Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

Zaburi 147:3 Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuziganga jeraha zao.  4 Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.  5 Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu, Akili zake hazina mpaka.

Ukitazama juu unaona nyota nyingi sana zisizo na idadi, mbali na hizo zilizo ndani ya upeo wa macho yetu, lakini pia zipo nyingine tusizoziona ambazo idadi yake ni mabilioni kwa mabilioni, matrilioni kwa matrilioni,..

Lakini hapa Mungu anatupa siri ya uweza wake, anasema zote hizo amezihesabu na kuzipa majina,..

Sasa Kwanini atuambie jambo kama hilo?

Ni kutuaminisha kuwa ikiwa anazifahamu  nyota zote zilizo mbali, nje-ndani, atashindwaje kutufahamu sisi? Atashindwaje kuziona taabu zetu na shida zetu, atashindwaje kuyaona mateso yetu na majeraha yetu?

Hivyo hapo anaposema ‘Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuziganga jeraha zao’. Anamaanisha, huweza kutufanya upya, endapo tutamkaribia.

1Petro 5:7  ‘huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu’.

Mkaribie Kristo akuponye kwasababu yeye yupo karibu sana na wewe zaidi ya nyota za angani.

Utukufu na uweza vina yeye milele na milele amina.

Maombi Yangu:

“Baba mwema, tumeona uweza wako, juu ya ulimwengu wako uliouumba, kwamba hakuna lolote usilolijua,wala usiloliweza, na sasa ninakukaribia Baba wa Upendo, kama ulivyoahidi kwenye Neno lako kwamba utaziganga jeraha zangu, Naomba sasa niponye moyo wangu, na mwili wangu, nifanye upya tena, nisimame mbele zako, nikutumikie. Ni katika jina la Yesu naomba nikuamini. Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NYOTA ZIPOTEAZO.

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

Agano ni nini? na kuna aina ngapi za maagano?

Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments