YESU MNAZARETI,  ANWANI YA MSALABA.

YESU MNAZARETI,  ANWANI YA MSALABA.

Je unaijua anwani ya msalaba?…na je unajua nguvu yake? Kama bado hujaifahamu basi leo ifahamu na anza kuitumia katika maombi yako, badala ya vitendea kazi vingine kama maji,chumvi na mafuta.

Yohana 19:19 “Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI.

20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulibiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa Kiebrania, na Kirumi, na Kiyunani”

Jina la YESU WA NAZARETI ndio ANWANI ya maombi ya kila Mkristo.

Umeahi kujiuliza kwanini haijaandikwa YESU MGALILAYA, au YESU MBETHLEHEMU mji ule aliozaliwa, badala yake imeandikwa YESU MNAZARETI?..na tena kwa lugha zote tatu (3), zilizokuu za dunia.

Kuna nini katika Nazareti?

Nazareti ndio mji uliotabiriwa na manabii kubeba utambulisho wa Masihi Mkuu ajaye… hivyo huo ni mji wa UTAMBULISHO KIBIBLIA.

Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo”.

Kwahiyo tunapotaja jina la YESU na kuelekeza yule wa NAZARETI tumelenga kwenye shabaha yenyewe hivyo mashetani yanaondoka, magonjwa yanaondoka, dhambi inaisha nguvu, kwasababu ndiye Masihi halisi aliyetajwa.

Hebu tulione hili zaidi…

Wakati Bwana YESU anamtokea Sauli alipokuwa anaenda Dameski kwa ajili ya kuwaua wakristo, utaona hakujitambulisha kama YESU wa Galilaya, au YESU aliye mbinguni, badala yake alijitambulisha kama YESU Mnazaeti ijapokuwa yupo mbinguni.

Matendo 22:6 “Ikawa nilipokuwa nikisafiri, nikikaribia Dameski, wakati wa adhuhuri, ghafula nuru kuu ilitoka mbinguni, ikanimulikia pande zote.

7 Nikaanguka nchi, nikasikia sauti ikiniambia, Sauli, Sauli, mbona unaniudhi?

8 Nikajibu, Wewe u nani, Bwana? Akaniambia, MIMI NI YESU MNAZARETI, ambaye wewe unaniudhi”.

Utaona pia Mitume wa Bwana YESU waliitumia hii anwani popote walipokwenda katika huduma zao.

Petro aliitumia alipokutana na yule kiwete aliyezaliwa katika hali ile..

Matendo 3:6 “Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.

7 Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu.

8 Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akiruka-ruka, na kumsifu Mungu.

9 Watu wote wakamwona akienda, akimsifu Mungu”.

Soma pia Matendo 2:22, Matendo 3:6, Matendo 4:10, Matendo 10:38, Matendo 26:9, Marko 1:24, Marko 16:6, Marko 10:47, Luka 24:9, Yohana 1:45, utazidi kuona jambo hilo.

Na hiyo pia ndio sababu Mungu aliruhusu Pilato aandike anwani ile juu ya msalaba… “YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI”. Kwa lugha zote kuu, ikimaanisha kuwa anwani ya wokovu wa msalaba kwa mataifa yote na lugha zote ni jina la YESU WA NAZARETI.

Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”

Maana yake njili inayohubiri msalaba pasipo kuhusisha anwani ya jina la YESU ni uchawi, maombi yoyote yasiyohusisha anwani ya jina la YESU ni unashiri na ibada za sanamu.

Kama anwani hiyo ya jina la YESU WA NAZARETI hata baada ya Bwana kupaa bado anaitumia akiwa mbinguni, sisi ni akina nani tuifanye iieshe matumizi katika zama zetu?, na kuweka mafuta, chumvi, maji au majina yetu kama mbadala??.

Tumia jina la YESU, liamini jina la YESU WA NAZARETI epuka matapeli, na jina la YESU HALIUZWI, EPUKA MATAPELI!.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest

0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments