Kwanini Mungu aseme “Alaaniwe azuiaye upanga wake usimwage damu” (Yeremia 48:10).

Kwanini Mungu aseme “Alaaniwe azuiaye upanga wake usimwage damu” (Yeremia 48:10).

Yeremia 48:10 “Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya Bwana kwa ulegevu; NA ALAANIWE AUZUIAYE UPANGA WAKE USIMWAGE DAMU”.

Je kufuatia mstari huo, Mungu anahimiza mauaji?

Jibu: Awali ya yote ni muhimu kuelewa tofauti ya Amri, Sheria na Hukumu za Mungu, sasa kuelewa juu ya mambo hayo, na tofauti zao kwa mapana, unaweza kufungua hapa >>>Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

Lakini kwa ufupi ni kwamba, sheria zote na amri zote zilizotolewa katika agano la kale, zilikuwa na hukumu.. Maana yake ni kwamba, ikitokea mtu kavunja sheria au amri mojawapo basi alistahili hukumu. Na hukumu hiyo ilikuwa ni lazima itekelezwe…isipotekelezwa ilikuwa ni dhambi mbele za Mungu kama tu ilivyo dhambi ya kuvunja amri.

Mfano mmojawapo wa hukumu ni ile hukumu ya mtu kupigwa mawe mpaka afe anapokamatwa katika uzinzi..

Mfano wa hukumu nyingine ni hii..

Kutoka 21:15 “Ampigaye baba yake au mama yake, sharti atauawa”.

Kwahiyo mtu yeyote aliyeonekana akimpiga mzazi wake, hukumu ilikuwa ni kifo..wasipomuua mtu huyo, Mungu alikuwa anawaadhibu!..kwahiyo ili waendelee kukaa salama, Bwana Mungu asiwapige, ilikuwa ni lazima wamuue huyo kijana aliyempiga mzazi wake.

Hali kadhalika ilikuwepo hukumu nyingine ya mtu yeyote anayekwenda kuabudu miungu mingine.. ilikuwa ni sheria kwamba mtu akienda kuabudu miungu mingine sharti auawe, haijalishi ni mzazi wako au ndugu yako, ni lazima utamwua aidha kwa kumpiga mawe au kwa upanga.. Usipomwua ulikuwa unalaaniwa na Mungu.

Kumbukumbu 13:6 “Atakapokushawishi kwa siri ndugu yako, mwana wa mamaako, au mwana wako, au binti yako, au mke wa kifuani mwako, au rafiki yako aliye kama moyo wako, akikuambia, Twende tukaabudu miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako;

7 katika miungu ya mataifa yaliyo kando-kando yenu karibu nawe au mbali nawe, tokea ncha moja ya dunia hata ncha ya pili ya dunia;

8 USIMKUBALIE WALA USIMSIKIZE; WALA JICHO LAKO LISIMWONEE HURUMA, WALA USIMWACHE, WALA USIMFICHE;

9 MWUE KWELI; MKONO WAKO NA UWE WA KWANZA JUU YAKE KATIKA KUMWUA, NA BAADAYE MIKONO YA WATU WOTE.

10 Nawe mtupie mawe hata afe; kwa kuwa alitaka kukupotoa na Bwana, Mungu wako aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.

11 Na Israeli wote watasikia na kuogopa, wasifanye tena uovu mfano wa huo katikati yako”.

Vile vile ilikuwepo hukumu ya kwamba, mtu yeyote au kikundi chochote kikizuka katikati ya jamii ya Israeli, ambacho kinawashawishi watu kuabudu miungu mingine mbali na Mungu wa Israeli. Bwana Mungu alitoa ruhusa ya watu hao kuuliwa kwa makali ya upanga.

Kumbukumbu 13:12 “Ukisikia yasemwa habari ya miji yako mmojawapo, akupayo Bwana, Mungu wako, ukae humo, ukiambiwa,

13 KUMETOKA KATIKATI YAKO MABARADHULI KADHA WA KADHA, WAMEWAPOTOA WENYEJI WA MJI WAO, WAKISEMA, TWENDENI TUKAABUDU MIUNGU MINGINE MSIYOIJUA;

14 ndipo nawe uulize na kutafuta, ukiuliza kwa bidii; nawe angalia, ikiwa kweli, na jambo lile halina shaka, kwamba machukizo mfano wa haya yafanyika katikati yako;

15 HAKIKA YAKO UWAPIGE WENYEJI WA MJI ULE KWA MAKALI YA UPANGA, KWA KUWAANGAMIZA KABISA, PAMOJA NA VITU VYOTE VILIVYOMO, NA WANYAMA WALIO HUMO, KWA MAKALI YA UPANGA

Umeona?.. Hiyo ndio sababu Bwana kasema hapo kwenye Yeremia 48:10 “..ALAANIWE AUZUIAYE UPANGA WAKE USIMWAGE DAMU”.

Damu inayomwagwa ni ya watu waliomwacha Mungu wa Israeli na sheria zake kwa makusudi.

Lakini swali ni je!..  Hata sasa katika agano jipya hii sheria ipo??.

Jibu ni la!. Katika agano jipya hatuna hiyo amri!..haturuhusiwi kumwua mzinzi, wala mlevi, wala mwizi.. bali tunapaswa tuziue zile roho zilizopo ndani yao, zinazowashawishi wao kufanya mambo hayo.. na roho hizo ni roho za mapepo..hizo ndio tunazozipiga kwa Upanga wa Roho, huku na sisi tukiwa tumejivika silaha zote za roho.

Waefeso 6:11 “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, JUU YA MAJESHI YA PEPO WABAYA KATIKA ULIMWENGU WA ROHO.

13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;

18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote”.

Tukiweza kuzivaa hizi silaha na kuutumia vizuri upanga wa roho, ndipo tutakapoweza kuziadhibu roho zote, zilizopo ndani ya watu na kuwaacha watu huru.

2Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;

4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;

6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

Kwanini Bwana Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wakanunue upanga?

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments