Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri.

Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri.

SWALI: Mwandishi, alimaanisha nini, kusema Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, msinichunguze kwa kuwa ni mweusi-mweusi? (Wimbo 1:5-6)


JIBU: Tusome,

Wimbo 1:5 “Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, Enyi binti za Yerusalemu, Mfano wa hema za Kedari, Kama mapazia yake Sulemani.

6 Msinichunguze kwa kuwa ni mweusi-mweusi, Kwa sababu jua limeniunguza. Wana wa mamangu walinikasirikia, Waliniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu; Bali shamba langu mwenyewe sikulilinda”.

Huyu ni mwanamke , anayejaribu kueleza hali yake ya nje jinsi inavyoonekana, ilivyo tofauti na uhalisia wake wa ndani. Anaanza kwa kusema mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, Yaani japokuwa naonekana ni mweusi, nisiyevutia, lakini ninao uzuri wa kupendwa hata na mfalme,

Mstari wa 6 anaendelea kueleza Weusi wake, ulitokana na nini,.. Anasema, ulitokana na kazi za mashambani, ambazo aliwekwa kama mlinzi azisimamie, ikiwa na maana muda wote a jua linapochomoza jua linapozama, ni lazima awepo pale alitunze,

Wakati ndugu zake, wakiwa wamestarehe nyumbani kwenye uvuli wa makasri, wakila na kufurahi, yeye yupo mashambani anatanga na jua.

Na kwa kawaida, mtu anayekaa kwenye jua muda mrefu Ngozi yake itakuwa nyeusi tu, na vilevile itapunguza mvuto. Ndicho kilichomkuta huyu binti, aliyekuwa tofauti na mabinti wengine, kama ilivyozoeleka kuwa  mabinti huwa hawakai mashambani, wala hawafanyi shughuli  za ulinzi, . Lakini yeye alikuwa hivyo, na katika hayo yote anasema bado anaoozuri unaotoka ndani.

Hii inafunua nini kwetu, au ni ujumbe gani tunapitishiwa sisi ?

Huyu binti anafananishwa na watumishi wa Mungu, wanaotumika katika shamba la Mungu, ambao pengine kutwa kucha wanajitaabisha kuwapelekea wengine Habari njema,(Vijinini na mijini, na kwa njia mbalimbali), sasa kwa taabu hizo, kwa kawaida ni lazima watakosa vitu vingi vyema, kwasababu muda wote wapo mashambani, pengine watakuwa wadhaifu kimwili/au kimwonekano, watakuwa hawana mali, watakuwa hawana mvuto wowote. Lakini Bwana anawaona ni wazuri sana,

Mtume Paulo aliliona hilo akasema,

2Wakorintho 4:16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. 17 Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana;

 18 tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.

Kuonyesha kuwa utu wetu wa nje, waweza kuchakaa kwasababu ya utumishi, lakini ule wa ndani wafanywa upya kila siku, Sehemu nyingine aliandika Maisha ya utumishi ni ya kufa kila siku, kujitoa kwa wengine na sio kwa ajili yako, kama huyu binti (1Wakorintho 15:31).

Hivyo na wewe ambaye, unamtumikia Bwana kwa uaminifu, pengine  wajiuliza, mbona mwonekano wangu haupo, kama nilivyokuwa hapo nyuma simtumikii? Fahamu kuwa upo shambani, jua litakuwa ni lako, lakini uzuri wako unatoka ndani na Mungu anauona, na anapendezwa na wewe.

Siku zitakuja, utapewa mwili wa utukufu, mwili usioonja uharibifu, mwili wa milele, ndipo utakapojua kuwa wewe ulipendwa na Bwana, na hiyo haikuwa kwa mwonekano wako, lakini kwa uaminifu wako.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UBATILI.

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”?

Kuvyaza ni nini katika biblia? (Ayubu 21:10).

KWANINI MIMI?

ANGALIA UZURI WAKO, USIGEUKE KUWA KITANZI CHAKO.

NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.

Donda-Ndugu ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments