Ni halali kubatiza watoto wadogo?

Ni halali kubatiza watoto wadogo?

JIBU: Si halali kuwabatiza watoto wadogo, kwasababu, ubatizo huwa unafuata baada ya TOBA ya dhati kutoka ndani ya moyo, kwamba mtu anatubu kwanza kwa kumaanisha kuziacha kabisa dhambi zake na maisha yake ya dhambi ya zamani aliyokua anaishi na kumpa Bwana maisha yake ayaongoze kuanzia huo wakati, sasa baada ya toba kinachofuata ndio Ubatizo, kwahiyo kinachotangulia ni Toba kwanza halafu ufuate ubatizo. Na sio ubatizo kisha Toba.

Hivyo kwanini watoto wachanga hawabatizwi? ni kwasababu hiyo hiyo, bado hawajajua jema na baya, bado hawajajitambua kwamba wao ni wenye dhambi, bado hawajaujua msalaba na umuhimu wake, bado hawajaona umuhimu wa kuzaliwa mara ya pili, kwa ufupi bado hawajajitambua kwa namna yoyote, hata akilini tu ya mambo kawaida hawana, wataelewaje mambo ya rohoni?, hivyo hawawezi kubatizwa. Wao wanawekewa mikono tu ili kubarikiwa sawasawa na BWANA YESU alivyofanya kwa wale watoto waliomwendea wakati akiwa katika huduma yake.(Marko 10:16).

 Kwahiyo kufanya hivyo au ni sawa na umemchukua mtu asiyeamini na kwenda kumbatiza kwa nguvu na kusema tayari ameshabatizwa, unaona hapo utakuwa hujambatiza kwasababu ubatizo halisi unatokana na maamuzi kwanza ya mtu binafsi kwamba ametubu na kuamua kubatizwa na sio kumbatiza kwa niaba ya mwingine au kubatizwa kwa kuepuka matatizo, au kitimiza makusudi ya dhehebu lako..hapana Kufanya hivyo sio sawa kulingana na maandiko.

 Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

JE, KAMA HAUNA UBATIZO SAHIHI HAUWEZI KUWA NA ROHO MTAKATIFU?

NINI MAANA YA KIPAIMARA?..NA JE! NI JAMBO LA KIMAANDIKO?

NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!

MWANA WA MUNGU.

MELKIZEDEKI NI NANI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Huruma Bimbiga
Huruma Bimbiga
2 years ago

Usiandike kitu usichokijua. Fanya utafiti na usome Biblia kwa kina ndipo uwe na mashiko katika hoja zako. Ulivyoelezea Kipaimara na Ubatizo wa Watoto inaonesha hujafanya utafiti wala kusoma vya kutosha.