Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu?

Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu?

Wivu ni nini kibiblia na kuna aina ngapi za Wivu unaowapata watu? Na je ni dhambi kuwa na Wivu?

Katika kitabu cha Wagalatia biblia imetaja “Wivu” kuwa ni mojawapo ya tunda la mwili. Sasa swali ninapopata wivu wa kimaendeleo nafanya dhambi? Au ninapopata wivu wa mwanandoa mwenzangu kukosa uaminifu je nayo ni dhambi?


Jibu: Tusome,

Wagalatia 5:19-21
19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi..

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira……….. ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”

Ni kweli Wivu ni mojawapo wa matendo ya mwili ambayo ni dhambi mtu kuwa nayo, lakini kama ya kuingia ndani zaidi katika andiko hili..ni vizuri kuzijua kwanza aina za wivu..

Upo “Wivu wa kiMungu” na vile vile upo “wivu wa kidunia”, ni kama tu “hasira” au “hofu”. Ipo hasira ya kiMungu na vile vile ipo hasira ya kidunia au ya kiulimwengu.

Hasira ya kidunia ni ile inayoyoishia au inayompelekea mtu kutenda dhambi, kama kutukana, kuua, kuonea, kuiba n.k.. kwaufupi matunda yake ni mabaya daima… Lakini hasira ya kiMungu ni ile inaiyoishia katika kumjenga mtu na kumtengeneza zaidi, na kumrudisha kwa Mungu au katika njia sahihi kwa upendo.

Mfano wa hasira ya kiMungu ni ile Bwana Yesu aliyokuwa nayo juu ya Mafarisayo na Masadukayo.
Utaona Mafarisayo na Masadukayo walikuwa wanamwudhi sana Bwana lakini hasira ya Bwana haikuishia katika kuwatukana, au kuwashushia moto na kuwaangamiza ingawa alikuwa na uwezo huo, au kuwaharibu kwa njia yoyote ile… bali katika kuwahurumia..

Marko 3:1-5 “Akaingia tena katika sinagogi; na palikuwako huko mtu mwenye mkono uliopooza;

2 wakamvizia ili kuona kama atamponya siku ya sabato; wapate kumshitaki.

3 Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, Simama katikati.

4 Akawauliza, Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya? Kuponya roho au kuiua? Wakanyamaza.

5 AKAWAKAZIA MACHO PANDE ZOTE KWA HASIRA, AKIONA HUZUNI kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena”.

Hasira ya namna hii biblia imesema tuwe nayo ila tusitende dhambi, jua lisizame tukiwa nayo bado mioyoni..(Waefeso 4:26).

Sasa tukirudi katika Mantiki ya hofu na wivu ni hivyo hivyo, ipo hofu ya kiMungu na ya ipo hofu ya kidunia, vile vile upo wivu wa kiMungu na upo wivu wa kidunia.
Wivu wa kidunia ni ule unaoishia kutenda dhambi.. Mfano mtu atamwonea mwingine wivu kwasababu kapata kitu fulani ambacho yeye hajakipata, hivyo atatamani au atatafuta njia yule mtu akipoteze kile kitu ndipo atulie.

Mfano wa wivu huu ni ule aliokuwa nao Kaini, alipoona sadaka ya ndugu yake imekubaliwa na kwake imekataliwa. Badala atafute njia ya kuboresha sadaka yake ikubalike mbele za Mungu kama ya ndugu yake, yeye akatafuta kumwua ndugu yake, (wivu unaoish kuleta chuki, masengenyo, vinyongo, visasi ni wa kishetani)..ambao ni dhambi mtu kuwa nao sawasawa na hiyo Wagalatia 5:20.

Wivu wa kiMungu ni ule unaomfanya mtu atamani kuwa mwema kama mwingine alivyo mwema, unaomfanya mtu atamani kufanya vizuri kama mwingine anavyofanya vizuri pasipo kumtakia madhara yule mwingine, (kwa ufupi haufurahii kuanguka wala kupunguka kwa mwingine)..zaidi sana mafanikio ya mwingine yanakuwa siku zote ni darasa kwake….

Wivu huu sio mbaya na si dhambi mtu kuwa nao, kwasababu matunda yake ni mazuri..
Mfano wa huu ni ule Mtume Paulo, aliojaribu kuutia kwa ndugu zake Waisraeli ili wamgeukie Mungu zaidi.

Warumi 11:14 “nipate kuwatia wivu walio damu moja na mimi na kuwaokoa baadhi yao”.

Lakini pia upo Wivu mwingine wa KiMungu ambao unaishia kuharibu vitu vya kishetani lakini si kimharibu mtu..

Mfano wa wivu huu ni alikuwa nao Bwana Yesu juu ya Hekalu la Mungu, alipoingia na kukuta watu wanafanya biashara ndani ya hekalu, maandiko yanasema Bwana alizipindua meza zao, na kuharibu biashara zao lakini si kuwaharibu wao.. Na wanafunzi wake wakakumbuka andiko la wivu wa nyumba ya Mungu utamla (Yohana 2:17).

Wivu huu pia na sisi tunapaswa tuwe nao tunapoona kazi ya Mungu inachafuka, ni lazima tusimame kuziharibu hizo kazi za shetani kwa maombi na kwa mafundisho sahihi, lakini si kwa kuwadhuru watu au kuwatukana, au kuwaletea madhara yoyote ya kimwili.

Wivu wa namna hii pia upo katikati ya wanandoa na wanafamilia, kama kuna kiashiria chochote cha mwanandoa au mwanafamilia kutoka kwenye mstari wa uaminifu, au nidhamu, au maadili au heshima…Wivu wa namna hii huwa unanyanyuka!, sasa vibaya yule aliyemwaminifu, au aliye imara katika ndoa au familia kusimama na kuharibu au kuziba upenyo wowote ambao shetani anataka kuchukua nafasi ndani ya hiyo familia au ndoa…lakini kwa hekima pasipo kumdhuru mtu.

Lakini wivu wa wanandoa au wanafamilia unaoishia kuua huo hautokani na Mungu!.

Je na wewe unasumbuliwa na dhambi ya Wivu wa kidunia ambao unaishia kusengenya, kuona hasira, kuua, kutukana n.k Na hujui utatokaje katika hilo shimo?.

Bwana Yesu amekuja kwaajili ya kututoa katika hayo mashimo, kwa nguvu zetu hatuwezi kutoka huko wala kujitoa.
Nguvu pekee ya kututoa huko ni kwa njia kwa ya Roho Mtakatifu, kwa somo kamili kuhusiana na Roho Mtakatifu, jinsi ya kumpomea na jinsi.atakavyokuwezesha kushinda yale usiyoweza kuyashinda basi tutumie ujumbe inbox ili uweze kupata somo hilo.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JIHADHARI NA DHAMBI YA WIVU/HUSUDA.

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

MWE NA HASIRA, ILA MSITENDE DHAMBI.

USHUJAA WA ROHONI HAUANGALII UZOEFU WAKO.

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest

4 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Ezra ndambuki / from Kenya
Ezra ndambuki / from Kenya
1 year ago

Kweli mwalimu humefundisha na ukatufundisha vyema kadhalika mimi nashindwa kweli kuacha Dhabi ya wivu nakunipelekea katika masengenyo,chuki,hasira n.k nisaindie mchungaji

Michael Paul
Michael Paul
1 year ago

Amina,Barikiwa sana Mtumishi wa Mungu