Ubora wa Kuhubiri au kufundisha haupimwi kwa elimu kubwa ya biblia, au mifano mizuri, au utashi fulani wa kupangilia maneno. Hapana, bali ni uwezo wa kupenya katika mioyo ya watu.
Haimaanishi kuwa na elimu ya biblia haichangii ubora wa fundisho au hubiri..inachangia sana lakini hiyo ni kama gamba la juu sana..ambalo linaweza lisitoe pia matokeo yoyote.
Pale fundisho linapoweza kuingia ndani ya moyo wa mtu, kupambanua, kuchoma, kulainisha, kupindua-pindua, kukarabati, kuponya hadi kumfanya mtu kuwa na mwitikio wa dhahiri wa nje. Hilo ndio linaitwa fundisho au hubiri kibiblia.
Sasa tendo hilo mpaka kufikiwa, si jambo rahisi hata kidogo, hakuna utashi wa kibinadamu unaweza kufanya hivyo.
Kwasababu hakuna anayejua ndani ya mtu mwingine kuna nini?
Lakini lililo gumu zaidi ni kuwa hata yeye mwenyewe hajijui vema, kama anahitaji matengenezo katika eneo fulani la moyo wake. Anaweza akawa ana hofu akadhani huwenda chanzo cha hofu hiyo ni ule ugonjwa uliomshika, kumbe chanzo ni kingine kabisa.
Kwasababu mwanadamu mwenyewe moyo wake ni fumbo kubwa.
Yeremia 17:9
[9]Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?
Umeona jinsi ilivyo ngumu sana. Ikiwa yeye mwenyewe hajijui, wewe mtu wa tatu utayajulia wapi yaliyomo moyoni mwake? Lakini Mungu anataka uyahubiri yahusuyo moyo wake.
Usifikiri unapomwona mtu, labda ana huzuni, au furaha au ana tabia za ulevi, wizi, , ukadhani anahitaji fundisho linaloendana na hiyo tabia unayoiona kwa nje.
Unaweza ukakosa shabaha kwa maili nyingi sana, ukifikiri tu hivyo.
Utamwona analia, pengine ni mgonjwa, amefiwa, amepoteza kila kitu kama ilivyokuwa kwa Ayubu na wewe unamfuata na fundisho la faraja, ukadhani kuwa ndio uponyaji wake utakapotokea.
Kumbe Mungu anajua anataka makemeo, na makaripio ili aponywe.
Wakati mwingine utasimama kwenye mkusanyiko wa watu wengi labda mia. Huko huko wapo wanaohitaji faraja, wanaohitaji unabii, wanaohitaji maonyo, wanaohitaji maarifa, wanaohitaji kufunguliwa. Sasa wewe unasimama na fundisho lako lenye mlengo mmoja wa makemeo, unadhani wote watahudumiwa na hilo. Kama ukikosa namna ya ki-ungu, unaweza ukawa unazungumza maneno yako.
Na lengo la Mungu ni watu wote wahudumiwe na Neno.
Hapo ndio linakuja suala la hakuna mbobezi wa fundisho au hubiri. Inahitaji hekima nyingine itokayo juu, ya kuhubiri usichokuwa na ufahamu nacho, au ujuzi nacho.
Siku ile ya Pentekoste, kilichotendeka mpaka ikapelekea watu wale kuchomwa mioyo, na hatimaye kuamini kwa idadi ile kubwa ya watu.
Haikuwa kwasababu walipaza sauti sana, au walihubiri kwa ujasiri sana, au maneno yao yalikuwa na elimu kubwa ya theolojia..
Hapana angalia utaona yalikuwa ni maneno ya kawaida kabisa… lakini yaliyoundwa na Roho Mtakatifu kwa namna ambayo yalipenya katika moyo wa kila mmoja.
Utaona, hatua ya kwanza walinena kwa lugha ambazo hata wao wenyewe hawakuzijua, lugha hizo zilikuwa zinawahubiria wengine.. zinanena mambo yao ya sirini, zinawakemea, zinawafariji, zinawaponya, zinawashuhudia Kristo.
Mpaka baadaye wanamaliza kunena tayari injili imeshahubiriwa wasijue ni kitu gani kimehubiriwa.
Petro aliposimama kumalizia maneno yake, wote wamenywea wanasubiri tu kupewa maelekezo ni nini cha kufanya baada ya pale..
Matendo ya Mitume 2:37
[37]Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
Hao ni watu wasio na elimu yoyote, walikuwapo waandishi, na mafarisayo wenye elimu lakini hakuna matokeo yoyote ya mafundisho yao.
Hata leo hii mimi na wewe.. Tujue kuwa kuhubiri na kufundisha hakutegemei sana ujuzi, au utashi, bali kunategemea zaidi Roho Mtakatifu.
Kwanini Roho Mtakatifu?
Kwasababu yeye ndiye anayeweza kuzama ndani ya mioyo ya watu na kujua shida zao, na kuwaponya.
Ni nini tunapaswa kufanya, ili fundisho likazame moyoni, lisitoke kwa makisio yetu?
Jambo kuu ni Kuwa na maandalizi ya kutosha.
Maandalizi hayo yapo kwa namna mbili.
1) Kumwandalia Roho Mtakatifu njia ya kuanzia..Ndio hapo unahitaji kwanza kusoma na kuandaa somo / fundisho. Kumbuka Ni lazama utenge muda kuandaa fundisho ambalo utalihubiri. Andika, na ujue pa kuanzia, bila kuwa na maandalizi hayo, unasema nitaenda tu kuzungumza. Ujue tayari umeizuia njia ya Roho Mtakatifu kufundisha.
2) Lakini hilo peke yake halitoshi, hatua nyingine ni kuomba maingilio ya Roho Mtakatifu yawe makubwa. Hapo ndipo unatenga muda mrefu wa kuomba, ili Roho Mtakatifu akatembee kwenye vyumba vya ndani kabisa ambavyo wewe hujui, wakati utakaposimama na kufundisha, kushuhudia.
Sasa ukimaliza hapo. Jiandae kwenda kusema ulichokusudia.. kumbuka mhubiri anayetumia dakika kumi kufundisha lakini amekuwa na maandalizi ya masaa matano kwenye kusoma na maombi. Ana nguvu zaidi ya yule atakayefundisha masaa matano, halafu alijiandaa kwa dakika tano.
Mwisho Ukienda kufundisha na kuona mazungumzo yako yanasogea nje ya mada, au taarifa nyingine zinakuja kichwani mwako tofauti na zile ulizoziandika kwenye daftari ujue ni kazi za Roho Mtakatifu usizizuie.
Baadaye utakuja kusikia tu shuhuda, na hata kama hazitasemwa, ujue Neno lako halijakwenda bure.
Tukiwa wahubiri na waalimu wa namna hii. Roho nyingi za watu zitaokolewa.
Kuhubiri ni kusema tusichokijua, cha wengine.
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu katika kujifunza Neno na Maombi. Kusoma Neno bila Maombi, au kuomba bila Neno ni sawa na kitamba cha bendera kisicho na mlingoti, kupitia mfululizo huu wa tafakari tutapata mwongozo sahihi wa kuomba kupitia maandiko ya kwenye Biblia.
MAPENZI YA MUNGU.
Bwana YESU alisema si kila aniambiaye Bwana Bwana atakayeingia katika ufalme, bali yule afanyaye mapenzi ya Baba wa mbinguni.
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. 22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? 23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Sasa basi kama kigezo cha kuingia mbinguni ni “KUFANYA MAPENZI YA MUNGU”, hivyo tukimwomba MUNGU atusaidie kuyajua na kuyafanya mapenzi yake tutakuwa tunaomba jambo sahihi kabisa.
1. OMBA KUYAJUA MAPENZI YA MUNGU KWAKO (Tumia dakika 30)
Katika Eneo la kiroho.
Katika Eneo la kimaisha.
Katika Eneo la kifamilia.
2. OMBA KUYATENDA MAPENZI YA MUNGU. (Tumia dakika 30)
Utauliza katika kuyatenda mapenzi ya MUNGU kuna haja ya kuomba?. Jibu ni Ndio! Kwasababu pasipo yeye kutusaidia sisi hatuwezi kufanya lolote. (Soma Yohana 15:5).
Katika Eneo la kifikra
Katika eneo la Viungo
3. KEMEA KILA ROHO INAYOKUZUIA WEWE KUYAFANYA MAPENZI YA MUNGU.
Zipo roho za adui zinazozua kuyafanya mapenzi ya MUNGU, roho hizi zinazuia fikra zako za ndani zisifikiri, wala kupenda kuyafanya mapenzi ya MUNGU, ndio hapo utatamani kwenda kushuhudia habari za wokovu, ndani ya fikra zako woga unaingia au aibu au kukosa ujasiri, tumia muda kuzikemea.
Pia zinazuia viungo vyako visiwe tayari kufanya mapenzi ya MUNGU, ndio hapo utatamani kwenda kuhubiri au kwenda kufanya kazi yoyote iliyo halali na ghafla udhaifu wa mwili utaingia kama uchovu, uvivu, au ugonjwa. Hivyo chukua muda kukemea roho hizo na Bwana atakufungua.
1Petro 4:2 “Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani. 3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali; 4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana”.
1Petro 4:2 “Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana”.
Bwana akubariki usikose sehemu ya Pili ya Mwongozo huu wa Neno na Maombi, kwa msaada zaidi wasiliana nasi kwa namba tajwa hapa chini.
– Hapa utamwomba Bwana akufunulie kuyajua mapenzi yake katika kazi unazozifanya au elimu, ni kipi sahihi unapaswa ukifanye ukiwa hapo kazini, ni watu gani sahihi unapaswa ushirikiane nao ili usifanye kinyume jambo nje na mapenzi ya MUNGU pia kama unatafuta kazi, basi omba MUNGU akakufunulie kazi sahihi na kukuongoza hapo.
iii. Katika eneo la kifamilia.
– Hapa omba Bwana akakuoneshe mapenzi yake kuishi na mke, mume, na watoto, au wazazi pia ombea wanafamilia yako wote wakayajue mapenzi ya MUNGU na kuyafanya.
2 Wafalme 13:20 “Elisha akafa, nao wakamzika. Basi vikosi vya Wamoabi wakaingia katika nchi mwanzo wa mwaka.
21 Ikawa, walipokuwa wakimzika mtu, angalia, waliona kikosi; wakamtupa yule mtu kaburini mwa Elisha; mara yule maiti alipoigusa mifupa ya Elisha, alifufuka, akasimama kwa miguu”
Kumbukumbu la Torati 30:15 “Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya”.
Mathayo 16:24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.
25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.
26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
27 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake” .
Ulishawahi kutafakari kwanini yule mwanamke aliyemzaa yule mtoto wa kiume, kupewa uwezo wa kukimbilia nyikani, kama njia ya kuepushwa na joka lile?
Kwanini asichuliwe mashambani, au mjini, au milimani, kinyume chake iwe nyikani.
Ufunuo 12:13-14
[13]Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume. [14]Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.
[13]Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.
[14]Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.
Nyikani ni mahali ambapo hapana uzuri wowote, hapana mahitaji yoyote ya msingi, mahali pasipovutia, kwasasa tunaweza kusema ni nyakati za ukame, ambazo huoni, jambo lolote, huoni hatua yoyote dhahiri,ijapokuwa unajitahidi sana..huoni mafanikio yoyote, huoni mazingira rafiki..
Wakati mwingine ni kipindi cha kupungukiwa kwa muda mrefu, upo pale pale.
Tunapofikia hatua hii, mara nyingi tunamlilia Mungu atuondoe huko, tunahuzunika, tunanyong’onyea, tunasinyaa kiroho, tunamlilia Mungu kwa juhudi nyingi atuvushe..
Ni kweli kabisa jangwa si zuri, lakini wakati mwingine Bwana hulitumia kutuepusha na yule mwovu. Njia pekee iliyompasa huyu mwanamke kuepushwa na joka lile, ilikuwa ni kukimbilia jangwani, na si vinginevyo.
Hivyo ujikutapo katika nyakati mbalimbali ngumu, maadamu upo ndani ya Kristo na unaendelea vema katika imani, fahamu pia huko ulipo Mungu anakuandaa na unatimiza kusudi la Mungu.
Tuwapo katika mazingira yoyote, suluhisho si kulalamika bali ni kuomba, kushukuru na kuitafuta hekima.
WhatsApp
Luka 15:13 “Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati. 14 Alipokuwa amekwisha tumia vyote, NJAA KUU ILIINGIA NCHI ILE, YEYE NAYE AKAANZA KUHITAJI. 15 Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe”. 16 Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, WALA HAPANA MTU ALIYEMPA KITU”.
2 Wafalme 6:25 “Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha”.
Luka 15:17 “Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. 18 Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; 19 sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako. 20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana”.
YAFAHAMU NA YATENDE MAPENZI YA MUNGU.
NAMNA GANI NITAPOKEA NGUVU ZA BWANA YESU?.
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?
NINI TUNAJIFUNZA KWA MWANA MPOTEVU NA NDUGUYE?
Dhambi pekee inayotajwa kwenye Biblia yenye laana ya umaskini na inayofilisi ni “Uasherati”.
Luka 15:13 “Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; AKATAPANYA MALI ZAKE HUKO KWA MAISHA YA UASHERATI”.
Ukitaka kufilisika kuwa mwasherati… kila utakachokipata kitapukutika na hutajua kimeishaje.
Labda unawaza kwamba mali zitaisha tu kwa “kuonga” (kwa kuwapa makahaba). Ndio hiyo namna ya kwanza ya kufilisika, Lakini nataka nikuambie hata usipoonga pesa yoyote, ukawa unafanya uasherati bila kugharimika….nataka nikuambie kuwa bado tu utaanguka kiuchumi, utaombea na kila aina ya watumishi na kutoa kila aina ya sadaka na hautafunguliwa.
Kwasababu uasherati “unaondoa akili”
Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.
Uasherati unaondoa akili ya “maendeleo”…kwahiyo hata pasipo kuonga mwanamke bado tu utafilisika, ndio maana hata wanawake wanaofanya uasherati maisha yao yanafanana tu na wanaume waasherati, wote wanasumbuka, kwasababu hata pesa wanazopewa na wanaume hazijawahi kuwasiadia chochote kwasababu tayari kile kitendo kimewatolea akili.
Haujawahi kusikia popote kahaba kapata pesa za kutosha sasa ameacha kazi hiyo na kupitia mtaji wa ukahaba wake sasa anajishughulisha na jambo jingine, wote utaona hata wapate fedha nyingi bado watarudi katika hiyo kazi.
Dhambi ya uasherati inatajwa kama ubaya mkubwa..
Mwanzo 39:9 “Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?”.
Ndugu ukitaka kufunguliwa kimaisha acha uasherati kabisa, jitenge na huyo binti unayemwita “girl friend”..kama unataka kuishi naye funga naye ndoa takatifu na halali inayojulikana na sio ufanye uasherati.
Binti, achana na huyo kijana unayemwita “boyfriend”..ukitaka kuishi naye funga naye ndoa halali ya kibiblia, lakini maisha ya uasherati unayoendelea nayo yanakuondolea akili za asili na zile zile za neema.
Matokeo ya mwisho ya uasherati ni hukumu ya MUNGU.
1 Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; WAASHERATI HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti”.
Hii ndio hasara kubwa inayotokana na uasherati, (kuukosa uzima wa milele).
Ni heri ukose mali zote za duniani kuliko uukose uzima wa milele, kwani dunia inaita na mambo yake yote.
Lakini pamoja na hayo, kwanini uteseke duniani na bado uteseke baada ya kifo?.
Amua leo kumpa YESU KRISTO maisha yako, akusafishe dhambi zako na kukutakasa.
Huo uasherati ambao unaona ni mgumu kuuacha, ni kwasababu haujaokoka sawasawa, wewe fanya maamuzi thabiti ya kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, na ondoa vichocheo vyote vya uasherati katika maisha yako kama mavazi ya kizinzi ( ya kubana maungo, na mitindo yote ya kidunia).
Pia jitenge na makundi ya watu wenye mizaha, na acha mahusiano hayo yasiyo rasmi, futa namba zote za watu unaozungumza nao mambo ya kihuni, na kiri mbele yao kwamba umeokoka, uone kama Roho Mtakatifu hatakutengeneza, na uasherati wote utakufa ndani yako itabaki historia tu.
Lakini ukitubu na kuendelea kuishi maisha yale yale ya siku zote, nakuambia hitaona matokeo yoyote zaidi sana ndio utazama zaidi katika dhambi.
Ikiwa utahitaji kuokoka utaweza kuwasiliana nasi kwa namba zilizopo hapa chini na utasaidika kwa Neema ya MUNGU.
Shalom.
Swali: Biblia inasema “Tukiongozwa na Roho hatupo chini ya sheria”(Wagalatia 5:18) maana yake nini andiko hili?
Jibu: Tuanzie ule mstari wa 16 ili tuelewe vizuri..
Wagalatia 5:16 “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. 17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. 18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria”.
Wagalatia 5:16 “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria”.
Awali ya yote ni vizuri kujua roho inayozungumziwa hapo ni roho gani?.. si roho ya mtu, bali roho ya MUNGU (Yaani Roho mtakatifu) ndio maana imeanza kwa herufu kubwa… maana yake “Tukiongozwa na Roho Mtakatifu hatupo chini ya sheria”
Sasa anaposema “tukiongozwa na Roho hatupo chini ya sheria” haimaanishi kuwa tunapookoka basi tuna ruhusa ya kufanya kila kitu, au kutenda jambo lolote, au kuvaa vyovyote au kuishi vyovyote, na kwamba tupo juu ya sheria.
La! Hiyo sio tafsiri yake.. ili tuelewe vizuri maana au tafsiri halisi ya andiko hilo, hebu takafakari mfano huu.
Mwalimu wa Hisabati anawaambia wanafunzi wake kuwa “Mkitumia kikokoteo (yaani calculator) hamtateseka na kanuni/sheria za mahesabu”.. maana yake ni kwamba mtafanya mahesabu yale yale lakini katika urahisi, lakini si kukwepa mahesabu… ikiwa na maana kuwa ile calculator inarahisisha kufanya mahesabu bila mwanafunzi kutumia kanuni.
Ni ivyo hivyo katika hilo andiko anaposema “Mkiongozwa na Roho hampo chini ya sheria”… maana yake sheria za kumcha MUNGU ambazo kwa udhaifu wa mwili ni ngumu, kama vile zile sheria za hisabati, kwa kupitia Roho Mtakatifu zinakuwa nyepesi.
Maana yake kama Biblia imesema “Usizini” au “Usiseme uongo”… kutimiza sheria hiyo ya kukaa bila kudanganya au bila kufanya zinaa ya nje au moyoni ni ngumu.. lakini kwa msaada wa Roho Mtakatifu inawezekana kutimiza sheria hiyo kirahisi,
Ndio maana hapo kwenye mstari wa 16 anasema “Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili”.
Na hapa ndipo tunapoona umuhimu mkubwa wa kujazwa Roho Mtakatifu kama Biblia inavyotufundisha..
Waefeso 5:18 “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho”.
Watu waliojaa Roho Mtakatifu kweli kweli hawaoni shida kuishi maisha matakatifu yasiyo na dhambi, wengine wote wanaweza kuwashangaa wanawezaje kuishi bila wizi, matusi, rushwa, zinaa, ulevi na bado wanayafurahia hayo maisha, pasipo kujua siri kuwa ni Roho Mtakatifu aliye ndani yao, anawasaidia udhaifu wao.
Na ili tujae Roho Mtakatifu ni lazima tufahamu kanuni ya kumpata Roho Mtakatifu, kama tu ili tupate kikokoteo wepesi (calculator) itakachotusaidia kutatua mahesabu magumu kwa haraka na wepesi ni lazima tujue jinsi ya kuipata au mahali pa kuipata na gharama zake.
Sasa tunampataje Roho Mtakatifu ili tuwezi kuishi pasipo sheria??
Tunampata kwa kanuni ifuatayo..
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.
Kwa njia ya kutubu dhambi kwa kumaanisha kuiacha!, na kubatizwa kwa Maji mengi kwa jina la Bwana YESU, yule Roho ataingia ndani ya kuwezesha uwezo huo mkubwa wa kuishi kwa utakatifu bila mapambano makubwa moyoni.
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho Mengine
ZIDI KUTAFUTA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU.
Ahadi Ya Roho Mtakatifu.
KUWA NA MAFUTA YOTE YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO.
ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.
KAZI ZA ROHO MTAKATIFU
Shalom, jina la Mwokozi YESU libarikiwe, karibu tujifunze pamoja Biblia, Neno la Mungu wetu.
Maandiko yanatabiri kuwa siku za mwisho kutatokea aina ya watu wasiotaka “suluhu” katika nyanja mbalimbali za kifamilia hata kikanisa.
2 Timotheo 3:1 “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, 3 wasiowapenda wa kwao, WASIOTAKA KUFANYA SULUHU, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema”.
2 Timotheo 3:1 “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.
2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,
3 wasiowapenda wa kwao, WASIOTAKA KUFANYA SULUHU, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema”.
Tabia ya kutotaka kufanya Suluhu imwsababisha ndoa nyingi kuvunjika, familia nyingi kutengana, makanisa kuanguka , undugu kuisha, na hata urafiki mwema kuisha..
Jambo ambalo si jema machoni pa MUNGU wetu.
Lakini pamoja na hayo yote, yawezekana zimetumika njia nyingi kuleta suluhu na mapatano imeshindikana..
Yawezekana mazungumzo na vikao vimefanyika vya kutosha lakini hakuna suluhu, yawezekana umejaribu au mmejaribu kuweka mambo sawa kwa kila njia lakini bado hakuna mapatano wala makubaliano.
Kama njia zote hizo hazijaleta matokeo basi ipo kanuni moja ya kibiblia nzuri sana ambayo mtu akisimama na hiyo vizuri basi hata wale maadui zake atapatana nao.
Na njia hiyo si nyingine zaidi ya ile tunayoisoma katika Mithali 16:7.
Mithali 16:7 “Njia za mtu zikimpendeza BWANA, Hata adui zake huwapatanisha naye”.
Ikiwa na maana kwamba Mtu akizitengeneza njia zake zikawa thabiti kwa MUNGU, na hata MUNGU akapendezwa naye, basi hatawale waliokuwa wanampiga vita, Mungu ataweka amani, hata wale waliokuwa wanamchukia Mungu ataweka upendo.
Lakini ni lazima njia za Mtu kwanza zimpendeze MUNGU,
Labda tujifunze mfano mmoja wa kwenye Biblia tuweze kuelewa zaidi, tumrejee Yakobo ndugu yake Esau,
Tunaona baada ya Yakobo kuchukua mbaraka wa ndugu yake, mara moja Esau aliapa kumuua, jambo lililomfanya Yakobo akimbie.
Lakini pamoja na kukimbia kwake Yakobo alijua fika kuwa hataweza kumkimbia ndugu yake milele, na hivyo alitamani mapatano naye.
Sasa Yakobk alichokifanya sio kuandika barua nyingi za kuomba msamaha kwa Esau, bali katika mazingira ya kujitenga alitengeneza njia zake kwa MUNGU, katika ukamilifu na usafi, na wala hakuketi kumsema kaka yake, na MUNGU akapendezwa naye na kumpatanisba na ndugu yake Esau ambaye aliapa kumuua hapo kwanza.
Mwanzo 33:1 “Yakobo akainua macho yake, akaona, na tazama, Esau anakuja na watu mia nne pamoja naye. Akawagawanyia Lea, na Raheli, na wale vijakazi wawili, wana wao…… 3 Akapita mwenyewe mbele yao, akainama mpaka nchi mara saba, hata alipomkaribia ndugu yake. 4 Esau akaja mbio kumlaki, akamkumbatia, na kumwangukia shingoni, akambusu; nao wakalia. 5 Akainua macho yake, akawaona wale wanawake na watoto, akauliza, Ni nani hawa walio pamoja nawe? Akasema, Ni watoto Mungu aliompa mtumwa wako kwa neema yake. 6 Ndipo wale vijakazi, na wana wao, wakakaribia wakainama. 7Lea naye, na wanawe, wakakaribia wakainama. Baadaye Yusufu na Raheli wakakaribia, wakainama. 8 Akasema, Kundi hili lote nililolikuta, maana yake ni nini? Akasema, Kunipatia kibali machoni pa bwana wangu. 9 Esau akasema, Ninayo tele, ndugu yangu, uliyo nayo na yawe yako. 10 Yakobo akasema, Sivyo; kama nimekubalika machoni pako tafadhali upokee zawadi yangu mkononi mwangu, iwapo nimeona uso wako kama kuona uso wa Mungu, ukapendezwa nami. 11 Pokea, tafadhali, mbaraka wangu, ulioletewa, kwa sababu Mungu amenineemesha, na kwa sababu ninavyo hivi vyote Akamshurutisha, naye akapokea. 12 Kisha Esau akamwambia, Twende zetu, tusafiri, nami nitakutangulia”.
Mwanzo 33:1 “Yakobo akainua macho yake, akaona, na tazama, Esau anakuja na watu mia nne pamoja naye. Akawagawanyia Lea, na Raheli, na wale vijakazi wawili, wana wao……
3 Akapita mwenyewe mbele yao, akainama mpaka nchi mara saba, hata alipomkaribia ndugu yake.
4 Esau akaja mbio kumlaki, akamkumbatia, na kumwangukia shingoni, akambusu; nao wakalia.
5 Akainua macho yake, akawaona wale wanawake na watoto, akauliza, Ni nani hawa walio pamoja nawe? Akasema, Ni watoto Mungu aliompa mtumwa wako kwa neema yake.
6 Ndipo wale vijakazi, na wana wao, wakakaribia wakainama.
7Lea naye, na wanawe, wakakaribia wakainama. Baadaye Yusufu na Raheli wakakaribia, wakainama.
8 Akasema, Kundi hili lote nililolikuta, maana yake ni nini? Akasema, Kunipatia kibali machoni pa bwana wangu.
9 Esau akasema, Ninayo tele, ndugu yangu, uliyo nayo na yawe yako.
10 Yakobo akasema, Sivyo; kama nimekubalika machoni pako tafadhali upokee zawadi yangu mkononi mwangu, iwapo nimeona uso wako kama kuona uso wa Mungu, ukapendezwa nami.
11 Pokea, tafadhali, mbaraka wangu, ulioletewa, kwa sababu Mungu amenineemesha, na kwa sababu ninavyo hivi vyote Akamshurutisha, naye akapokea.
12 Kisha Esau akamwambia, Twende zetu, tusafiri, nami nitakutangulia”.
Unaona hiyo kanuni?.. Kama njia za Yakobo zingekuwa mbovu nyumbani kwa Labani, hakika wakati huu wa kukuata na Esau ageuawa.
Yawezekana nawe ndoa yako haijakaa sawa na mke wako au mume wako. Usikimbilie manung’uniko na malalamiko na kusema umbea huku na kule, wala usitafute kujitetea sa a au kujionesha kuwa wewe ni mwenye haki.
Unaweza kujitenga kwa muda (si vibaya kujitenga kwa amani).. lakini ukiwa katika kujitenga ombi lako kuu liwe ni Kupata suluhu jema na patano zuri, huku ukizitengeneza njia zako lwa MUNGU.
Nakuhakikishia kukingana na Biblia kama njia zako zitampendeza Bwana, basi tegemea matokeo ya ajabu katika eneo hilo la mapatano au suluhu, utaona yule mume ambaye alikuwa anakusumbua sasa anatulia, yule mke rafiki, yule ndugu anakupenda na kuifuata imani yako.
Sasa Swali unatengenezaje njia yako kwa Bwana?. Si kwa njia nyingine bali kutii Neno la MUNGU.
Zaburi 119:9 “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako”
Neno la MUNGU kwanza linasema tutubu, na kuimini injili (Marko 1:15). Na pia kubatizwa kwa maji na kwa Roho mtakatifu (Marko 16:16), na kuishi maisha ya utakatifu baada ya hapo (Waebrania 12:14).
Kwa kulitii hilo Neno basi mlango wa mapatano kwatu umefunguka?.
Je umempa Bwana YESU maisha yako?
Kama bado unasubiri nini?. Tubu leo na kuiamini injili.
Katika maandiko ukikutana na kisa kinaishia kwa kusema ‘hata leo’. Basi kuwa makini hapo kwasababu lipo la kukusaidia.
Kwamfano Ibrahimu alipopanda kule mlimani kumtolea Mungu sadaka kwa Isaka, Mungu alimpa kondoo badala yake, Kwa tukio hilo Ibrahimu akapaita mahali pale Yehova-yire. (Maana yake Mungu-mpaji). Hivyo jambo lile maandiko yanasema liliendelea kutamkwa na watu kwa wakati mwingine mwingi sana kama usemi uliohai ‘Yehova-yire’, Mungu atupaye.
Mwanzo 22:13-14
[13]Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe. [14]Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire, kama watu wasemavyo hata leo, Katika mlima wa BWANA itapatikana.
[13]Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
[14]Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,
kama watu wasemavyo hata leo, Katika mlima wa BWANA itapatikana.
Mfano mwingi ni wakati wa Yoshua alipoiangamiza nyumba ya Akani, msaliti, biblia inasema;
Yoshua 7:26
[26]Kisha wakakusanya juu yake chungu kubwa ya mawe hata leo; naye BWANA akauacha ukali wa hasira yake. Kwa sababu hiyo jina la mahali pale likaitwa, Bonde la Akori, hata hivi leo.
Ikiwa na maana bonde hilo liliendelea kuitwa vile vile hadi wakati wa mwandishi. ‘Ipo sababu’.
Mfano mwingine ni kipindi cha Yehu alipoyavunja mahekalu ya Baali..
2 Wafalme 10:27
[27]Wakaibomoa nguzo ya Baali, na kuiangusha nyumba ya Baali, wakaifanya choo hata leo.
Ikiwa na maana mpaka wakati mwandishi anaandika hicho kitabu eneo hilo lilikuwa ni choo.
Mahali pengine ni hapa..
Israeli kuwa hatarini kuvamiwa na wamoabu, wakamlilia Mungu, kisha kawaambia hawatapigana vita bali watakwenda kuokota nyara, kazi yao iwe ni kusifu na kuimba tu. Maadui zao wakauana wao kwa wao Na eneo lile wakaliita bonde la baraka hata leo.
2 Mambo ya Nyakati 20:25-26
[25]Nao Yehoshafati na watu wake walipokuja kuchukua nyara zao, wakaona kati yao wingi wa mali, na mavazi, na johari za thamani, walivyojivulia, zaidi kuliko wawezavyo kuchukua; wakawa siku tatu katika kuteka nyara, maana zilikuwa nyingi sana. [26]Hata siku ya nne wakakusanyika katika bonde la Baraka; maana ndipo walipombarikia BWANA; kwa hiyo jina lake mahali pale pakaitwa Bonde la Baraka hata leo.
[25]Nao Yehoshafati na watu wake walipokuja kuchukua nyara zao, wakaona kati yao wingi wa mali, na mavazi, na johari za thamani, walivyojivulia, zaidi kuliko wawezavyo kuchukua; wakawa siku tatu katika kuteka nyara, maana zilikuwa nyingi sana.
[26]Hata siku ya nne wakakusanyika katika bonde la Baraka; maana ndipo walipombarikia BWANA; kwa hiyo jina lake mahali pale pakaitwa Bonde la Baraka hata leo.
Mahali pengine ni wakati wa kifo cha Yuda, lile shamba lililonunuliwa liliitwa konde la damu mpaka nyakati za mwandishi..
Mathayo 27:8
[8]Kwa hiyo konde lile huitwa konde la damu hata leo.
Sasa biblia kusema ‘hata leo’ sio tu kutoa uthibitisho wa tukio kwamba kweli lilitokea ..lakini ni vema kujua tafsiri yake rohoni…kwamba kuna minyororo aidha ya baraka au laana inatembea mpaka leo.
Kwamfano watu waliposema Yehova-yire walijua Mungu ni mpaji wakati wote…hivyo wakamwona katika mazingira hayo..ndio maana wakasema ‘hata sasa’ si tu wakati wa Ibrahimu.
Neno hilo lipo hai hata leo rohoni. Ukiamini Mungu aliyomtendea Ibrahimu anakwenda kukutendea na wewe, utapokea…kwasababu lipo hivyo hata leo.
Anaposema mahali pale pakaitwa bonde la baraka hata leo. Ni kweli rohoni hata leo bonde hilo lipo.
Ukiamini kwamba katika kumwimbia Mungu unaingia katika bonde la baraka. Utapokea vingi kwa Mungu, sawasawa na walivyopokea Israeli kipindi cha Yehoshafati vitani.
Hivyo mambo mengi na matukio mengi yanaendelea kutembea katika roho hata sasa…Je! Macho yako yanaona?
Ukiwa mwovu kama Akani, kumbuka bonde la Akori lipo mpaka leo, ikiwa utakuwa msaliti kama Yuda konde la damu lipo hata leo utazikiwa huko.
Chagua mema, yaishi mema, upokee mema