Nchi ya Nodi ambayo Kaini alikimbilia ndio nchi gani kwasasa?(Mwanzo 4:16).

by Admin | 25 October 2022 08:46 pm10

Jibu: Tusome,

Mwanzo 4:15 “BWANA akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. BWANA akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga.

16 Kaini akatoka mbele za uso wa BWANA, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni

17 Kaini akamjua mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Henoko; akajenga mji akauita Henoko, kwa jina la mwanawe ”.

“Nodi” sio jina la nchi kama vile Tanzania, Kenya au Uganda bali ni sifa ya nchi..Tafsiri ya neno Nodi ni “kutanga”. Hili ni neno la kiebrania lenye maana hiyo ya “kutanga”.

Kwahiyo biblia iliposema kuwa Kaini alienda nchi ya Nodi, haikumaanisha kuwa alienda kwenye Nchi inayoitwa “Nodi”.. La! bali ilimaanisha kuwa Kaini alienda katika Nchi ya “Kutangatanga”.  Hakuwa na kikao maalumu, wala nchi maalumu sawasawa na laana Bwana Mungu aliyomlaania.

Mwanzo 4:11 “Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;

 12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; UTAKUWA MTORO NA MTU ASIYE NA KIKAO DUNIANI”.

Vile vile dhambi inaweza kutufanya tusiwe watu wa vikao duniani, (tukawa watu wa kutanga tanga tu kutwa kuchwa). Tunazunguka huku na kule kutafuta unafuu wa maisha lakini hatuoni..Acha leo kutanga tanga, Suluhisho ni moja tu!, mkimbilie Bwana Yesu leo, mlilie akusamehe dhambi zako na akuokoe, kwasababu damu yake hata sasa bado inaondoa dhambi..

Na ukifanya hivyo kwa imani atakuokoa na laana ambayo imetajwa juu ya wote wamwachao Bwana..

Zaburi 107:4 “Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; Hawakuona mji wa kukaa. 

5 Waliona njaa, waliona na kiu, Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao. 

6 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao. 

7 Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa”.

Bwana Yesu akubariki.

Ikiwa utatamani kujua zaidi Mke wa Kaini alitokea wapi basi fungua hapa >>>JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kaanani ni nchi gani kwasasa?

SISI NI WINDO BORA SANA, LA DHAMBI.

CHOCHOTE UMFANYIACHO KRISTO KINA THAMANI.

ANAKUJA KAMA “MWIVI” NA SI KAMA “ASKARI” FANYIKA CHOMBO CHA THAMANI.

LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/10/25/nchi-ya-nodi-ambayo-kaini-alikimbilia-ndio-nchi-gani-kwasasamwanzo-416/