?


JIBU: Kama tunavyosoma katika maandiko tunaona ziara ya mwisho ya mtume Paulo kwenda Yerusalemu baada ya miaka mingi sana, kwa mara ya kwanza alikutana na Yakobo pamoja na wazee baadhi watakatifu wa Yerusalemu, na moja kwa moja alianza kuwasimulia mafanikio ya huduma yake, na jinsi alivyofanikiwa kuwavua watu wengi kwa Kristo na kuihubiri injili.

Yakobo na wazee wa kiyahudi waliposikia vile, walifurahi sana na kumtukuza Mungu, lakini walimpa taarifa nyingine ambazo, zilikuwa ni ngeni masikioni  mwa Paulo. Kwamba, habari zake zimevuma kwa wayahudi wote wa kikristo waliokaa Yerusalemu kuwa yeye amekuwa akiwafudisha watu waipuuzie torati ya Musa, sio tu kwa watu wa mataifa bali pia kwa wayahudi waliokoka, wasishike sheria  kama vile wasitahiriwe n.k.

Hivyo hiyo imemfanya Paulo aonekane kuwa ni mpingamizi mkubwa sana wa Torati kwa wayahudi, jambo ambalo sio kweli. Paulo aliwafundisha watu kwamba torati sio kipimo cha wokovu, bali neema inayotokana na kumwamini Kristo. Lakini hakuwa mpingamizi wa Torati kwa namna yoyote ile. Na ndio maana kuna wakati alimlazimisha hata Timotheo atahiriwe kwa ajili ya wayahudi. Kama angekuwa mpingamizi asingeruhusu hata kitendo cha kutahiriwa kufanyika(Matendo 16:1).

Hivyo, Yakobo, pamoja na wazee, walijua ukweli kuwa Paulo hawezi kufanya vile, ndipo hapo wakamashauri, kwamba ili kuondoa dukuduku hilo, hana budi kuwaonyesha wayahudi wote kuwa, yeye ahialifu torati hata kidogo. Ndipo wakamwambia, wapo watu wanne ambao wanakaribia kumaliza nadhiri zao (nadhiri ya mnadhiri), na kwamba aungane nao kuwahudumia, katika siku hizo, ili wayahudi watakapoona wajue kuwa Paulo, aihalifu torati.

Matendo 21:17 “Tulipofika Yerusalemu wale ndugu wakatukaribisha kwa furaha.

18 Hata siku ya pili yake Paulo akaingia kwa Yakobo pamoja nasi, na wazee wote walikuwako.

19 Na baada ya kuwaamkua, akawaeleza mambo yote moja moja Mungu aliyoyatenda katika Mataifa kwa huduma yake.

20 Nao waliposikia wakamtukuza Mungu, wakamwambia, Ndugu yetu, unaona jinsi Wayahudi walioamini walivyo elfu nyingi, nao wote wana wivu sana kwa ajili ya torati.

21 Nao wameambiwa habari zako, ya kwamba unawafundisha Wayahudi wote wakaao katika Mataifa kumwacha Musa, ukiwaambia wasiwatahiri watoto wao, wala wasizifuate desturi.

22 Basi, ni nini? Bila shaka watasikia kwamba umekuja.

23 Basi fanya neno hili tunalokuambia. Wako kwetu watu wanne waliofungwa na nadhiri.

24 Wachukue watu hao, ujitakase pamoja nao, na kuwagharimia ili wanyoe vichwa vyao, watu wote wapate kujua ya kuwa habari zile walizoambiwa juu yako si kitu, bali wewe mwenyewe unaenenda vizuri na kuishika torati”.

Sasa kwa kawaida, Mnadhiri kulingana na kitabu cha Hesabu 6, alikuwa haruhusiwi kuonyoa kichwa chake, wala kunywa divai, au mzabibu wa aina yoyote, wala kugusa maiti, mpaka siku zake zote zitakapotimia, Hivyo siku ya mwisho alikuwa anachukua, kondoo madume wawili na jike mmoja pamoja na vikapu vya unga, kwa ajili ya upatanisho.

Hivyo, kwa kuwa Paulo alilazimika kuungana nao katika nadhiri zao, basi, ilikuwa ni desturi uwahudumie kwa kuzichukua zao gharama zote za kinadhiri zilizohitajika. Hivyo Kwa kitendo hicho Paulo alionekana kuwa nay eye ni mtunzaji mzuri wa torati. Japo hilo pekee halikutosha kujiaminisha kwao kwa wayahudi, utaona walikuja kutaka kumkamata na kumuua.

Lakini Hiyo ndio sababu ya Paulo kuungana na wale watu wanne waliokuwa na nadhiri, ilikuwa ni ili kuwaonyesha wayahudi kuwa yeye haivunji torati.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Torati na manabii”?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments