Category Archive Uncategorized @sw-tz

MATUKIO KATIKA MAANDIKO YANAYOISHI HATA LEO.

Katika maandiko ukikutana na kisa kinaishia kwa kusema ‘hata leo’. Basi kuwa makini hapo kwasababu  lipo la kukusaidia.

Kwamfano Ibrahimu alipopanda kule mlimani kumtolea Mungu sadaka kwa Isaka, Mungu alimpa kondoo badala yake,  Kwa tukio hilo Ibrahimu akapaita mahali pale Yehova-yire. (Maana yake Mungu-mpaji). Hivyo jambo  lile maandiko yanasema liliendelea kutamkwa na watu kwa wakati mwingine mwingi sana  kama usemi uliohai ‘Yehova-yire’, Mungu atupaye.

Mwanzo 22:13-14

[13]Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe. 

[14]Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,

kama watu wasemavyo hata leo, Katika mlima wa BWANA itapatikana. 

Mfano mwingi ni wakati wa Yoshua alipoiangamiza nyumba ya Akani, msaliti, biblia inasema;

Yoshua 7:26

[26]Kisha wakakusanya juu yake chungu kubwa ya mawe hata leo; naye BWANA akauacha ukali wa hasira yake. Kwa sababu hiyo jina la mahali pale likaitwa, Bonde la Akori, hata hivi leo. 

Ikiwa na maana bonde hilo liliendelea kuitwa vile vile hadi wakati wa mwandishi. ‘Ipo sababu’.

Mfano mwingine ni kipindi cha Yehu alipoyavunja mahekalu ya Baali..

2 Wafalme 10:27

[27]Wakaibomoa nguzo ya Baali, na kuiangusha nyumba ya Baali, wakaifanya choo hata leo. 

Ikiwa na maana  mpaka wakati mwandishi anaandika hicho kitabu eneo hilo lilikuwa ni choo.

Mahali pengine ni hapa..

Israeli kuwa hatarini kuvamiwa na wamoabu, wakamlilia Mungu, kisha kawaambia hawatapigana vita bali watakwenda kuokota nyara,  kazi yao iwe ni kusifu na kuimba tu. Maadui zao wakauana wao kwa wao Na eneo lile wakaliita bonde la baraka hata leo.

2 Mambo ya Nyakati 20:25-26

[25]Nao Yehoshafati na watu wake walipokuja kuchukua nyara zao, wakaona kati yao wingi wa mali, na mavazi, na johari za thamani, walivyojivulia, zaidi kuliko wawezavyo kuchukua; wakawa siku tatu katika kuteka nyara, maana zilikuwa nyingi sana. 

[26]Hata siku ya nne wakakusanyika katika bonde la Baraka; maana ndipo walipombarikia BWANA; kwa hiyo jina lake mahali pale pakaitwa Bonde la Baraka hata leo. 

Mahali pengine ni wakati wa kifo cha Yuda, lile shamba lililonunuliwa liliitwa konde la damu mpaka nyakati za mwandishi..

Mathayo 27:8

[8]Kwa hiyo konde lile huitwa konde la damu hata leo. 

Sasa biblia kusema ‘hata leo’ sio tu kutoa uthibitisho wa tukio kwamba kweli lilitokea ..lakini ni vema kujua tafsiri yake rohoni…kwamba kuna minyororo aidha ya baraka au laana inatembea mpaka leo.

Kwamfano watu waliposema Yehova-yire walijua Mungu ni mpaji wakati wote…hivyo wakamwona katika mazingira hayo..ndio maana wakasema ‘hata sasa’ si tu wakati wa Ibrahimu.

Neno hilo lipo hai hata leo rohoni. Ukiamini Mungu aliyomtendea Ibrahimu anakwenda kukutendea na wewe, utapokea…kwasababu lipo hivyo hata leo.

Anaposema mahali pale pakaitwa bonde la baraka hata leo. Ni kweli rohoni hata leo bonde hilo lipo.

Ukiamini kwamba katika kumwimbia Mungu unaingia katika bonde la baraka. Utapokea vingi kwa Mungu, sawasawa na walivyopokea Israeli kipindi cha Yehoshafati vitani.

Hivyo mambo mengi na matukio mengi yanaendelea kutembea katika roho hata sasa…Je! Macho yako yanaona?

Ukiwa mwovu kama Akani, kumbuka bonde la Akori lipo mpaka leo, ikiwa utakuwa msaliti kama Yuda konde la damu lipo hata leo utazikiwa huko.

Chagua mema, yaishi mema, upokee mema

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TUMETOSHELEZWA KUWA WAHUDUMU WA AGANO JIPYA

Jina la YESU KRISTO lenye nguvu libarikiwe.

Neno la MUNGU linatufundisha kuwa sote tuliomwamini YESU, tumefanywa kuwa “Wahudumu wa Agano jipya”, maana yake tu watumishi na wahudumu wa Agano jipya, ambalo ni Agano la Roho na sio la mwilini.

Na siri kubwa ni kwamba utumishi huu tuliopewa, “Umejitosheleza” asilimia zote, hauna kasoro, ni wenye nguvu wa kubadilisha visivyobadilika, na ni wenye thawabu kubwa kuliko kazi zote.

2Wakorintho 3:6 “Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha”.

Sasa kufahamu kwa undani nini maana ya “Andiko huua bali roho huhuisha” fungua hapa>>> Nini maana ya “Andiko huua, bali Roho huhuisha (2Wakorintho 3:6)

Lakini ninachotaka tuone siku ya leo ni “Utoshelevu huu tuliopewa” kwamba tunapokuwa wahudumu wa Agano hili jipya tumepata bahati kubwa sana, kwasababu umejaa utoshelevu usio elezeka, na hiyo ndio maana wote wanaomtumikia MUNGU ijapokuwa watapitia dhiki, au mateso, au adha, lakini ndani yao wanajihisi washindi siku zote,

Ndani yao wanajivunia injili, ndani yao wanazo nguvu, hata kama utu wao wa nje unachakaa..

2Wakorintho 4:12 “Basi hapo mauti hufanya kazi ndani yetu, bali uzima ndani yenu.

…..16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku”.

Kwa ufupi wana heri kubwa wamtumikiao Bwana katika Agano hili jipya kwa mujibu wa Biblia, kwasababu ni wenye thamani na thawabu kubwa mbinguni.

Je wewe ni mhudumu wa Agano jipya?..Je unaitumia karama yako vizuri?.. au umeificha talanta yako ardhini, umepewa huduma ya uinjilisti je unaufanya kwa bidii?.. umepewa karama nyingine yoyote je unaitumia kwa uaminifu?..

Huenda hujui hicho ulichopewa kina uthamani kiasi gani, lakini nataka nikuambie kuwa huduma iliyowekwa ndani yako baada ya wewe kuokoka ni kubwa, na imejitosheleza, kinachotakiwa ni wewe kuanza kazi na sio kuendelea kungoja.

Amka leo kama umelala, anza kuhudumu madhabahuni kwa Bwana, Nenda shambani kwa Bwana kavune watu, thawabu yako itakuwa ni kubwa mbinguni kwani kilichowekwa ndani yako ni kikubwa wala usijidharau au mtu asikudharau, simama mtumikie aliyekuita, kwani muda haukungoji na bado ule mwisho umekaribia sana.

Bwana akubariki na kukuongezea Neema, ikiwa utataka msaada hatua za kuanza katika kumtumikia MUNGU, basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba hizi 0789001312.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE UTAKATIFU NI MATENDO YA SHERIA?

UKIMBIE UHURU WA ULIMWENGU

UPENDO WA KRISTO WATUBIDISHA;

Uradhi wa Mapenzi yake ni nini? (Waefeso 1:5)

UFANYE BIDII KATIKA KUSOMA.

PENDA KUHAKIKI MAMBO KABLA YA KUYAAMINI

 

Jina la Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe sana, karibu tujifunze biblia neno la MUNGU wetu (Zab 119:102).

Siku zote penda kuhakiki jambo kabla ya kuliamini, au kulipokea.. Taarifa yoyote inayokufikia, au unayoihisi kabla ya kufanya maamuzi ya kuamini au kutenda jambo, fanya uhakiki kwanza, Desturi ya kuhakiki jambo sio “kukosa imani” kama inavyoaminika na wengi bali ndio kipimo cha “ukomavu”.

Katika Biblia tunajifunza kwa MUNGU wetu kuwa naye pia ni Mungu wa kuhakiki mambo.. kwamfano zile taarifa za maovu ya watu wa Sodoma na Gomora zilishatangulia kumfikia, lakini kabla ya kufanya maamuzi ya kuiangamiza miji ile pamoja na watu wake, alishuka kwanza yeye mwenyewe kuhakiki kwa kile kilichotangulia kumfikia.

Tusome habari..

Mwanzo 18: 20 “Bwana akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,

21 BASI, NITASHUKA SASA NIONE KAMA WANAYOTENDA NI KIASI CHA KILIO KILICHONIJIA; NA KAMA SIVYO, NITAJUA.

22 Basi wale watu wakatoka huko wakaelekea Sodoma; lakini Ibrahimu alikuwa akali akisimama mbele za Bwana”.

Kupitia habari hiyo sio kwamba Bwana MUNGU alikuwa hayaamini masikio yake, wala malaika wake wala mashitaka yoyote yaliyopandishwa mbele zake juu ya watu wa Sodoma na Gomora, alikuwa anawaamini sana, lakini ilibidi yeye mwenyewe akahakiki ukweli na uzito wa mambo, ili hukumu yake iwe ya haki na kweli.

Ni mara ngapi umesikia habari za mtu fulani kuwa yuko hivi au yuko vile, na kabla haujachukua maamuzi juu yake umelifuatilia kwa undani uhakika wa maneno hayo?.. utaona kuwa ni mara chache sana.. Wengi tunaziamini sana taarifa za kuambiwa au kusimuliwa na si zile tulizozithibitisha wenyewe.

Tunapenda kuthibitishiwa mambo na si kuyathibitisha wenyewe, ni mara ngapi umefuatilia ukweli wa mambo kuhusu Mke wako kwa yale unayoyasikia?, au ya mume wako, au ya watoto wako au wazazi wako?.

Tumewahi kukutana na visa vya watoto kuaminishwa kuwa wazazi wao ni wachawi kwa maneno tu!, au kwa ndoto tu, na mwisho kuishia kuwachukia na kuwatenga wazazi wao jambo linalofunga Baraka na neema kwa mtoto asilimia mia moja.

Jifunze kuhakiki mambo yote, hata yale ya kiMUNGU, si kila hubiri ni la kuliamini au kulipokea asilimia zote bila kulihakiki, Ondoa ile desturi ya kuamini kila kitu, ndio tunajiandaa kuamini lakini si kuruhusu kuamini kila kinachotujia.

Kuhakiki mambo si dhambi.. Na kipimio kizuri cha kuhakiki mambo ni NENO LA MUNGU, kama wale watu wa Beroya.

Matendo 17:10 “Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi.

11 Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo”.

Ukiwa na uwezo mkubwa wa kulijua NENO la MUNGU, utakuwa na uwezo mkubwa pia wa kuhakiki mambo, kwani Neno la Mungu (Biblia) ni kitabu kulichojaa mafunzo ya kila aina ya maisha.

Ukitaka kuhakiki ndoto unazoziota kama ni halisi au batili, Biblia pekee ndio kipimio chako, ukitaka kuhakiki fundisho au hubiri unalolisikia kama ni halisi au gugu, ni Biblia tu, ukitaka kuhakiki njia yako ya kiroho, kibiashara, au kielimu kama ni sahihi, ni Biblia tu.

Ukitaka kuhakiki mke, au mume au mtoto kama yupo katika njia sahihi au sio sahihi ni Biblia, ukitaka kuhakiki taarifa unazozijua kama ni njema au za kupotosha ni Biblia tu.

Biblia ndio kitabu cha Maisha, imejaa hekima, maarifa, mwanga, mashauri, na maelekezo sahihi ya maisha, ikiwemo majibu ya maswali magumu, Biblia pekee ndio kitabu kinachoelezea mambo yajayo kwa usahihi kwa mtu mmoja mmoja, au kundi na hata Taifa na Dunia kwa ujumla.

Ndio kitabu pekee ambacho ukikisoma ni kama yupo mtu mwingine pembeni yako anakusemesha, tofauti na vitabu vingine vyote, ndio kitabu pekee chenye taarifa zisizofifia uhalisia kwa jinsi muda unavyozidi kwenda.

Anza uhakiki wa mambo leo kwa kusoma Biblia, sauti ya MUNGU iliyo wazi.

Ikiwa utahitaji kusaidiwa mwongozo wa usomaji wa Biblia, basi waweza wasiliana nasi kwa namba hizi 0789001312.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAMBO MANNE(4) YAFANYAYO NENO LA MUNGU.

NENO LA MUNGU NI UFUNUO MKAMILIFU.

Ipi tofauti ya Juhudi na bidii kibiblia. (Warumi 12:11)

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

Mgawanyo wa Vitabu vya Biblia

MTAZAME BWANA

Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO, libarikiwe daima.

Ipo faida kubwa sana ya kumwangalia Bwana, na Bwana kukuangalia wewe.. Wengi tunapenda Bwana atuangalie ila sisi tusimwangalie, hebu tutazame faida moja ya Bwana kutuangalia sisi na sisi kumwangalia Bwana, kwa kutafakari mfano ufuatao.

Mtu aliyesimama mbele yako ukimtazama naye akikutazama, ni wazi kuwa mbele yake ni nyuma yako wewe na nyuma yake ni mbele yako wewe, kwasababu mnatazamana, tofauti na kwamba mngetazama wote upande mmoja, endapo mngetazama wote upande mmoja mbele yako ingekuwa ni mbele yake pia, na nyuma yako ni nyuma yake pia.

Sasa Bwana anapotutazama sisi yale mambo yetu yaliyopita kwake ni kama yajayo, na yale yajayo ni kama yaliyopita… Kwahiyo wakati tunawaza nini kitatokea kesho, tayari Bwana alishakipanga na kukimaliza, wakati tunawaza ni mambo gani na gani yatatupata miaka 10 au 20 ijayo tayari Bwana alishashughulika nayo zamani, kwani mbele yetu sisi ni nyuma ya Bwana muda mrefu sana.

Vile vile mambo yetu yaliyopita ambayo yanaonekana kama hayawezi kutengenezekeka tena, hayawezi kurekebishika tena, kwa MUNGU wetu yanakuwa ni mambo yanayotengenezeka na ni mambo yanayopangika, kinachotakiwa ni kitu kimoja tu!… nacho ni kumwangalia Bwana.

Yeremia 31:28  “Tena itakuwa, kwa kadiri NILIVYOWAANGALIA, ili kung’oa, na kubomoa, na kuangusha, na kuangamiza, na kutesa; kwa kadiri iyo hiyo nitawaangalia, ili kujenga, na kupanda, asema Bwana”.

Tunamwangaliaje Bwana?.. Kwanza kwa kuungama makosa, na kutembea katika Neno lake, hapo Bwana pia atatuangalia kwasababu siku zote pia analitazama Neno lake apate kilitimiza (Yeremia 1:12).

Usiangalie matatizo yanayokuzunguka, bali mwangalie Bwana, usiangalie mambo ya kutisha yanayojiandaa kutokea wewe mtazame Bwana, usiangalie mambo yaliyopita yaliyoharibika wewe mwangalie, kwani unayoyaona kama hayawezi tena kurekebika BWANA anaweza kuyafanya upya tena, na unayoona kama hayataweza kutimia kwa Bwana mambo yako yajayo kwake ni kama yaliyopita, endapo ukimtazama.

Mtazame  Bwana!, Mtazame Bwana!.

Maran atha!.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je YESU KRISTO alikuwa na wadogo zake?

Tafsiri ya Wakolosai 2:18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu,

ZIDI KUTAFUTA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU.

UJIO WA BWANA YESU.

NIFANYE NINI PALE NINAPOSAHAU NDOTO NILIZOOTA?

Moja la lango ambalo Mungu hulitumia sana, kutufikishia  sisi taarifa zake, ni ndoto. Na kama ni lango la Mungu basi ni vema tufahamu kuwa ibilisi hatalipenda. Hivyo atahakikisha taarifa hizo anazivuruga au hazitufikii vema, kama tu vile anavyohakikisha watu hawaliewi Neno, au mahubiri, Ndivyo anavyofanya na kwenye ndoto pia.

Taarifa zitokazo kwa Mungu zinaangukia katika makundi matatu;

  1. Tahadhari
  2. Unabii
  3. Baraka

1) Tahadhari

Hizi ni taarifa za maonyo, au hatari zinazokuja mbeleni. Mfano wa taarifa hizi ni kama zile zilizomfikia Yusufu, alipokuwa Israeli, akaambiwa akimbilie Misri, kwasababu Herode anataka kumuua mtoto, na aliporudi baadaye, akaonywa tena asikae Yerusalemu, bali aende Nazareti.

Mathayo 2:19-22

19 Hata alipofariki Herode, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto huko Misri,
20 akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mamaye, ushike njia kwenda nchi ya Israeli; kwa maana wamekufa walioitafuta roho ya mtoto.
21 Akaondoka akamchukua mtoto na mamaye, akafika nchi ya Israeli.
22 Lakini aliposikia ya kwamba Arkelao anamiliki huko Uyahudi mahali pa Herode babaye, aliogopa kwenda huko; naye akiisha kuonywa katika ndoto, akasafiri pande za Galilaya,

Lengo la taarifa hizi ni mtu kuchukua hatua, aidha ya kivitendo au ya kimaombi.

Kwamfano Mungu anaweza kukuonyesha ajali, au msiba fulani. Hapo ujue hasaa unahitajika kuchukua hatua kimaombi kuharibu hizo roho za mauti, kwa kinywa chako.

2) Unabii

Hizi ni taarifa za mambo yajayo, Yale yatakayotokea baadaye, kwenye maisha yako, huduma, familia, nchi, au taifa. Mfano wa ndoto hizi, ni kama ile ya Farao juu ya miaka saba ya shibe na njaa, (Mwanzo 41) na Nebukadreza, juu ya ile sanamu kubwa, iliyowakilisha falme nne, zitakazokuja kusimama ulimwenguni (Danieli 2).

Halikadhalika Mungu anaweza kukuonyesha, maisha yako baadaye yatakuwaje, huduma yako baadaye, itasimamaje, maono yako baadaye yatafikia wapi, anaweza kukuonyesha mambo ya siku za mwisho, matukio yajayo, kuhusu nchi, watu, familia. Hatua unayopasa kuichukua ni kuomba, na kuandaa mazingira sasa. Mfano Farao aliposaidiwa tafsiri ya ndoto yake na Yusufu, alichukua hatua ya kuweka hazina ya vyakula kwasababu njaa ilikuwa inakuja mbele. Mungu akikuonyesha huduma yako itakuwa kubwa, anza leo kujiwekea hazina ya maarifa ya Neno la Mungu, anza kutendea kazi wito wako,. Akikuonyesha unawaombea watu wengi wanapona, anza leo kuwaombea watu hata kama hawaponi, omba hivyo hivyo kila siku, usikae tu ukasubiri ije kutimia huonyeshi jitahada yoyote, akikuonyesha biashara yako imekuwa, ongeza juhudi kufanya kazi.

3) Baraka

Mungu anaweza kuachia Neno la Baraka kwako, kwamfano ukaota, ndoto njema, labda unatiwa mafuta na Kristo, au unaambiwa maneno ya mafanikio kama vile  Sulemani alipotokewa na Mungu na kuelezwa atapokea Hekima, na kuwa na mali nyingi. Uotapo ndoto ambazo ni za mafanikio kwako, uamkapo, hakikisha unazinenea kwa Imani. Unasema

“Na iwe kwangu kwa jina la Yesu Kristo”. Kama tu vile unavyobatilisha ndoto za maovu, labda mauti, vivyo hivyo hizi unazipokea kwa kinywa chako. Ni muhimu sana.

Ibrahimu aliota ndoto

Mwanzo 51:1-6

Baada ya mambo hayo neno la Bwana likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.
2 Abramu akasema, Ee Bwana MUNGU, utanipa nini, nami naenda zangu hali sina mtoto, na atakayeimiliki nyumba yangu ni huyu Eliezeri, Mdameski?
3 Abramu akasema, Tazama, hukunipa uzao, na mtu aliyezaliwa nyumbani mwangu ndiye mrithi wangu.
4 Nalo neno la Bwana likamjia likinena, Huyu hatakurithi, bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi.
5 Akamleta nje, akasema, Tazama sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu. Akamwambia, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.
6 Akamwamini Bwana, naye akamhesabia jambo hili kuwa haki.

Sasa kinachotokea ni kwamba ndoto nyingi sana, za taarifa mbalimbali  kutoka kwa Mungu zinapotea akilini mwetu, na tunaona kawaida,

Ndoto hupotea kwa aidha namna mbili;

  • Tunakumbuka kwamba tuliota ndoto, lakini hatujui ni ndoto gani
  • Hatukumbuki kabisa kama tuliota ndoto yoyote. Lakini ipo ndoto tuliyoota

Namna mojawapo inaweza kutokea kwa mtu. Usikae ukafikiria kisa hukumbuki chochote, ukadhani hukuota ndoto yoyote. Zipo ndoto ulizoota. Hivyo ni vema ukajifunza namna ya kukabiliana na lango lako la ndoto. Ndio maana utaona wengine tukio likishatokea ndio anakumbuka kuwa alishawahi onyeshwa tukio hilo. Hiyo haitakiwi.

Nifanye nini ili nikumbuke ndoto zangu?

Njia tatu zinazoweza kumfanya mtu akumbuke ndoto.

i) Kuomba:

Kila asubuhi uamkapo, katika maombi yako, hakikisha unashika Kichwa chako, kisha unasema maneno haya

‘Baba, nafungua lango la ndoto zangu, yote uliyosema nami usiku nilipolala, ninayoyakumbuka na nisiyoyakumbuka yakawe bayana sasa kwa  kwa jina la Yesu, ndoto zilizoibiwa na ibilisi, kumbukumbu zangu, na fikra zangu zilizofutika, navirejesha vyote ndani ya ufahamu wangu sasa kwa jina la Yesu Kristo’.

Ukijifunza kuomba namna hiyo, tayari umekaribisha msaada wa Mungu, mahususi katika eneo lako la ndoto na hivyo urahisi wa kukumbuka unakuja.

ii) Utulivu (Kutafakari)

Ukishaomba, pendelea kupata utulivu, kisha tafakari kwanza Neno la Mungu. Kila asubuhi hakikisha unapata kwanza mkate wa uzima ambao ni Neno, tafakari Neno kwa muda kidogo, jiulize vifungu hivi vinamaana gani, je! Siku ya leo nitaviwekaje katika maisha yangu? Fanya tu hivyo tembea maeneo mbalimbali ya kwenye biblia, kisha tafakari tena juu ya maisha yako ya rohoni, juu ya maono yako, juu ya familia yako utajiboreshaje, baadaye juu ya ratiba zako za siku..

Katika wingi wa kutafakari, mara nyingi Mungu hurejesha ndoto zilizosahaulika, utashangaa katika tafakari Fulani hapo hapo unakumbuka kuna jambo uliota, linaloendana na tukio hilo. Ujue huo ni ujumbe wa Mungu.

Ukikosa muda wa kutosha asubuhi, Fanya hivyo muda wa usiku kabla ya kulala, Pata utulivu mwingi peke yako, Utakumbushwa ndoto nyingi.

iii) Mazungumzo

Njia nyingine ambayo humfanya Mungu arejeshe ndoto zetu kirahisi, ni katika mazungumzo, kumbuka kila eneo la maisha yako au wengine, yamkini Bwana alishawahi kusema na wewe, kwa njia ya ndoto, lakini hujui.

Kwamfano ukiwa na mwenzako, au wenzako, mnazungumza sana, Habari njema za kanisa, katika mazungumzo ya muda mrefu ikiwa lipo ambalo Bwana alikuonyesha, utaona kumbukumbu hiyo inakujia, au labda mnazungumza kwa kina Habari ya siku za mwisho, Kumbukumbu ya ndoto kama hiyo itakujia, au malengo ya maono yako.

Hivyo mazungumzo mazuri na yenye maana hurejesha fikra zilizopotea. Kwahiyo, jijengee desturi ya kuwa na mazungumzo mema.

Zingatia pia si kila ndoto hutoka kwa Mungu, ili kuweza kutofautisha ndoto za Mungu na za shetani, fungua link hii, uweze kupitia..>>>> https://wingulamashahidi.org/2019/09/03/nitajuaje-kama-ndoto-ni-ya-mungu-au-ya-shetani/

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

SIFA NJEMA YA KIRUKA NJIA

Kuna ndege anaitwa kiruka njia, ambaye anatajwa kama mmoja wa ndege najisi, kwenye Kumbukumbu 14:15, lakini ndege huyu anasifa moja ambayo, huwa ina  funzo kubwa sana la kiroho.

Tofauti na ndege wengine, ambao huruka aidha mchana, au usiku, kujitafutia chakula, kwamfano mwewe, mbayuwayu, korongo, tai, ni ndege wa mchana, lakini pia bundi, popo, ni ndege wa usiku, wote hawa hufanya kazi aidha majira ya kutwa nzima ya mchana, au usiku kucha.

Lakini kiruka njia, huruka zaidi, majira ya alfajiri sana, na jioni sana. Majira haya huyapendelea kwasababu, ni wakati wa mageuko ya siku, ambayo ndege wote wawindaji hujiandaa Kwenda mapumziko, au kuamka. Kwamfano muda wa jioni kama vile saa 12, ndege wakali wawindaji kama vile tai, mwewe, kipanga, n.k. wanaacha uwindaji, na kutafuta makao yao kupumzika, lakini pia wakati huo huo ndege wakali wa usiku kama vile bundi, hujiandaa kutoka waende kwenye mawindo yao saa mbili, Kwahiyo huo muda hapo Katikati mazingira kwake huwa si ya upinzani mkubwa.

Kwasababu yeye ni ndege dhaifu, na anaweza kuwindwa na ndege wakubwa, majira hayo kwake ni salama zaidi. Vivyo hivyo ule muda wa alfajiri sana, miale ya jua inapoanza kuonekana kwa mbali sana, hutoka na Kwenda kuwinda, muda huo ndege wa usiku ndio wanakwenda kulala, huku ndege wa mchana wanajiandaa kutoka, mpaka inapofika saa 12 asubuhi, tayari ameshamaliza uwindaji wake.

Licha ya kuwa wakati huo, ndege wengi hawapo hewani, lakini wakati huo, wa alfajiri sana na jioni sana, ndio makundi ya wadudu wengi wa ardhini hutoka kuruka juu, ikiwemo mbu, kumbikumbi, mchwa, nondo, mende n.k. kwasababu yeye hula wadudu, anaweza kukamata wadudu hata elfu moja ndani ya saa moja tu. Hivyo kwa muda mfupi sana akawa ameshashiba, zaidi ya mihangaiko mingi ya kutwa nzima, kugombania vyakula, na masumbufu mengi.

Ndege huyu mchana hupumzika zake, kwenye miti, na usiku pia, lakini hutumia alfajiri yake na jioni yake vizuri. Ndio maana ni vigumu kujulikana, kwasababu shughuli zake anazifanya wakati anga ni tulivu.

Hutufundisha nini?

Bwana alituambia tuwatafakari ndege (Mathayo 6:26)

Ni lazima tuthamini mida hii miwili, kuitumia kuwa uweponi mwa Bwana, Bwana Yesu alipendelea sana, kuamka alfajiri kuomba,

Marko 1:35 Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko.

 Ipo faida kubwa sana kuamka  mapema kuomba kwasababu, muda huo anga ni tulivu, wakati watu wamelala, wewe unapokea thawabu za siku kutoka kwa Bwana. Kuna usemi unaosema biashara ni asubuhi, kwasababu wameona  Riziki nyingi huwaga majira hayo, vivyo hivyo rohoni, ukijifunza kuomba majira hayo, na jioni pia kabla hujaimaliza siku, Basi utaona tofauti kubwa sana, na wepesi mwingi wa masumbufu ya siku.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?

MTEGO HUTEGWA BURE, MBELE YA MACHO YA NDEGE YE YOTE.

Je tamaa ni dhambi kulingana na Yakobo 1:15?

NIFINYANGE BWANA

Jina la Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe sana, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu lililo taa na mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).

Yeremia 18: 1 “Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema,

2 Ondoka, ukashuke mpaka NYUMBA YA MFINYANZI, na huko nitakusikizisha maneno yangu.

3 Basi nikashuka mpaka nyumba ya mfinyanzi, na tazama, alikuwa akifanya kazi yake kwa magurudumu. 4 NA CHOMBO KILE, ALICHOKUWA AKIKIFINYANGA, KILIPOHARIBIKA MKONONI MWAKE YULE MFINYANZI, ALIKIFANYIZA TENA KUWA CHOMBO KINGINE, kama alivyoona vema yule mfinyanzi kukifanya”.

Katika mstari wa 4 tunasoma kuwa Mfinyazi alikifinyanga chombo kilichoharibika na kuwa chombo kingine, zingatia hilo neno “chombo kingine” maana yake sio tena chombo kile cha kwanza kilichoharibika.

Tuchukue mfano labda mfinyazi huyu alifinyanga kikombe cha maji hapo kwanza, na baadae akaone kimeharibika au kina kasoro, ndipo anapokivunja vunja kile kikombe cha udongo na kuutia tena maji na kuufinyanga tena kuwa sahani..

Sasa udongo ni ule ule umeweza kutoa chombo kingine kipya tofauti na kile cha kwanza, na MUNGU alimwambia hivo hivyo YEREMIA, lakini Yeremia hayupo sasa, ila sisi tupo, hivyo anatuambia sisi kuwa tujifunze kwa Mfinyanzi kwa kuwa yeye (MUNGU) ndiye mfinyanzi mkuu wa maisha yetu.

Yeremia 18: 5 “Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,

6 Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile kama mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema Bwana. Angalieni, KAMA UDONGO ULIVYO KATIKA MKONO WA MFINYANZI, NDIVYO MLIVYO NINYI KATIKA MKONO WANGU, EE NYUMBA YA ISRAELI”.

Je wewe ni chombo cha aina gani?..

Kama maisha yako yametawaliwa na dhambi basi fahamu kuwa ni dhahiri kuwa wewe ni chombo kilichoharibika, kama maisha yako yametawaliwa na ugomvi, uasherati, wizi, masengenyo, kiburi na mambo mengine yote ambayo ni kinyume cha Neno la MUNGU (yaliyotajwa kwenye Wagalatia 5:19-20), huu ni wakati wa wewe kumkimbilia mfinyazi Mkuu YESU KRISTO, akufinyange kuwa chombo kingine cha heshima..

Warumi 9:21 “Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?”

Bwana YESU anaweza kukufanya kuwa mwingine kabisa, mtu wa maana kabisa, ambapo ile hali yako ya ulevi wa pombe au ulevi wa anasa inayokusumbua, kinachotakiwa tu ni kukiri kuwa wewe ni mkosaji mbele zake na unahitaji msaada wake,  na baada ya hapo kutubu dhambi zako mbele yake huku ukidhamiria kabisa kuacha mambo yote mabaya, na kumwambia naomba unifinyange tena, kupitia Roho wake mtakatifu atakayeingia ndani yako atakugeuza na kuwa mtu mwingine.

Kumbuka toba isiyo ya kumaanisha haileti matokeo yoyote kwa mtu anayetaka mabadiliko, hakikisha unapotubu dhamiria kujitakasa, kwa kujitenga na vichocheo vyote vya dhambi, kama ulikuwa ni mlevi acha kwenda Bar, kama ulikuwa unajiuza jizuie kwa bidii kwenda vituo vya ulivyokuwa unafanya biashara hiyo, ili uumpe nafasi Roho Mtakatifu ndani yako kukufinganya upya kuwa chombo kingine.

2Timotheo 2:21 “Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema”.

Bwana YESU akubariki sana.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ATAWAFANYIA WAMCHAO MATAKWA YAO.

Zaburi 145:19 “Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa”.

Pamoja na kwamba tumeagizwa kuomba “Mapenzi yake yatimie/yatimizwe (Mathayo 6:10”.

Lakini “Siri” moja kuu ni kwamba zaidi ya asilimia 90 ya Maombi ya wanaomcha MUNGU ni mapenzi ya MUNGU.Kwanini?..

Kwasababu maandiko yanatuambia hapo kuwa “Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa”.

Zingatia hilo neno “Atawafanyia wamchao matakwa yao”.

Kumbe Mungu anawapatia watu wake wanaomcha “Matakwa yao, yaani haja zao wanazozitaka”.

Kwa mtu anayemcha Mungu akiomba amani, ni asilimia kubwa ya hitaji lake hilo kuwa ni mapenzi ya MUNGU.

Mtu anayemcha MUNGU akiomba afya, ni asilimia zaidi ya nusu kuwa anaomba jambo ambalo ni mapenzi ya MUNGU.

Mtu anayemcha MUNGU akiomba akiomba mambo mengine yote ikiwemo mafanikio ya kiroho na kimwili ni mapenzi ya MUNGU, kwasababu MUNGU anawapa wamchao matakwa yao.

Je unataka kupewa matakwa yako na MUNGU?.Jibu ni rahisi “Mche Mungu tu”..Na Biblia inasema kumcha Mungu ndio hekima na kuepukana na uovu ndio ufahamu (Ayubu 28:28).

Sasa hatuwezi kumcha MUNGU kwa nguvu zetu, inahitajika kuwezeshwa na Roho Mtakatifu, kwasababu tabia ya kumcha MUNGU, ni zao la Roho Mtakatifu.Isaya 11:2 “Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, ROHO YA MAARIFA NA YA KUMCHA BWANA”.

Sasa kama kumcha Bwana ni zao la Roho Mtakatifu, je tunampataje Roho Mtakatifu..

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”

Kumbe kanuni ya kupokea Roho ni kutubu na kubatizwa kwa jina la YESU KRISTO!.

Basi maana yake tukitubu na kubatizwa tutapokea Roho Mtakatifu kama ilivyoandikwa, na matokeo ya kujaa Roho Mtakatifu, ni uwezo wa kumcha MUNGU kuingia ndani yako.Na matokeo ya kumcha MUNGU sana ni kusikiwa maombi yako na Bwana kukupa matakwa yako.

Je umeokoka?..Je unamcha Bwana?.

Zaburi 112:1 “Haleluya. Heri mtu yule amchaye BWANA, Apendezwaye sana na maagizo yake.

2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa”.

3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

AMBATANA NA WALIO HAI ROHONI.

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu, lililo taa na Mwanga wa njia yetu.

Utatamani kutembea na wenye vyeo vikubwa vya ulimwengu, ambao wengi wa hao ni wafu kiroho,

Utatamani kuolewa na wenye mali nyingi, na uwezo mkubwa ambao wengi wa hao ni wafu rohoni.

Utawadharau wanaoonekana dhaifu na wanyonge ambao Biblia inawataja kama matajiri wa imani na walio hai kiroho..

Yakobo 2:5 “Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao?”

Dada ni heri uambatane na huyo mtu ambaye unamwona leo ni maskini lakini anaye YESU, kuliko uende kuolewa na  tajiri ambaye  hana YESU maishani ( ni mfu kiroho).

Heri uwe na marafiki maskini lakini wanaye YESU kuliko uwe na marafiki matajiri ambao ndani yao hawana uzima.

Huyo tajiri kwako ni “Simba” na huyo maskini kwako ni “Mbwa”…ambaye ni kama hana hadhi mbele ya macho yako lakini Biblia inatufundisha kinyume na hilo..

Mhubiri 9:4 “Kwa kuwa liko tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai; (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa)”.

Ni afadhali mbwa, anayeishi, maana yake ni heri mtu maskini na mdhaifu mwenye uhai wa rohoni kuliko mtu aliye simba (yaani mwenye nguvu na mkali) lakini ni mfu rohoni.

Chagua  kwa makini nani wa kuambatana naye..

2 Wakorintho 6:14 “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?

15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari?Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?”

Bwana atusaidie..

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuadibu ni nini kibiblia? (Zaburi 94:12)

Kitendo cha kumtia mtu adabu ndio kuadibu. Maana yake kuchukua hatua za makusudi kuadhibu, au kukaripia, au kuonyoosha mwenendo lakini kwa lengo la kujenga sio kulipiza kisasi.

Neno hilo utalipata kwenye vifungu hivi.

Zaburi 94:12

[12]Ee BWANA, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako; 

Zaburi 94:10

[10]Awaadibuye mataifa asikemee? Amfundishaye mwanadamu asijue? 

Mungu akiitwa Baba, basi tujue kuwa sisi ni watoto wake, na kama ni watoto wake basi atatuadabisha pale tunapokosea..

Kubali kuadibiwa na Bwana…

Shalom.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Beliari ni nini? (2Wakorintho 6:15)

‘laana ya torati’ maana yake ni nini?

Mapokeo ni nini?