Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

SWALI: Warumi 5:7 “Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki; lakini yawezekana mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu aliye mwema”.

Bwana Yesu asifiwe mtumishi wa Mungu, Naomba ufafanuzi wa hilo andiko na pia nipate  kujua tofauti kati ya mtu mwenye haki na mtu mwema.


JIBU: Pamoja na kwamba Bwana Yesu kuja hapa duniani kuwaokoa watu waliopotea kabisa, (yaani watu wenye dhambi wasio na vimelea vyovyote wa utu, kama vile wauaji, wahalifu, mafisadi n.k.) alikuja pia kuwaokoa watu walio wema.

Sasa tukirudi kwenye mstari huo tunaona mwandishi anajaribu kutofautisha  kati ya mtu mwema na mtu mwenye haki.

Mtu mwenye haki ni yupi?

Mtu mwenye haki ni mtu mkamilifu sana, asiyekuwa na kosa lolote mbele za Mungu, Mtu wa namna hii kiuhalisia hajawahi kuwepo tangu duniani iumbwe. Kama wangekuwepo hakukuwa na sababu ya Yesu Kristo kushuka hapa duniani, na kufa kwa ajili yao, wapate wokovu, ya nini sasa? Wakati tayari wanaoukamilifu wote ndani yao..hakuna doa lolote ndani yao?

Na ndio maana hapo inasema.. ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki..

Lakini mtu mwema, ni mtu ambaye sio mwovu sana, ni mtu ambaye anajaribu kuishi maisha ya kawaida tu katika jamii, anajiheshimu, anawasaidia wengine, anao utu, anajitahidi kutenda mema kwa bidii na kufanya mambo yake kwa utulivu bila kuvunja sheria yoyote ya jamii husika au nchi n.k. Lakini katika jitihada zake zote, bado hajaweza kufikia kipimo cha yeye kuwa mtu mwenye haki mbele za Mungu..Yaani nguvu zake bado hazijajitosheleza kumfanya awe mkamilifu..hao ndio watu wema mwandishi anaowazungumzia hapo. Na ndio maana ukianzia mstari wa juu anasema;

Warumi 5:6 “Kwa maana HAPO TULIPOKUWA HATUNA NGUVU, wakati ulipotimia, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu.

7 Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki; lakini yawezekana mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu aliye mwema”.

Unaona anasema “hapo tulipokuwa hatuna nguvu”, ikiwa na maana tulishajaribu kujitahidi kwa nguvu zetu na kwa matendo yetu kumpendeza Mungu lakini bado tukashindwa kuufikia ule ukamilifu…Na  ndio Kristo alikuja kutufia pale msalabani, ili sasa kwa kumwamini tu yeye, tuhesabiwe haki mbele za Mungu.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa, kama tungekuwa wenye haki, basi Kristo asingekuja duniani, lakini kwasababu sote tumepungukiwa na utukufu wa Mungu,  (nikiwa na maana watu waovu sana na wa kawaida), Sote tunamuhitaji Kristo ayabadilishe maisha yetu. Kwasababu pasipo yeye, haijalishi tuna dini nzuri kiasi gani, tunafanya mazuri kiasi gani,  tunasaidia maskini wengi kiasi, bado hutuwezi kumpendeza Mungu, bila Kristo. Kwasababu hayo tayari yalishashindikana tangu zamani.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

USIOMBE MAOMBI YASIYOKUWA NA MAJIBU NA WALA USIMTUKANE MUNGU.

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

ESTA: Mlango wa 4

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments