Category Archive Uncategorized @sw-tz

Ipi tofauti ya Baraka na Mafanikio.

Mafanikio ni kitendo cha mtu kufanikisha jambo lolote aliloliadhimia liwe baya au zuri.

Mtu aliyedhamiria kununua shamba na akanunua, mtu huyo kafanikiwa (anayo mafanikio katika eneo hilo).

Vile vile mtu aliyedhamiria kufanya mambo mabaya mfano zinaa au ufisadi na akafanikiwa kufanya hivyo pia ana mafanikio, isipokuwa mafanikio yake hayo mwisho wake ni mbaya (yatamwangamiza).

Mithali 1:32 “Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, NA KUFANIKIWA KWAO WAPUMBAVU KUTAWAANGAMIZA”.

Lakini Baraka ni thawabu pekee itokayo kwa Mungu na kumfikia mtu akiwa hapa duniani, na hakuna baraka yoyofe inayoweza kumfikia mtu mbaya,

Tofauti na mafanikio ambayo hata mtu mwovu anaweza kuyapata, kwani hata shetani ana mafanikio ja utajiri lakini hana baraka yoyote, kinyume chake amelaaniwa.

Lakini baraka za MUNGU, ni kwa watu waliokubaliwa na MUNGU, na matokeo ya baraka za MUNGU pia ni mafanikio.

Na zipo aina kuu mbili za Baraka, ambazo ni baraka za rohoni na za mwilini.

Baraka za rohoni ni zile zinazotajwa katika Waefeso 1:3..

Waefeso 1:3 “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo”

Baraka za rohoni matunda yote ya Roho mtakatifu mtu anayoyapata baada ya kupokea wokovu, ambayo tunayasoma katika Wagalatia 5:22.

Na pia zipo baraka za mwilini, haya ni mafanikio katika afya na vitu vya ulimwengu huu (yaani mali).

Kumbukumbu  28:8 “BWANA ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako”.

Watu waliompokea YESU, wanayo ahadi ya baraka zote za rohoni na mwilini, ambazo ndani yake yapo mafanikio ya kiMungu.

Kwahiyo kwa hitimisho tunachotakiwa kukitafuta zaidi ni Baraka za MUNGU, na si mafanikio tu..kwani tukizipata baraka za MUNGU ndani yake pia kuna mafanikio.

Bwana atusaidie.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

LITUKUZE JINA LA BWANA

Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe daima.

Karibu tujifunze Biblia,

Je unajua ni kitu gani kilichotukuka sana kwa MUNGU?.

Hiko si kingine zaidi ya jina lake, tangu enzi MUNGU amekuwa akijitambulisha kwa JINA na si SURA.

Ndio maana katika ile sala ya Bwana, inaanza na “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe”..ndipo maombi mengine yafuate (Mathayo 6:9).

Na hata Bwana wetu YESU aliomba hivyo..

Yohana 12:28 “Baba, ulitukuze jina lako. Basi ikaja sauti kutoka mbinguni, Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena”.

Na kila kitu tunafanya kwa jina la MUNGU na si kwa sura ya MUNGU. ( Wakolosai 3:17).

Kwahiyo jina ni kitu kilichotukuka sana, lakini sasa inapotokea jina la mtu au watu linapoinuliwa zaidi ya jina la MUNGU, ni jambo linaloleta Wivu mkubwa kwa MUNGU wetu soma (Kutoka 34:14).

Ndilo kosa walilolifanya watu wa Babeli..walipojenga mji na mnara ambao lengo lake ni kujijengea jina, na wala si kumjengea Bwana jina.

Mwanzo 11:4 “Wakasema, Haya, na tujijengee mji, na mnara, na kilele chake kifike mbinguni, TUJIFANYIE JINA; ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote

15 BWANA akashuka ili auone mji na mnara waliokuwa wakiujenga wanadamu”.

Kama umempokea YESU yoyote uyafanyayo yafanye kwa utukufu wa jina la MUNGU na si wa jina lako.

Biashara yako iwe kwa utukufu wa jina la Bwana zaidi ya utukufu wako, watu wakiona kustawi kwako walitukuze jina la MUNGU wako na si jina lako.

Watu wakiona mwenendo wako jina la MUNGU wako litukuzwe na si litukanwe.

2 Wathesalonike 1:12 “jina la Bwana wetu Yesu litukuzwe ndani yenu, nanyi ndani yake, kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo”.

Tukienda kwa kanuni hiyo tutafanikiwa sana kiroho..

Maran atha.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

ONGEZA NGUVU ZAKO ZA ROHONI.

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, na leo tutajifunza umuhimu wa kuongeza nguvu za rohoni.

Biblia inasema…

Mithali 24:10 “Ukizimia siku ya taabu, Nguvu zako ni chache”.

Kuzimia kunakozungumziwa hapo ni ile hali ya kuzidiwa mpaka kufikia hatua ya kukata tamaa kabisa.

Kwa asili watu tuliompokea YESU hatujakusudiwa kuzimia wakati wa tabu.

Kwani tabu ni kama upepo kwa tiara, tiara inapokabiliana na upepo ndivyo inavyoruka juu zaidi.

Kama umeokoka na unaona dalili ya kuzimia au kukata tamaa au kuanguka kabisa unapokutana na tabu, ni ishara tosha kuwa nguvu zako za kiroho zipo chini.

Lakini kama changamoto na tabu kwako si kitu, na wala hazikuyumbishi..bali unasimama na kuendelea mbele kwa ushindi basi wewe nguvu zako za rohoni ni kubwa, shika sana ulicho nacho.

Sasa ikiwa umejigundua kuwa nguvu zako za rohoni ni chache, nataka nikuambie kuwa inawezekana leo hii kuzipandisha, ikiwa utakubali kufanya mambo macheche yafuatayo..

Lakini kabla ya kuyatazama mambo hayo naomba kwanza tusome andiko lifuatalo..

Isaya 40:29 “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo”.

Kama huna nguvu ya kusimama, bali umechoka na unakaribia kuzimia kutokana na hali unazozipitia, hili ni neno lako.

Hapo ulipo piga magoti, omba toba ya kumaanisha kabisa,  kisha dhamiria kutafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU (Matendo 2:38), hapo Roho Mtakatifu atakuja juu yako, na kukuongezea nguvu katika nyakati zote na vipindi vyote.

Pia zingatia kuwa na vipindi vya maombi binafsi kila siku, na vipindi vya maombi ya mkesha.

Bwana akubariki.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

NAMI NITAMPA ILE NYOTA YA ASUBUHI.

Ufunuo  2:26 “Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,

27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu.

28 Nami NITAMPA ILE NYOTA YA ASUBUHI”.

Je unaijua nyota ya ASUBUHI nini?

Hii si nyingine  zaidi ya YESU KRISTO mwenyewe.

Ufunuo 22:16 “Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile NYOTA YENYE KUNG’AA YA ASUBUHI”.

Ahadi ya kuishi na YESU milele ni ahadi kuu sana, ni furaha isiyo na kifani kuishi na YESU milele.

Ni furaha isiyo na kifani kumtazama milele yeye aliyemwaga damu yake pale msalabani kwaajili yetu sisi tusiostahili.

Lakini ni hasara kubwa sana kukosa kuwa na YESU milele. Ndio maana katika kitabu hiko cha Ufunuo Bwana  YESU mwenyewe anasema yeye ashindaye atampa “Ile nyota ya asubuhi”.

Maana yake yeye atakayeshinda atakaa na YESU milele.

Je umempokea YESU?.. Je una uhakika kwamba atakaporudi utakwenda naye mawinguni na kukaa naye milele?.

1 Wathesalonike 4:17 “Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo TUTAKUWA PAMOJA NA BWANA MILELE”.

Kama bado mpe leo YESU maisha yako kwa kutubu na kubatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu.

Shalom.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Biblia ina maana gani inaposema katika kuota kwao huutia mwili unajisi?

Yuda 1:7-8

[7]Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele. 

[8]Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu. 

Maandiko hayo, yanazunguzia tabia ya watu waasi ambao wameshaijua kweli lakini wamependa kuendelea katika dhambi zao.

Hivyo katika andiko hilo anasema katika kuota kwao huutia mwili uchafu…sasa huko kuota kunakozungumziwa hapo sio ile hali ya kulala na kuota ndoto…hapana bali ni maono yao, yaani ndoto zao za jinsi watakavyokuwa baadaye, namna wanavyojiona baadaye..sasa hiyo namna ndio sio nzuri bali ni ya kujitia mwili uchafu.

Kuutia mwili uchafu ni nini?

Kuutia mwili uchafu ni ile hali ya kuruhusu matendo yote ya mwilini kukutawala…matendo hayo yanazunguziwa vema katika Wagalatia 5:19-21

[19]Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 

[20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 

[21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. 

Haya ndio watu wanayoyaona mbele yao, wanayoyawaza na kuyatazamia wakati wote, wanayoyaota yaje kutokea..

Fikra za watu wengi leo ni ili baadaye waishi kiasherati, wafanye anasa kwa pombe, ulafi, waibe..

Hii ni kutufunulia pia kunajisika sio mpaka mtu akatende jambo lenyewe bali ile kulitamania, tu au kulitarajia mbeleni…tayari ameshajinajisi.

Jiulize kuota kwako ni kupi? Kama mtoto wa Mungu, lazima tujue sisi yatupasa kuota maendeleo ya kazi ya Mungu, kuota ukuaji wa kiroho, kuota upendo, kuota kuingia mbingu mpya na nchi mpya,..namna hiyo humfanya mtu kuendelea katika utakaso.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yuda alimaanisha nini kusema “wokovu ambao ni wetu sisi sote”

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

Print this post

USIGEUKE KWA KUUME WALA KWA KUSHOTO

Kama wewe ni msafiri utakuwa umegundua kuwa nyasi zilizopo katikati ya barabara zenye vumbi huwa haziathiriwi na tairi za gari.

Utakuta barabara inapitiwa kila siku na magari yenye tairi zenye nguvu na nzito lakini katikati ya barabara utaona mstari wa nyasi, zilizo salama kabisa.

Ikifunua kuwa si kila kilichopo katikati ya hatari kipo hatarini, kuna watu wanaonekana kama wapo katikati ya changamoto na hatari nyingi lakini wapo salama, na kuna wengine wanaonekana kama wapo pembezoni (mahali salama) lakini ndio wapo hatarini.

Watu waliosimama kweli na YESU, wanaonekana ambao hawasogezi mguu wao kulia wala kushoto, ni watu wanaoonekana wamwisho kabisa duniani, na wenye wanaopotea, watu waliojikana nafsi kwaajili ya YESU ni watu wanaonekana wamepotea,

Watu wanaotukanwa, na kudhalilika kwaajili ya misimamo yao ya kiimani wanaonekana kama wamepotea lakini ukweli ni kwamba wao ni mfano wa nyasi zilizopo katikati ya barabara, hazikanyagwi wala kuathiriwa na tairi za magari.

Siku zote wanasimama na Zaburi 23..

Zaburi 23:1 “BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”

Kama ulikuwa unasuasua katika Imani na Wokovu, huu ni wakati wako wa kusimama katika njia kuu.

Simama kwa imani na tembea kwa ujasiri katikati ya njia yako ya wokovu, usisogeze mguu wako kushoto wala kulia nawe utakuwa salama, na utaona wema wa MUNGU.

Mithali 4:25-27 “Macho yako yatazame mbele.

26 Ulisawazishe pito la mguu wako, Na njia zako zote zithibitike;

27 Usigeuke kwa kuume wala kwa kushoto; Ondoa mguu wako maovuni”.

Vile vile kama bado haujaokoka, fahamu ya kuwa hizi ni siku za mwisho, na Bwana amekaribia sana kurudi. Na upendo wake kwako ni ule ule usio na mwisho,

YESU anawapenda watu wote wa kike na kiume, wakubwa kwa wadogo, walio na maradhi na wenye afya, wenye uwezo na wasio na uwezo,

Maandiko yanasema kwa moyo mtu huamini hata kupata Haki na kwa kinywa hata kupata wokovu.(Warumi 8:9-10).

Leo hii mwamini moyoni na mkiri kinywani ubadilike na kuwa mwana wa MUNGU, Mzao wa mbinguni.(1Peteo 2:9).

Bwana akubariki.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

UMEUFIKILIA MLIMA SAYUNI?.

Waebrania 12:22 “Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi”

Nyakati za Nabii Musa,Ulikuwepo mlima uliojulikana kama mlima wa Mungu, au Sinai, au mlima Horebu.

Katika mlima huo, Mungu aliposhuka hakuruhusiwa mtu mwingine kuusogelea isipokuwa Musa tu peke yake, hata mnyama aliyekaribia alikufa.

Kwani ulikuwa umejaa utukufu wa MUNGU, ulioambatana na radi na umeme na ngurumo zinazotisha.

Na kutokana na hali hiyo, ni Musa tu peke yake ndiye aliyepata kibali cha kuusogelea mlima huo na kusikia sauti ya MUNGU, wengine wote walibaki chini, kusubiria kusikia kile Musa alichoambiwa na MUNGU.

Lakini katika agano jipya, tunasoma kwamba upo mlima mfano wa huo, lakini si katika mwili bali katika roho, na mlima huo una utukufu mkubwa kuliko ule wa Sinai, Musa alioupanda.

Mlima huu wa rohoni, nao pia unaitwa Sinai, ambao umejaa malaika wa Mungu, na wenye utukufu mwingi.

Tofauti na mlima ule wa kwanza wa mwilini ambao ni Musa tu ndiye aliyeruhusiwa kuupanda, mlima huu wa rohoni unapandwa na mtu yeyote aliye ndani ya imani kamili ya YESU KRISTO.

Waebrania 12:21 “Na hayo yaliyoonekana jinsi yalivyokuwa ya kutisha, hata Musa akasema, Nimeshikwa na hofu na kutetemeka.

Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi”,

Na faida za kuupanda mlima huu (Sinai ya rohoni) ni kwamba mtu atapata nafasi ya kumkaribia MUNGU zaidi na kumsikia MUNGU zaidi kuliko Musa alivyomsikia kule Sinai,

Pia atashuka na utukufu mkuu zaidi ya ule Musa aliokuwa nao aliposhuka hata uso wake ukang’aa.

Swali linarudi je wewe ni miongoni mwa watu walioufikia huo mlima wa MUNGU?.

Lakini labda utajiuliza pia mtu ataufikiaje huo mlima?..

Biblia imetupa majibu..

Zaburi 24:3 “Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?

4 Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila.

5 Atapokea baraka kwa BWANA, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake”.

Sasa tunapataje mikono safi na mioyo myeupe, itakayotufanya tustahili kufika katika mlima huo mtakatifu?.

Njia ni moja tu, kumwamini Bwana YESU, Kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha na kupokea Roho Mtakatifu, na kila siku kuishi maisha  ya utakatifu.

Kwa njia hiyo basi tutaweza kufikia kilele cha baraka, kwani ni Neema kuu tulipewa ya sisi kuufikia mlima wenye utukufu zaidi ya ule Musa aliopanda.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

SHIKA JEMBE NA SURURU CHIMBA MAHANDAKI. 

2 Wafalme 3:16-17

[16]Akasema, BWANA asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki. 

[17]Kwa kuwa BWANA asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu. 

Ilifika wakati wana wa Israeli, walikwama, baada ya kuona wapo katika eneo ambalo ni kame kupita kiasi, na hawana msaada, nguvu zimewaishia maadui zao wapo karibu kuwaangamiza..

Wakalia sana, Lakini baadaye wakapata akili ya kumlingana Mungu kwa kuulizia kupitia nabii wake Elisha. Lakini maagizo waliyopewa hayakuwa bado marahisi sana, kama walivyotegemea.

Hawakufanyiwa muujiza wa maji kutokea mwambani kama kipindi cha Musa, au mvua kushuka mbinguni…bali waliambiwa wachimbe mahandaki…yaani mashimo makubwa sana…pale jangwani..

Fikiri umechoka umeishiwa nguvu, halafu unaambiwa uchimbe mashimo..upige sururu chini, upige jembe chini, utoe jasho la kutosha si jambo jepesi..

Lakini baadaye tunaona Mungu anawaambia hamtaona mvua bali hayo mabonde yote yatajaa maji. Na ndivyo ilivyokuwa. Kwa waliochimba sana walipata maji sana, kwa waliochimba kidogo walipokea maji sawasawa na mashimo yao.

Je nini Bwana alikuwa analifundisha kanisa lake.

Katikati ya jangwa, Si muda wa kulia na kusumbuka, kinyume chake shika jembe lako, chepe lako anza kuchimba mashimo.

Kwanini watu wengi hawaioni mvua ya Mungu ya neema au baraka za rohoni zikidumu kwao lakini kwa wengine hudumu…sio kwamba Mungu anaupendeleo…hapana…bali wale wengine tayari wameshachimba mashimo marefu ya kuhifadhi maji mengi…Kwasababu mvua au umande wa Mungu sikuzote hushuka au hupanda juu ya nchi yote lakini wale wenye visima ndio hudumu na maji yake mda mrefu kwa wengine hudumu tu kwa muda mfupi pale juu, baadaye kidogo hupotelea ardhini…

Kuchimba handaki ni kudumu sana katika maombi, pamoja na kutendea kazi kile ulichokitaka kwa Mungu…

Kwa mfano unamwomba Mungu akupe mke/mume mwema, labda leo huoni kutokea kwa yoyote upo jangwani tu, unakaribia kukata tamaa…hakikisha unazidisha sana maombi, lakini pia unajitunza na kuanza kujifunza mafunzo ya kuwa mke/mume mwema, unaonyesha kivitendo zile sifa za mke mwema/mume mwema anazopaswa awe nazo kibiblia, kwamfano wewe ni mwanamume unafahamu kuwa yapo majukumu ya kibaba mbele yako, kwamba unapaswa uwajibike kwa kipato cha familia yako, lakini hilo kama hulisumbukii na bado unatarajia Bwana akuletee mke..ni kweli atakuletea, atapandisha umande wa maji juu ya nchi lakini hatimaye atashindwa kudumu na wewe katika hatua za awali akiona huwezi kusimama kwenye wajibu wako…baadaye utalalamika mbona wanawake wananikimbia..vilevile mwanamke akikosa tabia njema..wanaume watakuja na kumkimbia baadaye…kwasababu hakuwa na muda wa kujichimbia mahandaki yake, kitabia.

Kila eneo liwe la kihuduma, kikazi, kiafya..wekeza sana kwenye mahandaki kwasababu mvua/ umande utakuja tu…kwasababu kwa Mungu kushusha baraka si jambo la kulisumbukia sana, yeye anawanyeshea mvua waovu na wema alisema hivyo (Mathayo 5:45) bali kuzihifadhi hizo baraka ndio ugumu ulipo.

Mwanzo 2:6

[6]ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi. 

 

Wekeza kwenye maombi na kutendea kazi imani yako kwa vitendo. Zaidi ya kutarajia tu Mungu atende mwenyewe.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

 

Print this post

UKIMBIE UHURU WA ULIMWENGU

Umewahi kujua tofauti ya makundi haya mawili ya MBWA?.

Kundi la kwanza Mbwa wanaotembea huru barabarani na kundi la pili ni wale Mbwa wanaofugwa majumbani?.

Utaona Mbwa wanaozurula mitaani bila makao rasmi, huwa hawana afya, wanadharaulika, na ijapokuwa wanao uhuru wa kwenda popote watakapo lakini bado huwa hawana afya huwa ni wenye maradhi.

Utaona mbwa anayekatiza mitaani, ataona vyakula vingi vinapikwa, ataona minofu mingi ikitengenezwa na wanadamu, atasikia harufu ya kila aina ya chakula kizuri lakini hatakula?.

Lakini tukirudi kwa wale Mbwa wanaofugwa majumbani ni kinyume chake.

Wao wana afya kwasababu wanalishwa na wanaowafuga, pia ni jasiri kwasababu wanaaminiwa na wanaowafuga.

Hawana haja ya kuhangaika kutafuta chakula kwani wanaletewa, hawana haja ya kujitibu kwani wanatibiwa na wanaowafuga kwa ufupi wanaishi maisha ya raha isipokuwa tu hawana uhuru wa kuzurula ovyo na kukatiza mitaani.

Ni hivyo hivyo kwa watoto waliotoroka kwao na kuishi mitaani, huwa hawana afya njema, wala ustawi ijapokuwa wana uhuru wa kufika popote watakapo na kufanya chochote watakacho..

Lakini watoto wanaolelewa nyumbani hawana uhuru wa kwenda popote watakapo au kufanya chochote watakacho lakini ndio wenye ustawi mzuri na wanaofanikiwa.

Ni hivyo hivyo kwetu pia, Uhuru wa kufanya chochote na kutenda chochote tutakacho ni uhuru potofu ambao, mwisho wake ni kuharibika na kudharaulika.

Lakini tukikubali kulelewa na MUNGU kama watoto wanaopendwa basi tutafika mbali na kustawi sana.

Kama upo nje ya hifadhi rudi nyumbani kwa baba yako leo, kwa kutubu dhambi na kumkaribisha YESU, Na Bwana atakupokea na kukulea kama mtoto anayependwa sana.

Waefeso 5:1 “Hivyo mfuateni Mungu, kama watoto wanaopendwa”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Huduma ya kuendelea kuwa mwaminifu pale wachache wanapokusikiliza.

Huu ni mfululizo wa masomo yawahusuyo watumishi wa Mungu. 

Kuna makosa mengi yapo miongoni mwa mitazamo yetu sisi (watumishi wa Mungu), tunadhani mafanikio ni pale hasaa huduma yetu inaposhawishi mioyo ya wengi …pale tunapoona umati unaipokea, na kuishangilia.

Lakini tukifuatilia huduma za manabii wengi wa Mungu, kwenye biblia kama vile Isaya na Ezekieli, Yeremia hawakuwa na mafanikio makubwa ya mahubiri yao, kama tunavyodhani hivi leo, kinyume chake waliishia kukataliwa, kuteswa na kuuliwa, kwa ufupi huduma zao ziliwavunja sana moyo,  lakini kwasababu aliyewatuma ni Bwana,  injili yao imesimama vizazi na vizazi mpaka leo..

Walijua wanakwenda kuhubiri kwa watu ambao wana mioyo migumu sana…na Mungu aliwaeleza kabisa, lakini walifanya hivyo kwa uaminifu wote, kana kwamba wanauokoa umati wa watu.

Yeremia 7:27

[27]Nawe utawaambia maneno hayo yote; lakini hawatakusikiliza, nawe utawaita; lakini hawatakuitikia. 

Ezekieli 2:3-7

[3]Akaniambia, Mwanadamu, nakutuma kwa wana wa Israeli, kwa mataifa wanaoasi, walioniasi mimi; wao na baba zao wamekosa juu yangu, naam, hata hivi leo. 

[4]Na wana hao wana nyuso zisizo na haya, na mioyo yao ni migumu. Mimi nakutuma kwa hao; nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi. 

[5]Nao, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao. 

[6]Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma i pamoja nawe, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi. 

[7]Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana. 

Hakuna jambo linaloumiza kwa mtumishi wa Mungu pale unapoona unahubiria jamii kubwa ya watu lakini matokeo yoyote huoni kwao,…Ni vema ufahamu kuwa Mungu hakutumi ukawe mshawishi, anakutuma ukawe mwaminifu kwa kazi yake.

Kushindwa kwako katika huduma sio, kukosa watu wa kukusikiliza au watu kupungua kwenye huduma yako, kushindwa kwako ni kukosa uaminifu..hilo tu.

Leo hii ungewekwa kwenye nafasi ya Nuhu ambaye aliuhubiria ulimwengu kwa miaka mia moja na ishirini, na kuambulia tu familia yake, ungeshamkimbia Mungu siku nyingi na kusema sijatumwa, ungewekwa kwenye nafasi ya Yeremia, Mika, sefania ungesema huyu si Mungu, ni akili zangu zimenituma, ungesema ninachofanya ni uwendawazimu…hii sio huduma lazima kuna shida mahali, haiwezekani watu hawataki kugeuka, na kutubu, ungewekwa nafasi ya Musa ungesema hawa nilionao  sio watu wa Mungu ni kizazi cha nyoka, pamoja na ishara zote na miujiza…lakini bado wanatengeneza ndama wa shaba, wanaasi, wananung’unika…najitaabisha bure tu.

Kama mtumishi wa Mungu jitahidi sana kuwa mwaminifu, hata kama huoni ukuaji wowote, au mafanikio yoyote ya machoni, ya kuokoka kwa watu wengi…wewe ifanye kazi yake, mtumikie yeye, timiza ratiba zako. mtumikie Mungu kwa mtazamo huo wa uaminifu na sio wa matokeo, utadumu na hutapindishwa na chochote.

Kwani thawabu yako ni kubwa mbinguni. 

Mungu akubariki sana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.

SIKU ZA WATUMISHI WA MUNGU.

KARAMA TUZIPATAZO KWA MSAADA WA WATU WENGI.

Print this post