Kumbuka chapa ya mnyama imeshaanza kufanya kazi, na inaanzia ndani kisha ije nje Kumalizia! na hii inatenda kazi katika madhehebu yote yaliyofanya uzinzi na kanisa kahaba KATOLIKI, ni mara ngapi unaambiwa biblia inasema hivi, wewe unasema dhehebu letu haliamini hivyo?, ni mara ngapi unaulizwa wewe ni mkristo unajibu mimi ni wa-dhehebu fulani? Je unadhani ni ROHO MTAKATIFU ndiye aliyeleta hiyo migawanyiko? jibu ni hapana shetani ndiye aliyeleta hiyo migawanyiko, na bila kujua hilo dhehebu lako lina ushirika kamili na lile kanisa mama kahaba na ndio tunaona lile jina MAMA WA MAKAHABA limezaliwa huko. Sasa kwa dizaini hii utaachaje kushawishika kuipokea ile chapa?..umeshaipokea tayari moyoni mwako kilichobaki ni udhihirisho wa nje tu! ambao hauna tofauti na ule wa ndani. Biblia inasema tokeni kwake enyi watu wangu wala msishiriki dhambi zake, kutoka sio kwa miguu tu, bali kutoka moyoni kwanza kwa kubadilisha namna ya kumwabudu Mungu, Mungu ni ROHO nao wamwabuduo imewapasa kumwabudu katika roho na kweli, na sio kwa kupitia sanamu, wala dhehebu wala papa wala bikira Mariamu, wala kwa mapokeo wala kwa mtu mwingine yoyote, bali katika roho na kweli (ndani ya YESU KRISTO).