Nyuni ni nini?(Mathayo 13:32, Sefania 2:14)

Nyuni ni nini?(Mathayo 13:32, Sefania 2:14)

Nyuni ni neno linalomaanisha ndege.

Hivi ni baadhi ya vifungu katika biblia vinavyolitaja neno hilo;

Mathayo 13:31 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake;

32 nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake”.

Zaburi 102:5 “Kwa ajili ya sauti ya kuugua kwangu Mifupa yangu imegandamana na nyama yangu.

6 Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, Na kufanana na bundi wa mahameni”.

Sefania 2:14 “Na makundi ya wanyama watalala kati yake, wanyama wote wa mataifa; mwari-nyuni na nungu watakaa juu ya vichwa vya nguzo zake; sauti yao itasikiwa madirishani; vizingitini mwake mtakuwa ukiwa; kwa maana ameifunua kazi ya mierezi”.

Soma pia Kumb 14:11,Ayubu 12:7

Kibiblia watu wa mataifa(wasiomjua Mungu) wanafananishwa na nyuni wa angani, na ndio maana utaona Bwana Yesu anaufananisha ufalme wa mbinguni na chembe ya haradali na kusema japo ni ndoto kuliko mbegu zote..Lakini inapokuwa ndani ya mtu inageuka na kuwa kubwa sana, kiasi cha kutoa matawi makubwa na watu kukaa chini yake kupumzika(yaani kujifunza Neno la Mungu, na kupokea baraka zote)

Hivyo na sisi pia tunapewa hamasa, tupende kuutafuta ufalme wake, kwani leo hii unaweza kuonekana ni kitu kisichokuwa na maana, lakini kama tukiendelea kumtafuta Mungu na kutaka kujua mapenzi yake ni nini maishani mwetu, Basi kesho tutakuwa ni msaada mkubwa kwa maelfu ya watu(Nyuni) kumjua yeye.

Bwana akubariki.

Tazama tafsiri ya maneno mengine ya biblia chini.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Arabuni maana yake ni nini?

Kutabana ni nini? (Mika 5:12)

Fumbi ni nini?(Ayubu 6:15)

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments