TAA YA MWILI NI JICHO,

TAA YA MWILI NI JICHO,

Karibu tujifunze biblia,

Mathayo 6:22  “Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru.

23  Lakini jicho lako likiwa bovu, mwili wako wote utakuwa na giza. Basi ile nuru iliyomo ndani yako ikiwa giza; si giza hilo”

Umewahi kujiuliza ni kwa namna gani “Jicho” limefananishwa na “Taa ya mwili”?

Siku zote taa ikiwa inaangaza basi nyumba yote inakuwa na Nuru na ndipo vitu vyote vilivyomo ndani vinaweza kuonekana, lakini ikizima nyumba yote inakuwa giza na hakuna kitakachoonekana.

Hali kadhalika na jicho likiwa halioni, au likiwa limefumbwa basi kinachoonekana ni giza, huwezi kuona chochote, huwezi kuona mikono yako, wala miguu yako, wala kiungo kingine chochote, huwezi kuona mbele wala nyuma wala kitu kingine chochote. Kwa ufupi unakuwa ni kipofu!. Hayo ni matokeo ya jicho kuharibika!.

Sasa Bwana Yesu analinganisha Nuru iliyopo ndani yetu na jicho.. Kwamba Nuru iliyopo ndani yetu, kazi yake ni kutuongoza njia, kama vile Jicho linaloona linavyoongoza njia na kuusaidia mwili wote kusonga mbele,  vile vile Nuru iliyopo ndani yetu kazi yake ni kuongoza maisha yetu katika njia sahihi.

Sasa Nuru iliyopo ndani yetu au inayopaswa uwe ndani yetu ni nini?.

Mathayo 5:16 “Vivyo hivyo NURU YENU NA IANGAZE mbele ya watu, wapate kuyaona MATENDO YENU MEMA, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.

Umeona hapo?.. kumbe Nuru ni “Matendo yetu mema” .. kwamba matendo yetu yanapokuwa mema, basi ni sawa na macho yanayoona!.. Kumbe matendo yetu yakiwa mabaya sisi ni sawa na vipofu!, wala hatujui tunapokwenda!…kama Bwana Yesu alivyosema katika…

Mathayo 15:14  “Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili”.

Je unataka kuona mambo yaliyopo mbele yako? na njia unayoielekea? kama ni salama?.. je! Unataka kuona hatari inayokuja na kuepukana nayo?.. Basi fanya matendo mema!!…usiende kwa waganga wala wasoma nyota wala manabii, wewe yasafishe matendo yako tu!, na utaona mambo yajayo!..

Hiyo ndio siri nyingine iliyopo nyuma ya “Matendo yetu mazuri”.. sio tu yanaupendeza moyo wa Mungu na kutupa baraka.. bali pia yanatuongoza na kutufanya tuone mambo yajayo (yaliyopo mbele yetu).

Na unayasafishaje matendo yako?.. Si kwa nguvu zako bali kwa Neema iliyopo ndani ya damu ya Yesu, ambayo hiyo inakuja kwa njia ya kutubu dhambi na kumaanisha kuziacha pamoja na kupata ubatizo sahihi..

Hapo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukupa uwezo wa wewe kufanya matendo yampendezayo Mungu, na hivyo macho yako ya kiroho yatakuwa angavu… Utakuwa na uwezo wa kuona hatari zilizopo mbele yako na kuepukana nazo, utakuwa na uwezo mkubwa wa kuona hasara zilizopo mbele yako na kuzikwepa, utakuwa unauwezo wa kuona mema yaliyopo mbele yako na kuyafuata na vile vile utakuwa na uwezo wa kuona hatari inayokufuata nyuma yako n.k

Lakini kanuni ni hiyo moja tu!..Ifanye Nuru yako (matendo yako) yaangaze!

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TWAENENDA KWA IMANI NA SI KWA KUONA.

Kama ulimwengu ujao utakuwa na watakatifu tu, sasa hao watakaotawaliwa watatoka wapi?

RUHUSU TOHARA IPITE JUU YA KARAMA YAKO.

ITII SAUTI ILIYOPO NYUMA YA KILA ISHARA YA MUNGU!

LAKINI MAKINDA WAWEZA KUYATWAA UWE NAYO.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments