Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

Kifo ni ile hali ya uhai kutoka ndani ya kiumbe hai chochote. Kifo kinaweza kumtokea mtu, mnyama, bakteria, kirusi, mmea, jani n.k. Vyote hivi maadamu vina uhai ndani yao, vinapotokwa tu huo  uhai basi vinakuwa vimekufa.

Lakini Mauti ni nini?

Mauti ni kile kile kifo, isipokuwa ni mahususi tu kwa mwanadamu.. Huwezi kusema “mti” umekumbwa na mauti, au “mbwa” amepatwa na mauti.. Bali utasema, mti umekufa au mbwa amekufa. Ni mwanadamu tu ndiye anayekumbwa na mauti.

Lakini kwanini Kifo kitofautishwe na mauti?

Ni kuonyesha uzito wa hali hiyo kwa mwanadamu.. Kwamfano “Kilio” kinaweza kutokea kwa mtu yeyote yule, iwe ni mtoto au mtu mzima Lakini kikiwa kwa mtu mzima, hakiwezi kuchukuliwa kama kile cha mtoto, kwasababu kama vile wasemavyo wanajamii, “ukiona mtu mzima analia basi ujue kuna jambo”

Maana yake ni kuwa hadi mtu mzima anatoa machozi, ujue hayajaja bure bure tu, bali yana sababu nyuma yake, na matokeo mbele yake, kwasababu si desturi ya mtu mzima kulia. Nyuma yake utagundua aidha kuna msiba, au magonjwa, au kuumizwa moyo kusikoelezeka, kusalitiwa au kupoteza mali zake nyingi, au vitu, n.k.. Lakini mtoto mdogo anaweza akalia kwasababu zisizokuwa na maana au msingi wowote.

Vivyo hivyo katika kifo na mauti ni tendo lilelile..kuondoka kwa uhai.. isipokuwa linapokuja kwa mtu, linakuwa na uzito wa namna yake, kwasababu mwanadamu hakuumbiwa kifo, halidhalika kwa sifa yake na heshima na akili alizopewa na Mungu, jambo kama hilo ni anguko kubwa sana kwake..Mauti ni pigo kwa mwanadamu.

Sababu ya mauti kumpata mtu ni nini?

Ni dhambi..

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Sisi wanadamu tulipoasi, adhabu hii ya mauti ilitukumba.. Hilo ni pigo kubwa sana kwetu, tofauti na Wanyama, wenyewe hawajui chochote, wala hawaelewi, kufa na kupotea kwao ni kitu cha kawaida, lakini sisi tunajua kwamba ipo siku uhai utatutoka..

Lakini heri ingekuwa ni kifo cha miili yetu tu halafu basi.. Lakini Huko mbeleni pia baada ya kifo, kuna adhabu ya kifo cha roho. Hiyo ndio inayoitwa mauti ya pili..Ambazo roho hizi zitamalizwa kabisa katika lile ziwa la moto..Hapo ndipo utaona, tofauti ya kifo cha mnyama, na kile cha mwanadamu.

Ndugu, ukikumbwa na mauti sasa, toa yale mawazo kwamba utakuwa kama mnyama tu.. Hapana, ukifa katika dhambi, utanyoshea moja kwa moja hadi jehanamu, ukisubiri siku ya ufufuo ifike uhukumiwe kisha utupwe katika ziwa la moto milele na milele.

Lakini Habari njema ni kwamba, Bwana Yesu alikuja kukomesha mauti kwa mwanadamu, na kwamba yeyote amwaminiye yeye, anakuwa amevuta kutoka katika mauti na kuingia kwenye uzima..

Yohana 5:24 “Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani”.

Umeona? Yaani Yesu akikuoa mauti inakuwa haina nguvu tena ndani yake..

Hivyo ndugu, wasubiri nini, leo usimkaribishe Yesu moyoni mwako.? Kumbuka hakuna mtu mwenye garantii ya kuishi milele. Au anayeijua kesho yake kama atakuwa duniani au la. Ukifa katika dhambi ni nani atakayekuponya na mauti ya roho yako? Huko utakapokwenda utakuwa mgeni wa nani. Kama huna uhakika, unajisikiaje kubaki katika hali hiyo?

Lakini nafasi sasa unayo, Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo, yaani kuongozwa sala ya toba ya kumpokea Yesu.. Basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo huo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa kifo kinampata kiumbe hai chochote, lakini mauti ni mahususi kwa mwanadamu, kwasababu yenyewe inabeba maana kubwa zaidi ya kifo cha kutoka uhai tu. Mauti imebeba uchungu, majuto, masononeko, hukumu, nyuma yake, jambo ambalo kifo hakina.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

jiunge kwenye group la whatsapp la mafundisho ya kila siku kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Jehanamu ni nini?

Kuna hukumu za aina ngapi?

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

UNYAKUO.

DHAMBI YA MAUTI

BALI WANA WA UFALME WATATUPWA NJE!.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Robert Yandilo
Robert Yandilo
6 months ago

Mbarikiwe Sana watumishi wa Mungu, hakika najifunza Mambo mengi Sana kupitia ukurasa huu