Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?

Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?

JIBU: Hilo neno SHEHE lisikusumbue sana..kama tunavyofahamu lugha yetu ya Kiswahili maneno mengi yametoholewa kutoka katika lugha ya kiharabu..kwamfano neno shukrani, marhaba, salamu, sultani, sadaka, simba, msalaba,jehanamu, sheria, raisi,uasherati, hekalu, adhabu, adui, askari, lawama, dhamira,roho,damu, giza, tufani n.k. theluthi ya Lugha ya Kiswahili ni kiharabu.  (Hivyo kuna Neno shehe katika biblia pia)

Sasa kwasababu waarabu walikuwepo katika nchi yetu huku zamani zile na lugha yetu ilikuwa bado haijajitosheleza hivyo tukajikuta tunatumia maneno yao katika lugha zetu, na sio kiharabu tu hata na lugha nyingine za kigeni za watu waliotawala nchi yetu… Kwahiyo hilo neno SHEHE asili yake ni kiharabu, likiwa na maana ya Kiongozi, au mwalimu hususani anayehusiana na mambo ya kidini..na ndio maana ukisoma katika tafsiri nyingine za biblia mfano za kiingereza utaona linatumiwa neno Lords, or rulers badala yake…Neno hili unaweza ukaliona katika kitabu cha Yoshua 13:3,21, 17:7, 1Samweli 5:7,11, 6:4, Ezra 9:2 Nehemia 2:16.

Hivyo kwasababu ni Neno la kiharabu viongozi wa dini ya kiislamu walilitumia sana katika dini yao na ndio maana linaonekana kama ni neno la kiislamu lakini kiuhalisia sio..   kadhalika kama tu neno Rabi ni neno linalomaanisha mwalimu kwa kiyahudi, lakini kwasababu ni neno la lugha ya kiyahudi na linatumiwa sana na viongozi wa dini ya kiyahudi basi inachukuliwa hivyo mtu yeyote anayejiita Rabi yeye ni kiongozi wa dini ya kiyahudi lakini kiukweli sio hivyo hata kiongozi wa dini nyingine yoyote tofauti na ya kiyahudi anaweza kuitwa Rabi kwasababu maana halisi ya neno Rabi ni mwalimu…  

Kadhalika na Neno Mchungaji limezoeleka kutumiwa na viongozi wa dini ya kikristo, na halitumiwi na wengine lakini kiuhalisia hata kiongozi wa dini ya kibuddha anaweza kuitwa mchungaji.. Na ndivyo ilivyo hata kwa Neno shehe, kwahiyo pale katika maandiko neno hilo linasimama kama kiongozi wa imani wa dini husika kwa wayahudi na kwa wasio wayahudi.…  

Na pia katika agano jipya halijatumika sana hilo neno lakini badala yake yametumika maneno kama waalimu na wachungaji lakini kwa lugha ya kiharabu ndio hao hao.  

Ubarikiwe sana.


Mada zinazoendana:

KITABU CHA YASHARI KINACHOZUNGUMZIWA KATIKA 2SAMWELI 1:17-18, NI KITABU GANI?

IMANI “MAMA” NI IPI?

UNALITUMIA KWA HALALI NENO LA KWELI?.

EPUKA KUTOA UDHURU.

MUUNGANO WA DINI NA MADHEHEBU YOTE, UMEKARIBIA.

UFUNUO: MLANGO WA 11


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments