Category Archive maswali na majibu

Tafsiri ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;

SWALI: Maana ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake; Naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.


JIBU: Mstari huo una vipengele viwili cha kwanza ni Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake

Na cha pili ni naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.

Tukianzana na hicho cha kwanza. Tufahamu kuwa Mungu ameiandika injili yake sio tu kwenye kitabu chake, bali pia kwenye vitu vya asili, ndio maana Yesu alitumia mifano mingi ya namna hiyo, kuzungumza nao habari zake mwenyewe. Kuanzia wakulima, mimea, wanyama, wafanya biashara, wafalme n.k.

Sasa hapa anasema yeye atunzaye mtini atakula matunda yake. Kumbe kula matunda ni “kutunza”. Usipotunza huwezi pata chochote. Ili uone kazi yako, utaiwekea mbolea, utaipalilia, utaipiga dawa n.k. Na mwisho utakuwa mvumilivu aidha miaka mitatu/ minne ukisubiri  mazao.

Halidhalika rohoni. Sisi kama watoto wa Mungu (tuliookolewa), kila mmoja wetu anao “mtini” moyoni mwake, na huo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo. Wengi wasichojua ni kwamba Kristo huanza kama kichanga, kisha huwa kijana mdogo, baadaye huwa mtu mzima, na mwisho huanza kutenda kazi zake. Kama tu alivyokuwa hapa duniani alivyoishi na Mariamu na Yusufu, hakuanza kufanya chochote pindi anazaliwa.

Hivyo usipomlea ipasavyo hutafaidi matunda yake vema. Ndio mfano wa mpanzi ambao Yesu mwenyewe aliutoa, akasema zile mbegu ziliporushwa nyingine zikaishia njiani, nyingine kwenye miamba, nyingine kwenye miiba, na nyingine kwenye udongo mzuri, moja ikazaa thelathini, nyingine sitini, nyingine mia. Akatoa ufafanuzi wake, kwamba zile zilizofanikiwa kuzaa, ni kwamba zilichangiwa na KUVUMILIA (Luka 8:15). Sasa kuvumilia nini? Kuvumilia  hatua zote tatu za mwanzo, yaani dhiki kwa ajili ya Kristo, kujiepusha na anasa, udanganyifu wa mali, na uvivu wa kulitendea kazi Neno.

Ukuaji wa kiroho tafsiri yake ni ‘Kristo kukua ndani yako’. Ukiona upo  ndani ya wokovu kwa miaka mingi, halafu huoni matunda yoyote ya wokovu wako, katika ufalme wa Mungu, tatizo linakuwa hapo, hukuwa na nafasi ya kuutunza mtini wako.

Ukiokoka, ni lazima bidii ya kusoma Neno iwe ndani yako kila siku, usiwe mvivu wa maombi, vilevile epuka maisha ya kidunia, na ubize uliopitiliza, ambao unakufanya hata nafasi ya Mungu wako unakosa. Ukizingatia hayo, baada ya kipindi Fulani utaona Kristo anavyojengeka nafsini mwako , na kukutumia.

Lakini pia sehemu ya pili inasema naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa,. Ni hekima ya kawaida, ukiwa mfanyakazi mwema kwa bwana wako, hawezi kukuchikia kinyume chake atakupa heshima yako, lakini pia na watu wengine wote wa nyumbani kwake watafanya hivyo.

Si zaidi Mungu?

Heshima hasaa kwa Mungu wako, sio kumwambia “Shikamoo” au kuomba kwa sauti ya unyenyekevu, au kuinamisha kichwa uwapo ibadani. Heshima yake hasaa ni pale unapomtumikia, unapotii agizo lake la kuwaeleza wengine habari za injili, na pale naposimama katika nafasi yako kwenye mwili wa Kristo.

Tutafute kuheshimiwa na Bwana kwa kuwashuhudia wengine injili.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MTINI, WENYE MAJANI.

Biblia imemaanisha nini kusema Nyoka atakula mavumbi?(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)Je ile habari ya mtini kunyauka inajichanganya?(Opens in a new browser tab)

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo.

SWALI: Nini maana ya mstari huu Yohana 12:35

Basi Yesu akawaambia, Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako.

JIBU:  Yesu alipokuwa duniani, alijilinganisha na Nuru ya uimwengu huu (jua), Yohana 11:9-10…Na hivyo mara kwa mara katika mafundisho yake aliwasisitiza wayahudi juu ya jambo hilo, lakini hawakulielewa.

kwa kawaida jua huwa halizimi, lakini pia huwa halitulii mahali pamoja(kwa jinsi ya kawaida). Litachomoza, litazama,.litaendelea hivyo hivyo katika mzunguko wake. Wakati linaangaza upande mmoja, upande mwingine wa dunia ni giza.

Sasa wayahudi walipomwona Kristo, wengine walimpokea, wengine walimpinga, wengine walimwonea wivu, wengine walimwita mchawi.

Lakini wote hawa, Neema bado ilikuwa juu yao. Bado Kristo alikuwa anawakusanya kama vile kuku akusanyaye vifaranga vyake chini ya mbawa zake (Luka 13:34). Yesu hakudhubutu kwenda kuhubiri kwenye mataifa mengine ambayo yalihitaji hata kumfanya mfalme, ijapokuwa walikuwa wanampinga vikali.

Sasa ndio hapa akawaambia..kwambo hili halitaendelea sana…kuna wakati pia nuru hii  mnayoiona sasa itawafikie na wengine..

ndio hapo akawaambia..

“Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako”.

Maana yake ni kuwa anawaambia aminini mapema, kwasababu nguvu hii inayowalilia mioyoni mwenu itaondoka … Mkikataa neema, mkikataa kujazwa Roho,  Kamwe hamtaweza kulishinda giza kwa nguvu zenu.

Na tunaona ni kweli, jambo hilo liliendelea kwa kipindii kifupi, baada ya Kristo kufufuka, na kupaa, injili kidogo kidogo ikaanza kutoka kwa wahayudi.ikaenda kwa watu wa mataifa yaani mimi na wewe..

Tangu ule wakati, wa mitume, mpaka leo hii inakaribia sasa miaka 2000, wayahudi bado hawajafumbuliwa macho, kwasababu wokovu ni neema kuamini. Sio utashi wa mtu.

Sasa leo hii sisi watu wa mataifa tunayo injili, lakini kanuni ya Nuru ni ileile, huzunguka. Na kwetu pia haitadumu milele. Mungu aliahidi ule mwisho unapokaribia kufika (ambao ndio huu) atawarudia tena Israeli kwa kipindi kifupi. na hivyo kwa upande wetu, hakutakuwa na neema tena ya wokovu itakayokuwa imesalia..

Warumi 11:25-26

[25]Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

[26]Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa,

Mwokozi atakuja kutoka Sayuni;

Atamtenga Yakobo na maasia yake.

Hii ni kutufunisha pia Bwana hasemi na wayahudi tu, bali na anasema sisi pia…

Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako.

Je unaenda katika nuru hiyo? Kama bado wasubiri nini. Geuka leo uoshwe dhambi zako upokee uzima wa milele, usipofanya hivyo kamwe huwezi kulishinda giza.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,

(Opens in a new browser tab)Mistari ya biblia kuhusu maombi.(Opens in a new browser tab)

AGIZO LA UTUME.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

TUJIHADHARI NA KUKANWA!.

Mathayo 10:33 “Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni”

Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia.

Hebu tulitafakari kwa upana kidogo  hili neno “kukanwa”.

Kukanwa ni ile hali ya kukataliwa na mtu unayemjua, unayetembea naye daima, uliyeweka matumaini yako kwake, mnayekubaliana  au uliye na mahusiano naye ya karibu”

Na ipo tofauti ya “kukana na kusaliti”…kwa urefu juu ya tofauti ya maneno haya mawili fungua hapa 》》Tofauti kati ya kukana na kusaliti ni ipi?

Sasa Bwana YESU anasema kuwa tukimkana mbele ya watu naye atatukana mbele ya Baba yake kule mbinguni.

Hebu tengeneza unafika kule, halafu unakanwa na yule ambaye ulikuwa unaona anatembea na wewe kila siku, anakuponya, anakulinda, ukiliita jina lake maajabu yanatokea, pepo zinatoka na miujiza mingi inafanyika.

Halafu huyu huyu ambaye ulipokuwa duniani alikuwa haonyeshi dalili ya kukukataa lakini unafika kule anakukana anasema hakujui!..ni jambo gumu sana kuamini!.

Lakini ndivyo itakavyokuwa siku ile..

Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.”

Hatuna budi kukaza mwendo daima na kila siku tukihakiki ni lipi limpendezalo Bwana (Waefeso 5:10).

Mtume Paulo ijapokuwa alikuwa na wingi wa mafunuo lakini alisema maneno haya..

1 Wakorintho 9:26 “Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;

27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Na pia alisema…

Wafilipi 3:12 “Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu.

13 Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele;

14 nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MFALME ANAKUJA.

JINA LAKO NI LA NANI?

UWEZA WA MUNGU NJE YA WAKATI.

Kulabu ni nini katika biblia?(2Wafalme 19:27)

JE UNAMHUBIRI KRISTO KATIKA KWELI YOTE?.

Rudi Nyumbani

Print this post

Bwana YESU KRISTO anatuombeaje kule juu mbinguni? (Warumi 8:34)

Swali: Maandiko yanasema KRISTO ameketi kutuombea, hata tufanyapo dhambi?


Jibu: Tafadhali soma taratibu na kwa umakini…

Warumi 8:34 “Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; TENA NDIYE ANAYETUOMBEA”.

Ni kweli Neno la Mungu linasema BWANA WETU YESU KRISTO, katika mstari huo na linazidi kututhibitishia tena katika 1Yohana 2:1.

1Yohana 2:1 “Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi TUNAYE MWOMBEZI KWA BABA, Yesu Kristo mwenye haki”

Lakini ni vizuri kuzijua lugha za kiroho na namna ya kuzitafsiri, vinginevyo itatuwia vigumu sana kuielewa biblia na hata wakati mwingine kujikuta tunaabudu sanamu kwa kushindwa kuzipambanua lugha za kiroho,

Kwamfano kuna mahali Bwana YESU alisema Mtu asipoula mwili wangu, na kuinywa damu yangu hana uzima ndani yake (soma Yohana 6:53), sasa tukiuchukua huo mstari kama ulivyo na kwenda kutafuta mwili wa Bwana kama nyama, na Damu yake kama ilivyo na kuinywa, tutakuwa tumeshindwa kutafsiri vyema lugha ya biblia, na hivyo tutakuwa tumefanana na waganga na wachawi walao nyama na kunywa damu!.

Lakini kama tukiweza kuelewa maana ya mwili wake Bwana Yesu na damu yake kuwa ni ule mkate na kile kikombe, sawasawa na (Mathayo 26:26-27) tutakuwa tumeenda sawasawa na Neno la Mungu.

SASA KWA MSINGI HUU, TUTAKUWA TAYARI KUJIFUNZA NI KWA NAMNA GANI KRISTO ANATUOMBEA KWA BABA.

Katika hiko kitabu cha Warumi mlango wa 8:34 tuliposoma kuwa KRISTO ndiye anayetuombea, hebu turudi mistari kadhaa nyuma mpaka ule mstari wa 26, tuone jambo..

 Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini ROHO MWENYEWE HUTUOMBEA KWA kuugua kusikoweza kutamkwa.

27  Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu”

Angalia hapa; Katika ule mstari wa 34 tumesoma kuwa ni BWANA YESU ndiye anayetuombea, lakini tena katika mstari wa 26 ndani ya sura hiyo hiyo, tunasoma kuwa ni ROHO MTAKATIFU ndiye anayetuombea.. Sasa swali ni yupi kati ya hawa wawili anayetuombea kwa Baba?… ni Roho Mtakatifu au ni Bwana YESU??.

Sasa jibu la swali hili ni rahisi sana na ndio tunaelekea katika kiini cha mada hii.

Jibu la swali hili tunalipata katika kitabu kile cha 2Wakorintho 3:17, sikiliza Neno la Mungu linavyosema…

2Wakorintho 3:17  “Basi Bwana ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru”.

Hapo anasema lakini “Bwana” (yaani YESU)..ndiye “Roho”(yaani Roho Mtakatifu).. kumbuka hapo Roho imeanza kwa herufi kubwa kuwakilisha Roho Mtakatifu. (Popote pale Roho inapoanza kwa herufi kubwa inamaanisha Roho wa Mungu).

Hivyo kulingana na hayo maandiko, ni sahihi kabisa kusema BWANA YESU ndiye ROHO MTAKATIFU, na Roho mtakatifu ndiye Bwana YESU.. Kwahiyo mahali popote asemapo Roho Mtakatifu ni Bwana YESU ndiye kasema..

Ndio maana utaona katika kile kitabu cha Ufunuo Mlango wa 2 na wa 3 katika jumbe za yale makanisa saba, utaona ujumbe unaanza YESU ANASEMA, na unamaliza ROHO AYAAMBIA MAKANISA, ikiwa na maana kuwa Roho ndiye huyo huyo Bwana.

Vile vile Roho Mtakatifu akiomba ni  Bwana ameomba.

Sasa swali la mwisho ambalo litahitimisha Mada hii, ni je!, Kama Bwana YESU ndiye Roho Mtakatifu, je huyo Roho Mtakatifu anatuombeaje sawasawa na huo mstari wa 26?

Roho Mtakatifu (ambaye ndiye Bwana mwenyewe) hatuombei kama sisi tunavyoombeana!.. La! Yeye anaomba ndani yetu.. Maana yake tuombapo sisi, basi yale maombi yetu anayachukua na kuyapeleka mbele za Baba katika lugha nzuri Zaidi, katika maelezo mazuri Zaidi.

Lakini si kwamba tumelala au tunacheza, au tunafanya mambo yetu mengine basi wakati huo huo yeye kule anatuombea, hapana! Hiyo si tafsiri yake kabia..

Kwa urefu jinsi Roho Mtakatifu anavyotuombea fungua hapa utapata kuelewa vizuri sana >>ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba jinsi Bwana YESU anavyotuombea ni kwajinsi ya Roho Mtakatifu, na Roho Mtakatifu anachukua yale maombi yetu na kuyapeleka kwa Baba kwa lugha kamilifu Zaidi.. Hivyo kamwe usiwaze kuwa Bwana  YESU yupo mbinguni mbele za Baba, akisali kwaajili yetu, bali ni kwa njia ya Roho wake mtakatifu ndani yetu, ndipo anapotuombea.

Kwanini tunajifunza haya?.

Ni kwasababu zipo Imani zilizoanzishwa na ibilisi mwenyewe zisemazo kuwa “hatuna haja ya kuomba, kwasababu Bwana YESU yupo mbinguni anatuombea usiku na mchana”…

Kamwe usidanganyike na hayo mafundisho kwani ni mafundisho ya Adui, ibilisi… Tusipoomba na Roho Mtakatifu hawezi kuomba, na Roho Mtakatifu asipoomba ni Bwana hajaomba.. Lakini tuombapo, Roho Mtakatifu ni kipaza sauti chetu kwa Baba..kwahiyo maombi ni lazima… (Pitia tafadhali somo la jinsi Roho Mtakatifu anavyotuombea).

Na mwisho kabisa, hakuna mtakatifu yoyote aliyekufa au aliyenyakuliwa anayetuombea… NI YESU TU PEKE YAKE, kwa NJIA YA ROHO WAKE MTAKATIFU, ndiye anayetuombea.. Hivyo Mtakatifu Mariamu, hawezi kutuombea, wala Eliya, wala Musa, wala Henoko, wala mtu mwingine yoyote aliye hai wala aliyekufa…(Hawana na hatuna hivyo vigezo).

Kwahiyo lililo kubwa na la msingi sana, ni kutafuta Roho Mtakatifu kwasababu kwa kupitia huyo ndio maombi yetu yatafika na kukubaliwa, na tena mtu asiyekuwa na Roho Mtakatifu huyo si wake kulingana na biblia (Warumi 8:9)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Roho Mtakatifu ni nani?.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Ni dhambi kutumia njia za kisasa za uzazi wa mpango.

Kwanza ni vema kufahamu uzazi wa mpango ni nini na kama ni dhambi au la!.

Uzazi wa mpango ni kuzaa kwa mpangilio ulioutaka wewe, kwamfano ukijiwekea malengo ya kuzaa watoto 30, huo ni uzazi wa mpango maadamu yalikuwa ni malengo yako, au ukijiwekea malengo ya  kuzaa mmoja maisha yako yote huo pia ni uzazi wa mpango. Kinyume chake uzao usio wa mpango, ni ule wa  kutojali idadi ya watoto utakaouzaa, wala kutojali muda wa uzaaji wako.

Lakini je! Jambo hili linaruhusiwa na Mungu?

Ukweli ni kwamba uzazi wa mpango si dhambi. Kwasababu gani?

Licha ya kwamba Mungu ameweka maagizo yake kupitia biblia takatifu, lakini pia, ameweka hekima yake kupitia mambo ya asili (1Wakorintho 11:14, Warumi 1:20), Hivyo mambo ya asili yanatufundisha pia agizo la Mungu .

Si kila wakati mama atashika ujauzito, bali upo wakati wa hatari na wakati usio wa hatari. Sasa kwa hekima huo tayari ni utaratibu Mungu kamwekea mtu, atambue majira yake, achukue tahadhari. Umeona? Kwa namna nyingine Mungu anasema, kuna majira utapata mtoto, na kuna majira hutapata mtoto. Hivyo uamuzi ni wako, ukitaka kuzingatia mazunguko huo, ni wewe, usipojali pia ni wewe.

Sasa mtu ambaye anayechagua kuzingatia mzunguko huo wa asili wa Mungu, huyo tayari yupo katika uzazi wa mpango. Na pia ni agizo la Mungu tuwe na uwezo wa kuwatunza wale wa nyumbani kwetu (1Timotheo 5:8)

Lakini je! Vipi ambao wanatumia njia za kisasa za uzazi wa mpango je na wao wapo sawa?

Tukisema njia za kisasa, ni kama zile za kutumia vidonge, kutumia sindano, kutumia vizuizi kama mipira (kwa wanaume na wanawake), kuweka kitanzi, na kuweka vipandiki/vijiti.  Zote hizi ni njia za kisasa.

Hapa ni lazima tufahamu pia lengo ni nini?. Bila shaka lengo ni lile lile moja la uzazi wa mpango kwa wanandoa, na si vinginevyo. Lakini mwanadamu ameamua kutumia njia zake za kisasa, ili kufanikisha hilo?

Je! Ni kosa?

Ili kujibu swali hilo, tufikirie pia mambo mengine ya kisasa, leo hii tuna vitu vingi vya kisasa vimebuniwa na wanadamu, kwamfano kuna kuku wa kienyeji lakini pia wapo wa kisasa, kuna mchicha wa kienyeji lakini pia ipo ya kisasa, kuna matunda ya kienyeji lakini pia yapo ya kisasa. Je! Ni dhambi kutumia vitu hivyo, kwasababu vimebuniwa na mwanadamu?

Jibu ni hapana.

Lakini vinaweza kuwa na madhara yake, kwasababu mwanadamu hawezi kuumba kitu kiukamilifu. Ndio maana asilimia kubwa ya vitu hivi vya kisasa, huwa si vizuri kiafya. Vivyo hivyo katika matumizi ya njia za kisasa za uzazi wa mpango. Yaweza isiwe dhambi kwako kutumia. Lakini madhara ya kiafya, pia waweza kukumbana nayo. Wengine hupata shida ya vizazi, wengine ugumba kabisa kulingana na njia iliyotumika, lakini wengine hawapatwi na madhara. Hivyo amani ya Kristo iamue ndani yako.

Lakini ile y asili ni bora zaidi. Ukitumia njia ya kalenda, ni salama lakini pia Mungu ametubunia hiyo, ukijizoesha kuifuatilia utaweza tu kupangilia uzazi wako.

Lakini fahamu pia uzazi wa mpango, maadamu amani ya Kristo imeamua moyoni mwako, si dhambi mbele za Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je ni halali kwa mkristo kufanya biashara ya Forex?

JE! KUBET NI DHAMBI?

Je Kutoa Mimba ni dhambi?

Rudi Nyumbani

Print this post

Misunobari ni miti gani?

Jibu: Miti ya Misunobari tunaisoma katika kitabu cha Isaya 55:13 na sehemu nyingine baadhi katika biblia.

Isaya 55:13 “Badala ya michongoma utamea MSUNOBARI, Na badala ya mibigili, mhadesi; Jambo hili litakuwa la kumpatia Bwana jina, Litakuwa ishara ya milele isiyokatiliwa mbali”

“Misonubari” ni jamii moja na miti ya “Mierezi”. Tofauti ya Msonubari na mwerezi ni kwamba Misonubari yenyewe haiwi mirefu kama mierezi, na pia ina matawi myembamba kuliko mierezi, lakini kwa sehemu kubwa inafanana kimatumizi na mierezi, ndio maana sehemu karibia zote panapotajwa miti ya Mierezi basi na Misunobari pia inatajwa..

Zekaria 11:2 “Piga yowe, MSUNOBARI, maana mwerezi umeanguka, Kwa sababu miti iliyo mizuri imeharibika; Pigeni yowe, enyi mialoni ya Bashani, Kwa maana msitu wenye nguvu umeangamia”.

Soma pia 2Wafalme 19:23,  Isaya 14:8, Isaya 37:24,  Ezekieli 27:5 na Ezekieli 31:8.

Miti ya Misonubari na Mierezi ilitumika katika ujenzi wa nyumba za thamani na ilipatikana sana katika nchi ya Lebanoni..

Sasa kwa urefu kuhusu miti ya Mierezi na matumizi yake fungua hapa >>>Mwerezi ni nini?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.

Sala ya baraka (Hesabu 6:24-26).

Fahamu maana ya Mhubiri 10:9 Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo;

FAHAMU SEHEMU NNE (4)  APANDWAPO MWAMINI.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Elewa tafsiri ya Mithali 27:22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni.

SWALI: Nini tafsiri ya Mithali 27:22

Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni pamoja na ngano; Upumbavu wake hautamtoka.


JIBU: Kama tunavyojua mtwangio na kinu ni vyombo vinavyotumika kuponda-ponda nafaka ngumu kuwa unga, au wakati mwingine mimea migumu kuwa milaini. Mfano wa kisamvu ambacho ili kiweze kulika, majani yake huwezi yapika hivyo hivyo huna budi kuyatwanga twanga kidogo, yalainike ndipo upike ule.

Na vivyo hivyo, nafaka kama mahindi, au ngano, ili viweze kulika zamani vilikuwa vinatwangwa kwenye vinu ,tofauti na sasa vinasagwa na mashine.

Sasa katika mithali hiyo, Mungu anatoa, asili ya mtu mpumbavu, kwamba hata akitwangwa, mfano wa ngano kinuni, huo upumbavu hauwezi kumtoka. Yaani njia gani ya lazima itumike bado hawezi kuacha upumbavu.

Sasa ni vizuri kufahamu, mpumbavu ni nani?

Mpumbavu kibiblia sio mtu Fulani mjinga tu hapana, bali ni Neno pana, linalolenga kuanzia

mtu anayesema hakuna Mungu (zaburi 14:1)

Mtu mgomvi (Mithali 9:13),

Mtenda maovu (Mithali 10:23)

Anayejiona njia yake ni sawa machoni pake (Mithali 12:15)

Mwenye kiburi (Mithali 14:3)

Mwenye dharau (Mithali 15:5)

Yaani kwa kifupi mpumbavu ni mtu ambaye hana Mungu ndani yake. Kwasababu dhambi ndani ya mtu ndio chanzo cha Upumbavu wote.

Sasa mtu kama huyu, hakuna kitu kinachoweza kuutoa upumbavu huo ndani yake, waweza kusema elimu, lakini ni watu wangapi wameelimika, lakini walevi, watukanaji, mashoga. Hata atwangwe vipi kinuni hawezi lainika, ikiwa hajui ni kipi sahihi kinachoweza kutoa upumbavu huo.

Kumfunga mwizi, hakumfanyi wizi au tamaa ya kuiba itoke ndani yake, mara ngapi unasikia mwizi katoka jela, karudia wizi wake, au ni kiongozi ambaye anaaminiwa awe kielelezo cha kupambana na ufisadi, lakini yeye ndio anakamatwa katika ufisadi, au teja ametolewa hospitalini karudia, tena madawa la kulevya. Ndio maana jamii ijapojaribu kudhibiti vitendo viovu, bado haviishi, bali hubadilika tu maumbile. Kwasababu mpumbavu hata atwangwe kinuni, hawezi geuka, hakuna nidhamu inayoweza mbadilisha. Huwezi acha mwenendo wake mbovu kwa semina za kijamii, au kuwekewa sheria

Je! Ni kipi kinachoweza kumgeuza?

Ni Yesu Kristo tu. Yeye ndiye aliyetiwa mafuta, na Mungu kuwaokoa watu wa Mungu na kuwafungua. Amwaminiye  na kudhamiria moyoni mwake kumfuata, basi atageuzwa moja kwa moja na kuwa mtu mwingine, huo ni uhakika.

Alisema.

Yohana 1:12  Bali wote waliompokea aliwapa UWEZO wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.

Ni ahadi yake kuwa Ukimwamini jambo la kwanza ni kukusamehe dhambi zako, kwasababu ndio jambo lililomfanya aende msalabani kwa ajili yako miaka elfu mbili iliyopita,. Unakuwa huhesabiwi dhambi tena, unahesabiwa haki bure kwa neema yake. Lakini sambamba na hilo anakupa UWEZO wa kuwa kama yeye kwa nguvu za Roho wake Mtakatifu atakayemwachia ndani yako, pindi tu unapoamini.

Na baada ya hapo utashangaa tu unavyoanza kubadilika moyoni mwako.

Zingatia tu toba ya kweli, pamoja na ubatizo sahihi (kuzamishwa katika maji mengi kwa jina la Yesu Kristo). Na kumtii yeye.

Upumbavu utakutoka.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Fahamu Maana ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.

HAUWEZI KURUKA MADARASA YA MUNGU!

Nini maana ya Mithali 9:13 Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu?

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 26:2 Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake,

SWALI: Nini maana ya Mithali 26:2

Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake, Na kama mbayuwayu katika kuruka kwake; Kadhalika laana isiyo na sababu haimpigi mtu.


JIBU: Mungu anafananisha laana isiyo na sababu na ndege wanaotanga-tanga angani.

Kama tunavyojua ndege hawa aina ya shomoro na mbayuwayu, kila siku tunawaona wanaruka angani, kila siku tunawaona wapo hari-hari, wanaonekana kama wapo buzy, lakini katika kazi zao zote, na juhudi zao zote, na mikakati yao yote, kamwe huwezi ona yanaleta madhara yoyote kwa mwanadamu. Hata kama utawaharibia viota vyao, hata kama watakauwa na hasira na wewe, huwezi ona wanamshambulia mwanadamu, kwasababu uwezo huo hawana. Huwezi wafikiria na kila wanapokuona wanakimbia. Wewe mwenyewe ukiwaona huwezi kuwaogopa, tofauti na ukimwona nyoka, utajidhatiti asikuume. Lakini ndege huvai ‘chapeo’ kichwani kujilinda naye asikuume, kwasababu hana madhara.

Ndivyo Mungu anavyotufundisha, laana zisizo na sababu, haziwezi kukupata ni kama ndege tu angani, zitapita, na kuendelea na shughuli zake, kamwe haziwezi kukupata ikiwa wewe ni mtakatifu, Hii ni kutufundisha kuwa hatupaswi kuwa waoga wa maneno ya watu  (laana) ambayo hayana sababu.

Ukiona laana imekupata basi  ujue kulikuwa na sababu nyuma yake, (lakini sio tu maneno matupu mtu anayoyatoa), mfano wa laana hizi ni ile ya Elisha aliyowalaani wale vijana 42, walioraruliwa na dubu. Kwasababu walimdhihaki. (2Wafalme 2:22-25)

Lakini mfano wa laana zisizo na sababu, ni ile Goliathi aliyomlaani Daudi kwa miungu yake, ambayo  ilikuwa ni kazi bure..

1Samweli 17:42 Hata Mfilisti alipotazama huku na huku, akamwona Daudi akamdharau; kwa kuwa ni kijana tu mwekundu, tena ana sura nzuri.  43 Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake

Ni mfano mwingine ni ile Balaamu mchawi alivyojaribu kuwalaani Israeli ikashindakana, kwasababu huwezi laani vilivyobarikiwa. (Hesabu 23)

Hata leo, ikiwa wewe umeokoka, hupaswi kuogopa, maneno yoyote iwe ya waganga au wanadamu. Kwasababu wewe tayari ni mbarikiwa. Ni ajabu sana kuona mkristo,  analia na kutetemeka, eti! Mchawi kamwambia mwaka huu hautaisha atakuwa watoto wake wote watakuwa wamekufa!!. Mzee wa mila kamwambia atapata ajali kwasababu hakutambika kijijini mwaka huu.

Mwingine anawaza, mzazi kamwambia hatafanikiwa kwasababu kaamua kuokoka. Haa! Unaogopa nini hapo?. Hizo ni laana zisizo na sababu. Ishi kwa amani zione tu kama ndege wa angani ambao hukai kuwafikiria kama watakushambulia siku moja.

Ukiokolewa na Kristo umebarikiwa, wewe sio wa kunenewa maneno ovyo ovyo tu, na yakatokea. Wewe ni uzao wa kifalme usiotetemeshwa, ngome imara isiyoangushwa. Mwamba mgumu usiogharikishwa. Yatambue mamlaka na nguvu ulizopewa ndani ya Kristo. Usiogope!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Elewa maana ya Mithali 26:2 Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake,

Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani,

Maana yake nini, Mwe na hofu wala msitende dhambi? (Zaburi 4:4)

NUHU WA SASA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Daudi alikuwa na wake wangapi, na je ni halali kuwa na wake wengi?

Swali: Napenda kujua Daudi alikuwa na wake wangapi na je na sisi tunaruhusiwa kuwa na wake wengi?


Jibu: Mfalme Daudi alikuwa na wake nane (8), waliotajwa katika biblia, ambao ni..

  1. MIKALI – Aliyekuwa binti sauli (soma 1Samweli 18:20).
  2. ABIGAILI – Aliyekuwa mke wa Nabali (Soma 1Samweli 25:39)
  3. BATH-SHEBA – Aliyekuwa Mke wa Uria na baadaye kuja kuwa mama yake Sulemani (Soma 2Samweli 12:24).
  4. AHINOAMU – Aliyekuwa mwenyeji wa mji wa Yezreeli (Soma 1Samweli 25:43 na 2Samweli 3:2).
  5. MAAKA- Aliyekuwa binti wa mfalme wa nchi ya Geshuri, aliyeitwa Talmai (Soma 2Samweli 3:3).
  6. HAGITHI- (Soma 2Samweli 3:4 na 1Wafalme 1:5).
  7. ABITALI- (Soma 2Samweli 3:4).
  8. EGLA- (Soma 2Samweli 3:5).

Wake wengine aliokuwa nao hawakutajwa katika biblia, lakini alikuwa nao wengine wengi, pamoja na masuria (nyumba ndogo), aliowatwaa kutoka katika mji wake YERUSALEMU.

2Samweli 5:12 “Akajua Daudi ya kwamba Bwana amemweka imara awe mfalme juu ya Israeli, na ufalme wake ameutukuza kwa ajili ya watu wake, Israeli.

13 Naye Daudi akazidi kujitwalia masuria na wake huko Yerusalemu baada ya kutoka Hebroni; wakazaliwa zaidi kwa Daudi wana na binti. ”

Lakini swali ni je!, kama Daudi alioa wake wengi, basi na sisi ni halali kuoa wake wengi?..

Jibu ni la!, ikiwa ni halali sisi kuoa wake wengi kwa kumwangalia Daudi, basi ni halali pia na sisi kuua kwasababu Daudi pia aliua!..lakini kama si halali kuua basi vile vile si halali kuoa wake wengi, kama Bwana wetu YESU KRISTO alivyotufundisha…

Mathayo 19:4  “Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

5  akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?

6  Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe”

Hivyo ndoa ni ya mke mmoja na mume mmoja, kwa urefu Zaidi fungua hapa >>>JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI AU KUTOA TALAKA?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Swali: Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.

NIFANYE NINI ILI NISILALE NINAPOSOMA BIBLIA.

VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.

Vyemba ni nini kama tunavyosoma katika 2Samweli 18:14

JE! UNAWEZA KUWA NA GEUKO KAMA LA DAUDI?

Rudi Nyumbani

Print this post

Wakrete ni watu gani na walikuwaje  waongo? (Tito 1:12)

Swali: Biblia inasema wakrete walikuwa ni waongo na walishuhudiwa na nabii wao, je walikuwaje waongo  (walidanganya nini), na huyo nabii wao alikuwa nani?


Jibu: Wakrete ni jamii ya watu waliokuwa wanaishi mahali paitwapo “Krete” na Krete ni kisiwa kilichokuwepo katika nchi ya Ugiriki.

Sasa Mtume Paulo alimwandikia Tito waraka huu kumpa maagizo na maelekezo machache kuhusu kanisa na viongozi (katika uteuzi).. Kwa urefu kuhusiana na kitabu hiki cha Tito na maaelekezo Paulo aliyompa Tito kwa uongozo wa Roho Mtakatifu fungua hapa >>> MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.

Lakini kwa ufupi ni kwamba tabia mojawapo waliyokuwanayo watu wa Krete, ni UONGO, Walikuwa wanasifa ya kusema Uongo katika viwango vikubwa, kiasi kwamba mpaka mtu wa kwao, ambaye ni nabii wao wenyewe aliandika kuhusiana na tabia hiyo waliyonayo waKrete ya Uongo, pamoja na ulafi na uvivu.

Biblia haijamtaja huyo Nabii ni nani, na wala haijaandika kuhusu huo waraka, lakini hapa tunaona Mtume Paulo ana unukuu…”

Tito 1:12 “..MTU WA KWAO, NABII WAO WENYEWE, AMESEMA, WAKRETE NI WAONGO SIKU ZOTE, HAYAWANI WABAYA, WALAFI WAVIVU

Sasa tukirudi katika historia, alikuwepo mwana filosofia wa KRETE aliyeitwa “EPIMEDINES”.. Huyu alikuwa ni Nabii wa mungu wa kigiriki aliyeitwa “zeu”..ambaye anatajwa katika Matendo 14:12-13.

Huyu Epimedines pamojana na kuwa alikuwa ni nabii wa mungu huyo wa kigiriki, lakini pia alikuwa ni mwandika mashairi. Moja ya shairi lake aliloliandika (ambalo aliliandika kwa kumtukuza huyo mungu wao wa kigiriki aliyeitwa zeu) lilikuwa linasema hivi..

…“Walikutengenezea kaburi, takatifu, uliye juu (zeu), Wakrete, waongo siku zote, wanyama wabaya, wavivu wa tumbo. Lakini wewe hukufa: unaishi na unakaa milele. Kwa maana ndani yako tunaishi, tunakwenda na kuwa na uhai wetu”…

Ni shari la kumtukuza mungu wao (zeu), lakini lilikuwa maarufu Krete kote kwani huyu Epimedines aliaminika na  wakrete wote kuwa ni nabii. Na Paulo kwasababu ni msomaji, aliujua huu ushairi, na hivyo katika kusisitiza dhambi ya wakrete ya Uongo kuwa ni kweli, ndio ananukuu hayo maneno ya nabii wao aliyewashuhudia kuwa ni waongo.

Lengo la Mtume Paulo si kumthibitisha nabii wao huyo La!.. bali kuthibitisha Uongo wa wakrete ambao watu wote wanauona hata walio wa Imani ya mbali… Hivyo ndio anamwonya Tito aukemee huo!.

Tunachoweza kujifunza ni kuwa UONGO ni mbaya, kwani biblia inashuhudia kuwa ibilisi ndiye baba wa Uongo, hivyo wote wadanganyi wote ni watoto wa ibilisi.

Yohana 8:44 “ Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”.

Bwana atusaidie tushinde dhambi.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WANNE WALIO WAONGO.

Mzushi ni nani kibiblia? (Tito 3:10).

UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.

Mungu anachukia kuachana (Malaki 2:16)

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Rudi Nyumbani

Print this post