NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe.

Je unajua ni kwanini Bwana Yesu aliwaagiza Mitume wake pamoja na sisi wote kwamba tuende ulimwenguni kote tukawafanye watu wote kuwa WANAFUNZI na si WAKRISTO? (Mathayo 28:19).

Je! Unajua neno Ukristo mara ya kwanza lilizaliwa wapi?

Tusome Matendo 11:26..

Matendo 11:26 “hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na WANAFUNZI waliitwa WAKRISTO kwanza hapo Antiokia”.

Umeona hapo?..Maana yake kabla akina Petro, akina Yohana, na wengine wote waliomwamini Yesu kujulikana kama wakristo, walikuwa wanajulikana kama wanafunzi, hapo kabla.

Maana yake kuwa mkristo ni kuwa MWANAFUNZI WA YESU. Hili ni jambo la muhimu kujua sana.

Sasa swali tunakuwaje wanafunzi wa Bwana Yesu?..au watu wa kanisa la kwanza walikuwa wanafanyikaje kuwa wanafunzi?.

Bwana Yesu alitoa vigezo..Katika kitabu cha Luka..

Luka 14:27 “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”

Sasa tukirudi katika Matendo biblia inasema “Wanafunzi waliitwa wakisto kwa mara ya kwanza hapo Antiokia”..Maana yake mkristo yeyote ni mwanafunzi.

Kwa mantiki hiyo basi sentensi ya Bwana aliyoisema katika Luka 14:27 ni sahihi kabisa kuiweka hivi…

“Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa MKRISTO”.

Umeona hapo?..Hebu tosegee tena mbele kidogo..

Luka 14:26 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,

26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake;  naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Maana ya hiyo sentensi ni kwamba..

26 “Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, HAWEZI KUWA MKRISTO”.

Kuchukia wazazi kunakozungumziwa hapo kuwachukia kwa chuki, bali kuchukia mawazo yao au mipango yao inayokinzana na mapenzi ya Mungu, kwamfano mzazi au ndugu anakuambia inakupasa urithi mikoba ya uchawi, au urithi chuki zake kwa mtu fulani, hapo Bwana anasema hatuna budi kuyachukia hayo mawazo na kuyakataa na kutoshirikiana nao hata kama watakutenga..hapo ni sawa na umewachukia ndugu zako, Kristo anakokuzungumzia..na ndio vigezo vya kuwa mwanafunzi yaani MKRISTO.

Tusogee tena mbele kidogo..

Bwana anasema..

Luka 14:33 “Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Kufuatia Matendo 11:26 inayosema kuwa Wanafunzi ndio wakristo..basi ni sahihi kabisa kuyaweka haya maneno ya Bwana katika hii Luka 14:33 hivi…

“Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, HAWEZI KUWA MKRISTO”.

Hiyo ikifunua kuwa kumbe miongoni mwa lile kundi lote lililokuwa linamfuata Bwana, wakristo walikuwa ni wachache sana..yaani ni wale wanafunzi wake tu, wa kike na wakiume, ambao walijikana nafsi na kujitwika misalaba yao na kumfuata Bwana Wengine wote hawakuwa wakristo.

Na maandiko yanasema Yesu ni yeye yule, jana na leo na hata milele. (Waebrania 13:8).

Ikiwa na maana kuwa kama vigezo vyake vya mtu kuwa mwanafunzi (yaani mkristo) vilikuwa ni kujikana nafsi na kubeba msalaba…basi vitakuwa ndio hivuo hivyo hata leo, kwasababu yeye ni yule yule habadiliki..

Waebrania 13:8 “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”.

Je! Wewe ni MKRISTO?…Umejikana nafsi? Umeuchukia ulimwengu na kuuacha?..kama bado basi fahamu kuwa wewe si mkristo, haijalishi unasali katika dhehebu kubwa au umebatizwa, bado sio mkristo.

Kama bado unalewa, au unazini, au unavaa nguo za kubana na kuonyesha maungo yako, bado sio mkristo..

Amua leo kujikana nafsi na kuubeba msalaba wako, wacha dunia ikuone umechanganyikiwa lakini wewe unajua unayafanya mapenzi ya Baba yako aliye mbinguni..

Bwana Yesu alisema..“Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake? ( Marko 8:36 ).

Itakufaidia nini uonekane wa kisasa halafu huendi mbinguni??

Bwana atupe macho ya kuona.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
1 year ago

Amen

Anonymous
Anonymous
1 year ago

Asante Sana neno lako limenibariki,na sasa nimeelewa vizuri..Mungu awabariki muendelee kutoa elimu zaidi.

Baraka Richard
Baraka Richard
2 years ago

Bwana Yesu asifiwe watumishi Nashukuru Kwamasomo manzuri Mungu awabariki Naomba Niunganishwe kwenye Mitandao ya kijamii kama Wathsap ili nisher na wengine.