Title July 2024

Epafrodito ni nani kwenye biblia?

Epafrodito alikuwa ni mmoja wa watendakazi wa makanisa yaliyokuwa Filipi. Anajulikana kama mhudumu wa mahitaji ya mtume Paulo. Tunaona upendo wa Kanisa la Filipi jinsi lilivyomkumbuka Mtume Paulo alipokuwa kifungoni Rumi. Hivyo likaazimu kumtumia mahitaji yake ya kifedha. Ndipo likamchagua huyu Epafrodito. Kusafiri umbali wote huo mrefu na kiasi hicho kingi cha fedha mpaka Rumi.

Wafilipi 4:18  Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu.

Na jambo hili lilikuwa ni desturi yao, kumtimizia Paulo mahitaji yake mara kwa mara (Wafilipi 4:16)

Lakini tunaona mbeleni katika waraka wa Paulo, anaeleza hali ya ndugu huyu ambaye Paulo  alimwita pia mtume,jinsi ilivyobadilika kwa kuugua sana karibu na kufa, akiwa katika kazi hiyo hiyo ya kumuhudumia Paulo. Lakini  Ijapokuwa alikuwa katika hali mbaya bado hakuacha kumuhudumia Paulo,

Tunasoma katika hali yake ngumu ya kuumwa, Mungu alimhurumia akamponya. Hatujui aliugua ugonjwa gani, lakini ni ugonjwa uliomdhoofisha kwelikweli, kiasi cha kudhaniwa ‘huyu ni wa kufa tu’, na bila shaka ulikaa ndani yake muda mrefu.

Lakini alipomaliza huduma yake, Ndio tunaona Paulo anawaandikia wafilipi waraka huo, na kuurejesha kwao kwa mkono wa huyo huyo Epafrodito,na ndani yake akielezea pia, shida zilizomkuta.

Wafilipi 2:25  Lakini naliona imenilazimu kumtuma kwenu Epafrodito, ndugu yangu, mtenda kazi pamoja nami, askari pamoja nami; tena ni mtume wenu na mhudumu wa mahitaji yangu.

26  Kwa kuwa alikuwa na shauku kwenu ninyi nyote, akahuzunika sana, kwa sababu mlisikia ya kwamba alikuwa hawezi.

27  Kwa maana alikuwa hawezi kweli kweli, karibu na kufa; lakini Mungu alimhurumia; wala si yeye peke yake, ila na mimi pia; nisiwe na huzuni juu ya huzuni.

28  Kwa hiyo nimefanya bidii nyingi zaidi kumtuma, ili mtakapomwona tena mpate kufurahi, nami nipunguziwe huzuni yangu.

29  Mpokeeni, basi, katika Bwana, kwa furaha yote, mkawahesabu watu kama huyu kuwa watu wa kuheshimiwa.

30  Maana kwa ajili ya kazi ya Kristo alikaribia kufa akaponza roho yake; ili kusudi ayatimize yaliyopungua katika huduma yenu kwangu.

Ni nini tunajifunza kwa mtumishi wa Mungu huyu?

Upendo wa kujali hali za wengine. 

Biblia inasema upendo hautafuti mambo yake wenyewe (1Wakorintho 13). Alikuwa tayari kufa, ili askari mwenzake asikose mahitaji yake. Si ajabu Paulo alimwita mtume. Mungu anathamini sana, utume wa namna hii.

Lakini Tunajifunza huruma ya Mungu ijapokuwa alikuwa karibu na kufa, bado Mungu aliweza kumponya akawa mzima kabisa. Hata mimi na wewe, je tunaweza kufikia hatua mbaya ambayo hata madaktari wanasema haiwezekani kupona? Kama ndio mkumbuke Epafrodito, una hali ngumu unayoweza kusema hapa sivuki, mwisho umefika? Mkumbuke Epafrodito. Yote yanawezekana kwa Mungu.

Ikiwa ni mtumishi wa Mungu, usiohofu uteterekapo kiafya au kihali, Mungu anakuona, atakutia nguvu, usiache kumwamini.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

USIFE NA DHAMBI ZAKO!

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

Rudi Nyumbani

Print this post

Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)

Epafra ndiye alikuwa mwangalizi wa kanisa la Kolosai, Paulo alimtambua  kama mhuhudumu mwaminifu wa Kristo. Kiasili naye pia alikuwa mwenyeji wa mji huo huo wa kolosai kufuatana na kauli Paulo aliyoisema katika Wakolosai 4:12, “aliye mtu wa kwenu”

Waraka huu unaonyesha Epafra kama  mhudumu ‘mwaminifu’ wa Kristo. Ikiwa na maana alijitoa kikamilifu kwenye kazi ya Mungu bila kupunguza chochote, mtumwa aliyegawa posho kwa wakati.

Aliyeitwa pia mjoli wa Paulo. Ikimaanisha mtendakazi pamoja na Paulo katika shamba la Bwana.

Lakini pia Paulo alikuwa ni kiongozi na mshauri wake. Tunaona aliwasilisha ripoti zake kwake, za maendeleo ya kanisa. Jinsi upendo wao ulivyokuwa mwingi.

Wakolosai 1:7  kama mlivyofundishwa na Epafra, mjoli wetu mpenzi, aliye mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yenu

8  naye alitueleza upendo wenu katika Roho.

Epafra alikuwa na juhudi sio tu kwa kanisa la Kolosai, bali pia na makanisani mengine ambayo ni  Laodikia na Hierapoli (Wakolosai 4:13).

Tunasoma pia Epafra alikuwa mtu wa bidii  ki-maombi kwa ajili ya kanisa la Kolosai

Wakolosai 4:12  Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu katika maombi yake, ili kwamba msimame wakamilifu na kuthibitika sana katika mapenzi yote ya Mungu.

13  Maana namshuhudia kwamba ana juhudi nyingi kwa ajili yenu, na kwa ajili ya hao walioko Laodikia, na kwa ajili ya hao walioko Hierapoli.

Lakini mbeleni katika waraka wa Paulo kwa Filemoni tunaona alikuja pia kufungwa, pamoja na Paulo kule Rumi.

Filemoni 1:23  Epafra, aliyefungwa pamoja nami katika Kristo Yesu, akusalimu;

Ni nini tunajifunza katika maisha ya Epafra?

Kujitoa kwake kimaombi, kwa kanisa ili lisimame kamilifu na kuthibitika katika mapenzi ya Mungu. Epafra alikuwa na juhudi isiyo ya kawaida katika kuliombea kanisa. Alijua kanisa lisipoombewa haliwezi kusimama vema. Hivyo aliwekeza sana katika maombi na kuwa pia na bidii katika uaminifu kwenye  huduma.

Bidii yake hakika ilizaa matunda, na ndio maana Bwana akaruhusu habari zake ziandikwe, na kusomwa hadi leo.

Je! Na sisi tunathamini maombi katika kuliombea kanisa? Unapoona watu wamepoa kiroho, watu wanaishi kimwili kanisani, wanafanya mambo ya aibu, sio kumnyooshea kidole mchungaji, au shemasi au mzee wa kanisa na kumlaumu. Hapo huwezi tatua tatizo. Shida ipo kwenye kupungukiwa kwa maombi. Chukua muda mwingi kuliombea kanisa kuliko kuzungumza. Bwana atayatenda yote uliyoyatamani.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya kuabudu malaika? (Wakolosai 2:18)

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,

UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; (Luka 17:10) 

SWALI: Naomba kufahamu maudhui iliyo nyuma ya  Luka 17:10 inayosema..

[10]Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.


JIBU: Kufahamu kwanini Yesu  aliwaambia wanafunzi wake maneno hayo. Ukianzia juu utaona ni kufuatana na swali walilomuuliza kuhusiana na IMANI. Walimfuata na kumwomba awaongezee Imani.

Lakini Yesu aliwajibu na kuwaambia kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali mngeuambia mkuyu huu ng’oka ukapandwe baharini nao ungewatii.

Luka 17:6

[6]Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng’oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.

Akimaanisha kuwa  sio suala la kuongezewa Imani, ili mweze kufanya makubwa, bali kile kidogo sana kinaweza tenda yote. Na kidogo hicho mitume walikuwa nacho ndani yao, ambacho hata mimi na wewe tunacho. Isipokuwa hawakujua namna ya kukitoa.

Ndipo Yesu akaendelea kuwaambia kwa mifano sasa, ili jambo hilo litokee, kanuni yake ni kuwa wanapaswa wawe kama watumwa wasiokuwa na faida kwa Bwana wao. Sasa kwa namna gani? fuatilia mfano wenyewe…

Luka 17:7-10

[7]Lakini, ni nani kwenu mwenye mtumwa alimaye au achungaye ng’ombe, atakayemwambia mara arudipo kutoka shambani, Njoo upesi, keti, ule chakula?

[8]Je! Hatamwambia, Nifanyie tayari chakula, nile; jifunge unitumikie, hata niishe kula na kunywa, ndipo nawe utakapokula na kunywa?

[9]Je! Atampa asante yule mtumwa, kwa sababu ameyafanya aliyoagizwa?

[10]Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.

Mfano huo unajieleza, zamani mtumwa aliponunuliwa hakuwa anafanya kazi kama mwajiriwa, bali kama mnyama tu mfano wa punda ambapo kazi yake ilikuwa ni moja tu kumuhudumia Bwana wake, na sio kujitafutia maisha.

Sasa hapo Yesu anatumia mfano wa huyo Bwana mwenye mtumwa wake ambaye amemweka kuwa mkulima wa shamba lake, ambaye asubuhi huondoka jioni hurudi kwa Bwana wake.

Anasema, je atakaporudi atamwambia kaa hapo upumzike? wakati mimi bado sijala? Ni wazi kuwa ataongezewa majukumu, mpaka ahakikishe Bwana wake ameshiba, hana mahitaji tena ndipo sasa na yeye apewe nafasi ya kupumzika na kula.

Hivyo Yesu alitumia mfano huo, kuwaambia wanafunzi wake, jinsi na wenyewe wanavyopaswa kuwa kwa Mungu.

“[10]Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.”

Akiwa na maana, mkihitaji hilo jambo la IMANI mjaliwe, yawapaswa muwe kama watumwa wasiokuwa na faida. Mtumikieni kwanza Bwana wenu sana, kama watu wasiotazamia malipo yoyote.

Ukihubiri sana miaka ishirini, unatanga na jua huoni faida yoyote iliyoongezeka kwenye maisha yako, huoni maendeleo yoyote. Usimuulize Bwana mbona hujanipa chochote mpaka leo. kuwa kama mtumwa asiye na faida.

Huu ndio utumishi Bwana anaoutaka kwetu, leo hii wahubiri wengi, watumishi wengi, wachungaji wengi wamepoa, wamerudi nyuma kwasababu walitazamia malipo kutoka kwa Bwana katika kwa kile walichokuwa wanakifanya, na waliopoona hawapati, kinyume chake maisha yao ndio yanakuwa magumu, wakaacha utumishi wakaenda kutafuta mambo yao.

Ndugu ni lazima tuelewe kanuni za Mungu wetu. Ikiwa unaenda kuifanya kazi ya Bwana ili ukusanye sadaka, upate unafuu kimaisha..Ni heri ukaacha ukatafute biashara nzuri uwekeze nguvu zako huko. Mungu anaweza asikupe chochote kwa miaka mingi, unataabika tu,  je utaendelea kumtumikia?

tukubali kuwa watumwa wasio na faida. Akitupa sawa, asipotupa sawa. Lakini tujue kuwa sikuzote anatuwazia yaliyo mema.

Ujumbe wa Bwana hapo ni kwamba tukitaka imani itoke tuwe watumwa wa namna hii.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.

Tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu.

Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani.

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu mana ya Zaburi 48:14 Yeye ndiye atakayetuongoza

SWALI: Ipi tafsiri ya Zaburi 48:14 ?

[14]Kwa maana ndivyo alivyo MUNGU, Mungu wetu. Milele na milele  Yeye ndiye atakayetuongoza.


JIBU: Mwandishi anajivunia sifa ya Mungu wao wa milele. kwamba ndiye atakayewaongoza.

Akiwa na maana atayewaongoza katika mambo yao yote, kwamba kamwe hawezi kuwaacha, atakayewaongoza njia sahihi ya uzima, njia sahihi ya kupigana vita, ya kujenga na kupanda.

Ndivyo ilivyokuwa kwa wana wa Israeli. Mungu alikuwa nao jangwani kwa nguzo ya moto na wingu kuwaongoza, aliwapelekea malaika wake kuwalinda, aliwafundisha namna ya kupata faida katika shughuli zao, akawainulia na waamuzi, pamoja na wafalme na manabii kuwachunga na mwisho akawaletea mkombozi, ambaye ndio ukamilifu wa yote. Kuonyesha wema wake na kiu yake ya kuwaongoza  watu wake.

Hata sasa, sifa yake ndio hiyo hiyo, ndio maana na sisi tuna ujasiri wa kusema…

‘Yeye ndiye atakayetuongoza’.Sio tu kwa wakati huo, bali mpaka siku ya kufa kwetu.

Alipokuja mwokozi hakutuacha hivi hivi kama mayatima, bali alituachia msaidizi ambaye anatuongoza na kututia katika kweli yote, ndiye Roho Mtakatifu.

Yohana 16:13

[13]Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Bwana akubariki.

Je umempokea Yesu?  Kama bado ni nini unasubiri ? Fungua hapa kwa mwongozo wa sala  ya toba ya imani. >>>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.

Fahamu maana ya Mhubiri 10:9 Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo;

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

Rudi Nyumbani

Print this post

‘Waibao watu ‘ sawasawa na 1Timotheo 1:10 humaanisha nini?

SWALI: Biblia inapowataja ‘waibao watu ‘ sawasawa na 1Timotheo 1:10 humaanisha nini?


JIBU: Tusome;

1 Timotheo 1:8-10

[8]Lakini twajua ya kuwa sheria ni njema, kama mtu akiitumia kwa njia iliyo halali;

[9]akilifahamu neno hili, ya kuwa sheria haimhusu mtu wa haki, bali waasi, na wasio wataratibu, na makafiri, na wenye dhambi, na wanajisi, na wasiomcha Mungu, na wapigao baba zao, na wapigao mama zao, na wauaji,

[10]na wazinifu, na wafiraji, na WAIBAO WATU, na waongo, nao waapao kwa uongo; na likiwapo neno lo lote linginelo lisilopatana na mafundisho yenye uzima;

Tangu zamani dhambi ya wizi, haikuwa tu katika vitu na mali, bali ilikuwa hata katika watu. Ndio kilele cha juu kabisa cha wizi.

Wizi huu ulikuwa na  malengo mbalimbali mojawapo ilikuwa ni kuwapeleka vitani, lakini pia kuwauza kama watumwa mfano katika biblia utamwona Yusufu (Soma Mwanzo 40:14-15). Na kama tunavyofahamu pia katika historia bara la Afrika lilikumbwa na tatizo hili, katika karne ya 17, waafrika wengi waliibiwa, na kuuza katika mabara ya ulaya.

Lakini kwa nyakati hizi wizi huu, umekuwa mbaya zaidi, kwasababu watu hawaibi tena watu kwa lengo la kuwatumikisha, bali kwa lengo la kuwafanyisha biashara ya kikahaba, wengine kuwaua ili wachukue viungo vyao kwa kazi za kishirikina, wengine wauze viungo vyao vya ndani kama vile figo, ili wapate fedha.

Jambo ambalo ni baya sana, ndio maana kwenye maandiko katika enzi za agano la kale adhabu ya wizi wa watu  haikuwa ndogo bali kifo.

Kumbukumbu la Torati 24:7

[7]Mtu akionekana anamwiba nduguze mmojawapo katika wana wa Israeli, akamfanya kama mtumwa, au kumwuza; na afe mwivi huyo; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako.

Lakini sisi katika agano jipya, hatuna ruhusa ya kuua watu wa namna hiyo, isipokuwa tuonapo vitendo kama hivyo vikitokea ni ripoti katika vyombo vya dola, hapo utaisaidia jamii, kudhibiti uovu kama huo Lakini pia kumwomba Mungu, aiondoe roho hii chafu isiwepo katikati ya  jamii zetu, ili kuiponya kuiponya jamii.

Na Mungu atakubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea. Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ALIJARIBIWA SAWASAWA NA SISI KATIKA MAMBO YOTE.

Je! Malaika wanazaliana?

USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE.

Mikono iliyotakata ni mikono ya namna gani? (1Timotheo 2:8).

Rudi Nyumbani

Print this post

Marimari ni nini? (Luka 7:37)

Jibu: Tureje..

Luka 7:37  “Na tazama, mwanamke mmoja wa mji ule, aliyekuwa mwenye dhambi, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya MARIMARI yenye marhamu”.

 “Marimari” ni jina lingine la “Marumaru”, kwahiyo popote katika biblia palipotajwa Marimari ni sawasawa na Marumaru. Na marimari ni mawe ya kaboni, ambayo yanatumika katika urembo wa ujenzi, mawe haya ni maarufu sana kwa kutengenezea Tiles za ukutani au chini.

Vile vile yanatumika kutengenezea baadhi ya vyombo vya kinakshi mfano wa cha hicho cha mwanamke katika Luka 7:37 n.k

Maandiko mengine yanayotaja Marimari ni pamoja na 1Nyakati 29:2, Wimbo ulio bora 5:15 na Ufunuo 18:12… lakini andiko lililotaja Marimari kama Marumaru ni Esta 1:6.

Je umempokea BWANA YESU, na kubatizwa katika ubatizo sahihi?.. Je unatambua kuwa tunaishi katika majira ya kurudi kwa YESU mara ya pili, na wakati wowote parapanda ya mwisho inalia?

Je macho yako yanaona hayo yote?.. kama huyaoni hayo basi fahamu kuwa upo gizani na yule mkuu wa giza (shetani) amekupofusha macho ili usione, Leo harakisha kupokea msaada kutoka kwa YESU.

Ikiwa utahitaji kumpokea YESU leo, basi fuatiliza sala hii hapa >>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Sala ya baraka (Hesabu 6:24-26).

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

SI KILA KILICHO HALALI KINAFAA.

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je ni sawa kuukubali udhaifu kama mtume Paulo alivyojisifia kwa huo? (2Wakorintho 12:9-10)

SWALI: Je udhaifu ni jambo la kulikubali? Kama tunavyoona mtume Paulo akiusifia katika;

2 Wakorintho 12:9-10
[9]Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juuyangu.

[10]Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.

Paulo Hajisifii udhaufu, kana kwamba ni mzuri wa kuvutia, hapana hakuna udhaifu ulio mzuri umfanyao mtu ajiivunie huo……lakini linapokuja eneo la Mungu, udhaifu humnyenyekesha mtu, na hivyo humfanya mtu huyo kutegemea zaidi nguvu za Mungu, kuliko uweza wake mwenyewe ndicho kilichokuwa kwa Paulo.

Anasema hakuwa mtu mwenye ujuzi wa maneno, au utashi mwingi wa kitume kama wanavyodhaniwa watumishi wa Mungu wote kuwa nao.

2 Wakorintho 10:10

[10]Maana wasema, Nyaraka zake ni nzito, hodari; bali akiwapo mwenyewe mwilini ni dhaifu, na maneno yake si kitu.

Lakini katika udhaifu huo wa kunena, maelfu ya watu walikuja kwa Kristo, katika udhaifu huo wa kimwili miujiza mikubwa ilifanyika kwa mikono yake. Hivyo akamshukuru Mungu kwa hilo, ili watu wasidhani ni kwa uwezo wake au kipawa chake fulani maalumu aliweza kuyafanikisha hayo.

Ndivyo tunavyojifunza hata kwa Musa, Mungu kumtumia kwa viwango vile haikuwa katika uweza wake wowote, kwasababu alikiri mbele za Mungu yeye sio mnenaji.(Kutoka 4:10), lakini pia Mungu alimshuhudia kuwa ni mpole kuliko watu wote waliokuwa duniani kipindi kile. Tofauti labda na makuhani wengine au manabii waliokuja au kuwepo kabla yake.(Hesabu 12:3)

hata leo, pale tunapojiona ni wadhaifu fulani mbele za Mungu kimaumbile au kiusemi, au kihali, hapo ndipo mahali pazuri pa kitumiwa na yeye. Usifadhaike wala usife moyo ukasema mimi siwezi, amini tu, kwasababu yeye hategemei ulichonacho, bali Neno lake moyoni mwako, ukiliweka yote yawezekana kwako. Amini tu.

1 Wakorintho 1:26-29

[26]Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;

[27]bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;

[28]tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; [29]mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu. 

fuatilia ushuhuda hizi zitakujenga..

USHUHUDA WA RICKY:

JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?

Lakini hilo halimaanishi kwamba udhaifu wowote ni mzuri, kwamba tujivunie katika hayo, hapana hakuna raha katika ulemavu, au katika ububu, au katika upofu..Lakini tujapo kwa Kristo ni mtaji mzuri wa Mungu kututumia. Hiyo ni kutudhuhirishia kuwa kwa Mungu hakuna kiungo hata kimoja ambacho hakiwezi kumtumikie yeye. Sote kwa pamoja tuwe na elimu tusiwe na elimu, tuwe na afya tusiwe na afya, tuwe na vijijini tuwe mijini, tunajukumu la kumtumikia Mungu, na kufanya vema kabisa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.


Mafundisho mengine:

MUNGU ALIVICHAGUA VITU AMBAVYO HAVIKO.

USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.

Ipi tofuati ya “Kutakabari” na “kutakabali”?

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)

Swali: Katika Mhubiri 9:16, neno la Mungu linasema kuwa hekima ya maskini haisikilizwi, je na sisi tunapaswa tusizisikilize hekima/mashauri ya watu wasio na kitu, ili kujinusuru..au andiko lina maana gani?


Jibu: Turejee..

Mhubiri 9:16 “Ndipo niliposema, Bora hekima kuliko nguvu; WALAKINI HEKIMA YA MASKINI HUDHARAULIWA, WALA MANENO YAKE HAYASIKILIZWI”.

Tukiusoma huo mstari peke yake ni rahisi kuona au kujifunza kuwa “hatupaswi kusikiliza watu maskini” hususani wanapopendekeza mambo.. (na watu maskini ni pamoja na kundi la watu wasio na elimu kabisa).. Lakini hebu tuanzie ule mstari wa 13, tuone kama hiyo ndio maana yake.

Mhubiri 9:13 “Pia nimeona hekima chini ya jua, nayo ni kama hivi, tena kwangu mimi ilionekana kuwa ni neno kubwa.

14 Palikuwa na mji mdogo, na watu ndani yake walikuwa wachache; akaja mfalme mkuu juu yake, akauhusuru, akajenga ngome kubwa ili kuupiga.

15 BASI, KULIONEKANA HUMO MTU MASKINI MWENYE HEKIMA, naye kwa hekima yake akauokoa mji ule lakini hata hivyo hapakuwa na mtu ye yote aliyemkumbuka yule mtu maskini.

16 Ndipo niliposema, BORA HEKIMA KULIKO NGUVU; walakini hekima ya maskini hudharauliwa, wala maneno yake hayasikilizwi”.

Huyu Maskini alikuwa na Hekima ya kuuokoa mji, ijapokuwa hakuwa na elimu, wala ujuzi mwingi, pengine wala hakuwa katika siasa ya nchi, lakini alitoa wazo bora, na kufanya nchi isiingie katika vita. Lakini baada ya mji kuokoka na kuwa na Amani, hawakumkumbuka yule maskini kwa kumpa thawabu.

Hilo halikumshangaza sana Sulemani, lililomshangaza Zaidi ni kuona  kuwa “KWANINI HEKIMA ZA MASKINI HAZISIKILIZWI”.. na wakati hao wanazo hekima za kuweza hata kuunusuru mji usiangamie!!!, kama mfano wa huyo tuliyemsoma hapo juu.

Hilo likamshangaza sana Sulemani, na ushauri wake ni kwamba tuwatafute hao (maskini) na kujaribu kusikiliza mashauri yao na tusiwadharau kwani baadhi yao wamebeba vitu vikubwa…

Na ndipo akasema Bora kuwa na hekima kama huyu kijana maskini kuliko kuwa na nguvu (za kimwili na kifedha na kielimu) na kukosa hekima.

Mhubiri 9:16 “Ndipo niliposema, Bora hekima kuliko nguvu; WALAKINI HEKIMA YA MASKINI HUDHARAULIWA, WALA MANENO YAKE HAYASIKILIZWI”.

Hivyo kwa tafakari hiyo tutakuwa tumeshapata jibu kuwa sio kwamba Biblia inatufundisha kutowasikiliza maskini au kuwadharau…bali kinyume chake inatufundisha “tusiwe na dharau nao, kwani kwa sehemu moja, wapo baadhi wenye hekima hata za kuweza kuokoa Taifa, mfano wa huyo tuliyemsoma hapo juu”.

Hivyo ndugu usimdharau mtu ambaye unaona ni mnyonge kuliko wewe, ambaye unaona pengine hana mali kama ulizonazo wewe, au hana uwezo kama ulionao wewe, au hana elimu kama uliyo nayo wewe… Watu hao unaowadharau wewe baadhi yao wamebeba vitu vikubwa sana kwaajili yako, ambavyo vinaweza kukusaidia wewe au watu wako!.

Hivyo sikiliza watu wote, na chuja mambo yote. Si wote walio maskini ni wajinga, na pia si maskini wote wana hekima… vile vile si wote walio matajiri wanazo akili, wengi hawana akili wala hekima ingawa mbele za watu wanaweza kusifika..

Biblia inasema heri kijana maskini mwenye hekima, kuliko mfalme mzee halafu mpumbavu (Soma Mhubiri 4:13).

Hivyo hatuna budi kuwa watu wanyenyekevu daima na wenye kusikiliza.

Bwana atusidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwa namna gani Bwana YESU atagawiwa sehemu pamoja na wakuu? (Isaya 53:12)

Swali: Katika Isaya 53:13 tunausoma unabii wa Masihi (yaani YESU), Kwamba atakuja kugawiwa sehemu pamoja na wakuu…je! hawa wakuu ni akina nani atakaokuja kugawiwa nao sehemu?…na nini kinagawiwa hapo?


Jibu: Turejee…

Isaya 53:12 “Kwa hiyo nitamgawia sehemu PAMOJA NA WAKUU, Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari; Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa, Akahesabiwa pamoja na hao wakosao. Walakini ALICHUKUA DHAMBI ZA WATU WENGI, Na kuwaombea wakosaji”.

Mstari huo ni kweli unamhusu BWANA YESU (Aliye Masihi) na ni  rahisi kutafsirika hivi “kwamba kuna wakuu wanaoishi ambao Bwana YESU naye atakuja kupewa sehemu pamoja nao”.

Tafakari hii sio sahihi, na wala sio maana ya maandiko hayo…kwani hakuna mwanadamu yoyote anayeweza kulinganishwa na YESU wakati huu wa sasa na hata baada ya maisha.

Sasa maana halisi ya mstari huo ni ipi?.

Maana ya mstari huo ni hii… “Mungu atamgawia sehemu Bwana YESU na pia atawagawia sehemu WAKUU”…Maana yake Bwana ana sehemu yake na hao wakuu wana sehemu yao..lakini wote watakuwa na sehemu.

Ndio tukiunganisha maneno hayo mawili tunapata sentensi hiyo “ Mungu atamgawia  sehemu pamoja na WAKUU”...

Sasa hiyo sehemu ni ipi na hao wakuu ni akina nani?

“Sehemu” inayozungumziwa hapo ni “Mji wa kimbuinguni, Yerusalemu Mpya” (Soma Ufunuo 22:19).

Na “Wakuu” wanaozungumziwa hapo ni watakatifu watakaoshinda siku ile,  hao ndio wanaoitwa “wakuu”. (Wale watu wote walioishi maisha ya kujinyenyekeza kama watoto walipokuwa duniani) sawasawa na Mathayo 18:2-3.

Mathayo 18:2 “Ni nani basi aliye MKUU katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,

3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”

Soma pia Luka 7:28 utaliona jambo hilo hilo.

Kwahiyo sehemu ya BWANA YESU ni KITI CHA ENZI CHA DAIMA… na sehemu ya watakatifu watakaoshinda, ambao wataitwa wakuu ni YERUSALEMU MPYA.

Na wanadamu wengine ambao hawatakuwepo katika hilo kundi la ‘wakuu’, basi hawana sehemu yoyote katika mji mtakatifu, bali biblia inasema sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti.

Ufunuo wa Yohana 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, SEHEMU YAO NI KATIKA LILE ZIWA LIWAKALO MOTO NA KIBERITI. HII NDIYO MAUTI YA PILI”.

Tujitahidi tukapate sehemu pamoja na Bwana WETU.

Tujinyenyekeze kama watoto, tukatae udunia na kumwamini YESU, tuache dhambi na tuichukie, tutafute haki na kusimama imara.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MKUU WA ANGA.

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Mbari ni nini kibiblia?

Mbinguni ni sehemu gani?

Fahamu Namna ya Kuomba.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mhubiri 10:15 Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja,

SWALI: Je, mstari huu tunaousoma kwenye Mhubiri 10:15 una maana gani?

Mhubiri 10:15

[15]Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja, Maana hajui hata njia ya kuuendea mji.


JIBU: Kwa namna ya kawaida ya kibinadamu tunajua watu wengi hutamani kuishi mijini kuliko mashambani. Kwasababu mijini huduma zote hupatikana, na ni mahali pa raha. Hata kazi, mtu anazozifanya mashambani, wengi wao ni ili matunda yake wakayafurahie mjini, Au wakaziuze bidhaa zao huko wawe matajiri.

lakini tengeneza picha mtu, ambaye anajitaabiisha kufanya kazi kwa lengo la kuzifurahia mjini, halafu hajui njia ya kufika huko, kinyume chake ndio anakwenda mbali zaidi na mji, anaelekea majangwani au mabondeni?  ni wazi kuwa mtu kama huyo  hawezi kuwa na raha katika kazi yake, kwasababu taabu yake haina faida, alikosa malengo au hakuwa na maarifa sahihi.

Ni ufunuo gani upo nyuma yake?

Na sisi pia tuliomwamini Kristo. Tuna mji ambao tunatarajia kuungia, ndio ule Yerusalemu mpya ishukayo kutoka mbinguni kwa Baba..

Ufunuo  21:2-3

[2]Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe. 

 [3]Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. 

Anaendelea kusema…

Ufunuo  22:14-15

[14]Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. 

[15]Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

Huo ndio ule mji halisi ambao hata Ibrahimu aliona, ikamfanya aishi maisha kama ya mpitaji hapa duniani.

Waebrania 11:8-10

[8]Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako. 

 [9]Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile. 

 [10]Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu. 

Umeona na sisi ili tuweze kuonekana tumestahili kuuingia katika mji huo wa mbinguni hatuna budi tuwe tumeokolewa na YESU KRISTO. Kwasababu yeye ndio NJIA ya kuuingia mji.

Ukiwa nje ya Kristo tafsiri yake wewe ni mpumbavu, kwasababu taabu yako yote ya hapa duniani, haikufikishi popote haikuepeki mjini mwa Mungu, itakuchosha tu, utakuwa na magorofa, utaijaza akaunti fedha, utakuwa ni miradi mikubwa lakini mwisho utakufa, na kwenda kaburini. Lakini ukiiona njia na kuifuata Yerusalemu basi hufanyi kazi ya bure, unapojiwekea hazina kule hufanya kazi ya kushosha, ni uzima baada ya kifo. Utafaidi matunda yake

Je umeokoka?

Ikiwa bado na unatamani kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo >>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yerusalemu ni nini?

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)Maana ya Mhubiri 1:9 “wala jambo jipya hakuna chini ya jua”. (Opens in a new browser tab)

MJI WENYE MISINGI.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post