YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.

YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.

Yote namtolea Yesu_tenzi za rohoni|Swahili hymn.


Wimbo huu uliandikwa na ndugu mmoja wa kimarekani aliyeitwa Judson W. Van DeVenter, Ndugu huyu alilelewa katika mazingira ya kikristo, aliokoka akiwa na miaka 17, kuanzia huo wakati wito wa kujitoa kikamilifu ulianza  kuita ndani yake,lakini bado hakufanya uamuzi huo. DeVenter alifanikiwa kusoma  mpaka chuo kikuu na kutunikiwa shahaba ya Sanaa, aliajiriwa kama mwalimu na mwongozaji katika shule za sanaa, hiyo ilimfanya aweze kusafiri sehemu nyingi mbalimbali katika bara la Ulaya kutokana na kazi yake ya sanaa.

Zaidi ya hilo alisomea pia na kufundisha elimu ya muziki, ilimchukua miaka 5 mpaka “Kumtolea yote Yesu”, Na hiyo ilikuwa ni baada ya marafiki zake kumshawishi sana, aingie katika kazi ya kumtumikia Mungu.

Mwaka 1896 Siku moja alipokuwa anafanya huduma ya muziki katika kanisani, hii ndio siku aliyoamua kuyasalimisha maisha yake ya ki-utumishi moja kwa moja kwa Kristo akiwa na miaka 41, aliamua kujitoa moja kwa moja kwa ajili ya kuifanya kazi ya unjilisti, na ndipo hapo huu wimbo “Yote namtolea Yesu” ulipozaliwa ndani ya moyo wake.

YOTE WA YESU.

Yote Namtolea Yesu.
Nampa moyo wote,
Nitampenda siku zote,
Namwandama kila saa.
 
Yote kwa Yesu,
Yote kwa Yesu,
Yote kwako, Ee Mwokozi,
Natoa sasa.
 
Yote namtolea Yesu,
Nainamia pake;
Nimeacha na anasa,
Kwako Yesu nipokee
 
Yote kwa Yesu,
Yote kwa Yesu,
Yote kwako, Ee Mwokozi,
Natoa sasa.
 
 Yote namtolea Yesu,
Nifanye niwe wako;
Nipe Roho yako, Bwana,
Anilinde daima,
 
Yote kwa Yesu,
Yote kwa Yesu,
Yote kwako, Ee Mwokozi,
Natoa sasa.
 
Yote namtolea Yesu,
Nami naona sasa;
Furaha ya ukombozi;
Nasifu jina lake. 
 
Yote kwa Yesu,
Yote kwa Yesu,
Yote kwako, Ee Mwokozi,
Natoa sasa.

*****

Je! Na sisi tunapouimba wimbo huu tunaweza kumtolea Yote Yesu?. Je! mali zetu tunaweza kumpa yeye, nguvu zetu tunaweza kuzielekeza kwake?, akili zetu tunaweza kuzitumia ziitende kazi ya Mungu? Kama sivyo basi wimbo huu tutauimba kinafki.

Bwana atutupe kutambua hayo.

Shalom.

Je! Umeokoka? Ikiwa bado hujaokoka na unahitaji kuokoka leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA


Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo mbalimbali ya Neno la Mungu, kwa njia ya whatsapp yako, basi tutumie ujumbe kwa namba hii :+255 789001312

Mada Nyinginezo:

YESU KWETU NI RAFIKI

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

MAONO YA NABII AMOSI.

 

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments