HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

Jina la mwokozi wetu Yesu Kristo lihimidiwe milele. Karibu tuyatafakari maandiko. Na leo tutaona ofisi kuu tatu za shetani, ambazo, zinafanya kazi humu duniani.

Biblia inasema..

Ufunuo 16:13 “Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.

14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi”.

Hapa, tunaona watatu wanatajwa, ambao ni;

  1. Joka
  2. Mnyama
  3. Nabii wa uongo

Haya ni mapepo makuu matatu ya juu sana na yanayofanya kazi kwa kushirikiana, na kichwa chao akiwa ni ibilisi mwenyewe. Muunganiko huu ndio unaoukamilisha utawala mchafu wa mashetani unaofanya kazi duniani.

Sasa Ofisi ambayo, inafanya kazi sasa kwa nguvu ni hiyo ya JOKA, lakini hizo nyingine mbili zilizosalia yaani ya Mnyama na Nabii wa Uongo, kwasasa zinafanya kazi katika siri, lakini zitakuja kufanya kazi vema, katika kipindi cha dhiki, baada ya unyakuo kupita. Kipindi hicho ndio zitawepa mamlaka kamili ya kujidhihirisha duniani.

Sasa tuone kazi za hizi roho tatu ni zipi;

  1. Tukianzana na huyo wa kwanza yaani Joka.

Kama tunavyofahamu kazi kuu ya JOKA ni kumeza: Biblia inapomtaja joka (shetani), inalenga moja kwa moja katika kummeza Kristo mahali popote anapozaliwa,

soma Ufunuo 12:3-5

“3 Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.

4 Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake.

5 Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi”.

Na ndio maana utaona pindi Kristo anazaliwa duniani, Joka hili lilisimama ndani ya Herode, kutaka kumuua, lakini lilishindwa..Hivyo mahali popote Kristo anapozaliwa, ni lazima joka ajitokeze kuleta vita, hata sasa mtu anapotaka kuokoka kwa kumaanisha kweli kumfuata Kristo, ajue kuwa ni lazima atakutana na vita vya hili joka, kwasababu sikuzote halitaki kumwona Kristo katika mioyo ya watu.

Na ndio mwishoni biblia inasema, likaenda kusimama katika mchanga wa bahari, yaani mahali ambapo, nchi kavu na Habari vinakutana, fukwe (beach), Yaani ikifunua kuwa lipo mpakani, kuwazuia watu wanataoka kutoka katika giza kuja katika nuru, hapo ndipo vita ilipo.. Kwa maelezo marefu juu ya hili fungua link hii usome >>>> NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI.

Ufunuo 12:17 “Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari”.

Hivyo, fahamu kuwa ukitaka kuwa mtakatifu, basi ujue pia joka litasimama kukupinga vikali. Lakini halitaweza kukushinda, ikiwa umedhamiria kweli kumfuata Kristo. Lakini ukiwa nusu nusu, yaani unataka hutaki, litameza Kristo wako, na hutazalisha chochote katika wokovu wako.

          2.  Mnyama.

Biblia inapotaja mnyama, inazungumzia utawala ya ibilisi kupitia falme kubwa za dunia. Alishatumia falme za dunia kadha wa kadha huko nyuma, kama vile Babeli, Umedi, Uyunani na Rumi, kuangusha watakatifu wa Mungu. Na utaunyanyua tena ufalme mwingine ambao utakuwa na nguvu sana, ufalme huu kichwa chake kitakuwa ni RUMI,  na utafanya kazi kwa kipindi kifupi sana yaani miaka pungufu ya saba (7), lakini utaleta, mabadiliko makubwa sana duniani, kiasi kwamba kila mtu atalazimishwa aufuate huo utawala.

Usipoufuata, hutaweza kuuza wala kununua, wala kuajiriwa. Biblia inasema utawala huo wa kishetani ambao utakuwa na chapa ya 666 nyuma yake, utafurahiwa na watu wote watatakaokuwa wamesalia, ambao majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha mwana-kondoo kabla ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu. Lakini wale wote watakaoonyesha dalili ya kuukataa au kuupinga, mwisho wao utakuwa ni kifo cha mateso makali sana ya dhiki.

Ufunuo 13:8 “Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia”.

Jambo ambalo wengi wetu hatulijui ni kuwa, utawala huu tayari ulishafanya kazi huko nyuma,ambao ni ni Rumi, na ulishawaua watakatifu wengi sana Zaidi ya milioni 80, Lakini sasa Mungu ameuzuia kwa muda, lakini ndio utakaokuja kuzuka tena na kuyaongoza mataifa yote, katika utawala mpya, moyo wa utawala huo ni Vatican, Rumi, utakuwa na nguvu nyingi Zaidi ya ule wa kwanza, kwasababu utakuwa na sapoti ya mataifa yote makubwa unayoyajua leo hii duniani.

Ufunuo 17:8 “Yule mnyama uliyemwona alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu na kwenda kwenye uharibifu. Na hao wakaao juu ya nchi, wasioandikwa majina yao katika kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, watastaajabu wamwonapo yule mnyama, ya kwamba alikuwako, naye hayuko, naye atakuwako”.

   3.   Nabii wa Uongo.

Kama jina lake lilivyo, ni nabii, kazi yake ni kuwapotosha watu, kwa kuwapa maagizo ya uongo, wadhani kuwa wanapokea maagizo kutoka kwa Mungu kumbe ni kwa ibilisi. Biblia inasema hata sasa wapo manabii wa uongo, ambao wanaiga kazi ya mkuu wao, atakayekuja. Nabii huyu ndiye mpinga-kristo mwenyewe.

1Yohana 2:18 “Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho”.

Mpinga-Kristo huyu ambaye atakuja rasmi mara baada ya unyakuo wa kanisa kupita, atapewa uwezo wa kufanya ishara za uongo na shetani mwenyewe,atapewa uwezo wa kutenda miujiza feki kama ile ya Yane na Yambre kipindi cha Musa.

2Wathesalonike 2:6 “Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.

7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.

8 Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;

9 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo”;

Na kazi yake kubwa itakuwa ni kuwashurutisha watu, waipokee ile chapa ya mnyama, na wengi watamuamini sana na kuipokea kwasababu ya zile ishara atakazokuwa anazifanya duniani.

Ufunuo 13:12 “Naye atumia uwezo wote wa mnyama yule wa kwanza mbele yake. Naye aifanya dunia na wote wakaao ndani yake wamsujudie mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.

13 Naye afanya ishara kubwa, hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu.

14 Naye awakosesha wale wakaao juu ya nchi, kwa ishara zile alizopewa kuzifanya mbele ya huyo mnyama, akiwaambia wakaao juu ya nchi kumfanyia sanamu yule mnyama, aliyekuwa na jeraha la upanga naye akaishi.

15 Akapewa kutia pumzi katika ile sanamu ya mnyama, hata ile sanamu ya mnyama inene, na kuwafanya hao wote wasioisujudu sanamu ya mnyama wauawe.

16 Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao;

17 tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.

18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.

Na mwisho kabisa, roho hizi zote tatu, yaani ya joka, mnyama na nabii wa uongo, zitaungana, na kuwaendelea wafalme wote wa duniani, ikiwemo wa hilo taifa lako unaloishi,  ili wapatane kwa kitu kimoja, kupigana na Mungu mwenyezi, pale Israeli, katika vita ile ya Harmagedoni, kipindi hicho ndicho Kristo atahitimisha vyote kwa kuwaua wanadamu wengi sana, na kuanzisha utawala wake mpya wa amani wa miaka elfu moja hapa duniani, naye atatawala kama MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA. Haleluya.

Hivyo ndugu, fahamu kuwa hizi ni nyakati za mwisho, kipindi kifupi sana tumebakiwa nacho,  Unyakuo ni siku yoyote, dalili zote zimeshatimia, mfumo wa yule mnyama upo tayari, unatendakazi tu kwa siri kwa dini ya uongo ya rumi, ni wakati wowote kunyanyuka, Tubu dhambi zako mgeukie Bwana Yesu kwa kumaanisha. Kubali kujitwika msalaba wako umfuate, kwasababu parapanda italia siku yoyote.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

UFUNUO: Mlango wa 12

UFUNUO: Mlango wa 13

UFUNUO: Mlango wa 17

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

DANIELI: Mlango wa 1

NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
6 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Nico sanga
Nico sanga
1 year ago

Nimebarikiwa na neno, amen.

Hosea Stephano Ndimcheye
Hosea Stephano Ndimcheye
2 years ago

Mungu awabariki sana kwa neno la Mungu.

Emmanuel Kitengule
Emmanuel Kitengule
2 years ago

Barikiwa sana mwalimu, kwa kweli kanisa kama kanisa kwa siku hizi za mwisho tunahitaji maarifa ya KWELI yakayotupa imani thabiti na kusimama badala kujidanganya kwenye ujinga.Kazi unayoifanya ni kubwa sana kwani inaotutoa upofu na matongotongo, Mungu na azidi kukuinua sana kwa kweli.