WAFALME WATOKAO MAWIO YA JUA.

WAFALME WATOKAO MAWIO YA JUA.

Ufunuo 16:12 “Na huyo wa sita akakimimina kitasa chake juu ya mto ule mkubwa Frati; maji yake yakakauka, ili njia itengenezwe kwa wafalme watokao katika maawio ya jua.
13 Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.
14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.
15 (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)
16 Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har-Magedoni”
 
Tukizunguza kwa lugha ya rohoni mto au bahari sikuzote unasimama kama kizuizi, Wana wa Israeli walipokuwa wanatoka Jangwani kuingia Nchi ya Ahadi walikutana na kizuizi cha Mto Yordani..Na kwa umati mkubwa kama ule wa mamilioni ya watu, pamoja na watoto wao, na mizigo yao mikubwa na mifugo yao mingi ilikuwa ni ngumu sana kuuvuka ule mto kwa njia ya kawaida ya mitumbwi, , ingekuwa ni rahisi kama ingekuwa ni mtu mmoja au wachache tu, lakini kwa wingi ule ilikuwa ni ngumu ilihitaji kitendo cha muujiza.. Na hilo ndio lililowapa matumaini watu wa Yeriko kwasababu walijua shughuli nzito itawakuta pale, ni lazima wakwame tu, lakini tunaona muujiza Mungu alioufanya wa kuukausha mto ule wa Yordani ili watu wake wavuke, na ule ndio ilikuwa mwisho wa Taifa lijulikanalo kama Yeriko.
 
Vivyo hivyo hata sasa katika Roho ipo mito mingi ambayo inasimama kama ukingo mbele yetu , ipo mito iliyowekwa na Mungu ili kutuzuia sisi na mashambulizi ya ibilisi na vilevile ipo mito iliyopandwa na shetani ili kutuzuia sisi tusifikie malengo yetu aliyotuwekea Mungu.. Tukisoma kitabu cha Mwanzo tunaona pale Edeni Mungu alitokeza mto mmoja mkubwa kuulitilia bustani maji ambao baadaye uligawanyika na kuwa vichwa vinne wakwanza uliitwa Pishoni, wa pili uliitwa Gihoni, wa tatu uliitwa Hidekeli na wa nne ambao ndio wa mwisho uliitwa Frati. Sasa hii mto inamaana kubwa katika roho. Adamu na hawa walipoasi pale bustanini, ilianza kukauka mmoja baada ya mwingine na ilipokauka ndio ilikuwa chanzo cha shambulizi moja baada ya lingine.
 
Sasa tukirudi kwenye kitabu cha Ufunuo tunaona malaika wa sita akiamuriwa kumimina kitasa chake juu ya nchi, na alipokimimina tu maji ya mto ule wa mwisho uitwao Frati ukakauka na njia ikapatikana kwa wafalme watokao katika mawio ya jua kupanda kuleta uharibifu..Ukisoma kitabu cha Ufunuo utaona kuwa hawa wafalme wa mawio ndio watakaoenda kusababisha Vita ile ya mwisho ya Harmagedoni. Na siku hiyo Biblia inasema litakusanyika jeshi kubwa, yaani wanajeshi MILIONI 200 watahusika katika vita hii, usidhani hilo jeshi dogo, jaribu kifikiria jeshi tu la ulinzi la Tanzania linaowanajeshi kama laki na kumi hivi, piga hesabu hili la Harmagedoni ni mara ngapi ya letu..Ni zaidi ya mara 1800 ya Jeshi letu, na hapo bado silaha za vita na makombora yatakayotumika.
 
Watu walioishi miaka ya mwanzoni mwa karne ya 19/20 ilikuwa ni ngumu sana kufahamu hawa wafalme watokao mawio ya jua watakuwa ni wakina nani hasa, kwasababu mawio siku zote ni mashariki jua linapochomozea, na kwa wakati ule hakukuwa na taifa lolote la mashariki ambalo lilikuwa hata na dalili ya kuwa na nguvu kijeshi au kiuchumi au kisiasa, kwani mataifa ya Magharibi kama tunavyofahamu katika historia kama vile Ulaya na Marekani ndio yaliyokuwa yana nguvu kwa namna zote, na mataifa karibu mengine yote yalikuwa ni makoloni yao, lakini leo hii tunaona sasa ni jinsi gani huu unabii unavyokwenda kutimia kwa haraka sana, mataifa ya Mashariki ndiyo yanayozidi kuwa utiishio kwa dunia ya sasa, taifa kama Korea, Japan na China.. ni tishio kwa usalama wa dunia.. Leo hii tunaona vuguvugu na vitisho vya vita kati ya mataifa haya na yale ya magharibi lakini huo ni mwanzo tu wa uchungu…Vita hasaa vyenyewe vinakuja kuwa kati yao wakiongoza mataifa mengine duniani dhidi ya taifa teule la Mungu Israeli.
 
Na mambo hayo hayapo mbali kutokea..Inasubiriwa amri moja tu itolewe ya kukauka huu mto wa rohoni Frati, hapo ndipo matendo halisi yatafuata..Teknolojia iliyopo sasa bomu moja tu la Hydrogen likiachiwa katika mji wenye idadi ya wastani wa watu inauwa zaidi ya watu milioni 34, hilo ni moja, silaha kama hizo zipo maelfu duniani katika mataifa mbalimbali..
 
Ni wakati gani huu tunaishi?, na ni kwanini tunajikumbusha haya? Ni kwasabab mwisho wa mambo yote umekaribia, ya nini kujitumainisha na mambo yanayopita ya hapa duniani, hata ukipata ulimwengu wote Kristo akiwa mbali na wewe ni hasara siku ile ukaachwa hivyo vyote vitakusaidia nini, kama sio vilio na maombolezo.
 
Mguekie Kristo sasa kabla mlango wa neema haujafungwa.
 
Maran Atha.
 

Mada zinazoendana:

UFUNUO: Mlango wa 16.

SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!

Naomba kuuliza kati ya Unyakuo wa kanisa, Dhiki kuu, Vita vya har-magedoni, Utawala wa miaka 1000, Vita ya gogu na magogu, hukumu ya kiti cha enzi cheupe. Je, ni nini kinaanza na kingine kufuata kwa mpangilio wa matukio hayo?

UNYAKUO.

MAMBO YATAKAYOTOKEA ISRAELI SIKU ZA HIVI KARIBUNI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
2 years ago

Amina ubarikiwe mtumishi je unavitabu vya uchambuz wa kitabu cha UFUNUO na DANIEL