SWALI: Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’.
Luka 13:33
[33]Pamoja na hayo imenipasa kushika njia yangu leo na kesho na kesho kutwa; kwa kuwa haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu.
JIBU: Bwana Yesu alikuwa anaeleza asili ya mji wa Yerusalemu nyakati zote ulivyokuwa wa mauaji, mji ambao ungepaswa uwe wa kupokea manabii wa Mungu, lakini kinyume chake uligeuka mji wa kuwaua Manabii…
Sasa kusema maneno yale ni kutokana na taarifa aliyoletewa na wale mafarisayo kuwa Herode anataka kumwangamiza, hivyo aondoke pale aende mji mwingine…ndipo Bwana Yesu akawaambia ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’ yaani haipaswi nabii afe nje ya Yerusalemu…
Manabii wengi wa Mungu, waliuliwa pale pale Yerusalemu hivyo hata na yeye kuangamia hapo si jambo geni, …
Na ndivyo ilivyokuwa
Mfano wa hao katika maandiko alikuwa;
Zekaria mwana wa Yehoyada (2Nyakati 24:20-21). Ambaye aliuliwa hekaluni
Mwingine ni Uria nabii (Yeremia 26:20 – 24)
Na manabii wengine wengi ambao hawajatajwa, moja kwa moja katika maandiko waliuawa Yerusalemu…ndio sababu ya Yesu kusema maneno Haya;
Mathayo 23:37-39
[37]Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!
[38]Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.
[39]Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.
Jambo hili hujirudi sasa rohoni..
Watu wote ambao wanaipinga injili mioyoni mwao leo, hata kama hawajashiriki moja kwa moja kuwarushia mawe watu wa Mungu, ni shirika moja tu na wale waliokuwa wanawaua manabii wa Bwana zamani.
Ndivyo walivyodhani mafarisayo kwamba wenyewe hawahusiki na mauaji ya manabii wa Bwana, angali wanampinga yeye waziwazi, kwa unafiki wao aliwaambia maneno haya..
Mathayo 23:29-36
[29]Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki,
[30]na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii.
[31]Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii.
[32]Kijazeni basi kipimo cha baba zenu.
[33]Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?
[34]Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji;
[35]hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu.
[36]Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
Hii ni hatari kubwa sana kwa walio nje ya Kristo.
Mwamini Yesu leo uoshwe dhambi zako. Upokee uzima wa milele. Kwingineko si salama.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.
SWALI: Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, ni vita ya namna gani tunashindana nayo katika ulimwengu wa Roho?
JIBU: Katika biblia tunaposoma Neno “pepo”, ni vema tufahamu ufunuo wake upo katika namna mbili;
Yote mawili unapaswa kufahamu, Ili ujue ni nani unashughulika naye katika vita hivyo vya kiroho.
Kwamfano, ukisoma ile waefeso 6:12 inayosema kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, bali juu ya falme na mamlaka na wakuu wa giza hili pamoja na majeshi ya mapepo wabaya.. Sasa hao wanaotajwa hasaa ni malaika waasi.
Lakini hawa malaika waasi, huwa na mapando yao, ambayo huyapanda ndani ya watu, mfano wa hayo ni magonjwa, ukichaa, ububu, udhaifu (Marko 9:25)uuaji, uchungu, majivuno, kiburi, masengenyo n.k.. na haya mapando wakati mwingine huitwa mapepo, kwasababu asili yao ni kutoka kwa hao malaika waasi.
Luka 13:11 Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.
Pepo linalozungumziwa hapo, hasaa sio yale mashetani, bali ni pando la udhaifu waliloliweka ndani ya huo mwanamke.
Hizi zote ni kazi za shetani na malaika zake duniani. Sasa mapando haya ndio tunaweza kuyaua (kwa kuyang’oa), lakini sio wale malaika waasi. Ndio maana Bwana Yesu alisema..
Mathayo 15:13 Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang’olewa
Wale malaika waasi (yaani wakuu wa giza, wafalme, majeshi ya mapepo yote)hatuwezi kuwaua, kwa maombi au kwa namna yoyote, isipokuwa tayari wameshawekewa hukumu yao, siku ile ya mwisho ambapo watatupwa wote kwenye lile ziwa la moto.
Na mapando haya, Bwana Yesu alitoa maelezo yake vema, wakati ambapo adui hupandwa ndani ya mtu..
alisema.
Mathayo 13:24 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?
29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.
30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.
Kumbe wakati ambapo watu wamelala, ndipo hupanda mbegu zake. Yaani wakati ambapo watu wamekuwa walegevu kiroho ndipo shetani hupata nguvu ya kuja kupachika, mbegu zake za uharibifu, zitakazokuja kusumbua baadaye. Ndio maana ni lazima ujue kanuni mbalimbali za kumpinga shetani.
Na haya mapando, yanaweza kuwekwa kwa mtu yeyote, hata mtu aliyeokoka, anaweza kuwa nayo. Ndio maana utaona wapo watu wengine wameokoka, lakini wanasumbuliwa na mapepo, kiuhalisia, hawana malaika wale waasi ndani yao, wanayo mapando yao.
Ni sawa, na mtu ambaye anamilika chombo kama komputa, akiwa anaitumia kwa matumizi yake tu ya sikuzote, tu ambayo ni lazima, si rahisi computa hiyo kuvamiwa na virusi, lakini akianza kutembea mitandaoni, kisha kubofya, au kupakua kila kitu anachokiona ni wazi kuwa chombo hicho kipo hatarini kuvamiwa na virusi, na matokeo yake ni kuwa mfumo wote wa kumpyuta unaliwa, au kuharibifu chombo kabisa, ndio maana wanaweka ulinzi (anti-virus) sikuzote,
Vivyo hivyo na maisha ya mwanadamu yakiwa ovyo ovyo, hawezi kukwepa mapando ya mashetani ambayo yamezaa kila mahali. Mtu yeyote ambaye hajaokoka tayari kuna pepo fulani ndani yake.
Kwamfano, mwingine, labda mkristo ameokoka, halafu akiwa kanisani, anaanza kuruhusu masengenyo kinyume na mchungaji wake, au mama-mchungaji, sasa mtu kama huyo akiwa anaendelea na tabia hiyo..matokeo yake ni kwamba pepo la uchungu litamvaa, ataanza kuwachukia viongozi wake hata bila sababu, na kuzusha vita, na uharibifu hata wengine. Yeye atadhani ni tabia yake kumbe sio, bali pepo limeshamvaa la uchungu.
Nikupe huu ushuhuda, Kulikuwa na mama mmoja kanisa, kipindi chote ulikuwa ukikutana naye, anamzungumzia vibaya mama mchungaji wa kanisa alilokuwa mwanzo, hapo mwanzo alikuwa vizuri tu kiroho, lakini kwa jinsi siku zilivyozidi kwenda, akiendeleza chuki zake, , hali yake ilikuja kubadilika ghafla, akaomba tumwombee, tulipomwombea alilipuka mapepo, lile pepo likawa linasema “mama mchungaji” yaani asili yangu ni chuki kwa mama mchungaji, tulipolikemea likamwacha akarudia hali yake ya kawaida, akawa mtu mzuri tu.
Samsoni, alipokwenda kuwashindana na wafilisti, hakushughulika kwanza na wafilisti, bali mashamba yao ya ngano. (mapando yao). Kwa kuyachoma moto. Vivyo hivyo na sisi ili tuyamalize nguvu haya mashetani, tuangushe ngome zao. Ni lazima fikra zetu hasaa zielekee mapando yao.
Injili:
Kwamfano kuwaangusha wakuu wa giza sio kuwatumia makombora ya moto hapo angani. Hapana, bali ni kwenda kuhubiri injili ili watu wamsikie Kristo waokoke,
Ndio maana Yesu alipowatuma wanafunzi wake wawili wawili kuhubiri waliporudi Yesu aliwaambia ‘nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme’.
Kumbe anguko lake lilikuwa katika kuhubiri na si kumtumia makombora.
Maombi:
Hii ni silaha kubwa, ya kumpinga shetani. Maombi huruhusu, utendaji kazi wa Mungu ndani ya maisha ya mwamini, usipokuwa mwombaji tarajia shetani kuyapangalia maisha yao. Yesu alituagiza tukeshe kuomba tusije ingia majaribuni.
Upendo:
Upendo hupinga, wivu, chuki, uchungu, mashindano, uzinzi, n.k. ambayo haya yote huzaliwa mahali ambapo hapana upendo. Ni lazima kila siku wewe kama mwamini kila siku ujifunze kutendea kazi upendo….ili uondoe mazingira ya mashetani kuangua mayao yao hapo.
Neno:
Ukiwa na Neno la Mungu la kutosha ndani yako, adui hawezi kukushinda. Utakumbuka kule jangwani, shetani alipojaribu kumpandia Kristo maneno ya uongo kwa kupitia biblia, yeye mwenyewe alilitumia Neno la Kweli, kumpinga. Watu wengi wanavamiwa na maroho ya upotevu, kwasababu hawana Neno la Mungu mioyoni mwao. Jifunze kusoma biblia. Ni silaha inayoitwa Upanga.
Imani:
Imani huzaa ujasiri, na ujasiri hutoa mamlaka ndani yako. Biblia huiita imani “Ngao” Shetani anapenda kutumia silaha ya woga, ili kuzimisha utendaji kazi wa Mungu mioyoni mwetu. Hatuna budi kusimama kwa utimilifu wa imani kumtumikia Mungu.
Kukemea:
Fahamu adui ni mpingamizi sikuzote, hapembelezwi, bali analazimishwa kutoka, Yesu alimkemea shetani alipotaka kumjaribu kwa kinywa cha Petro, aliyakemewa mapepo yote sugu, yaliyokuwa ndani ya watu yawatoke. Hivyo na wewe pia ukutanapo na kazi hizi za mwovu, jifunze kutumia kinywa chako, kwa mamlaka uliyopewa na Kristo kukemea haraka sana, kila pepo, au kimelea chochote cha uovu kinachozaliwa na adui.
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, mashetani hawafi, lakini kazi zao zinakufa.. Hatuwaui hao, bali tunaziua kazi zao. Usipoteze muda mwingi kumrushia shetani mabovu hawezi kufa, bali tuma nguvu zako nyingi kurushia mabovu mapanda yake, kwa kanuni hizo tulizojifunza. Utawashinda kabisa kabisa.
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?
MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.
SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.
Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?
Ili tuelewe vizuri utofauti uliopo kati ya Agano jipya na la kale, tutafakari mifano ya kawaida ya maisha;
Hebu tafakari juu ya Elimu ya Awali (msingi) na Elimu ya Sekondari.. Utaona ulipokuwa shule ya msingi ulijifunza mahesabu ya kujumlisha na kuzidisha kwa kutumia vitu vya asili kama vijiti au mawe.. Lakini ulipofika sekondari ulitumia kikokotoo (yaani calculator).
Sasa mabadiliko hayo hayaifanyi elimu ya msingi kuwa batili, kwasababu tu vipo vikokotoo..La bali zinaithibitisha zaidi ile elimu ya msingi.. kwasababu kikokotoo (calculator) kinapiga mahesabu yale yale ya kujumlisha na kuzidisha kwa kasi na ufasaha zaidi.
Ni hivyo hivyo kwa Agano la kale na Agano jipya..
Mambo yaliyopo ndani ya Agano jipya ni mambo yale yale yaliyopo ndani ya agano la kale isipokuwa katika ufunuo bora zaidi na ufasaha mkubwa zaidi..
Tafakari tena mfano huu…
Toleo la kwanza la simu yako miaka 15 iliyopita..bila shaka lilikuwa ni mfano wa “tochi”, lenye mipaka mingi ya matumizi lakini toleo la pili la sasahivi ni “smart” ambalo unaweza kuingia internet, kupakua applications, kutazama video na hata kusikiliza nyimbo.
Kwahiyo Toleo jipya halijaja kuondoa chochote kilichopokuwepo kwenye toleo la kale, isipokuwa limeboresha zaidi vile vilivyopo na kuongeza vingine vya ziada.. maana yake Kama mtu alikuwa anasikiliza tu sauti pekee, sasa katika toleo jipya atasikika sauti pamoja na picha ya anayeongea..
Hali kadhalika kama toleo la kwanza la simu lilikuwa linachukua muda kuwaka na linahifadhi nambari za simu za watu 100 tu, basi toleo jipya litakuwa linawahi kuwaka na pia kuhifadhi namba za watu hadi 1,000.
Ni hivyo hivyo katika habari ya Agano la kale na Agano Jipya..
Agano jipya ni toleo bora zaidi la agano la kale, ni kitu kile kile isipokuwa kimeandikwa na kutendeka katika ubora mkubwa zaidi, na ufunuo mkubwa zaidi..
Kwamfano katika agano la kale, kafara na dhabihu zilikuwa ni za wanyama lakini tunapokuja katika Agano jipya dhabihu zimeboreshwa zaidi, badala ya kutumika damu za wanyama, inatumika damu ya MTU, YESU KRISTO (Ambayo ni bora zaidi).
Vile vile katika Agano la kale, amri ziliandikwa kwenye mbao za mawe kule mlima Sinai, lakini katika agano jipya amri na sheria za Mungu zinaandikwa katika mioyo yetu kiufunuo zaidi.
Yeremia 31:31 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu”.
Katika Agano la kale Uzinzi ulijulikana katika mwili tu (Kutoka 20:14) lakini katika Agano jipya uzinzi unajulikana katika mwili na roho kwa ufunuo bora zaidi (Soma Mathayo 5:28)
Katika Agano la kale uuaji ulijulikana katika mwili tu (Kutoka 20:13), lakini katika Agano jipya uuaji unajulikana katika mwili na roho kwa ufunuo bora zaidi (Soma Mathayo 5:21-22).
Katika Agano la Kale ni watu wachache tu ndio walishukiwa na Roho wa Mungu, (ambao walikuwa ni Manabii na Waamuzi) lakini katika Agano jipya watu wote wanayo fursa la kushukiwa na Roho Mtakatifu (Matendo 2:17-18).
Kwahiyo Agano jipya ni mwendelezo wa Agano la kale katika ubora zaidi na utimilifu na ufunuo mkamilifu, ndio maana Bwana YESU alisema hakuja kuitangua torati bali kuitimiliza.
Mathayo 5:17 “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza”.
Na Roho Mtakatifu ndiye Msaidizi wetu tuliyepewa ambaye atatusaidia kulielewa Agano la Kale na Agano jipya, hivyo hatuna budi kumtafuta huyo kwa bidii zote.
Na Roho Mtakatifu ni ahadi ya Bure kwetu kwa watu wote pasipo kujali umri (Matendo 2:37-38), tukimpata Roho Mtakatifu basi tutazidi kuielewa Biblia.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Orodha ya majina ya Miji ya Biblia (Agano la kale) na Sasa
Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?
Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?
SWALI: Nini maana ya Yeremia 31:30 “Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi”.
JIBU: Zamani za agano la kale katika taifa la Israeli, kulikuwa na usemi maarufu, unaosema “Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi”.
Kikawaida zabibu au matunda mengine yenye asidi nyingi mtu alapo , huwa meno yanatia ganzi, lakini kamwe haiwezekani mtu mwingine akatiwa ganzi kwa ulaji wa mwingine.
Hapa Waisraeli wakiwa wanamaanisha kuwa adhabu za Mungu huwa zinatembea hata kwa kizazi cha watu, Lakini Mungu kwa kinywa cha Yeremia anawasahihisha kuwa hilo si jambo lake..Anawaambia kila mtu ataadhibiwa sawasawa na uovu wake, wala watoto hawatauchukua uovu wa wazazi wao..Jambo ambalo alilirudia pia kwa kinywa cha Nabii Ezekieli (Ezekieli 18:20).
Lakini pia ukisoma muktadha wa vifungu hivyo, utaona anatoa unabii wa agano jipya ambalo atalifanya na watu wake kupitia Yesu Kristo, akimaanisha kuwa wokovu wake pia , utakuwa ni wa mtu binafsi, mmoja mmoja. Tusome habari yote tokea juu.
Yeremia 31: 27 Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapoipanda nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda, mbegu ya mwanadamu na mbegu ya mnyama.
28 Tena itakuwa, kwa kadiri nilivyowaangalia, ili kung’oa, na kubomoa, na kuangusha, na kuangamiza, na kutesa; kwa kadiri iyo hiyo nitawaangalia, ili kujenga, na kupanda, asema Bwana.
29 Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi.
30 Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi.
31 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
Hivyo vifungu hivi, vinatupa kutambua kuwa wajibu wa kulitunza agano la Mungu ni la mtu binafsi, sawasawa na alivyokuja kulifunua katika agano jipya kupitia Yesu Kristo, kwamba ijapokuwa wokovu umeachiliwa kwa wote, lakini haupokelewi kijumuiya, kifamilia, au kikabila, bali kibinafsi.
Kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe. (Wagalatia 6:5)
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tafsiri ya Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.
Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?
Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?
SWALI: Je! Ni sahihi kwa mkristo kujifunza, au kufundishwa na AI (Artificial Inteligence), mfano wa Chatgpt, deepseek n.k.
JIBU: Ili kujibu swali hili ni vema, kutambua mashine hizi za akili bandia (AI), zinafanya kazi gani.
Kwa ufupi ni kuwa AI, inafanya kazi ya kuchakata taarifa nyingi, kutoka katika vyanzo vingi vilivyopo mitandaoni, mfano vitabu, makala, sauti, machapisho n.k, na hivyo inazichanganya taarifa hizo zote kwa kuangalia muktadha unaofanana na kuzifupisha, na kukujibu.
Hivyo kimsingi, ni chombo ambacho kinatoa msaada mkubwa katika ulimwengu wa sasa, na ndio ukweli usiopingika..Kwasababu kinarahisisha utafutaji wa taarifa. Lakini pamoja na hayo haimaanishi kuwa kinatoa kwa ufasaha wote.
Sasa tukija kwenye eneo la kiroho. Je ni vema mkristo kwenda kuuliza AI, au kuandaa maombi au masomo kupitia hiyo, n.k.
Ukweli ni kwamba Imani, sio taarifa, ni zaidi ya taarifa.. Hizi AI, zinatoa tu taarifa lakini hazitoi mafunuo. Hazina pumzi ya Roho Mtakatifu ndani yake.
Ikiwa unataka kuongeza maarifa kwa sehemu fulani zinaweza kukusaidia, lakini sio kukujenga nafsi, kwani inahitaji pumzi ya Mungu na miongozo ya Mungu wewe kujengwa nafsi, na sio taarifa.
Kwamfano ikiwa wewe ni mchungaji halafu, kila inapokaribia jumapili unachowaza ni kwenda chatgpt, kuiambia ikuandalie somo la kufundisha jumapili, ndugu hapo hesabu kuwa umepotea kama sio kukengeuka… Tumia hiyo kwenye biashara zako, masomo yako, projekti zao lakini sio kwenye mambo ya kiroho. Hilo liepuke kabisa.
Kufundisha Neno inahitaji ‘Neno’ mwenyewe (Yesu) akae ndani yako, kwasababu ni UHAI sio taarifa (Waebrania 4:12) ndio hapo itakupasa kupiga magoti kwanza uombe, kwa muda mrefu, utafakari moyoni mwako, ukae kwenye utulivu wa kutosha, ndipo Mungu alipande somo lake moyoni mwako. Ambalo yeye mwenyewe anajua litakuwenda kuwagusa vipi watu wake, wenye changamoto mbalimbali, kwamfano, pengine mtu mmoja alikuwa anakaribia kwenda kujinyonga kwasababu ya ugumu wa maisha na mateso fulani, na Mungu kamwona anataka amsaidie, kwa kuliweka somo linalohusiana na mapito ya Ayubu ili ainuliwe imani. Kinyume chake kwasababu ya uvivu wako wewe unakwenda kuiambia chatgpt (akili bandia), ikuandalie somo. Halafu jumapili utakwenda na taarifa zao sio mafunuo. Badala uokoe roho inayokwenda kujinyonga, unaiambia, “leo tunajifunza kanuni kumi za kudumisha ndoa na mahusiano kibiblia”. Hapo unafanya nini sasa?
Au Neno fulani Bwana anataka kukupa la wakati wako, sasa ikiwa unakimbilia AI ikusaidie, hutaki kuchukua muda wako binafsi kutafakari na kuomba ‘jiandae kukutana na ukame wa kiroho.
Visaidizi hivi, hatupaswi kuvifanya ndio sehemu ya imani yetu, kwamba kila kitu tutegemee kule, hivi ni tone dogo sana kati ya bahari kubwa. Roho Mtakatifu alishatuandalia njia zake, kuu za kujengwa na yeye.
Wekeza zaidi, kuomba msaada kwa wakufunzi wako, viongozi wako, ndugu zako katika Kristo, wekeza katika maombi, mifungo, tafakari, na kujisomea mwenyewe Neno. kwa njia hizi hakika Bwana atasema nawe na kujengwa zaidi kuliko visaidizi. Lakini pia ikiwa pana umuhimu wa kujiongezea taarifa kwa vile unavyovijua, visaidizi hivi vitakufaa (Katika uangalizi maalumu), vinginevyo utajidumaza kiroho.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.
Kama mwamini ni lazima ujue kila kitakachotekea siku za mwisho, na kile Mungu alichokiahidi kuhusu maisha yajayo
Siku za mwisho zilianza wakati ule wa pentekoste Roho alipomiminwa duniani, kwa watu wote, na hizo zinaendelea hadi sasa mpaka wakati ambapo Kristo atatokea ulimwengu kwa mara ya pili kuleta hukumu na ufalme wake mpya.
Ni ukweli usiopingika kwamba tupo ukiongoni kabisa mwa siku za mwisho.Ingawa Biblia haitupi tarehe kamili (Mathayo 24:36), inatupa ishara na maagizo ya kuwa macho na wenye tumaini wa siku hiyo kuu.
Hii inaonyesha kwamba historia inaelekea kwenye mwisho ulioamriwa na Mungu.
Yesu aliahidi atarudi tena (Yohana 14:3). Kurudi kwake hakutakuwa kwa siri, bali kutakuwa kwa utukufu, nguvu na hukumu.
[11]Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.
. — Matendo 1:11
Hili si tumaini la kubahatisha — ni matumaini ya hakika yaliyowekwa juu ya ahadi za Mungu.
“Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu.” — Wakolosai 1:27
Kimaandiko, utukufu humaanisha:
Uwepo wa Mungu unaoonekana (Kutoka 33:18-20)
Utakatifu wake ulio mkuu na mkamilifu (Isaya 6:3)
Hali ya mwisho ya waamini — kufanana na Kristo milele (Warumi 8:17; 2 Wakorintho 3:18)
1 Wakorintho 15:52
[52]kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.
Hakutakuwa na ugonjwa, uchovu, wala mauti tena. Tutakuwa na miili kama wa Yesu baada ya kufufuka kwake (Wafilipi 3:20-21).
ii) Makao ya Milele
Yesu amekwenda kutuandalia makao (Yohana 14:2). Mbingu mpya na dunia mpya hazitakuwa na huzuni, machozi wala laana (Ufunuo 21:1-5).
iv) . Kumwona Mungu Uso kwa Uso
Hatutamtazama tena kwa imani bali tutamwona moja kwa moja (Ufunuo 22:4). Tutamtumikia na kumtukuza milele (Ufunuo 22:5).
🔸Kuwa Macho
Kanisa la kwanza liliishi kwa umakini mkubwa. Wakijua kuwa Yesu anaweza kurudi wakati wowote (Tito 2:13).
→ Usicheleweshe toba wala kuwa mzembe kiroho.
🔸Ishi Maisha Matakatifu
“Kila mwenye tumaini hilo ndani yake hujitakasa, kama Yeye alivyo mtakatifu.” — 1 Yohana 3:3
Ufahamu wa kurudi kwa Kristo unapaswa kutuchochea kuishi maisha ya utakatifu na utii.
🔸 Kuwa na Tumaini
Tufahamu kuwa Majaribu haya ni ya muda. Tumaini letu ni nanga ya roho zetu (Waebrania 6:19).
🔸 Tembea na Ujumbe kwa wengine.
Milele ni halisi. Ndio maana tunahubiri Injili—kwa sababu maisha ya watu yana hatma ya milele.
“Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo!” — Ufunuo 22:17
“Amina. Njoo, Bwana Yesu.” — Ufunuo 22:20
Sauti ya kanisa si hofu, bali ni shauku. Nyakati za mwisho si mwisho wa matumaini, bali ni mwanzo wa utukufu wa milele kwa wote waliomo ndani ya Kristo.
Mafundisho ya ziada kuhusu Siku za Mwisho.
KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.
NYUMBANI MWA BABA YANGU MNA MAKAO MENGI.
SIFA SITA (6), ZINAZOIKAMILISHA ILE SIKU YA BWANA ITISHAYO.
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Biblia unapozungumzia kuhusu kupewa jina jipya inamaanisha nini?
Vita vya kiroho ni mapambano yasiyoonekana kwa macho ya kawaida, yanayofanyika katika ulimwengu wa roho kati ya ufalme wa Mungu na ufalme wa giza (Shetani na mapepo yake).
Ingawa hayaonekani, lakini vita vyao ni vibaya zaidi ya vile vinavyoonekana, kwani vinamuathiri mwanadamu kotekote, mwilini lakini pia rohoni katika mawazo yetu, hisia, tabia, ndoa, huduma, na hata afya.
Biblia inasema:
Waefeso 6:12
Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho
Mfano:
Mtu anayeokoka anaweza ghafla kuanza kupata majaribu makubwa ya kuudhiwa na watenda dhambi, jambo ambalo huko nyuma hakuwahi kuliona, mpaka anawaza kwamba maisha wa wokovu ni magumu. Hili ni shambulio la kiroho, linalolenga kumrudisha nyuma kiroho.
Ulipompokea Yesu, uliingia katika Ufalme wa Mungu. Na moja kwa moja ulifanyija adui wa Shetani.
Shetani alikupoteza na sasa anafanya kila juhudi kukurudisha, kukuzuia usikue kiroho, au kukushawishi uishi maisha yasiyo ya ushindi.
“Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake.” (Wakolosai 1:13)
Maandiko yanatuambia Shetani alikuwa malaika aliyeasi (Isaya 14:12–15).
Anaendesha vita kwa kutumia uongo, hofu, mashaka, tamaa, magonjwa, migawanyiko, na kushambulia akili zetu.
Uongo – Anapandikiza mawazo kama: “Hujasamehewa” au “Mungu hajasikia maombi yako.”
Vishawishi – Hutumia tamaa za mwili, pesa, au kiburi kukushawishi.
Kuchosha kiroho – Anakufanya uchoke au kupoteza hamu ya kusoma Biblia au kuomba.
Kuvuruga mahusiano – Kupitia fitina, chuki, au hasira isiyoisha.
“Yeye ni mwongo na baba wa huo.” (Yohana 8:44)
Waefeso 6:10–18 inatupa silaha saba za kiroho za kujilinda na kushambulia nguvu za giza:
3.1 Kweli kiunoni.
Kuwa na ujuzi wa kweli ya Neno la Mungu na kuiishi.
Hii inasaidia kutambua uongo wa Shetani.
Mfano: Unapofikiri “Mungu hanipendi,” Neno la Mungu linasema “Hakika amekupenda kwa upendo wa milele.” (Yeremia 31:3)
3.2 Dirii ya Haki
Maisha ya uadilifu na kutokubaliana na dhambi.
Haki hii inatoka kwa Yesu, sio kwa matendo yako.
“Yeye asiyemjua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye.” (2 Wakorintho 5:21)
3.3 Viatu vya Injili ya Amani (utayari miguuni)
Kuwa tayari kueneza habari njema na kuishi kwa amani.
Mtu aliye tayari kushuhudia haogopi mapambano.
3.4 Ngao ya Imani
Imani huuzima mishale ya hofu, mashaka, na huzuni.
Unaposema, “Mungu atanitetea,” hata wakati hali ni ngumu, hiyo ni imani.
3.5 Chapeo ya Wokovu
Linda mawazo yako kwa kufikiri mambo yanayohusiana na wokovu wako.
Kukumbuka kwamba umeokolewa hukufanya usiyumbishwe na hila za adui.
3.6 Upanga wa Roho (Neno la Mungu)
Neno la Mungu ni silaha ya kushambulia.
Yesu alilitumia aliposhambuliwa na Shetani (Mathayo 4:1–11).
3.7 Maombi
Maombi ni silaha ya nguvu inayoweza kubadilisha hali yoyote.
Omba kwa ajili yako, familia yako, kanisa, na hata waliopotea.
Waefeso 6:18
[18]kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
Soma Biblia kila siku – Neno la Mungu hukujenga kiroho.
Omba kila siku – Ushindi unapatikana kwa kusali daima.
Kataa dhambi kimaamuzi – Usingojee hisia, fanya uamuzi wa kiroho.
Tembea na Wakristo wengine – Ushirika hukupa nguvu.
Fanya ibada (Sifu na abudu) – Hukuza uwepo wa Mungu na huvunja vifungo vya giza.
Tubu haraka unapokosea – Usimpe shetani nafasi ya kukushitaki.
5.1 Vita vya Kiroho Sio:
Kila shida ni mapepo – Baadhi ya mambo ni matokeo ya maamuzi au mazingira. Hivyo ni wajibu kuchunguza chanzo cha tatizo ni je Adui kweli au!
Kukemea tu– Mamlaka ya kiroho hutegemea maisha ya utii kwa Kristo. Utiifu wako
Kuwa na hofu – Kwamba tuigope, au tuishi kwa mashaka, kana kwamba tuwezekeze nguvu zetu zote kupamba a nayo. Hapana Tuna mamlaka kupitia Yesu.
“Nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge, na kushinda nguvu zote za adui; wala hakuna kitakachowadhuru.” (Luka 10:19)
Ukiwa ndani ya Kristo, huna sababu ya kuogopa. Mapambano yapo, lakini ushindi ni wako kupitia Yesu Kristo.
“Katika mambo haya yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.” (Warumi 8:37)
Waefeso 6:11 – “Vaeni silaha zote za Mungu…”
Yakobo 4:7 – “Mtiini Mungu, mpingeni ibilisi naye atawakimbia.”
2 Wakorintho 10:4 – “Silaha za vita vyetu si za mwili…”
1 Petro 5:8 – “Muwe na kiasi na kukesha… ibilisi yenu… hutafuta mtu wa kummeza.”
Masomo ya ziada kukusaidia kuvishinda vya kiroho
NGUVU YA “KUKATAA” UNAPOPAMBANA VITA VYA KIROHO
Maana ya Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;
JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
BWANA ni mtu wa vita, BWANA ndilo jina lake.(Kutoka 15:3)
Mishale ya moto ya mwovu inayozungumziwa kwenye Waefeso 6:16 ni ipi?
Kila mwamini ameitwa kuieneza injili ya Yesu Kristo. Ambayo huitwa habari njema.
Mathayo 28:19-20
[19]Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
[20]na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Habari njema ni nini? Ni habari za wokovu kwa mwanadamu, ulioletwa na kupitia mtu mmoja Yesu Kristo kwa tendo la kufa na kufufuka kwake kaburini.
Kama tulivyotangulia kuona hapo juu, kuwa siku Yesu alipoondoka hakutuacha bila wajibu, bali kila mmoja wetu alipewa sehemu ya huduma katika shamba lake. Ya kuenenda ulimwenguni kote kuwafanya watu kuwa wanafunzi wake.
Kazi hii sehemu nyingine anaifananisha na talanta, ambayo amempa kila mwamini na anataka kila mmoja aizalishe (Mathayo 25:14-30), sehemu nyingine anaifananisha na matunda, anasema sisi ni matawi na yeye ni mzabibu kwamba tumzalie matunda, (Yohana 15:1-7),sehemu nyingine nyingine anaiita posho, huku yeye akijiita bwana, na sisi mawakili wake, akitutaka tutoe posho kwa wakati kwa watu wake, (Luka 12:42-48)
Sasa ukiangalia utaona sehemu zote hizo tunazofananishwa nazo, kama mtu hajafanya chochote au hajazalisha chochote, haachwi hivi hivi, bali kuna aidha kuondolewa sehemu ya thawabu yake, au kukataliwa kabisa.
Ndio maana ni lazima tujue mwamini yoyote yule, ni lazima aishi maisha ya kuwashuhudia wengine injili.
Warumi 10:14 Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri?
Ni lazima ujue kuwa hukumu ipo na kuzimu pia ipo, na inawameza wengi, Na watu hawawezi kuokoka tu wenyewe hivi hivi bila kusikia injili kama wewe ulivyosikia. Tengeneza picha unamwona baba yako, au mama yako kwenye ziwa la moto, halafu anakuambia laiti ningelijua ukweli nisingekuwa huku, utajisikiaje? Ukilijua hili basi huruma ya ki-Mungu itakujaa tu ndani yako, na utasukumwa kujitoa kuwaendea wenye dhambi, kama Kristo alivyotujia sisi, kutoka mbinguni, na kama mitume walivyowaendea watu, ili kuhakikisha wanaokoka.
Luka 15:7 Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu
Mungu hufurahi malaika pia hufurahi, wanapoona roho za watu zinaokoka,duniani, Hivyo sisi kama wana wa Mungu ni wajibu wetu kuyatenda yale tu ambayo yanamfanya Baba yetu afurahi, na hilo si lingine zaidi ya kutoka na kwenda kuwashuhudia watu injili.Hapo tunaufanya moyo wa Mungu hufurahi sana.
Ni ukweli usiopingika kuwa kila mmoja wetu kuna mahali Mungu amemtoa mpaka hapo alipomfikisha, anayo mengi ya kushuhudia kuhusu uzuri wa Kristo.
Wazia yule kichaa ambaye alikuwa katika hali mbaya kule makaburini, uchi, usiku na mchana, ameshindikana kwa vifungo vyote. Lakini Yesu alipokutana naye saa ile ile alipona, akataka kuambatana na Yesu, lakini Yesu akamwambia nenda nyumbani kwa watu wako uwasimulie matendo makuu ambayo Mungu amekutendea, Na tunaona alikwenda kusimulia yote mji ule, na watu wengi wakamwamini Kristo, kwa ushuhuda wake tu.
Marko 5:20 Akaenda zake, akaanza kuhubiri katika Dekapoli, ni mambo gani makuu Yesu aliyomtendea; watu wote wakastaajabu
Hata wewe, wazia uzuri ulioupata pindi ulipompokea Kristo, utamani pia mwingine aupate, na huo ndio upendo, umeonja uzuri wa Kristo unakwenda kuwaambia na wengine mfano tu wa yule mwanamke pale kisimani.
Sawasawa na agizo ambalo Yesu alimwagiza yule mtu ambaye aliteswa Na mapepo akamfungua. (Marko 5:19-20)
Hii ni njia bora, ambayo utapata nguvu ya kikanisa, kwasababu mule akutanapo na vipawa mbalimbali vya Mungu, hurahisisha zaidi moyo wake, kuamini ujumbe uliompelekea.
Ishi maisha yanayomuhakisi Kristo. Kwasababu matendo yako ni injili kuwa wengine kumgeukia Kristo. (1Petro 3: 1-2)
Hivi Ni kama vitabu, kanda, luninga, na kwa dunia ya sasa, Vitu kama whatsapp, websites, panaweza pakawa mahali Ambapo injili yetu kupaa sana na kuwavuta wengi ndani ya ufalme. Ulimwengu wa sasa, upo mtandaoni, hivyo tumia fursa hiyo, kushea mafundisho, mahubiri sahihi ya Neno la Mungu kwa marafiki zako, familia, ndugu, majirani, huko huko Mungu ataanza kazi ya wokovu ndani yao.
Haya ni mambo ya kukumbuka kila uendapo kushuhudia, ili usishindwe na hofu.
Usiwe na hofu ikiwa huoni mwitikio wowote, kwa yule unayemweleza habari ya wokovu, fahamu kuwa ipo mbegu imemwingia ambaye itakuja kumea tu kwa wakati wake.
Uinjilisti wa wawili huwa mrahisi zaidi ya ule wa mmoja (isipokuwa unao uzoefu). Yesu aliwatuma wanafunzi wake wawili wawili, alijua ujasiri utaongezeka lakini wangeweza kufanya zaidi, pale mmoja anapochoka anamtia nguvu mwenzake. Vivyo hivyo na wewe katika hatua za awali ongozana na kiongozi wako, au mshirika mwenza katika kazi ya injili.
Yohana 3:16
Warumi 3:23
Warumi 6:23
Warumi 10:9–10
2 Wakorintho 5:17
Kwa mwongozo wa namna ya kutembea katika baadhi ya vifungu hivyo, pitia hili fundisho >>> NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.
Mafundisho ya ziada
KWANINI TUNAPASWA KWENDA KUIHUBIRI INJILI KWA UJASIRI WOTE?
IHUBIRI INJILI, KILA MAHALI KWASABABU AKUZAYE NI MUNGU.
HEKIMA NANE(8) ZA KIUINJILISTI, KATIKA KUWAVUA WATU KWA KRISTO.
JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?
KUTOKUIHUBIRI INJILI,KUNA MADHARA GANI?
KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Fahamu maana ya Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;
KILA MTU NA AMCHE BABA YAKE NA MAMA YAKE.
MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.
Swali: Huwa tunasema.. “tusome maandiko” na wakati mwingine “tusome Neno”..ipi tofauti ya maneno haya mawili?.
Jibu: Tuanze na Neno au Neno la Mungu.
“Neno” ni sauti ya MUNGU yenye ujumbe inayokuja kwa mtu kwa njia ya maono au ndoto au njozi..
Kwamfano katika biblia utaona lugha iliyotumika kwa manabii wote waliojiliwa na sauti ya Mungu iliyobeba ujumbe ni hiyo ya “Neno la Mungu”
Mwanzo 15:1 “Baada ya mambo hayo NENO LA BWANA likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.
Soma pia 1Wafalme 17:8, Isaya 38:4, Yeremia 1:11, Ezekieli 1:3, Ezekieli 12:21, Hosea 1:1, Yona 1:1, Mika 1:1, Sefania 1:1 n.k
Hata sisi wakati mwingine tunapotaka kuzungumza na mtu, tunaweza kutumia lugha hiyo kwa kumwambia “nina neno nataka kusema nawe”… au kama kuna mtu amekuambia jambo unaweza kusema “mtu Fulani kaniambia neno”.. kwahiyo ni hivyo hivyo hata katika biblia, Neno la Mungu ni sauti ya MUNGU.
Sasa kama “Neno” tafsiri yake ndio hiyo, vipi kuhusu “Andiko”?
Andiko ni Neno la Mungu lililo katika maandishi… Kwamfano; hilo Neno lililomjia Abramu, kwake yeye ni Neno la Mungu lakini kwetu sisi ni andiko, ndio maana tunalisoma.. Na Nguvu ya andiko na Neno ni ile ile.
Hivyo maneno ya Mungu yote yaliyoandikwa katika Biblia ni “MAANDIKO”.. Hata wewe maneno yako unayoyasema unaweza kuyaandika katika kitabu, na yakawa ni maandiko kwasababu ni maneno yaliyoandikwa.. Hali kadhalika, kila Neno la Mungu kwenye Biblia ni andiko.
Hivyo mtu anayesema “tusome maandiko” na Yule anayesema “tusome Neno la Mungu” ni kitu kimoja.. na nguvu ni ile ile..
Na kila Andiko lenye pumzi ya Mungu linafaa kwa mafundisho, kuonya, kuongoza na kuadibisha..
2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”
Kwa urefu kuhusiana na kazi ya MAANDIKO inayofanya kwa mtu fungua hapa >>MAMBO MANNE(4) YAFANYAYO NENO LA MUNGU.
Je umempokea YESU?, Umebatizwa katika ubatizo sahihi?..una uhakika Bwana YESU akirudi unaenda naye?.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?
TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.
ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.