Je watu wa kale walitumia vifaa gani kuandikia?

Je watu wa kale walitumia vifaa gani kuandikia?

Watu wa kale walitumia wino, na kalamu pamoja na karasati kuweka kumbukumbu zao kama tunavyofanya sasa..

Isipokuwa wino wao, kalamu zao na karatasi zao zilikuwa tofauti na hizi tunazotumia sasa..

Mtume Yohana katika nyaraka zake aliandika hivi; 

3 Yohana 1:13

[13]Nalikuwa na mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kukuandikia kwa wino na kalamu. 

Kuonyesha kuwa unandishi wao ulitegemea wino na kalamu, kama tu huu wetu.

Je! Wino wa kale ulitengenezwaje?

Tofauti na huu wa kwetu unaotengenezwa na kemikali mbalimbali..wino wa zamani ulikuwa unatengenezwa na MASINZI. Masinzi hayo yalikuwa yanavunwa aidha kutoka  katika mafuta yaliyochomwa au kuni pale yanapoganda katika chombo kama sufuria kwa pembeni.

Wino wa kale

Sasa yalipokusanywa kama poda, baadaye yanachanganywa na gundi inayotoka katika mmea wa mpira..lengo la kufanya hivyo ni kuufanya wino huo ushikamane vizuri ili  wakati wa uandishi wino usitapakae ovyo.

Hivyo mwandishi anapoununua wino huo anachofanya ni kuchanganya na maji, kisha kutumia kalamu yake kuchovya na kuandika katika hilo karatasi lao.

Je! Kalamu zao ziliundwaje

Tofauti na kalamu zetu hizi, ambazo zinatengenezwa kwa mirija ya pastiki na chuma. Kalamu za zamani ziliundwa na mmea ujulikanao kama MWANZI ambayo hata huku sehemu kadhaa hutumika.. Mianzi hii ilichongwa kwa pembeni kuacha ncha. Ili kuruhusu wembamba wa uandishi katika karatasi  kama tu kalamu zetu za kisasa zilivyo.Tazama picha.

Kalamu za kale

Je karatasi za kale zilikuwaje?

Karatasi za zamani zilifanana hizi isipokuwa zenyewe zilikuwa ni nene, ziliundwa na mmea ujulikanao kama mafunjo(Ayubu 8:11).

Mmea huu ulichongwa kulingana na ukubwa wa karatasi, kisha kuchanjwa chanjwa katika vipisi vidogo, ambavyo baaadaye vililowekwa katika maji ili vilainike..kisha vinawekwa katika ubao ulionyooka, kisha vinalazwa kipisi kimoja baada ya kingine, na vingine kupita kwa kukatiza..kisha panawekwa ngozi ya mnyama kwa juu , na baada ya hapo kukandamizwa, ili vipisi hivyo vishikane,

Na kuachwa siku kadhaa, baadaye wakitoa, tayari karatasi hiyo nene hutokea… ngumu na imara kuliko hata hizi tulizonazo sasa. Ndizo walizotumia watu wa kale kuandikia.

karatasi za kale

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je! Unatambua kuwa unyakuo wa kanisa upo karibu? Umejiandaaje? Ikiwa bado hujafanya hivyo na unahitaji msaada huo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi;

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

BWANA alimaanisha nini kwenye mstari huu Marko 2:21″ Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu?

Yerusalemu ni nini?

Kaniki ni nini katika biblia? (Yeremia 8:21).

Karismatiki ni nini?

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments