Ayari ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Ayari ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Ayari ni mtu aliyekosa utu,  mchoyo  na asiyejali watu,  anayejipenda mwenyewe, na mwenye hasira nyingi na madanganyifu. Kwa ufupi ni mtu asiyependa watu kwa ujumla.

Mfano wa watu hawa katika biblia ni Nabali, ambaye pamoja na kwamba Daudi na wenzake walimfanyia wema mwingi, hakujali kuwastahi hata kwa maji au kwa chakula (1Samweli 25).. na mwingine ni yule Tajiri wa Lazaro ambaye aliishi hapa duniani katika maisha ya anasa na ya ubinafsi, akafa katika dhambi zake, akaenda kuzimu.(Luka 16)

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi kwenye biblia;

Isaya 32:5 “Mpumbavu hataitwa tena mwungwana, WALA AYARI HATASEMWA KWAMBA NI KARIMU.

6 Maana mpumbavu atanena yaliyo upumbavu, na moyo wake utafanya maovu, ili kutenda hila na kusema yasiyo kweli juu ya Bwana, ili kuziacha nafsi za watu wenye njaa hazina kitu, na kukikomesha kinywaji chake mwenye kiu.

7 Tena VYOMBO VYAKE AYARI NI VIBAYA; hutunga hila mbaya, ili kuwaangamiza wanyonge kwa maneno ya uongo, mtu mhitaji ajaposema maneno yenye haki.

8 Bali mwungwana huwaza mambo ya kiungwana, naye hushika sana mambo ya kiungwana”.

Kwa mfano katika habari hiyo, kama ukianzia  mistari ya juu mstari wa kwanza utapata picha kamili ni nini kilikuwa kinazungumziwa,  anasema..

Isaya 32:1 Tazama, mfalme atamiliki kwa haki, na wakuu watatawala kwa hukumu.

Huo ni unabii unaomzungumzia Kristo katika utawala wake wa amani utaokuja huko mbeleni, kwasababu yeye ndiye atakayemiliki kama mfalme, Na katika huo utawala wake, hakutakuwa na kupindisha haki, kama ilivyo sasahivi, kwa sasahivi fisadi ndio anaonekana mwerevu, Mtu mbinafsi, ndiye anayeonekana  ana akili. Wapumbavu ndio wanaopewa uongozi, mtoa rushwa ndiye anayeonekana  ni mkarimu, Ayari (mtu asiyependa watu) ndio anayehesheshimika na kuogopeka katika jamii n.k.

Lakini katika huo utawala wa Amani wa miaka 1000 wa Yesu Kristo hapa duniani, hilo jambo halitakuwepo,  anasema..

“Mpumbavu hataitwa tena mwungwana, wala AYARI hatasemwa kwamba ni karimu”.

Hii ikiwa na maana kuwa watenda haki ndio watasifika katika haki yao, bali watendao uovu, watakutana na fimbo ya chuma ya Yesu Kristo, (Ufunuo 2:27).

Fahamu kuwa, kwa Mungu hakuna upendeleo, hata leo hii ikiwa utakufa katika hali yako ya dhambi, hakuna nafasi ya pili, kama umestahili mbingu, utakwenda mbinguni, kama umestahili Jehanum, utakwenda Jehanum, nafasi ya kutubu ipo leo, haipo baada ya kufa, hivyo mgeukie Yesu Kristo ayaokoe Maisha yako. Kwasababu hizi ni siku za mwisho.. Wakati ambao mtu kufanya dhambi ndio anasifiwa.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO? 

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

Mafundisho

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments