Ghafla tu wananchi waliokuwa wanakaa Yerusalemu wakati ule walishangaa JENGO hili hapa limeshakamilika, wakati wanadhani kwamba jengo ndio linaanza kujengwa, kumbe hawajui kuwa ndio linakaribia kumalizika..kwasababu wakati wa ujenzi wake wenyewe walitegemea wasikie milio ya nyundo, na mashine, na mashoka, na misumeno, na sauti za kelele nyingi za wafanyakazi, ili wajue kuwa ujenzi ndio unaanza lakini mambo hayakuwa hivyo. Kwa nje! Ilionekana kama ni kazi iliyolala tu,