Category Archive Uncategorized @sw-tz

Biblia inaposema upanga wa mmoja ukawa kinyume na mwenzake inamaana gani? (Ezekieli 38:21)

SWALI: Je ni kitu gani hasaa kilikuwa kinatokea mpaka wafikie hatua kama ile, je! Ni utahira ulikuwa unawapata au ni nini hasaa?


JIBU: Silaha mojawapo ambayo tuona Mungu alikuwa akiitumia kuwashindania watu wake mara myingi wawapo vitani, Ni hii ya “machafuko” yaani Ni kuwavuraga maadui washindwe kuelewana na hatimaye kuanza kushambuliana wao kwa wao.

Kwamfano wa matukio kama hayo tunaweza kuyathibitisha katika habari hizi;

Wana wa Israeli Walipoizunguka Yeriko.

Waamuzi 7:22

[22]Wakazipiga zile tarumbeta mia tatu, naye BWANA akaufanya upanga wa kila mtu uwe juu ya mwenziwe, na juu ya jeshi lote, jeshi likakimbia mpaka Bethshita, kuendelea Serera, hata mpaka wa Abel-Mehola, karibu na Tabathi.

Sasa tuone ni njia zipi alikuwa anazitumia Mungu mpaka wauane wao kwa wao, watu ambao walikuwa wamekubaliana kabisa kwenda vitani?

1). Bumbuazi

Hii ni hali ya kutoweza fikiri vema, kuwa kama mtu fulani nusu aliyerukwa na akili.

Kumbukumbu la Torati 28:28

[28]BWANA atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu, na kwa bumbuazi la moyoni;

Hii ni hali yakutokuwa sawa katika ufahamu, unamwona mwenzako kuwa ndiye adui, na hatimaye vita vinaanza kabla hata ya maadui wenyewe kufika..hili ndio yamkini Bwana alilowapiga watu wa Yeriko.

Kama tu vile Mungu alivyowapiga upofu watu wa Sodoma na Gomora wasione mlango wa Lutu, vivyo hivyo hawa wanapigwa katika eneo la fikra wasifiri vema wauane, wao kwa wao.

2) Kutofautiana kauli.

Hii ni namna ambayo mnapisha usemi. Kiasi kwamba hakuna mtu wa kumsikiliza mwenzake, huyu anataka hili, Yule hili, kila mmoja haafikiani na mwenzake hatimaye chuki inatokea, matengano na mwisho kuanza kupigana wao kwa wao.

Watu wa Babeli walipigwa ‘usemi’ isipokuwa tu wao hawakufikia hatua ya kuuana, lakini ni namna tu hii hii .(Mwanzo 10)

3) Shuku na visasi

Hii ni hali ya kuwashuku wenzako kuwa ni wasaliti, hivyo ghafla kupoteza imani nao, na kuanzisha vita ili kujilinda…mfano wa hili tunaliona kwenye ile vita ya Yuda na majeshi ya wamoabu, waamoni na wameuni walipokutanika kupigana na taifa la Mungu..ghafla moabu Na amoni wakaipiga Seiri, halafu baadaye wakarudiana Wao kwa wao.

2 Mambo ya Nyakati 20:22-23

[22]Nao walipoanza kuimba na kusifu, BWANA akaweka waviziao juu ya wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, waliokuja juu ya Yuda; nao wakapigwa.

[23]Kwani wana wa Amoni na wa Moabu waliwaondokea wenyeji wa mlima Seiri kuwaulia mbali na kuwaharibu; nao walipokwisha kuwakomesha hao wakaao Seiri, wakajitia kuharibu kila mtu mwenziwe.

Hii ya visasi inatokeaje?

Labda mmoja alikuwa na chuki na mwenzake, hivyo unamlipizia kisasi, na huyu naye kaona ndugu yake kauliwa anaamka kumtetea, mara kabila hili na hili hatimaye taifa zima linaiingia katika kujiharibu.

Hivyo Mungu anapotaka kutupigania, silaha hii huwa anaitumia hata katika agano jipya hususani hapo kwenye kugonganisha ndimi.

Kwamfano mtume Paulo alipokamatwa awekwe barazani ili ahukumiwe…kwa hekima ya Roho alipewa kujua kuwa katikati ya baraza wapo mafarisayo na masadukayo. Hivyo alilolifanya ni kuwachonganisha ndimi, badala ya kumshambulia yeye..wakaanza kushambuliana wao kwa wao…hiyo ni silaha ya Bwana ambayo kwa hekima ya Roho aliitamka..

Matendo ya Mitume 23:6-7

[6]Paulo alipotambua ya kuwa sehemu moja ni Masadukayo, na sehemu ya pili ni Mafarisayo, akapaza sauti yake katika ile baraza, Ndugu zangu, mimi ni Farisayo mwana wa Farisayo; mimi ninahukumiwa kwa ajili ya tumaini la ufufuo wa wafu.

[7]Alipokwisha kunena hayo palikuwa na mashindano baina ya Mafarisayo na Masadukayo, mkutano ukafarakana.

Ni vema kufahamu aina hii ya silaha ni mbaya kuliko ile ya kushindana na adui yako.

Lakini ni vema kufahamu kuwa hata shetani hutumia silaha hii, pale tunapotoka nje ya mpango wa Mungu.

Israeli iliingia kwenye vita vya wao kwa wao, na kupelekea mauaji mengi sana…

Ni nini kilitokea?

Baadhi ya wana wa Benyamini waliendekeza dhambi ya uasherati mpaka ikafikia hatua inayokaribia ile ya sodoma Na Gomora na Israeli yote ilipopata taarifa, wakataka wawatoe hao watu wauliwe, lakini wabenyamini wakawaficha kwasababu ni watu wa kabila lao. Machafuko yakaanzia hapo, hatimaye wakauana Sana. (Waamuzi 19-21)

Hata sasa silaha hii shetani hupenda kuirusha kwenye kanisa la Mungu, watu wapoteze upendo na utakatifu ili waanze kulana na kung’atana..kwasababu ya wivu, visasi na vinyongo.

Wagalatia 5:14-15

[14]Maana torati yote imetimilika katika neno moja, nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako.

[15]Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.

Lazima tuijue hila hii ya shetani na kukataa kuipa nafasi.. Na Bwana atatuhifadhi, na matokeo itakuwa ni yeye kuleta machafuko kwa maadui zetu wanaposimama Kinyume na sisi.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

Nini maana ya huu mstari ” Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;”?(2Timotheo 4:7)

Print this post

Ipi tofauti ya Kukemea na kukaripia? (2Timotheo 4:2)

Jibu: Tuanzie ule mstari wa kwanza..

2Timotheo 4:1 “Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake;

2 lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, KARIPIA, KEMEA, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.

“Kukaripia” ni kulaani au kukosoa kosa lilolofanyika… Kwamfano mama anaweza kumkaripia mwanae kwa tabia ya Uvivu, kwamba aiache hiyo tabia, kwani ni mbaya na itamletea madhara huko mbeleni..na kukaripia mara nyingi kunaambatana na kutoa elimu,ushauri au darasa juu ya hilo kosa..

Lakini “Kukemea” inaenda mbali zaidi, kwani kunahusisha kulaani kitendo kibaya na  kutoa amri ya zuio ya jambo hilo lisiendelee kutokea… Kwamfano Mama anaweza kumkemea mwanae kwa kosa la Wizi, Kwamba tendo hilo ni kosa na lisirudiwe tena! (hiyo inakuwa ni amri, sio ombi tena wala ushauri).

Serikali inaweza kukemea vitendo vya mauaji, ubakaji  au rushwa.. kwamba vitendo hivyo ni vibaya na havipaswi kutendeka kwani ni uvunjifu wa sheria, hivyo kutofanya hayo ni amri na sio ombi wala ushauri..

Na katika Biblia, Neno la Mungu linatuagiza “Kukaripia” na “Kukemea”

2Timotheo 4:2 “lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, KARIPIA, KEMEA, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.

Zipo tabia au mienendo iliyopo kati ya watu ambayo kiuhalisia inahitaji “kukaripiwa” na mingine “kukemewa”  na Neno la Mungu linatufundisha kufanya hivyo bila kuogopa pale inapobidi. (hususani ndani ya kanisa)

Kwamfano vitendo vya wivu, uvivu, uzembe, utegeaji ndani ya kanisa, (hivyo katika hali ya uchanga vinaweza kukaripiwa tu na vikaisha), lakini vinapozidi mipaka vinapaswa vikemewe!.

Lakini vitendo vingine kama vya Ulevi, Uchawi, uzinzi, uasherati, wizi, utukanaji, fitina na vingine vinavyofanana na hivyo, havihitaji kukaripiwa bali KUKEMEWA, kwamba visiendelee kufanyanyika na hiyo inakuwa ni “Amri” na sio “Ombi wala ushauri”, maana yake mtu akiendelea kufanya hayo makusudi baada ya kuonywa mara nyingi, ni haki yake kutengwa kwa muda mpaka atakapojirekebisha ili asilichafue kanisa la Kristo.

1Wakorintho 5:11 “Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.

12 Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?

13 Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu”.

Hapo anaposema “ndugu” anamaanisha Ndugu katika Imani (mkristo), hususani Yule ambaye tayari analijua Neno la Mungu, lakini hataki kubadilika yuko vile vile ndani ya kanisa ni mlevi, au mzinzi,  au mwizi, huyo kama amekemewa na hakubali kubadilika, Biblia imetoa ruhusa ya kumtenga kwa muda, ili asilichafue kanisa..

Lengo la kumtenga ni ili atafakari na asione kanisani ni mahali pa kufanyia mchezo, au pango la wanyang’anyi.. Akifanyiwa hivyo itampa muda wa kutafakari na kama ni mtu wa kujali basi atatambua makosa yake na kujirekebisha na hivyo atarudishwa kanisani… Lakini kwa wale wengine walioingia kwenye wokovu hivi karibuni (ambao bado ni wachanga) hao hawawezi kutengwa wanapofanya makosa yale yale waliotokea nayo duniani kwani bado ni wachanga wanahitaji kufundishwa zaidi..Lakini kwa wale wengine waliokaa miaka na hawabadiliki, Neno limeruhusu kuwatenga kwa muda.

Hivyo kwa hitimisho ni lazima kukaripia mabaya, lakini pia kukeme na kuonya pia..Kwani hata Bwana Yesu Kristo huwa anatukemea pale tunapoondoka kwenye njia (Ufunuo 3:19)

Neno hilo “Kukemea” linaweza kutumika pia katika kutoa pepo, kwasababu pepo anapokuwa ndani ya mtu, huwa anamtesa Yule mtu, na si haki yake kumtesa.. hivyo tunapoamuru pepo atoke ndani ya mtu maana yake tunatoa “AMRI” sio “Ombi”.. kwamba hizo shughuli zake anazozifanya ndani ya mtu, zisimame na amtoke Yule mtu, Pepo hatulikaripii bali tunalikemea (Luka 9:42)

Bwana atubariki na kutusaidia sote.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAMBO MANNE(4) YAFANYAYO NENO LA MUNGU.

Vita vya kiroho, na mwamini Mpya.

Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)

NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.

Kumwambia mtu mwenye dhambi kuwa atakwenda kuzimu asipotubu Je! ni kuhukumu?

Print this post

FUNGUA KINYWA CHA ROHO MTAKATIFU KIHUDUMU.

Ahadi mojawapo ya Roho Mtakatifu Kwa wote waliompokea ni kupewa uwezo wa kuzungumza “ufahamu wa Mungu”, kwa vinywa vyao.

Ufahamu huu unaweza kujifunua katika maumbile mbalimbali aidha kwa kueleza habari zilizopita, au habari zijazo, au zinazoendelea sasa hivi, au kutoa maelekezo, au faraja, au neno la hekima, au maarifa, au uponyaji au baraka..Namna zote hizi kwa lugha rahisi kuitwa utabiri/ unabii.

Ukiwa kama mwamini ni vema kufahamu sehemu kubwa sana ambayo Roho Mtakatifu anaitumia kuhudumu ni katika vinywa vyetu. Ndio maana siku ile ya kwanza ya pentekoste aliposhuka, alikaa juu ya wale watu kama “ndimi za moto”. Maana yake ni kuwa huduma yake hasaa hujidhihirisha katika ndimi…ndio maana akaweka moto wake juu ya ndimi zao, lugha zao zikabadilishwa wakaanza kunena kwa lugha mpya.

Kwahiyo kinywa cha mtu aliyeokoka, ni kinywa cha Mungu duniani. Usipojifunza kukifungua kinywa chako kiufasaha, ujue hiyo ni namna mojawapo ya kumzimisha Roho Mtakatifu ndani yako.

Watu wengi hawajui kuwa kila mmoja amepewa uwezo wa kutabiri/ kuhutubu na sio suala la huduma fulani ya kinabii tu, hapana utauliza hilo lipo wapi kwenye maandiko? Soma..

Matendo 2:17 wana wenu na binti zenu watatabiri..

Lakini pia 1 Wakorintho 14:31. Inasema..

[31]Kwa maana ninyi nyote mwaweza kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe.

Kuhutubu kama ilivyotumika hapo, ni kutabiri/ kusema ufahamu wa Mungu. Jambo ambalo ni la wote sio baadhi.

Sasa unafunguaje kinywa cha Roho Mtakatifu na unafanya hivyo katika mazingira gani?

Usisubiri mpaka karama fulani ije juu yako, yaani kuonyeshwa/kufunuliwa.. hapana…kwasababu tayari una Roho Mtakatifu ndani yako anza kusema maneno yanayolanda na ahadi za Neno la Mungu, bila kufikiri- fikiri

Kwamfano…

Umepelekwa kwenye mashtaka fulani kwa ajili ya Neno. Au unatakiwa uwasilishe hoja, au ufundishe Neno, au uhubiri, au umekwenda mtaaani kushuhudia.. usianze kusema mimi nitawezaje kuhubiri, au kujieleza, sijui sheria, sijui vizuri biblia, sijui kupangilia maneno…hupaswi kufikiri hivyo. bali ukumbuke ulishapewa kinywa cha moto, tangu siku ulipoamini, wewe nenda kisha anza kuzungumza huko huko katikati ya maneno yako Roho Mtakatifu ataunganika na wewe.

Mathayo 10:18-20

[18]nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.

[19]Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.

[20]Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.

Mwingine atakuambia mimi siwezi kuomba masafa marefu ninaishiwa na maneno…ndugu hupaswi kukatisha maneno na kuacha Kuomba, ukaenda kulala.. endelea kutafakari huku ukizunguza na Mungu wako Habari mbalimbali za kwenye maandiko, na ghafla tu baada ya muda kidogo utaona unaingia kwenye mkondo fulani wa kimaombi, linatoka neno hili kwenye ufahamu linakuja neno hili la kuombea…ulikuwa umepanga uombe Saa 1, unajikuta unaomba matatu.hapo ni Roho Mtakatifu amekupa Kinywa cha kuomba..na ndani ya maombi hayo ni utabiri tosha, kwasababu sio ufahamu wako, bali ni wa Mungu ndani yako.

Vilevile jifunze kutoa sauti katika uombaji wako wa mara kwa mara..ndio tunafahamu Maombi sio sauti, hata kimoyo- moyo Mungu anasikia, lakini usimzimishe Roho..

Watu wengi wanatamani kunena kwa lugha lakini, wanazuia vinywa vyao kutoa sauti.. wanategemea vipi wanene kwa lugha mpya..unapojiachia Kwenye maombi huku unatoa sauti ni rahisi sana kujazwa Roho Na kuomba kwa lugha.

Eneo lingine labda mtu ni mgonjwa..anahitaji maombi…Fungua kinywa chako kwa ujasiri mtamkie uponyaji…unaweza kudhani ni maneno yako, hujui kumbe Ni Roho Mtakatifu Ameyaingilia na kulifanya tayari kuwa Neno la kinabii la uponyaji, na hatimaye anapokea uponyaji wake saa hiyo hiyo.

Uwapo na Watoto wako, Acha kuzungumza nao, habari za kidunia dunia tu..wawekee mikono wabariki kwa Imani kama vile Isaka alivyowabariki Yakobo na Esau na maneno yale yakawa kweli. Vivyo hivyo na wewe tabiri juu ya watoto wako unataka wawe nani wawapo watu wazima.

Uwapo kazini na marafiki zako, penda kuzungumza maneno ya ki-Mungu wakati mwingi kwasababu huko huko unabii unaweza kupita bila wewe kujijua… mwangalie kayafa

Yohana 11:49-52

[49]Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote;

[50]wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima.

[51]Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo.

[52]Wala si kwa ajili ya taifa hilo tu; lakini pamoja na hayo awakusanye watoto wa Mungu waliotawanyika, ili wawe wamoja.

Hivyo kinywa cha ni kinywa cha Roho Mtakatifu usikifunge Bali kijaze Maneno ya Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.

TULITAFUTE KWA BIDII TUNDA LA ROHO.

KWA KUWA ROHO BORA ILIKUWA NDANI YAKE.

Print this post

Ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo.

SWALI: Tukisoma Kitabu cha Waebrania tunaona mwandishi akitaja vitu viwili vya Mungu visivyoweza Kubadilika ambavyo tumepewa viwe kama nanga ya Roho, je ni vipi hivyo? Au Maana yake ni nini?

Waebrania 6:17-19

[17]Katika neno hilo Mungu, akitaka kuwaonyesha zaidi sana warithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati;

[18]ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu;

[19]tuliyo nayo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu, yaingiayo hata mle mlimo ndani ya pazia,


JIBU: Ukisoma hiyo habari vifungu vya juu na vile vinavyoendelea mbele yake. Habari inayozungumziwa pale ni ya Ibrahimu na jinsi Mungu alivyompa ahadi ya mbaraka pamoja na uzao wake. Na jinsi alivyokuja kuitimiza

Lakini tunaonyeshwa ahadi ile pekee aliyopewa, haikutosha kumfanya Ibrahimu, aamini bali Mungu Ili kumthibitishia kuwa atavipokea kweli kweli basi aliongezea Na kiapo.

Mwanzo 22:15-17

[15]Malaika wa BWANA akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni

[16]akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema BWANA, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,

[17]katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;

Kwasababu kiapo ni kifungo cha mwisho ambacho Mtu humaliza shuku zote, mashaka yote mijadala yote..

Ilimbidi Mungu aweke kiapo ijapokuwa angetimiza Ahadi zake bila kiapo. Lakini ilimbidi afanye vile ili kumpa uthabiti Ibrahimu juu ya maadhimio yake.

Hivyo mambo hayo mawili yasiyoweza Kubadilika ya Mungu ni;

1)Neno lake(ambalo lilikuja kama ahadi),

2) lakini pia Kiapo, ambacho hukata maneno yote.

Na kweli tunakuja kuona yote Mungu aliyomuahidi Ibrahimu yalitokea kama yalivyo..

Lakini Ahadi hiyo haikuishia kwa Ibrahimu, bali ilitimilizwa yote na Bwana wetu Yesu Kristo.

Ambao sisi tuliomwamini, tunaingizwa Katika ahadi hizo..alizozithibitisha Kwa kiapo kupitia Bwana wetu Yesu Kristo. Ambaye Mungu alimthibitisha kama kuhani mkuu wa milele mfano wa Melkizedeki kuhani Wa Ibrahimu (rohoni)..

Waebrania 7:21-25

[21](maana wale walifanywa makuhani pasipo kiapo; bali yeye, pamoja na kiapo, kwa yeye aliyemwambia, Bwana ameapa wala hataghairi, Wewe u kuhani milele;)

[22]basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.

[23]Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae;

[24]bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.

[25]Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.

Hivyo sisi tuna Neno la ahadi..kwamba tunaomwamini tunapokea uzima wa milele kama yeye.. Lakini pia jambo Hilo amelikolezea Kwa kiapo kuwa hatalibatilisha..Ni hakikisho kubwa sana..Haleluya!

Hivyo ni wajibu wetu kuendelea mbele kwaujasiri na bidiii katika imani na kumtumikia yeye kwasababu yupo pamoja nasi, wala kamwe hawezi kutuacha hata Iweje.

Kwasababu Neno lake ni hakika, alilotuahikikishia Na kiapo juu.

Je umempokea Bwana Yesu kwenye Maisha yako?. Fahamu kuwa hakuna tumaini lolote nje ya Kristo. Okoka leo.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Je mkristo anaruhusiwa kuoa mke wa ndugu yake aliyefariki?

Katika agano la lake, iliruhusiwa Kufanya hivyo, ikiwa mtu amefiwa na ndugu yake na hana mtoto, aliruhusiwa kwenda kumwoa mke wa ndugu yake ili amwinulie uzao, lakini halikuwa kwa lengo la kimahisiano ya kindoa kana kwamba ni wapenzi. Bali kwa kusudi tu la kumwinulia uzao.

Kumbukumbu la Torati 25:5-10

[5]Watakapoketi pamoja mtu na nduguye, mmojawapo akafa, wala hana mwana wa kiume, mke wa yule aliyekufa asiolewe nje na mgeni; nduguye yule mumewe amwingilie amweke kwake awe mkewe, kumfanyia yampasayo nduguye mumewe. 

[6]Na iwe, yule mzaliwa wa kwanza atakayemzaa, amfuate nduguye aliyekufa kwa jina lake, lisije likafutwa jina lake katika Israeli. 

[7]Na yule mtu kwamba hapendi kumtwaa mke wa nduguye, aende huyo mke wa nduguye langoni kwa wazee, akawaambie, Nduguye mume wangu yuakataa kumsimamishia nduguye jina katika Israeli, hataki kunitimizia yampasayo nduguye mume wangu. 

[8]Ndipo wamwite wazee wa mji wake waseme naye; naye akisimama na kusema, Sitaki mimi kumtwaa mwanamke huyu, 

[9]ndipo mke wa nduguye amkaribie mbele ya hao wazee, amvue kiatu chake mguuni mwake, na kumtemea mate ya uso; kisha atajibu yule mwanamke, aseme, Mume akataaye kumjengea nduguye nyumba yake na afanywe hivi. 

[10]Na jina lake katika Israeli liitwe, Nyumba ya mvuliwa kiatu. 

Halikadhalika tunapokuja kwenye agano jipya hatuoni pia agizo lolote la moja kwa moja linalokatazama ndugu kuoa mke wa ndugu yake aliyekufa…

Zaidi inasema mwanamke Yeyote anapokuwa mjane yupo huru kuolewa na ‘Yeyote’ amtakaye katika Bwana.. 

1 Wakorintho 7:39

[39]Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa mumewe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu. 

Warumi 7:3

[3]Basi wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume mwingine. 

Hiyo ikimaanisha kuwa anaweza akawa huru kuolewa hata na ndugu wa kaka yake (aliyefariki)…

Lakini lazima tufahamu kuwa si kila jambo linalohalalishwa kibiblia linaweza likafaa katika mazingira yote au majira yote, yapo mambo mengine ya kuzingatia, mfano utamaduni wa mahali fulani..

Kwasababu Biblia bado inatuambia…

1 Wakorintho 10:23

[23]Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo. 

Kwa mfano kwa wayahudi ilikuwa ni tamaduni Watu kusalimiana kwa ‘busu’ la upendo. Lakini katika mazingira ya jamii zetu jambo kama hilo huleta ukakasi, au kutoa tafsiri nyingine hata kama nia sio mbaya..ndio maana tunaishia kipeana mikono, na ikizidi sana kukumbatiana kwa jinsia tu zinazofanana.

 

Vivyo hivyo katika jambo hili, kuoa mke wa ndugu yako aliyefariki, kijamii halina munyu ndani yake.

 

Hivyo twaweza sema kijamii halikubaliki, lakini kibiblia halijakatazwa..ukiniomba mimi ushauri nitakuambia usifanye hivyo..kaoe pengine..lakini ukimwoa mke wa ndugu yako aliyekufa pia hujafanya dhambi ikiwa tu, pana makubaliano kamili katika pande zote mbili, lakini pia wewe mwenye uwe haupo katika ndoa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> 

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE.

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

https://wingulamashahidi.org/2019/08/31/bwana-yesu-alikuwa-anamaanisha-nini-kusema-marko-219%e2%80%b3walioalikwa-harusini-wawezaje-kufunga-maada

Print this post

Umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu

SWALI: Yule tajiri alimaanisha nini kumwambia Lazaro, achovye ncha ya kidole chake majini uuburudishe ulimi wake?

Luka 16:24

[24]Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.

JIBU:

Habari hiyo la Tajiri na Lazaro, Bwana Yesu aliieleza kufunua uhalisia wa jehanamu jinsi ulivyo… Na mambo ambayo mtu aliyeukataa wokovu atakutana nayo baada ya kifo.

Anaeleza jinsi yule tajiri alivyokufa katika hali ya dhambi..na hatimaye akajikuta mahali pale pa mateso, ambapo hakutana hata ndugu zake wafike, tunaona hata alipoomba mtu atokaye kwa wafu aende kuwahubiria ndugu zake akaambiwa hawatashawishwa…Ni kuonyesha kuwa mahali pale palikuwa pa mateso Sana, kiasi cha kutaka mwingine yeyote kufika.

Lakini tukio lingine tunaonyeshwa akimwomba Ibrahimu Amruhusu Lazaro achovye ncha ya kidole Chake majini amburudishe ulimi wake, nalo pia akaambiwa haiwezekaia kwasababu kuna kizuizi kikubwa Sana katikati yao.

Sasa swali linakuja tukio lile linamaana gani Je kiu kile ni halisi au ni ufunuo?.

Bwana Yesu alipokuja duniani.. aliona Dunia nzima ina Kiu kikubwa sana.. na hivyo inahitaji maji ya kuweza iponya.

Sasa maji inayohitaji sio haya ya mtoni..bali maji ya rohoni ambayo ni ya uzima, na mtu pekee awezayo kutoa hayo ni yeye mwenyewe..hakuwahi kutokea mtu aliyeweza kuyatoa.

Kama tunavyojua mwili ukikosa maji, mwishowe utakufa..Ndivyo ilivyokuwa sisi sote, hapo mwanzo kabla ya Kristo, Wote tulikuwa wafu kiroho..

Utauliza vipi kwa watakatifu wa kale kama akina Musa na Eliya?…Wale walikuwa wanaishi kwa ahadi ya Kristo, Hivyo walitii madhihirisho yake aliyokuwa akijifunua kwao kwa namna mbalimbali huku wakiiongejea ahadi kamili ya ukombozi ambayo alikuja kuikamilisha yeye mwenyewe (Yesu Kristo) alipofufuka Katika wafu..(waebrania 11)

Yeye mwenyewe Alisema..

Yohana 7:37-39

[37]Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.

[38]Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.

[39]Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.

Sasa kiu hii ni ya nini?

Ya maisha….

Tangu zamani mwanadamu amekuwa akitafuta ‘maisha’ ambayo hata sasa hajayapata…ndio maana wengi wanakimbilia kutafuta elimu, fedha na utajiri wakidhani kuwa ndio wamepata maisha, lakini hivyo vipo mbali sana na maisha …vitakufanya ule vizuri tu, unywe vizuri, ulale vizuri kama maandalizi ya heri ya kifo chako baadaye..kwasababu Haviwezi kukudumishia maisha.. vinapooza tu kiu..lakini haviondoi kiu.

Yesu amekuja kuondoa kiu.

Sasa watu Ambao watapuuzia kuyapokea maji hayo ambayo Yesu anatupa…wakifa Katika hali hiyo hiyo huko waendapo ni majuto makubwa.

Kwasababu watataka hata tone dogo la maji hawatapata…yaani kiwango kidogo tu cha neema ya uzima hawatapata…

Leo Yesu hatupi maji tu, kwa kipimo fulani bali anapanda kabisa chemchemi za maji ndani yetu Ambazo zinabubujika uzima wa milele.

Yohana 4:14

[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

Madhara ya kukosa maji ya uzima si tu baada ya kufa…hata hapa Hapa duniani.. mtu ambaye hana Kristo rohoni anajulikana kama nchi kamena matokeo yake ni kuwa makao ya mapepo yanakuwa Ndani yake hata kama hujui..

Angalia Yesu alichokisema juu ya hilo.

Mathayo 12:43-45

[43]Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.

[44]Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.

[45]Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.

Yanakwenda mahali pasipo na maji…yaani moyo ambao hauna Kristo ndani yake.

Ndugu…umeona hatari waliyonao wenye dhambi, hapa duniani na baada ya kifo?

Shetani asikupumbaze, tubu leo kwa kumpokea Bwana Yesu katika maisha yako ili upate ondoleo la dhambi zako haraka sana.

Hizi ni siku za mwisho, dunia hii inakwisha…vilevile hujui ni siku Gani utakufa…Acha kuchezea maisha yako, ukafanana na yule tajiri aliyekosa maji ya uzima angali akiwa hai.

Okoka leo..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Jehanamu ni nini?

MILANGO YA KUZIMU.

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Print this post

Yesu alimaanisha nini kusema ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’?

SWALI: Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’.

Luka 13:33

[33]Pamoja na hayo imenipasa kushika njia yangu leo na kesho na kesho kutwa; kwa kuwa haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu.


JIBU: Bwana Yesu alikuwa anaeleza asili ya mji wa Yerusalemu nyakati zote ulivyokuwa wa mauaji, mji ambao ungepaswa uwe wa kupokea manabii wa Mungu, lakini kinyume chake uligeuka mji wa kuwaua Manabii…

Sasa kusema maneno yale ni kutokana na taarifa aliyoletewa na wale mafarisayo kuwa Herode anataka kumwangamiza, hivyo aondoke pale aende mji mwingine…ndipo Bwana Yesu akawaambia ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’ yaani haipaswi nabii afe nje ya Yerusalemu…

Akimaanisha nini?

Manabii wengi wa Mungu, waliuliwa pale pale Yerusalemu hivyo hata na yeye kuangamia hapo si jambo geni, …

Na ndivyo ilivyokuwa

Mfano wa hao katika maandiko alikuwa;

Zekaria mwana wa Yehoyada (2Nyakati 24:20-21). Ambaye aliuliwa hekaluni

Mwingine ni Uria nabii (Yeremia 26:20 – 24)

Na manabii wengine wengi ambao hawajatajwa, moja kwa moja katika maandiko waliuawa Yerusalemu…ndio sababu ya Yesu kusema maneno Haya;

Mathayo 23:37-39

[37]Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!

[38]Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa. 

[39]Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana. 

Jambo hili hujirudi sasa rohoni..

Watu wote ambao wanaipinga injili mioyoni mwao leo, hata kama hawajashiriki moja kwa moja kuwarushia mawe watu wa Mungu, ni shirika moja tu na wale waliokuwa wanawaua manabii wa Bwana zamani.

Ndivyo walivyodhani mafarisayo kwamba wenyewe hawahusiki na mauaji ya manabii wa Bwana, angali wanampinga yeye waziwazi, kwa unafiki wao aliwaambia maneno haya..

Mathayo 23:29-36

[29]Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki,

[30]na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii.

[31]Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii.

[32]Kijazeni basi kipimo cha baba zenu.

[33]Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?

[34]Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji;

[35]hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu.

[36]Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.

Hii ni hatari kubwa sana kwa walio nje ya Kristo.

Mwamini Yesu leo uoshwe dhambi zako. Upokee uzima wa milele. Kwingineko si salama.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Kwanini MUNGU aangamize watoto kwenye gharika ya Nuhu?

Print this post

Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?

SWALI: Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, ni vita ya namna gani tunashindana nayo katika ulimwengu wa Roho?


JIBU: Katika biblia tunaposoma Neno “pepo”, ni vema tufahamu ufunuo wake upo katika namna mbili;

  1. Pepo: Kama malaika muasi
  2. Pepo: Kama pando la malaika muasi

Yote mawili unapaswa kufahamu, Ili ujue ni nani unashughulika naye katika vita hivyo vya kiroho.

Kwamfano, ukisoma ile waefeso 6:12 inayosema kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, bali juu ya falme na mamlaka na wakuu wa giza hili pamoja na majeshi ya mapepo wabaya.. Sasa hao wanaotajwa hasaa ni malaika waasi.

Lakini hawa malaika waasi, huwa na mapando yao, ambayo huyapanda ndani ya watu, mfano wa hayo ni magonjwa, ukichaa, ububu, udhaifu (Marko 9:25)uuaji, uchungu, majivuno, kiburi, masengenyo n.k.. na haya mapando wakati mwingine huitwa mapepo, kwasababu asili yao ni kutoka kwa hao malaika waasi.

Luka 13:11 Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.

Pepo linalozungumziwa hapo, hasaa sio yale mashetani, bali ni pando la udhaifu waliloliweka ndani ya huo mwanamke.

Hizi zote ni kazi za shetani na malaika zake duniani. Sasa mapando haya ndio tunaweza kuyaua (kwa kuyang’oa), lakini sio wale malaika waasi. Ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 15:13 Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang’olewa

Wale malaika waasi (yaani wakuu wa giza, wafalme, majeshi ya mapepo yote)hatuwezi kuwaua, kwa maombi au kwa namna yoyote, isipokuwa tayari wameshawekewa hukumu yao, siku ile ya mwisho ambapo watatupwa wote kwenye lile ziwa la moto.

Na mapando haya, Bwana Yesu alitoa maelezo yake vema, wakati ambapo adui hupandwa ndani ya mtu..

alisema.

Mathayo 13:24 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?
29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.
30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.

Kumbe wakati ambapo watu wamelala, ndipo hupanda mbegu zake. Yaani wakati ambapo watu wamekuwa walegevu kiroho ndipo shetani hupata nguvu ya kuja kupachika, mbegu zake za uharibifu, zitakazokuja kusumbua baadaye. Ndio maana ni lazima ujue kanuni mbalimbali za kumpinga shetani.

Na haya mapando, yanaweza kuwekwa kwa mtu yeyote, hata mtu aliyeokoka, anaweza kuwa nayo. Ndio maana utaona wapo watu wengine wameokoka, lakini wanasumbuliwa na mapepo, kiuhalisia, hawana malaika wale waasi ndani yao, wanayo mapando yao.

Ni sawa, na mtu ambaye anamilika chombo kama komputa, akiwa anaitumia kwa matumizi yake tu ya sikuzote, tu ambayo ni lazima, si rahisi computa hiyo kuvamiwa na virusi, lakini akianza kutembea mitandaoni, kisha kubofya, au kupakua kila kitu anachokiona ni wazi kuwa chombo hicho kipo hatarini kuvamiwa na virusi, na matokeo yake ni kuwa mfumo wote wa kumpyuta unaliwa, au kuharibifu chombo kabisa, ndio maana wanaweka ulinzi (anti-virus) sikuzote,

Vivyo hivyo na maisha ya mwanadamu yakiwa ovyo ovyo, hawezi kukwepa mapando ya mashetani ambayo yamezaa kila mahali. Mtu yeyote ambaye hajaokoka tayari kuna pepo fulani ndani yake.

Kwamfano, mwingine, labda mkristo  ameokoka, halafu akiwa kanisani, anaanza kuruhusu masengenyo kinyume na mchungaji wake, au mama-mchungaji, sasa mtu kama huyo akiwa anaendelea na tabia hiyo..matokeo yake ni kwamba pepo la uchungu litamvaa, ataanza kuwachukia viongozi wake hata bila sababu, na kuzusha vita, na uharibifu hata  wengine. Yeye atadhani ni tabia yake kumbe sio, bali pepo limeshamvaa la uchungu.

Nikupe huu ushuhuda, Kulikuwa na mama mmoja kanisa, kipindi chote ulikuwa ukikutana naye, anamzungumzia vibaya mama mchungaji wa kanisa alilokuwa mwanzo, hapo mwanzo alikuwa vizuri tu kiroho, lakini kwa jinsi siku zilivyozidi kwenda, akiendeleza chuki zake, , hali yake ilikuja kubadilika ghafla, akaomba tumwombee, tulipomwombea alilipuka mapepo, lile pepo likawa linasema “mama mchungaji” yaani asili yangu ni chuki kwa mama mchungaji, tulipolikemea likamwacha akarudia hali yake ya kawaida, akawa mtu mzuri tu.

Samsoni, alipokwenda kuwashindana na wafilisti, hakushughulika  kwanza na wafilisti, bali mashamba yao ya ngano. (mapando yao). Kwa kuyachoma moto. Vivyo hivyo na sisi ili tuyamalize nguvu haya mashetani, tuangushe ngome zao. Ni lazima fikra zetu hasaa zielekee mapando yao.

NAMNA YA KUSHINDANA VITA VYA KIROHO:

Injili:

Kwamfano kuwaangusha wakuu wa giza sio kuwatumia makombora ya moto hapo angani. Hapana, bali ni kwenda kuhubiri injili ili watu wamsikie Kristo waokoke,

Ndio maana Yesu alipowatuma wanafunzi wake wawili wawili kuhubiri waliporudi Yesu aliwaambia ‘nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme’.

Kumbe anguko lake lilikuwa katika kuhubiri na si kumtumia makombora.

Maombi:

Hii ni silaha kubwa, ya kumpinga shetani. Maombi huruhusu, utendaji kazi wa Mungu ndani ya maisha ya mwamini, usipokuwa mwombaji tarajia shetani kuyapangalia maisha yao. Yesu alituagiza tukeshe kuomba tusije ingia majaribuni.

Upendo:

Upendo hupinga, wivu, chuki, uchungu, mashindano, uzinzi, n.k. ambayo haya yote huzaliwa mahali ambapo hapana upendo. Ni lazima kila siku wewe kama mwamini kila siku ujifunze kutendea kazi upendo….ili uondoe mazingira ya mashetani kuangua mayao yao hapo.

Neno:

Ukiwa na Neno la Mungu la kutosha ndani yako, adui hawezi kukushinda. Utakumbuka kule jangwani, shetani alipojaribu kumpandia Kristo maneno ya uongo kwa kupitia biblia, yeye mwenyewe alilitumia Neno la Kweli, kumpinga. Watu wengi wanavamiwa na maroho ya upotevu, kwasababu hawana Neno la Mungu mioyoni mwao. Jifunze kusoma biblia. Ni silaha inayoitwa Upanga.

Imani:

Imani huzaa ujasiri, na ujasiri hutoa mamlaka ndani yako. Biblia huiita imani “Ngao” Shetani anapenda kutumia silaha ya woga, ili kuzimisha utendaji kazi wa Mungu mioyoni mwetu. Hatuna budi kusimama kwa utimilifu wa imani kumtumikia Mungu.

Kukemea:

Fahamu adui ni mpingamizi sikuzote, hapembelezwi, bali analazimishwa kutoka, Yesu alimkemea shetani alipotaka kumjaribu kwa kinywa cha Petro, aliyakemewa mapepo yote sugu, yaliyokuwa ndani ya watu yawatoke. Hivyo na wewe pia ukutanapo na kazi hizi za mwovu, jifunze kutumia kinywa chako, kwa mamlaka uliyopewa na Kristo kukemea haraka sana, kila pepo, au kimelea chochote cha uovu kinachozaliwa na adui.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, mashetani hawafi, lakini kazi zao zinakufa.. Hatuwaui hao, bali tunaziua kazi zao. Usipoteze muda mwingi kumrushia shetani mabovu hawezi kufa, bali tuma nguvu zako nyingi kurushia mabovu mapanda yake, kwa kanuni hizo tulizojifunza. Utawashinda kabisa kabisa.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Print this post

Ipi Tofauti ya Agano jipya na Agano la Kale?.

Ili tuelewe vizuri utofauti uliopo kati ya Agano jipya na la kale,  tutafakari mifano ya kawaida ya maisha;

Hebu tafakari juu ya Elimu ya Awali (msingi) na Elimu ya Sekondari.. Utaona ulipokuwa shule ya msingi ulijifunza mahesabu ya  kujumlisha na kuzidisha kwa kutumia vitu vya asili kama vijiti au mawe.. Lakini ulipofika sekondari ulitumia kikokotoo (yaani calculator).

Sasa mabadiliko hayo hayaifanyi elimu ya msingi kuwa batili, kwasababu tu vipo vikokotoo..La bali zinaithibitisha zaidi ile elimu ya msingi.. kwasababu kikokotoo (calculator) kinapiga mahesabu yale yale ya kujumlisha na kuzidisha kwa kasi  na ufasaha zaidi.

Ni hivyo hivyo kwa Agano la kale na Agano jipya..

Mambo yaliyopo ndani ya Agano jipya ni mambo yale yale yaliyopo ndani ya agano la kale isipokuwa katika ufunuo bora zaidi na ufasaha mkubwa zaidi..

Tafakari tena mfano huu…

Toleo la kwanza la simu yako miaka 15 iliyopita..bila shaka lilikuwa ni mfano wa  “tochi”, lenye mipaka mingi ya matumizi lakini toleo la pili la sasahivi ni “smart” ambalo unaweza kuingia internet, kupakua applications, kutazama video na hata kusikiliza nyimbo.

Kwahiyo Toleo jipya halijaja kuondoa chochote kilichopokuwepo kwenye toleo la kale, isipokuwa limeboresha zaidi vile vilivyopo na kuongeza vingine vya ziada.. maana yake Kama mtu alikuwa anasikiliza tu sauti pekee, sasa katika toleo jipya atasikika sauti pamoja na picha ya anayeongea..

Hali kadhalika kama toleo la kwanza la simu lilikuwa linachukua muda kuwaka na linahifadhi nambari za simu za watu 100 tu, basi toleo jipya litakuwa linawahi kuwaka na pia kuhifadhi namba za watu hadi 1,000.

Ni hivyo hivyo katika habari ya Agano la kale na Agano Jipya..  

Agano jipya ni toleo bora zaidi la agano la kale,  ni kitu kile kile isipokuwa kimeandikwa na kutendeka katika ubora mkubwa zaidi, na ufunuo mkubwa zaidi..

Kwamfano katika agano la kale, kafara na dhabihu zilikuwa ni za wanyama lakini tunapokuja katika Agano jipya dhabihu zimeboreshwa zaidi,  badala ya kutumika damu za wanyama, inatumika damu ya MTU, YESU KRISTO (Ambayo ni bora zaidi).

Vile vile katika Agano la kale, amri ziliandikwa kwenye mbao za mawe kule mlima Sinai, lakini katika agano jipya amri na sheria za Mungu zinaandikwa katika mioyo yetu kiufunuo zaidi.

Yeremia 31:31  “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.

32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.

33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu”.

Katika Agano la kale Uzinzi ulijulikana katika mwili tu (Kutoka 20:14) lakini katika Agano jipya uzinzi unajulikana katika mwili na roho kwa ufunuo bora zaidi (Soma Mathayo 5:28)

Katika Agano la kale uuaji ulijulikana katika mwili tu (Kutoka 20:13), lakini katika Agano jipya uuaji unajulikana katika mwili na roho kwa ufunuo bora zaidi (Soma Mathayo 5:21-22).

Katika Agano la Kale ni watu wachache tu ndio walishukiwa na Roho wa Mungu, (ambao walikuwa ni Manabii na Waamuzi) lakini katika Agano jipya watu wote wanayo fursa la kushukiwa na Roho Mtakatifu (Matendo 2:17-18).

Kwahiyo Agano  jipya ni mwendelezo wa Agano la kale katika ubora zaidi na utimilifu na ufunuo mkamilifu, ndio maana Bwana YESU alisema hakuja kuitangua torati bali kuitimiliza.

Mathayo 5:17 “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza”.

Na Roho Mtakatifu ndiye Msaidizi wetu tuliyepewa ambaye atatusaidia kulielewa Agano la Kale na Agano jipya, hivyo hatuna budi kumtafuta huyo kwa bidii zote.

Na Roho Mtakatifu ni ahadi ya Bure kwetu kwa watu wote pasipo kujali umri (Matendo 2:37-38), tukimpata Roho Mtakatifu basi tutazidi kuielewa Biblia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Orodha ya majina ya Miji ya Biblia (Agano la kale) na Sasa

Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?

MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.

NGUVU YA UPENDO WA KRISTO.

Print this post

kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi

SWALI: Nini maana ya Yeremia 31:30 “Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi”.


JIBU: Zamani za agano la kale katika taifa la Israeli, kulikuwa na usemi maarufu, unaosema “Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi”.

Kikawaida zabibu au matunda mengine yenye asidi nyingi mtu alapo , huwa meno yanatia  ganzi, lakini kamwe haiwezekani mtu mwingine akatiwa ganzi kwa ulaji wa mwingine.

Hapa Waisraeli wakiwa wanamaanisha kuwa adhabu za Mungu huwa zinatembea hata kwa kizazi cha watu,  Lakini Mungu kwa kinywa cha Yeremia anawasahihisha kuwa hilo si jambo lake..Anawaambia kila mtu ataadhibiwa sawasawa na uovu wake, wala watoto hawatauchukua uovu wa wazazi wao..Jambo ambalo alilirudia pia kwa kinywa cha Nabii Ezekieli (Ezekieli 18:20).

Lakini pia ukisoma muktadha wa vifungu hivyo, utaona anatoa unabii wa agano jipya ambalo atalifanya na watu wake kupitia Yesu Kristo, akimaanisha kuwa wokovu wake pia , utakuwa ni wa mtu binafsi, mmoja mmoja. Tusome habari yote tokea juu.

Yeremia 31: 27 Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapoipanda nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda, mbegu ya mwanadamu na mbegu ya mnyama.
28 Tena itakuwa, kwa kadiri nilivyowaangalia, ili kung’oa, na kubomoa, na kuangusha, na kuangamiza, na kutesa; kwa kadiri iyo hiyo nitawaangalia, ili kujenga, na kupanda, asema Bwana.
29 Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi.
30 Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi.
31 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

Hivyo vifungu hivi, vinatupa kutambua kuwa wajibu wa kulitunza  agano la Mungu ni la mtu binafsi, sawasawa na alivyokuja kulifunua katika agano jipya kupitia Yesu Kristo, kwamba ijapokuwa wokovu umeachiliwa kwa wote, lakini haupokelewi kijumuiya, kifamilia, au kikabila, bali kibinafsi.

Kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe. (Wagalatia 6:5)

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tafsiri ya Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.

Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?

Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?

 

 

 

Print this post