ANAKUJA KAMA “MWIVI” NA SI KAMA “ASKARI” FANYIKA CHOMBO CHA THAMANI.

ANAKUJA KAMA “MWIVI” NA SI KAMA “ASKARI” FANYIKA CHOMBO CHA THAMANI.

Kikawaida tumezoea kujifunza mambo mema kutoka kwa maaskari, kwamfano pindi tunapoyaona majeshi ya polisi katika magwaride yao, jinsi yalivyo na utaratibu mzuri, huwa tunavutiwa nayo.. tunapoyaona yakiwa katika mafunzo ya kukamata wahalifu, tunavutiwa nayo.. na hata wakati mwingine kuitamani kazi ya uaskari..

Lakini kamwe huwa hatuvutiwi na tabia za mwizi!, na wala hatutamani kuwa wezi. Kwasababu mwizi, anakuja kwa lengo la kuchukia kitu ambacho ni cha mwingine, pasipo taarifa!..jambo ambalo linaudhi sana na lisilokubalika.

Lakini Neno la Mungu linasema “Bwana Yesu atakuja kama mwivi” na “si kama askari”

Na kama tunavyojua mwizi lengo lake ni kuiba vile vya thamani na si kingine!. Hivyo Bwana Yesu anakuja duniani kuiba vile vilivyo vya thamani na kuviacha vile visivyo vya thamani..

Ulimwengu huu unafananishwa na NYUMBA.. ambamo ndani yake kuna watu wema na waovu. Na mkuu wa huu ulimwengu ni shetani, na malaika zake..

 Kama vile mwizi ajavyo usiku, haji kuiba vitu vibaya bali vile vizuri vyenye thamani, ndivyo Bwana Yesu atakavyokuja kuiba watu wake  (wale walio watakatifu na wenye thamani machoni pake) na kwenda nao mbinguni.

Kufumba na kufumbua, ufalme wa giza utashangaa baadhi ya watu hawapo tena duniani,  wale ambao walidhani wapo chini yao, wale ambao walidhani siku moja watawatumia kwa shughuli zao za giza.. watashangaa wametoweka duniani, siku hiyo hata shetani haijui.. ghafla atashangaa tu watu baadhi hawapo!

Luka 17:34 “Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.

35  Wanawake wawili watakuwa wakisaga pamoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.

36  Watu wawili watakuwa shambani, mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa”

Je! Hiyo sio tabia ya mwizi??.. hebu jiulize unakaa na mwanao ndani, mmelala asubuhi unakuta hayupo na milango imefungwa kwa ndani vile vile, umekaa na mume wako ghafla unashagaa katoweka..upo kazini na mtu Fulani ambaye unamjua ni mtu anayejishughulisha sana na masuala ya wokovu, ghafla unashangaa hayupo!!!

Ndugu yupo Mwivi anayeutazama sasa ulimwengu kutoka juu!.. Anatazama vile vilivyo vya thamani!.. anapanga mipango!.. na mipango imeshakamilika kitambo sana, atakuja saa tusiyodhani.. kufumba na kufumbua wale tuliokuwa tunawajua wanampendeza Mungu, watanyakuliwa.. na mkuu wa ulimwengu huu (atakasirika) kwasababu vile vilivyo vya thamani vimeondoka!, kama vile mtu anavyoamka asubuhi na kukuta vitu vyake vya thamani vimeibwa, atajikuta anavichukia hata vile vilivyoachwa na hata kuviharibu kwa hasira.

Ndicho kitakachotokea baada ya unyakuo, wakati watakatifu wapo mbinguni,  wale walioachwa watakutana na ghadhabu ya mpinga kristo, katika dhiki kuu.

Je wewe ni chombo cha thamani?..

Kumbuka vyombo vya thamani ni wale wote waliomwamini Yesu, na kutubu dhambi zao, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu na kupokea Roho Mtakatifu.. Hao ndio biblia inawaita watakatifu.

Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.

Na hao ndio waliopo sasa katika shabaha ya Bwana, (yaani kuja kuwatwaa na kwenda nao mbinguni). Lakini wengine watakaosalia wakati wa kurudi Bwana, biblia inasema watapitia dhiki kuu, pamoja na mapigo ya siku ya Bwana.

Je wewe ni chombo cha thamani ulimwengu?.. au kisicho cha thamani?

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

USINIE MAKUU.

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments