Kumwambia mtu mwenye dhambi kuwa atakwenda kuzimu asipotubu Je! ni kuhukumu?

Kumwambia mtu mwenye dhambi kuwa atakwenda kuzimu asipotubu Je! ni kuhukumu?

JIBU: Kumhukumu mtu ni kitendo cha kumshtaki mtu mbele za Mungu kuwa anakasoro Fulani zinazopaswa adhabu. Na wengi wanao hukumu wanalengo la kujihesabia wao haki, na hawana lengo la kumwonesha mtu njia bali wanalengo la kuhitimishia kwamba yeye yupo hivi au vile.au atapatwa na hili au lile, na wala hawatoi njia ya mtu kuepukana na hatari hiyo.
 
Lakini kumfundisha mtu mambo anayopaswa kujiepusha nayo sio kumhukumu, au kumweleza mtu asipofanya jambo Fulani zuri, litampata jambo Fulani baya huko sio kuhukumu. Ni sawa na Mzazi anayemwambia mwanaye usipokuwa mtiifu sasa, mambo mabaya yatakukuta katika Maisha yako huko mbeleni, hivyo hapo hajamhukumu bali amemwonya!. Haijalishi atamhorodheshea mambo mangapi mabaya au mazuri…hata kama atamworodheshea mambo 100 mabaya, hapo bado hajamhukumu, bali amempa angalizo la mambo ya mbeleni.
 
Kadhalika Biblia haijatupa sisi ruhusa ya kuhukumu, Mhukumu ni mmoja tu! Lakini imetupa ruhusa ya kuonyana kwa Neno, Wakolosai 3:16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu”.
 
2 Timotheo 4:1 “Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake;
2 lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.
3 Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti;
4 nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo”
 
Kwahiyo Unaposikia unahubiriwa kuwa wala rushwa sehemu yao ni katika ziwa la moto, hapo hujahukumiwa bali umeonywa, walevi wote, waasherati wote na waabudu sanamu hawataurithi uzima wa milele, wasipotubu! fahamu tu ni umeonywa yatakayokupata mbele endapo ukiendelea kushupaza shingo yako, Kwasababu ndivyo Biblia inavyosema katika,
 
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.
 
Hivyo usione unahubiriwa dhambi zako ukadhani kuwa unahukumiwa, kinyume chake ni unapendwa ili ugeuke usiangamie. Vile vile usiogope kumweleza mtu matokeo ya dhambi zake kwa kuogopa labda utakuwa unahukumu.
 
Mungu akubariki.

Mada zinazoendana:

KUNA HUKUMU ZA AINA NGAPI?

Biblia inasema ” HAMJUI YA KUWA MTAWAHUKUMU MALAIKA? (1Wakorintho 6:2-3) ”. je! sisi tutawahukumuje Malaika?.

NI UTHIBITISHO UPI UNAOONYESHA KUWA KUNA MBINGUNI NA KUZIMU?

KUZIMU NI MAHALI PA NAMNA GANI ,JE! HUKO WANAISHI WATU WAKIFA NA KWENDA KUPATA MATESO AU NI VINGINEVYO?

NI HALALI KUBATIZA WATOTO WADOGO?

USHUHUDA WA RICKY:


Rudi Nyumbani:

 

 

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments