KANSA/SARATANI INATIBIKA.

KANSA/SARATANI INATIBIKA.

Ni kweli Mungu amewapa wanadamu maarifa, ili yale yanayowezekana katika uwezo wao yatendeke, lakini  ipo wazi kuwa si kila tatizo mwanadamu anaweza kulitatua haijalishi ataonyesha bidii kubwa kiasi gani.

Yapo magonjwa ambayo, sisi kama wanadamu hatuwezi kuyatibu, isipokuwa Mungu tu peke yake.

Yeye mwenyewe alisema..

Yeremia 32:27 “Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza”?

Na sehemu nyingine pia Yesu alisema..

Mathayo 19:26b … Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu YOTE YAWEZEKANA.

Ikiwa na maana hakuna moja linaloshindikana kwake.

Huo ugonjwa wa Satarani, iwe ni ya koo, au ya damu, au ya ngozi, au ya matiti, au ya Shingo ya mfuko wa kizazi, au ya utumbo, au kongosho, au ini, au Mapafu ,au ubongo, au macho, au mifupa, au misuli, au Matezi n.k

Yote hayo, si kitu kwa Mungu. Kumbuka Sababu nyingine kubwa iliyomleta Bwana Yesu duniani, ilikuwa ni kutuponya magonjwa yetu. Na ndio maana ilimgharimu ateseke sana pale msalabani kwa mateso mengi, ili kwa kupigwa kwake kule wewe na mimi tupone.

1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.

Mathayo 8:16 “Hata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo; akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya WOTE waliokuwa hawawezi,

17 ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu”.

Hivyo, anachotaka kwanza kwako, ni wewe umwamini kwa moyo wako wote. Utubu dhambi zako zote, ikiwa ulikuwa bado hujamkaribisha katika maisha yako, Kisha baada ya hapo ndipo akuponye magonjwa yako yote kama alivyoahidi katika Zaburi 103:3.

 “Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote,”

Hivyo ukiwa upo tayari leo, kutubu dhambi zako, na kumkaribisha Bwana Yesu katika maisha yako. Basi, fuatisha sala hii ndani ya moyo wako kwa imani, ukimaanisha kabisa kumgeukia yeye, na kwamba unamuahidi kuwa akishakuponya utamtumikia yeye daima. Ikiwa upo tayari basi hapo ulipo ikiwa upo katika mahali pa utulivu, unaweza kupiga magoti yako, kisha sema sala hii kwa Imani;

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa kama utakuwa umesema sala hiyo kwa Imani, na kwa kumaanisha kabisa kutoka katika moyo wako. Basi Kristo Yesu ameshakusamehe, hivyo kuwa na amani, na kuanzia sasa uwezo wa kukuponya anao.

Basi nitakwenda kukuombea ugonjwa wako, Kisha Bwana atakufanyia uponyaji.

“Bwana Yesu, nakushukuru wa mwana wako huyu, ambaye ameona kuwa hakuna kimbilio lingine isipokuwa wewe. Naomba Bwana ukamponye magonjwa yake yote yanayomsumbua, iwe ni saratani, au mengine yoyote. Haijalishi madaktari wamesema amebakiwa na wiki mbili aishi au miaka 10. Tunafahamu kuwa wewe ndiye mponyaji. Hivyo nakuombwa Bwana, umponye Mama/dada/baba/kijana/mtoto huyu, anayesoma ujumbe huu. Na kuanzia sasa akawe mzima na huru, akakutumikie na kulitangaza jina lako lako daima kwa watu wote.

Asante Bwana kwa kumponya. Amen”.

Hivyo, kuanzia sasa, uponyaji wako umeshaingia katika mwili wako. Maombi tuliyoyaomba ni mafupi tu, lakini uamini kuwa tayari yameshaumba uponyaji katika mwili wako. Hivyo nachotaka kwako kuanzia sasa, utazame, mahali unapoumwa, na pia anza kufanya mazoezi, au pashughulishe pale ambapo ulikuwa huwezi kufanya chochote, au maajabu ya Yesu Kristo utayaona.

Bwana akubariki sana.

Kwa mawasiliano ili kujifunza zaidi biblia/ Ushauri/ Maombezi/ Shuhuda/Ibada, basi wasiliana nasi kwa namba hizi +255789001312/ +255693036618

Bwana akubariki.

Yerema 30: 17a “Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana,..”

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

YESU MPONYAJI.

JE! UKIMWI UNATIBIKA?

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments