Jibu: Turejee,
Ufunuo 3:14 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye ‘ALIYE AMINA’, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu”
Neno Amina maana yake ni “Na iwe hivyo”.. Neno hili kwa lugha ya kiingereza ni “Amen” Hivyo Popote panapotajwa “Amina” au “Amen” maana yake ni “na iwe hivyo”.
Sasa kwanini Bwana Yesu ajitambulishe kwa neon hilo?..
Ni kuyatofautisha maneno yake na wengine! Kwamba maneno yake ni Thabiti.
Sasa ili tuelewe vizuri, turejee pale Bwana Yesu aliposema kuwa “Mimi ndimi Njia, na Kweli na Uzima, mtu haji kwa Baba ila kwa njia yangu mimi (Yohana 14:6)”.
Tukiunyambua huo mstari vizuri, tunapata sentensi mbili 1. Yeye ndiye Njia, 2. Mtu haji kwa Baba ila kwa njia yake yeye.
Hapo Bwana anajiita kuwa yeye “Njia” anajifananisha yeye na kitu kisicho na uhai..lakini anazidi kufafanua ni kwa jinsi gani yeye ni njia kwa kuendelea kusema… “mtu hafiki kwa Baba isipokuwa kwa njia yake yeye” ikiwa na maana kuwa, kwa maneno ya Yesu na maisha yake, tukiyafuata hayo tutafika mbinguni (hayo ndio njia)… Njia zipo nyingi, lakini zote hizo hazimpeleki mtu mbinguni, isipokuwa njia ya Yesu tu! Ambayo ni Neno lake.
Sasa tukirejea tena hapo Bwana aliposema yeye ni “Amina” utaona mbele kidogo anaendelea kufafanua ni kwa namna gani yeye ni “Amina”.
Ufunuo 3:14 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, SHAHIDI ALIYE MWAMINIFU NA WA KWELI, MWANZO WA KUUMBA KWA MUNGU”.
Anasema yeye ni Amina, Shahidi aliye mwaminifu, mwanzo wa kuumbwa kwa Mungu. Maana yake maneno yake ni hakika!, akisema amesema ni lazima iwe hivyo!.. Amina yake ni amina kweli.. wengine wanazo amina lakini zinaweza zisitimie kama walivyoseme. Lakini yeye (Yesu) maneno yake ni hakika!.. akisema basi ni lazima “ITAKUWA HIVYO KAMA ALIVYOSEMA” Ndio maana anaitwa Shahidi mwaminifu.. hajawahi kusema jambo halafu lisitimie..Ni mwaminifu kwa maneno yake siku zote.
Tusome,
Marko 13:31 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.
2Wakorintho 1:20 “Maana ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena kwa hiyo katika yeye ni Amin; Mungu apate kutukuzwa kwa sisi”.
Je umemtumainia huyu ambaye Maneno yake hayapiti?. Alisema “Aaminiye na kubatizwa ataokoka (Marko 16:16)” je unadhani kutakuwa na kanuni nyingine Zaidi ya hiyo?.. Alisema wadhalimu, na wachawi, na wazinzi, na walevi hawataurithi ufalme wa mbinguni, je unadhani anadanganya??..ni kweli itakuwa hivyo!, maneno yake kamwe hayapiti, Amina yake ni amina kweli..
Je umempokea Yesu?, je umebatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu?.. Kama bado basi tafuta kufanya hivyo mapema.
Maran atha?
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.
Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharabu
Je Henoko aliyeenda na Mungu alikuwa ni mwana wa Kaini? (Mwanzo 4:16)
Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.
HUDUMA YA WALE MASHAHIDI WAWILI.
Rudi nyumbani
Print this post
Yohana 1:29 “Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!”.
Bwana Yesu sehemu nyingine anajulikana hivi kama Mwana-kondoo kufuatia tabia ya kondoo ilivyo.
Kondoo ni mnyama mpole sana na mnyenyekevu, tofauti na Mbuzi.. Kondoo Anapokatwa manyoya yake huwa hajigusi anatulia sana, na pia hawezi kujichunga mwenyewe huwa anamtegemea mchungaji asilimia mia. Tofauti na mbuzi au Ng’ombe.
Lakini pamoja na hayo kondoo aliyekomaa ambaye tayari kashaota pembe ijapokuwa ni mpole lakini kuna vipindi vichache vichache anakuwa na hasira hususani wakati wa mvua, na pia anapokutana na kondoo mwingine aliye wajinsia kama yake. Hivyo Bwana Yesu hajajifananisha na kondoo aliyekomaa, kwasababu anazo kasoro nyingi.. bali anajifananisha na kondoo mchanga, (mwana-kondoo) ambaye bado hata hajaota pembe, ambaye hawezi kupambana, aliye mnyenyekevu na mpole.
Bwana Yesu naye ni mpole mfano wa huyo.. Maandiko yanamshuhudia hivyo..
Mathayo 21:5 “Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, MPOLE, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda”.
Na yeye mwenyewe anajishuhudia hivyo katika Mathayo 11:28.
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. 29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; KWA KUWA MIMI NI MPOLE na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; 30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; KWA KUWA MIMI NI MPOLE na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.
Je umemfuata Yesu aliye mpole?..yeye anayeongea nawe kwa sauti ya upole moyoni mwako, kwamba utubu dhambi?.
Kama bado unasubiri nini?
Okoka leo na ukabatizwe na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu nawe utapata ondoleo la dhambi…na jina lako litaandikwa katika kitabu cha uzima cha mwanakondoo na utakuwa na nafasi katika mji ule, mbingu mpya na nchi mpya.
Ufunuo 21:27 “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”.
Maran atha.
Upole ni nini?
LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.
Je ni kweli Musa alikuwa mtu mpole kuliko wote duniani?
JE! UNAMPENDA BWANA?
MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;
Mwanzo 4: 16 “Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni. 17 Kaini akamjua mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Henoko; akajenga mji akauita Henoko, kwa jina la mwanawe”.
Mwanzo 4: 16 “Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni.
17 Kaini akamjua mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Henoko; akajenga mji akauita Henoko, kwa jina la mwanawe”.
Henoko aliyeenda na Mungu hakuwa mwana wa Kaini, kwasababu Uzao wa Kaini wote ulilaaniwa, na hivyo hakutoka nabii yeyote wala mtu yeyote mwenye rekodi ya kumpendeza Mungu katika huo uzao, bali uzao wote uligharikishwa na ile gharika.
Swali kama ni hivyo kwanini Henoko aonekane hapa kama ni uzao wa Kaini?.
Jibu ni kwamba Huyu Henoko anayetajwa hapa katika (Mwanzo 4:16) sio yule aliyeenda na Mungu, bali alikuwa ni Henoko mwingine, kwasababu jina hilo ‘Henoko’ hakuwa nalo mtu mmoja tu!, bali ni wengi waliitwa kwa jina hilo, kama tu leo majina yetu yanavyoweza kuwa ya watu wengine mahali pengine.
Lakini yule Henoko, aliyekuwa mtumishi wa Mungu, na aliyempendeza Mungu alitokea Uzao wa Sethi na habari zake tunazosoma katika Mwanzo mlango wa 5.
Mwanzo 5:18 “Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko. 19 Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake. 20 Siku zote za Yaredi ni miaka mia kenda na sitini na miwili, akafa. 21 Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela. 22 Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake. 23 Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano. 24 Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa”.
Mwanzo 5:18 “Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko.
19 Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.
20 Siku zote za Yaredi ni miaka mia kenda na sitini na miwili, akafa.
21 Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
22 Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake.
23 Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano.
24 Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa”.
Huyo ndio Henoko aliyeenda na Mungu, ambaye alikuwa mwana wa Yaredi wa uzao wa Sethi, na alikuwa ni mtu wa saba kutoka kwa Adamu (Yuda 1:14). Lakini yule mwingine alikuwa mwana wa Kaini.
Ni sawa Lameki aliyetajwa katika Mwanzo 4:18-19, ambaye alioa wake wawili, na yule aliyetajwa katika Mwanzo 5:28-31 ambaye alikuwa ni baba yake Nuhu… Hawa walikuwa ni Lameki wawili tofauti wenye tabia mbili tofauti, ingawa majina yao yalifanana…ndivyo ilivyo pia kwa hawa Henoko wawili tuliojifunza habari zao.
Sasa Ni jambo gani tunaloweza kujifunza kwa Henoko aliyeenda na Mungu?
Alikuwa ni mtu aliyeenda na Mungu; Maana yake Njia zake zilimpendeza Mungu mpaka kufikia hatua ya Mungu kumtwaa, na kabla ya Mungu kumtwaa biblia inasema alionyeshwa ujio wa Bwana, siku ile atakayokuja na watakatifu wake kwaajili ya vita vya Harmagedon na utawala wa miaka 1000 duniani.
Yuda 1:14 “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu, 15 ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake”
Yuda 1:14 “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,
15 ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake”
Bwana atusaidie na sisi tuwe watu wa kwenda na Bwana katika njia zake kama alivyokuwa Henoko.
Maran atha!
Je! tunapaswa kukiamini Kitabu cha Henoko?
JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?
Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?
Wanefili walikuwa ni watu gani?
EPUKA MAKUNDI ILI UTAKATIFU WAKO UDUMU!.
SWALI: Wakolosai 3:5 inamaana gani?. Tofauti kati ya tamaa mbaya na kutamani ni ipi?
JIBU: Wakolosai 3:5 Inasema..
“Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;”
Hapo anaanza kwa kusema vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi. Ikiwa na maana kuwa kuna viungo vya duniani ambavyo kazi yake kimsingi ni kutimiza mapenzi ya duniani (ya shetani). Tofuati na vile vya ki mbinguni ambavyo vinatimiza mapenzi ya Mungu. Viungo hivi sio mikono, miguu, macho, masikio au pua hapana, bali viungo vya rohoni.
Viungo vya kimbinguni vimeelezwa kwenye mstari wa 12-17. Lakini vya duniani ndio hivi vinavyozungumziwa hapa katika mstari wa 5, ambavyo tunapaswa tuviue. Navyo ni;
Uasherati unajumuisha kitendo chochote cha zinaa nje ya ndoa pamoja na mambo yafanywayo kinyume na asili. Ikiwemo Uzinzi, ufiraji, na ulawiti. Vitu hivi havipaswi vipewe nafasi kwa mtakatifu yoyote.
Uchafu ni kinyume na usafi. Mtu mchafu kimsingi anakuwa amebeba takataka katika mwili wake. Vivyo hivyo, mtu ambaye anaruhusu takataka za hii dunia zimtawale ni mchafu kiroho. Mfano wa takatakata hizi ni miziki ya kidunia, anasa, matusi, ulevi, kubeti, mazungumzo yasiyofaa, kutazama vitu visivyojenga mitandaoni, ushabiki n.k. Epuka kujitia unajisi na vitu vya ki-ulimwengu.
Kuzipa tamaa za mwili nafasi ya kukutawala. Na matokeo ya tamaa hizi mbaya kukutawala ndani yako, utaishia, ni kutazama picha chafu, muda wote kuwa na mazungumzo ya kizinzi, kuchat na jinsia tofauti na wewe kusikokuwa na sababu, kuvaa mavazi ya namna hiyo au kujiwekwa kimwili uvutie uzinzi kwa mwengine. Tabia hizi ndani yako unapaswa uziue.
Mawazo mabaya ni kinyume cha mawazo mazuri. Mtu mwenye mawazo mazuri huwaza yaliyo mazuri, ya kujenga. Lakini mwenye mawazo mabaya sikuzote ni kubomoa. Mawazo hayo ni pamoja na wivu, rushwa, uongo, wizi, uuaji, unafki, visasi,. Hivi havipaswi kuonekana ndani ya mkristo.
Kutamani kunakozungumziwa hapa sio kule kwa tamaa za mwili, hapana, bali tamaa ya mambo ya kidunia, mfano tamaa ya kuwa na mali, tamaa ya kufanana na watu wa kidunia, wanamiziki, wanamitindo n.k., na hizo ndizo zinazompelekea mtu, kugeuza vitu hivyo kuwa kama mungu wao, kuvitafuta na kuvisumbukia sikuzote .Na ndio maana mwandishi anamalizia kwa kusema “Ndiyo ibada ya sanamu” maana yake rohoni vinaonekana ni miungu kwao. Jiepushe na kutamani.
Hivyo tukifanikiwa kuviua viungo hivi, basi mwili hauwezi kuwa na matunda yoyote, kwasababu hakuna kiungo chake hata kimoja kina uhai. Lakini pia anasema,
Wakolosai 3:12 Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, 13 mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi. 14 Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu. 15 Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani. 16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu. 17 Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.
Wakolosai 3:12 Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu,
13 mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.
14 Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.
15 Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.
16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.
17 Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.
Hivyo ndivyo viungo vya kimbinguni, Tujitahidi vituvae.
Bwana akubariki.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Uasherati wa Kiroho maana yake nini?
WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.
Nini maana ya huu mstari “sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje”
WAPENDENI ADUI ZENU, WAOMBEENI WANAOWAUDHI.
Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu?
Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?
Swali: Katika kifo cha Ahabu, biblia inasema alikufa na gari lake likaenda kuoshwa katika birika ambalo wanaoga Makahaba, (1Wafalme 22:38)..hili birika walilokuwa wanaoga makahaba lilikuwaje?
Jibu: Turejee.
1Wafalme 22:37 “Hivyo akafa mfalme, akachukuliwa Samaria, wakamzika mfalme huko Samaria. 38 Wakaliosha gari penye birika la Samaria, na mbwa wakaramba damu yake; (basi ndipo walipooga makahaba); sawasawa na neno la Bwana alilolinena. 39 Na mambo yote ya Ahabu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, na nyumba ya pembe aliyoijenga, na miji yote aliyoijenga, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?”
1Wafalme 22:37 “Hivyo akafa mfalme, akachukuliwa Samaria, wakamzika mfalme huko Samaria.
38 Wakaliosha gari penye birika la Samaria, na mbwa wakaramba damu yake; (basi ndipo walipooga makahaba); sawasawa na neno la Bwana alilolinena.
39 Na mambo yote ya Ahabu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, na nyumba ya pembe aliyoijenga, na miji yote aliyoijenga, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?”
Ikumbukwe Ahabu alimwua Nabothi Myezreeli na kumdhulumu kiwanja chake, (1Wafalme 21:1-16), na baada ya kumwua ndipo unabii ukaja kupitia Eliya, kumwambia kuwa atakufa na damu yake italambwa na mbwa kama alivyomwua Nabothi (soma 1Wafalme 21:17-27).
Baada ya miaka mitatu, ndipo unabii huo unakuja kutimia, Mfalme Ahabu alikufa alipokuwa vitani na damu yake ikalambwa na mbwa mahali pale pale mbwa walipolamba damu ya Nabothi.
Lakini tunasoma tena jambo lingine lililoambatana na kifo cha Ahabu, kwamba mahali pale gari lake lilipooshwa ni mahali pia Makahaba wanapooga.
Sasa biblia haijaeleza kwa kina hili birika ambalo walikuwa wanaoga makahaba lilikuwaje. Lakini ni wazi kuwa hili halikuwa birika la kiyahudi, Kwani mabirika/ mabwawa ya kiyahudi yalikuwa yanatumika na makuhani na watu wa kawaida katika kuoga(kutawadhia) ili kujitoa unajisi.
Walawi 15: 16 “Na mtu ye yote akitokwa na shahawa yake, ndipo ataoga mwili wake wote majini, naye atakuwa najisi hata jioni”.
Soma pia Walawi 15:13, Kumbukumbu 23:10-11.
Lakini hili Birika/bwana hili ambalo makahaba walikuwa wanaoga, lilikuwa katika mji wa Samaria mtaa wa Yezreeli, ambao ndio ulikuwa kitovu cha ibada zote za mungu baali. Hivyo hili halikuwa bwawa la dini ya kiyahudi, bali lilikuwa ni bwawa la mungu baali. Huenda makahaba walikuwa wanaoga hapo kulingana na desturi zao za kibaali, kwani desturi nyingi za dini ya kibaali zilikuwa zinakaribia kufanana na za dini ya kiyahudi.. (mfano wa hizo utaona ni ile sadaka Ahabu aliyoitoa katika 1Wafalme 18:20-30).
Hivyo huenda nao pia walikuwa na desturi kama hiyo ya wayahudi ya kujiosha katika mabwawa/mabirikia.
Lakini lililo kubwa la kujifunza hapo ni kuwa Neno la Mungu kamwe halipiti.. Alisema Ahabu atakufa na damu yake italambwa na mbwa, na kweli alikufa sawasawa na neno hilo miaka mitatu baadaye, katika kifo cha aibu zaidi hata ya kile alichomuua Nabothi.
Na vile vile alisema, kuwa atarudi tena pamoja na ujira wake kulimlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo, Neno hilo halitapita, ni lazima litimie na sasa tupo katika siku za kurudi kwake, muda wowote unyakuo unatokea!
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo. 13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. 14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”
Je umeokoka kikweli kweli au bado una uvuguvugu?…Ufunuo 3:16 “Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu”.
Mathayo 24:35 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.
Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?
BIRIKA LA SILOAMU.
USIMPE NGUVU SHETANI.
Baali alikuwa nani?
Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?.
Matendo 21:25 “Lakini kwa habari za watu wa Mataifa walioamini, tuliandika na kutoa hukumu yetu ya wao kujilinda nafsi zao na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na kitu kilichosongolewa, na uasherati”
Vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu ni vyakula vyote vinavyotolewa kwa maagizo ya kishetani.Mfano wa vyakula hivyo ni vile vya kimila au vya waganga wa kienyeji.
Mfano wa vya kimilia ni vile ambavyo mtu anakula au analishwa kwa lengo la kumkinga na madhara fulani ya kiroho kama uchawi au kumpatanisha na roho fulani..
Ndio hapo utakuta mtu anaambiwa alete mbuzi, au kondoo na kisha yule kondoo achinjwe kama sadaka/kafara kwa mizimu na kisha ale sehemu ya nyama ya huyo mnyama aliyetolewa sadaka… Sasa endapo mtu huyo akila hiyo nyama au sehemu ya hiyo nyama tayari anakuwa amekula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu.
Au utakuta mtu anaenda kwa mganga wa kienyeji na yule mganga anamwambia ili tatizo lake litatulike basi alete mnyama fulani aidha mbuzi, au ng’ombe au kuku na achinjwe kama kafara na nyama yake au damu yake inywewe na mhusika.. Mtu anayekula hiyo nyama anakuwa tayari amekula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu.
Au anaweza asiambiwe alete mnyama, bali akaambiwa alete hata nafaka fulani na kisha ile nafaka ikatolewa kwa miungu na mtu akaambiwa ashiriki sehemu ya ile nafaka..sasa mtu huyo endapo akila kile chakula au sehemu ndogo ya kile chake basi anakuwa amekula chakula kichotolewa sadaka kwa sanamu.
Na mtu anayekula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu, anakuwa anajiungamanisha na ile madhabahu ya kishetani..ndivyo biblia inavyosema.
1 Wakorintho 10:19-22 “Basi niseme nini? Ya kwamba kile kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu? Au ya kwamba sanamu ni kitu?20 Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani.21 Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani.22 Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?
Hiyo ni tahadhari kwetu kuwa tujiepushe na vyakula vya namna hiyo kwani ni hatari kiroho.Lakini kama umealikwa mahali na umetengewa chakula ambacho kimetolewa sadaka kwa sanamu na ukala bila kujua kuwa kilikuwa kimetolewa sadaka kwa miungu, hapo hupaswi kuogopa kwasababu lile andiko ya kwamba “tutakula vitu vya kufisha navyo havitatudhuru (Marko16:18)” litatimia juu yako.
Lakini kama umeshajua kuwa chakula hicho ni cha miungu basi hapaswi kula kabisa..
Je umewahi kula au kulishwa chakula cha namna hiyo katika familia yenu au ukoo wenu au kwa waganga wa kienyeji?..Kama ndio basi fahamu kuwa siku ulipokula tayari ulijiungamanisha na hiyo miungu, na hivyo roho za hiyo miungu zitayaongoza maisha yako siku zote.
Hivyo suluhisho ili uweze kufunguka ni wewe kwanza kutubu mbele za Bwana kwa kumaanisha na kisha kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (Matendo 2:38) na mwisho kupokea Roho Mtakatifu..Kwa hatua hizo utakuwa umefunguliwa moja kwa moja.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.
“Kinga kilichotolewa motoni “Kinafunua nini kibiblia?
Sadaka ya Amani ilikuwaje?
Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?
HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU
SWALI: Kwanini wayahudi walimwambia Yesu kuwa hawajawahi kuwa watumwa wa mtu yeyote angali tunajua kuwa walishawahi kuwa watumwa kule Misri kwa miaka 400?
JIBU: Tusome;
Yohana 8:31 “Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; 32 tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru. 33 Wakamjibu, Sisi tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wo wote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru? 34 Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi. 35 Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote. 36 Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”.
Kauli ya hawa wayahudi haikuwa kauli ya kweli bali ya uongo uliowazi, Na lengo la majibu yao halikuwa kutafakari Yesu anayoyasema bali kumpinga tu, Na ndio maana hawakuona shida kuzungumza uongo wa wazi, kwani vitabu vyao vinaeleza walishawahi kuwa watumwa Misri,Babeli, Ashuru na sehemu kadha wa kadha walishawahi kutumikishwa na mataifa hata wakiwa katika taifa lao wenyewe.
Lakini Yesu hakulenga utumwa wa mwilini kama wao walivyodhani, bali ule wa rohoni, wa dhambi, yaani tamaa, wivu, uongo, mawazo mabaya, hasira n.k. Mambo ambayo walikuwa hawana.Lakini kwasababu lengo lao lilikuwa ni kumpinga waliendelea bado kusema uongo hata juu yake..Kwamfano ukisoma vifungu vinavyofuata katika mazungumzo yao, ule mstari wa 48 utaona wanasema kwamba yeye ni msamaria tena ana pepo. Jambo ambalo ni uongo mwingine wa makusudi. Kwani Walijua kabisa Yesu ni myahudi, na wazazi wake Yusufu, na ndugu zake wote wapo nao, mpaka kazi yao ya useremala waliyoifanya waliijua, tena wakamwita Rabi sehemu nyingine, lakini kwasababu wapo kibishi wakazusha uongo na kusema yeye ni msamaria, tena mwenye pepo.
Na ndio maana Bwana Yesu katika mazungumzo hayo hayo (Mstari wa 44) akawaeleza wazi kuwa wao ni wa Baba yao ibilisi kwasababu “hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo ”. kwasababu ya uongo wao.
Hii ni kutufundisha nini?
Tuipende kweli, Kwasababu tusipolipenda Neno la Mungu, shetani atatutumia kulipinga Neno hilo hilo kwa kushuhudia habari za uongo uliowazi na wala hututaona shida, kama ilivyokuwa kwa wayahudi hawa.
Je! Umeokoka, je! Unahakika wa maisha yako ya milele baada ya kifo? Je! Unatambua kuwa hizi ni siku za mwisho, na roho ya mpinga-Kristo inatenda kazi ndani ya watu ambao hawajaokolewa leo? Unasubiri nini usimgeukie muumba wako, tamaa za dunia zitakufikisha wapi?umefungwa Rohoni upo chini ya Utumwa wa dhambi, anayeweza kukuweka huru ni Yesu tu peke yake. Ikiwa upo tayari kuokoka leo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618 / +255789001312, kwa ajili ya mwongozo huo bure.
Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.(
WANA WA MAJOKA.
EPUKA MUHURI WA SHETANI
YULE JOKA WA ZAMANI.
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)
Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)
Jibu: Iskariote sio jina la mtu fulani, au la mzazi wa Yuda, bali ni jina lenye maana ya “Mtu wa Keriothi/ Kariote”…
Neno Iskariote ni neno la kigiriki lililoungwa na maneno mawili: “Is” ambalo maana yake ni “mwana wa” na la pili ni “Kariote”..likimaanisha mji wa Kariote au KeriothiKwahiyo ukiunganisha maneno hayo mawili maana yake ni “Mwana wa Keriothi”
Na Keriothi ni mji uliokuwepo katika Nchi la Moabu, ambayo kwasasa ni maeneo ya nchi ya Jordani.Na Wamaobu walikuwa ni watu wa mataifa, hawakuwa waIsraeli, kwa urefu kuhusu Taifa hili unaweza kufungua hapa >>> MOABU NI WAPI
Sasa swali ni je! Kwanini Yuda aitwe hivyo, na asiitwe tu Yuda! Kwanini atambulike kama Mwana wa Keriothi(Iskariote)?… kulikuwa na umuhimu gani yeye kutajwa kwa jina hilo?.
Jibu rahisi ni kwamba, alitajwa vile ili kumtofautisha na wakina Yuda wengine, kwasababu kulikuwa na watu wengi wanaoitwa Yuda ambao pia walikuwa wanafuatana na Yesu. Na Kuna mwingine alikuwa mdogo wake Yesu.
Kwa mfano utaona kuna wanafunzi wawili wa Bwana Yesu waliokuwa na majina yanayofanana..wote walikuwa wanaitwa Simoni, sasa ili kuwatofautisha ndio mmoja akajulikana kama Simoni Petro na mwingine Simoni Mkananayo. (Mathayo 10:2-4).
Vile vile kulikuwa na wanawake wengi waliomfuata Bwana walioitwa Mariamu, sasa ili kuwatofautisha hao akina Mariamu, ndipo hapo wengine wakatajwa kulingana na miji waliyotokea mfano Mariamu aliyetolewa pepo saba alijulikana kama Mariamu Magdalene, kufuatia mji aliotokea ujulikanao kama Magdalene. (Luka 8:2).
Na Yuda Iskariote aliitwa hivyo kufiatia mji ambao Baba yake alitokea (Keriothi).
Yohana 6:71 “Alimnena Yuda, mwana wa Simoni Iskariote; maana huyo ndiye atakayemsaliti; naye ni mmojawapo wa wale Thenashara”.
Soma pia Yohana 13:2, na Yohana 13:26, huenda baba yake Yuda alikuwa ni myahudi lakini mwenyeji wa Kerioth pamoja na Yuda mwanae.
Kuhusiana na mji wa Keriothi au Kariote, pitia mistari ifuatayo; Amosi 2:2, Yeremia 48:24, na Yoshua 15:25.
Na sisi Bwana anatujua majina yetu kulingana na tabia zetu.
Kutoka 33:17 “BWANA akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, nami nakujua jina lako”
Mbele za Mungu kila mtu anajulikana kwa tabia yake…fulani mcha Mungu, fulani mwombaji, fulani mkaribishaji, fulani mwizi, fulani mzinzi, fulani msengenyaji.
Bwana atujalie tujulikane kwa majina mazuri na mema mbele zake ili tupate neema.
Maran atha
NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.
ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.
JINA LA MUNGU NI LIPI?
TUUTAFUTE USEMI MMOJA. TUUJENGE MNARA WA MUNGU
Jibu: Kulikuwa na tukio zaidi ya moja la Bwana Yesu kupakwa mafuta…Tukio la kwanza ni hilo tunalolisoma katika injili tatu, (Mathayo 26:6-13 na Marko 14:3-8 na Yohana 12:1-3), ambapo biblia inaonyesha moja kwa moja kuwa ni Mariamu ndugu yake Lazaro, ndiye aliyempaka Bwana Marhamu siku sita kabla ya pasaka.
Yohana 12:1 “Basi, siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alifika Bethania, alipokuwapo Lazaro, yeye ambaye Yesu alimfufua katika wafu. 2 Basi wakamwandalia karamu huko; naye Martha akatumikia; na Lazaro alikuwa mmojawapo wa wale walioketi chakulani pamoja naye. 3 Basi Mariamu akatwaa ratli ya marhamu ya nardo safi yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu”.
Yohana 12:1 “Basi, siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alifika Bethania, alipokuwapo Lazaro, yeye ambaye Yesu alimfufua katika wafu.
2 Basi wakamwandalia karamu huko; naye Martha akatumikia; na Lazaro alikuwa mmojawapo wa wale walioketi chakulani pamoja naye.
3 Basi Mariamu akatwaa ratli ya marhamu ya nardo safi yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu”.
Lakini tukirudi katika Injili ya Luka, tunasoma tukio lingine ambalo linakaribia sana kufanana na hili la Bethania, ambapo biblia inasema alitokea mwanamke mmoja mwenye dhambi na kuanguka miguuni pake na kulia huku akimpaka mafuta.
Jibu: Turejee..
Luka 7:36 “Mtu mmoja katika Mafarisayo alimwalika ale chakula kwake; akaingia katika nyumba yake yule Farisayo, akaketi chakulani. 37 Na tazama, mwanamke MMOJA WA MJI ULE, ALIYEKUWA MWENYE DHAMBI, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya marimari yenye marhamu. 38 Akasimama nyuma karibu na miguu yake, akilia, akaanza kumdondoshea miguu machozi yake, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake, akiibusu-busu miguu yake na kuipaka yale marhamu.”
Luka 7:36 “Mtu mmoja katika Mafarisayo alimwalika ale chakula kwake; akaingia katika nyumba yake yule Farisayo, akaketi chakulani.
37 Na tazama, mwanamke MMOJA WA MJI ULE, ALIYEKUWA MWENYE DHAMBI, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya marimari yenye marhamu.
38 Akasimama nyuma karibu na miguu yake, akilia, akaanza kumdondoshea miguu machozi yake, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake, akiibusu-busu miguu yake na kuipaka yale marhamu.”
Sasa ni viashiria gani vinatuthibitishia kuwa yale yalikuwa ni matukio mawili tofauti?
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa haya ni matukio mawili tofauti, yaliyotokea kukaribiana na biblia haikumtaja Yule mwanamke wa Galilaya alikuwa ni nani?.. labda huenda alikuwa ni Yule Yule Mariamu alimpaka mara mbili, au ni mwanamke mwingine ambaye biblia haijamtaja jina lake.
Lakini hayo yote si ya muhimu sana kuyajua, (kwamba ni nani, au ni matukio mangapi) lililo la muhimu kulijua ni tendo hilo la kiimani wanawake hawa waliloyoyafanya.. sasa kujua kwa undani Siri iliyokuwepo katika kumpaka Bwana mafuta fungua hapa >>> AKAKIVUNJA KIBWETA AKAIMIMINA KICHWANI PAKE.
Bwana atubariki.
SWALI: Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani? Ni mpangalio wake upoje kulingana na mwandishi?
JIBU: Kitabu Cha Zaburi hakikuandikwa na mtu mmoja, Bali ni mjumuisho wa waandishi mbalimbali. Kitabu hiki ndio kilichoandikwa na waandishi wengi kuliko vyote kwenye biblia.
Kiliandikwa katika nyakati mbalimbali Kwa kipindi Cha miaka elfu moja na zaidi..kitabu hiki kimebeba mashahiri, maombolezo, nyimbo na maombi.
Mfalme Daudi ndiye aliyeandika Kwa sehemu kubwa kitabu hichi;
Jumla Zaburi zilizojuliakana kuwa zimeandikwa na Daudi ni 73. Lakini pia zipo nyingine 2 ambazo hazikutajwa moja Kwa moja lakini waandishi wengine katika nyaraka zao walinukuu baadhi ya maneno kwenye Zaburi, na kusema ni ya Daudi.
Ambazo ni Zaburi 2 ambayo sehemu ya maandishi hayo yanatajwa katika Matendo 4:25,
Na Zaburi 95 Waebrania 4:7
Hivyo kudhaniwa kuwa Daudi aliandika Zaburi 75;
Hizi ndio orodha ya hizo Zaburi 73 alizoziandika yeye;
3-9
11-32
34-41
51-65
68-70
86
101
103,
108-110
122
124
131
133
138-145
2. SULEMANI
Mwandishi mwingine ni Sulemani yeye aliandika Zaburi mbili tu..ambazo ni Zaburi 72 na Zaburi 127″
3. ETHANI na HEMANI
Nyingine zimeandikwa na Ethani na Hemani, Hawa ni watu ambao waliokuwa na hekima nyingi mfano wa Mfalme Sulemani, wanatajwa katika vifungu hivi;
1 Wafalme 4:30-31
30 Hekima ya Sulemani ikapita hekima ya wana wote wa mashariki, na hekima zote za Misri.31 Kwa kuwa alikuwa na hekima kuliko watu wote; kuliko Ethani Mwezrahi, na Hemani, na Kalkoli, na Darda, wana wa Maholi; zikaenea sifa zake kati ya mataifa yote yaliyozunguka.
Ethani aliandika Zaburi moja tu nayo ni Zaburi 89
Hemani pia aliandika Zaburi moja ambayo ni Zaburi 88
4. MUSA
Mwandishi mwingine alikuwa ni Musa yeye pia aliandika Zaburi 1 ambayo ni ya 90.
5. ASAFU
Zaburi nyingine 12 ziliandikwa na Asafu na familia yake.
Ambazo ni
50, 73-83
6. WANA WA KORA
Wana wa Kora, waliandika Zaburi 11
42, 44-49,84-85, 87-88
7. WASIOTAMBULIKA
Na Zaburi nyingine 48, zilizobakia hazijulikani waandishi wake.
Hivyo Kwa ufupisho ni kwamba Daudi aliandika Zaburi 73, Sulemani 2, Musa 1, Ethani 1, Hemani 1, Asafu 12, Wana wa Kora 11, wasiotambulika ni 48.
Ikiwa utapenda kupata uchauzi zaidi ya kitabu Cha Zaburi pitia link hii >> https://wingulamashahidi.org/2020/11/27/vitabu-vya-biblia-sehemu-ya-9-kitabu-cha-zaburi/
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.
Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?
NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA
JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.
MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.
Kuhimidi ni nini?(Zaburi 31:21)