Fahamu Namna ya Kuomba.

Fahamu Namna ya Kuomba.

Wengi wa wanaompa Yesu Kristo maisha yao kwa mara ya kwanza, ndio maswali ya kwanza kwanza kujiuliza…nitaombaje! namna gani ya kuomba ili Mungu anisikie!

Kiuhalisia hakuna fomula fulani maalumu ya kuomba wala chuo fulani maalumu cha kujifunzia kuomba, Kwasababu Mungu wetu si mwanadamu wala hana udhaifu wa kutuelewa…Sehemu nyingine katika maandiko inasema “Baba yetu wa mbinguni anajua tujayohitaji hata kabla sisi hatujamwomba”

Unaona? kwa sentensi tu hiyo inaonesha kuwa Mungu si dhaifu wa kutuelewa sisi, kiasi kwamba tunahitaji course fulani tukasome ndipo atuelewe au kutusikia. Kitendo cha Kuwa mwanadamu tu! tayari Mungu anakuelewa kuliko unavyojielewa.

Hivyo mbele za Mungu, hatuendi na mpangilio mzuri wa Maneno kama tunavyoandaa hotuba kwenda kuisoma mbele za Mkuu wa Nchi…Isipokuwa tunakwenda na hoja zenye nguvu...Na hoja hizo ndio zile Bwana alizotufundisha wakati wa kuomba..katika Mathayo 6

“9 Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,

10 Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.

11 Utupe leo riziki yetu.

12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.

13 Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina”.

Kwamba tuombapo tuhakikishe tunaomba toba, na pia tuhakikishe nawasamehe wengine ili na sisi pia tusamehewe…Kadhalika tunapoomba tuhakikishe tunalitukuza jina la Yesu, na pia tunaomba ufalme wake uje…Na pia tusisahau kusema mapenzi yake yatimizwe…kwasababu sio kila kitu tunachokiomba ni mapenzi ya Mungu…Pia tunapaswa tumwombe Mungu atupe riziki zetu za kila siku, kama chakula, mavazi, malazi pamoja na fursa.

Kadhalika tunamwomba asitutie majaribuni hiyo inahusisha kumwomba Bwana atuepushe na yule mwovu katika maisha yetu, imani yetu, familia zetu, kazi zetu, huduma zetu za kila siku za kuwaleta watu kwa Kristo, tunazungukwa na nguvu za yule adui kila mahali, hivyo ni muhimu kumwomba Bwana atuepushe na mitego yake yote.

Na bila kusahau kurudisha utukufu, na kutambua kuwa uweza, nguvu na mamlaka vina yeye milele na milele…Hivyo hakuna kama yeye, na yeye ndiye mwanzo na mwisho.

Hizo ndio hoja zenye nguvu…usitazame ni maneno kiasi gani umekosea kuongea, wala ni lugha gani umezungumza wakati wa kuomba, hakikisha tu maombi yako yanahusisha hivyo vipengele.

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye
namba hizi: +255789001312/ +255693036618


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

FAIDA ZA MAOMBI.

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

TUMEAMBIWA TUNAPOSALI TUSIPAYUKE-PAYUKE, JE! HUKO KUPAYUKA PAYAUKA NDIO KUPI?

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments